Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Kuna shule inaitwa Mwakavuta (wenyeji wanaiita Mwakauta) nikavuta siku za kuripoti kwa kua nilitaka nitoke nyumbani baada ya valentine day.

Nafika siku hiyo ni jumapili siku ya wali. Nikala kidogo nikaugawa, naenda kuosha sahani ghafla ukungu umetanda kiasi hauwezi kuona hatua mbili mbele.
Nikasimama pale pale kwa zaidi ya dakika 45 ili ukungu upite nisije nikapotea nikaingia msituni. Sehemu yenye baridi kali kama haujavaa viatu au ni vyepesi vidole vya miguuni unaanza kuhisi vinachomwa chomwa na sindano. Nahisi ni dalili za kua frostbitten.

Ukungu unamalizikia vidole vikawa vinaonyesha kama damu imevilia. Tumelala bwenini nakutana na watu kutoka Chunya, Kilimanjaro, Moshi, Kigoma, Mafinga n.k. na wote wanasema baridi la pale si mchezo.

Asubuhi naamka. Njia za shule zote zina theluji, boksa niliyoiacha jana kwenye kamba imeganda kwa barafu.

Nikaanza kupima pros na cons.
-Kwanza walimu walituambia watoto wa O Level wote wana ngoma, kumbe na wale watoto waliambiwa sisi wote tuna ngoma. Ingawa wakinga siyo wabanaji lakini hilo doa litachukua muda wangu.

-Shule haina mabinti wazuri, hao waliopo wavuna mbao na wanakijiji wote mnawagombea.

-Unaweza kua na hela lakini hakuna cha kununua.

-Umbali mpaka wilayani ni 22KM na gari ni moja likipita limepita ama utembee, nilitembea aisee nilikoma, kila sehem ya mwili iliuma. Nilienda kupiga PPS hadi PPS zinatoka ndo nagundua kuna makamasi yalikua yananitoka. Sijui mpiga picha alidhani urembo.

-Rate ya kupiga puchu ikawa juu.

-Walimu wawili wa masomo yangu walikua wanakukaririsha kitu cha kitabuni hawakichambui wala nini halafu ni unasomewa sasa akiwa anasoma unagundua na yeye kuna vitu anavijua hapo. Mmoja alienda Mbeya akakaa zaidi ya mwezi huku somo limesimama.

-Chakula kibaya sijapata kujua. Kuna wadudu hua wanaranda randa kwenye balbu ukiwaua wanatoa harufu mbaya, sasa wale unawakuta kwenye maharage wapo kibao. Wali ikawa ndiyo luxury food, ugali unaula kidogo, asubuhi unanywea uji, makande, unakula kidogo asubuhi unanywea uji.
Wali ulisababisha watu wapigane, kulikua kuna paper two sasa form six wanajihisi wao ndiyo wanatakiwa kuanza, jamaa wa form five akafosi kingi ebwana washkaji wawili akaanza kumpiga.
Ila baadaye na yeye aliwatafuta mmoja mmoja na wakamheshimu.

Nilifeli kwa mengi.
pole sana mkuu
 
Akina sisi wa Mzizima na Shaaban Robert tunacomment wapi jamani?!
 
Ile Kilamanjato Boys noma sana wenyewe tuliita "Kiliboys" hapa nakumbuka:-
1. Dogo mmoja form one ilikuwa siku ya ijumaa mchana ni makande hapa kunakuwa na vurugu sana bwaloni, yule dogo kawahi kajaza sahani akala kiasi kilichobaki akafungia kwenye mzinga(sanduku la chuma) ili jioni aendelee na makande yake asipange foleni ya ugali, wahuni wakamtaim ametoa wakageuza sanduku lile chini juu na kulitikisa sana kisha wakalirudisha kama lilivyokuwa. Pata picha alivyokuja kufungua sanduku baadae, ikumbukwe sanduku hili ndio lina kila kitu kuanzia uniform na vitu vingine.

2. Uzuri wa hii shule hakuna kukacha prepo ukajificha bwenini, mabweni yalikuwa na vibwengo sana hasa hasa bweni la horombo.

3. Shule ilikuwa mbali sana na wilayani, haina fensi huwezi hata kutoroka ni pori tupu na kuna tembo porini kutokea Kenya.

SIKU HIZI NASIKIA IMEPOA IMEKUWA SHULE YA WANAWAKE.
 
Form one nimeingia nikaambiwa baada ya prepo saa nne nitasikia kengele niende assemble nikachukue machungwa [emoji16]
Nilienda nikajiona alone

Enzi hizo form five tunawaita chuwa

Unakaa ghorofani unampiga mtu water splash anaepita chini sometimes ya maji ya moto au mawe ila kama mbabe akigundua room anakuja kumwaga maji ya bafuni room nzima
Waafrika tumezaliwa na roho ya ukatili, eeh. Kumbe tusimlaumu Jiwe. Ukatili ni asili yetu.
 
