Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Daaaaaaah ningekua mimi ningemtimua jamaa siku hiyohyo nimalize mcheZo
Yaani hapo ni kidato cha 1? Nyie wengine naona mlikuwa tofauti na mimi. Mimi wakati niko kidato cha 5, ndevu zimeanza kutoka sasa, niliwahi kupendwa na msichana aliyekuwa anafanya kazi tayari. Alikuwa anafanya kazi TANESCO wilayani. Basi mchezo mchezo tu aka-fall in love. Akanikaribisha nyumbani kula chakula cha mchana nikaenda na mshikaji. Tukala, akatupa pesa, halafu tukaondoka. Weekend nyingine akanikaribisha pia, nikatokea na mshikaji tena. Tukala halafu tukaondoka. Baada ya muda kupita, akanikaribisha chakula cha jioni. Safari hii akasema niende mwenyewe tu. Hapo ndio nikafunguka macho. Sikwenda na mchezo ukaishia hapo. Mtu aliyetaka kunitoa kwenye mstari wa masomo wakati huo, sikumwelewa kabisa.
 
Daaaaaaah ningekua mimi ningemtimua jamaa siku hiyohyo nimalize mcheZo
Nilikuwa mtu wa book, mkuu. Nilianza kupenda baada ya kumaliza university. Na book halikuniangusha kabisa. Sasa hivi hata serikali ya CCM ikiamua kutokutoa mafao kabisa, mtalia wenyewe bila mimi.
 
Yaani hapo ni kidato cha 1? Nyie wengine naona mlikuwa tofauti na mimi. Mimi wakati niko kidato cha 5, ndevu zimeanza kutoka sasa, niliwahi kupendwa na msichana aliyekuwa anafanya kazi tayari. Alikuwa anafanya kazi TANESCO wilayani. Basi mchezo mchezo tu aka-fall in love. Akanikaribisha nyumbani kula chakula cha mchana nikaenda na mshikaji. Tukala, akatupa pesa, halafu tukaondoka. Weekend nyingine akanikaribisha pia, nikatokea na mshikaji tena. Tukala halafu tukaondoka. Baada ya muda kupita, akanikaribisha chakula cha jioni. Safari hii akasema niende mwenyewe tu. Hapo ndio nikafunguka macho. Sikwenda na mchezo ukaishia hapo. Mtu aliyetaka kunitoa kwenye mstari wa masomo wakati huo, sikumwelewa kabisa.
Kwamba ukamla afu ukampotezea au??
 
Miraji akumbukwe kwakweli, afande side na babu chacha sijui wako wapi nao!!!
lile bwawa la samaki limechimbwa Na wanafunzi,wahanga wa marehemu miraji.ile ofisi yake alikuwa anapaita Kandahar,hatoki mtu salama kule.
 
Ok hiki ninachoandika ni off topic.

Kuna jamaa aliripoti shule, bishoo si mchezo. Kuna jamaa akawa anamuonea onea tu akimkuta anakula anachukua chakula, anachukua madaftari yake. Halafu anamwambia kama unaweza si upigane? Ishu ilienda kama mwezi.

Maji yakikata kuna kama kijito cha maji ndiyo hua tunayafuata, basi yule bishoo akavaa traki raba na fulana akamkuta mshkaji yupo na sisi akamwambia twende mtoni. Jamaa akajibu kwa dharau "Unataka nikakuf.ire?" mshkaji akajibu hapana nataka tukapigane, Ila tuwe wawili tu atakayerudi shule hapa ndiyo mshindi, jamaa akakubali wakaenda.

Dakika 10 nyingi tunamuona bishoo anarudi. Akatuambia kamchukueni jamaa, tumefika kule yule jamaa kila unapomgusa analia akafuatwa na gari la shule gari lenyewe wipers hazifanyi kazi na ukungu umeshakuja ikabidi mmoja akae kwenye boneti awe anafuta futa na mwendo uwe wa kobe.

Baada ya kupona akatuambia "Yaani sijaambulia hata ngumi moja, huyo jamaa hafai" kumbe yule bishoo ni mshindi wa Judo ngazi ya mkoa huko mkoani kwao. Halafu ikatokea wakawa marafiki vibaya mno.
😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Niliripoti shule siku ya jumapili, ilikuwa ni siku ya wali. Nikapokelewa mpaka bwenini na wenzangu, kwa kuwa ilikuwa ni muda wa msosi basi nkabeba messtin yangu huyo mpaka jikoni. Kufika kule nkakuta wageni wenzangu tukaambiwa leo nyie mtakula ugali na maharage wali mtaanza kula wiki ijayo.

Nikachukua chakula nilichopewa, nikaonja kidogo nikaona ladha hairidhishi pia kulikuwa na wadudu wanaogelea basi nikamwaga jalalani.
Kwa siku mbili mfululizo hali ikawa ile ile nashindwa kula na maji nannua ya chupa kwenye duka la shule. Siku ya tatu nikajisemea moyoni nitaishi kibishoo mpaka lini..?, nikafungua moyo nikaanza kuishi kikamanda na life likasonga freeeshi tu mpaka namaliza shule.
 
Kuna shule inaitwa Mwakavuta (wenyeji wanaiita Mwakauta) nikavuta siku za kuripoti kwa kua nilitaka nitoke nyumbani baada ya valentine day.

Nafika siku hiyo ni jumapili siku ya wali. Nikala kidogo nikaugawa, naenda kuosha sahani ghafla ukungu umetanda kiasi hauwezi kuona hatua mbili mbele.
Nikasimama pale pale kwa zaidi ya dakika 45 ili ukungu upite nisije nikapotea nikaingia msituni. Sehemu yenye baridi kali kama haujavaa viatu au ni vyepesi vidole vya miguuni unaanza kuhisi vinachomwa chomwa na sindano. Nahisi ni dalili za kua frostbitten.

Ukungu unamalizikia vidole vikawa vinaonyesha kama damu imevilia. Tumelala bwenini nakutana na watu kutoka Chunya, Kilimanjaro, Moshi, Kigoma, Mafinga n.k. na wote wanasema baridi la pale si mchezo.

Asubuhi naamka. Njia za shule zote zina theluji, boksa niliyoiacha jana kwenye kamba imeganda kwa barafu.

Nikaanza kupima pros na cons.
-Kwanza walimu walituambia watoto wa O Level wote wana ngoma, kumbe na wale watoto waliambiwa sisi wote tuna ngoma. Ingawa wakinga siyo wabanaji lakini hilo doa litachukua muda wangu.

-Shule haina mabinti wazuri, hao waliopo wavuna mbao na wanakijiji wote mnawagombea.

-Unaweza kua na hela lakini hakuna cha kununua.

-Umbali mpaka wilayani ni 22KM na gari ni moja likipita limepita ama utembee, nilitembea aisee nilikoma, kila sehem ya mwili iliuma. Nilienda kupiga PPS hadi PPS zinatoka ndo nagundua kuna makamasi yalikua yananitoka. Sijui mpiga picha alidhani urembo.

-Rate ya kupiga puchu ikawa juu.

-Walimu wawili wa masomo yangu walikua wanakukaririsha kitu cha kitabuni hawakichambui wala nini halafu ni unasomewa sasa akiwa anasoma unagundua na yeye kuna vitu anavijua hapo. Mmoja alienda Mbeya akakaa zaidi ya mwezi huku somo limesimama.

-Chakula kibaya sijapata kujua. Kuna wadudu hua wanaranda randa kwenye balbu ukiwaua wanatoa harufu mbaya, sasa wale unawakuta kwenye maharage wapo kibao. Wali ikawa ndiyo luxury food, ugali unaula kidogo, asubuhi unanywea uji, makande, unakula kidogo asubuhi unanywea uji.
Wali ulisababisha watu wapigane, kulikua kuna paper two sasa form six wanajihisi wao ndiyo wanatakiwa kuanza, jamaa wa form five akafosi kingi ebwana washkaji wawili akaanza kumpiga.
Ila baadaye na yeye aliwatafuta mmoja mmoja na wakamheshimu.

Nilifeli kwa mengi.
Dah mwenyekiti, kama kawaida yako!!
 
Ok hiki ninachoandika ni off topic.

Kuna jamaa aliripoti shule, bishoo si mchezo. Kuna jamaa akawa anamuonea onea tu akimkuta anakula anachukua chakula, anachukua madaftari yake. Halafu anamwambia kama unaweza si upigane? Ishu ilienda kama mwezi.

Maji yakikata kuna kama kijito cha maji ndiyo hua tunayafuata, basi yule bishoo akavaa traki raba na fulana akamkuta mshkaji yupo na sisi akamwambia twende mtoni. Jamaa akajibu kwa dharau "Unataka nikakuf.ire?" mshkaji akajibu hapana nataka tukapigane, Ila tuwe wawili tu atakayerudi shule hapa ndiyo mshindi, jamaa akakubali wakaenda.

Dakika 10 nyingi tunamuona bishoo anarudi. Akatuambia kamchukueni jamaa, tumefika kule yule jamaa kila unapomgusa analia akafuatwa na gari la shule gari lenyewe wipers hazifanyi kazi na ukungu umeshakuja ikabidi mmoja akae kwenye boneti awe anafuta futa na mwendo uwe wa kobe.

Baada ya kupona akatuambia "Yaani sijaambulia hata ngumi moja, huyo jamaa hafai" kumbe yule bishoo ni mshindi wa Judo ngazi ya mkoa huko mkoani kwao. Halafu ikatokea wakawa marafiki vibaya mno.
Ha ha ha haaaaaaa... Mwenyekiti ilifaa wewe ndio uwe mwenye huu uzi.. Omba hati miliki basi kwa mzee mama.
 
Ile nimefika tu form V pale mjini Tanga, nilifika kwa kuchelewa kama wiki 3. Nakuta watu wanasolve necta ya form VI tena maswali ya complex number wakati hata topic nilikuwa siijui inahusu nini. Nilipagawa.
 
Back
Top Bottom