Mwaka 1992 wakati naanza boarding form i ilikuwa balaa sana,mbeya moja hiyo baridi kama lote hata kufua ngumu mikono inauma balaa.
Blanket nilikuwa ninarudisha home enzi zile hata washing machine hakuna. House boy alikuwa anapambana nalo
 
Ile Kilamanjato Boys noma sana wenyewe tuliita "Kiliboys" hapa nakumbuka:-
1. Dogo mmoja form one ilikuwa siku ya ijumaa mchana ni makande hapa kunakuwa na vurugu sana bwaloni, yule dogo kawahi kajaza sahani akala kiasi kilichobaki akafungia kwenye mzinga(sanduku la chuma) ili jioni aendelee na makande yake asipange foleni ya ugali, wahuni wakamtaim ametoa wakageuza sanduku lile chini juu na kulitikisa sana kisha wakalirudisha kama lilivyokuwa. Pata picha alivyokuja kufungua sanduku baadae, ikumbukwe sanduku hili ndio lina kila kitu kuanzia uniform na vitu vingine.

2. Uzuri wa hii shule hakuna kukacha prepo ukajificha bwenini, mabweni yalikuwa na vibwengo sana hasa hasa bweni la horombo.

3. Shule ilikuwa mbali sana na wilayani, haina fensi huwezi hata kutoroka ni pori tupu na kuna tembo porini kutokea Kenya.

SIKU HIZI NASIKIA IMEPOA IMEKUWA SHULE YA WANAWAKE.
Hubby alisoma hapo alitoka na Div One O level
 
Kila mtu anaongelea form five, wenzenu tumeanza boarding tangu standard 5 enzi hizo za Nyerere tunapiga mchaka mchaka kila asubuhi na kupiga gwaride na ngoma kuingia darasni lakini lazima kwenda kwenye ibada ya asubuhi. Ilikuwa shule ya Fransiscan sisters. Mlo mzuri. Sec. Ilikuwa the best when it comes for food and accademic. Sitasema maana nitajulikana wapi. Ila atakayejua nani waliwaita wenzie Pimbi atajua nilisoma wapi.
Noah hongera, boarding mimi nilianza Primary lakini shule za RC zilikuwa na tofauti kubwa na za serikali.
Shule za RC kabichi lililaangwa kwa Nyanja na kitunguu na ugali wa sembe kama home tu .
 
Wakati naripoti kidato cha 1, mzee alinipeleka hadi shuleni. Nilipofika shuleni, nikakabidhiwa kwa mwalimu wa nidhamu. Mzee alisoma shule za zamani za mkoloni. Akawa anaongea Kiingereza na mwalimu wa nidhamu lakini mwalimu anajibu kwa Kiswahili. Mzee akaruhusiwa kuondoka. Alipoondoka, mwalimu akanikabidhi kwa kijana mmoja ambaye alikuwa kidato cha 4 anipeleke bwenini. Tulipofika bwenini. Yule bwana akaanza kuongea kimombo huku akiwaambia wenzie, "we have a newcomer". Nilikuwa siwezi kuongea kimombo lakini kwa mbali nilikuwa naelewaelewa. Huyu wa kidato cha 4 alikuwa anasoma na kijana mmoja anayetoka kijijini kwetu. Kwa hiyo akaniunganisha kwake. Maisha yakaanza.

Kulikuwa hakuna maji shuleni. Kula ni mpaka uchote maji mtoni kwa ndoo na kuyapeleka jikoni. Kazi ambayo wanafunzi walifanya kwa zamu. Kuoga lazima uende mtoni. Kwa vile ilikuwa mkoa wa Kagera, kulikuwa na kazi ya kumenya ndizi kwa chakula cha shule. Usipomenya, hakuna kula. Hili nalo tulilifanya kwa zamu. Chooni ukiingia, utanuka harufu ya choo kwa saa nzima baada ya kutoka. Kwa hiyo, kupunguza harufu, unavua nguo na kuziacha nje kabla ya kutumia choo. Juma la kwanza shuleni, niliharisha sana. Nikata kuacha shule. Ila pesa zangu alikuwa nazo yule kijana tunaetoka naye kijiji kimoja. Nilipomuomba pesa ili nirudi kijijini alikataa kunipa. Kidato cha pili walikuwa wanatuvamia usiku tumelala na kutupiga na kukimbia. Kuna wanafunzi wenzetu wawili waliamua kuacha shule na kurudi kijijini kwao! Mateso yalikuwa ni mateso.

Mungu anisamehe. Umasikini unaweza kufanya ufanye mambo mabaya na ujute. Wakati bado niko O-level, kuna siku nilitapeli. Nilikuwa sina pesa. Nikamuuzia mtu tiketi ya meli iliyokwisha tumika. Na mimi pia nilikuwa nasafiri siku hiyo. Ili nisitambulike kirahisi, nikabadilisha nguo baada ya kuuza tiketi. Wakati nakwenda kupanda meli, nikamwona niliyemuuzia amekataliwa kuingia katika meli. Na akaniona na kunitambua japo nilikana. Nilichukuliwa juu juu na kupigwa makofi lakini niliendelea kukana. Mwishoe waliniruhusu kuingia katika meli na nikamwacha yule bwana. Sijui aliruhusiwa kusafiri ama la. Kwa kweli ili jambo bado nalijutia hadi leo.

Nilichofanya ni kuwaepusha watoto wangu na maisha ya aina hii.
 
Siku ya kwanza nafika shule nikamtongoza mama mmoja alikua mpishi Wa canteen ya shule..akanikubali basi nilikula bure canteen mwaka mzima lakini nikaja kutembea na mtoto wake aliekuwa anasoma hapo kidato cha pili hapo ndipo huduma za mama zilipokata ila mtoto akawa ananihudumia zaidi ya mama mtu
 
Siku ya kwanza nafika shule nikamtongoza mama mmoja alikua mpishi Wa canteen ya shule..akanikubali basi nilikula bure canteen mwaka mzima lakini nikaja kutembea na mtoto wake aliekuwa anasoma hapo kidato cha pili hapo ndipo huduma za mama zilipokata ila mtoto akawa ananihudumia zaidi ya mama mtu
Duuh...[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Ukalaa mama na mwana
 
Siku ya kwanza nafika shule nikamtongoza mama mmoja alikua mpishi Wa canteen ya shule..akanikubali basi nilikula bure canteen mwaka mzima lakini nikaja kutembea na mtoto wake aliekuwa anasoma hapo kidato cha pili hapo ndipo huduma za mama zilipokata ila mtoto akawa ananihudumia zaidi ya mama mtu
Yaani hapo ni kidato cha 1? Nyie wengine naona mlikuwa tofauti na mimi. Mimi wakati niko kidato cha 5, ndevu zimeanza kutoka sasa, niliwahi kupendwa na msichana aliyekuwa anafanya kazi tayari. Alikuwa anafanya kazi TANESCO wilayani. Basi mchezo mchezo tu aka-fall in love. Akanikaribisha nyumbani kula chakula cha mchana nikaenda na mshikaji. Tukala, akatupa pesa, halafu tukaondoka. Weekend nyingine akanikaribisha pia, nikatokea na mshikaji tena. Tukala halafu tukaondoka. Baada ya muda kupita, akanikaribisha chakula cha jioni. Safari hii akasema niende mwenyewe tu. Hapo ndio nikafunguka macho. Sikwenda na mchezo ukaishia hapo. Mtu aliyetaka kunitoa kwenye mstari wa masomo wakati huo, sikumwelewa kabisa.
 
Ile Kilamanjato Boys noma sana wenyewe tuliita "Kiliboys" hapa nakumbuka:-
1. Dogo mmoja form one ilikuwa siku ya ijumaa mchana ni makande hapa kunakuwa na vurugu sana bwaloni, yule dogo kawahi kajaza sahani akala kiasi kilichobaki akafungia kwenye mzinga(sanduku la chuma) ili jioni aendelee na makande yake asipange foleni ya ugali, wahuni wakamtaim ametoa wakageuza sanduku lile chini juu na kulitikisa sana kisha wakalirudisha kama lilivyokuwa. Pata picha alivyokuja kufungua sanduku baadae, ikumbukwe sanduku hili ndio lina kila kitu kuanzia uniform na vitu vingine.

2. Uzuri wa hii shule hakuna kukacha prepo ukajificha bwenini, mabweni yalikuwa na vibwengo sana hasa hasa bweni la horombo.

3. Shule ilikuwa mbali sana na wilayani, haina fensi huwezi hata kutoroka ni pori tupu na kuna tembo porini kutokea Kenya.

SIKU HIZI NASIKIA IMEPOA IMEKUWA SHULE YA WANAWAKE.

Krokomu!
Katika shule za kanisa katoliki zilizoshindikana.
 
Aisee...ilikuwa hatari sanaa! Hilo ziwa inaelekea lilikuwa na kina kirefu sana daah...
hatari mkuu ni mazuri kusimuliwa ila huo usiku ulikua ni wa shida sana, shule ina hadi walemavu wa ngozi, wasiona, na viwete lakin hawa jamaa ffu walivyofika skonga hawakua wanaangalia sura ni kichapo tu bwenini hakubaki mtu tulikutana aubuh kila mmoja akitokea anakojua yeye.
 
Back
Top Bottom