Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

duuh kwa kweli unastahili pongezi mimi mbona ningetoka NDUKI tu kwani Seminar presentation ilikuwa na marks ngapi? sidhani kama zinazidi marks 10
Ahaaaaa aaaaa Joshua_ok umenikumbusha 4m 2 niliingia mitini. Ahaaaa
 
Nakumbuka miaka ya nyuma nilishawahi kwenda Interview ya Bank Teller CRDB pale Azikiwe daah sijui ndo kiingereza au uoga maana nilikuwa nikiulizwa swali najibu kwa sauti kubwa kama napiga ADHANA MSIKITINI (Swalaa Swalaa saa 11 alfajiri) mpaka yule HR akaniambia ndugu hebu RELAX hiii sio vita!! si unajua tena umemaliza shule umekaa mtaani kazi huna ghafla uaitwa interview wee nilikremu vitu balaa kufika tu mi natapika hata nisivyoulizwa
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mimi nakumbuka tulikuwa tunawasilisha seminar ya IT. Swali lilikuwa "what is folder" hapo tupi first year. Mwasilishaji alitafuta maneno yote yakagoma kuja japo alimeza usiku mzima. Gafla akajibu folder is like a kabati, where there are cups, plates and so on" alipomaliza jasho lilikuwa linamtoka balaa. Ikabid mwl. amwambie kakae. Kiingereza si mchezo.
Ume niuwa Kwa kucheka duh hatari
 
Tuliwahi kusafiri na Mstahiki Meya wa jiji Fulani hapa Tanzania (jina kapuni) kwenda kwenye mkutano wa kimataifa huko UK (London) sasa kumbe yeye sijui hakuambiwa au alifurahia per diem tu kufika kule waandaji wakawa wanamkumbusha kuwa unapaswa ku-chair one of the session katika mkutano duuh mstahiki meya akaniomba nimsaidie nikamuambia kwa wakati huo ndo nitakuwa nawasilisha pepa (mada) pengine waliamua kumteua yeye maana tunatoka nchi moja iwe rahisi kuni-introduce daah jamaa alipoona haina jinsi ilibidi asepe kiaina hakuonekana kwenye ile session duuh ikabidi nimuombee udhuru nika-act kama session chair kisha nikawasilisha mada/pepa. Sasa baadae jioni namuona kwenye msosi namuuliza mstahiki ulikuwa wapi akadai alibanwa na tumbo la kuhara
Ahaaaaa franktemu
 
Dah kila nikisoma comments za watu hapa nabaki kucheka tu. . Kingereza ni nouma asee Weka mbali na watoto
 
Ila wakulu wengi kiingereza chao kipo very low. ukiacha mzee wa mambo ya mbele (nje)
 
Siku moja tupo kwenye seminar ya koz moja inaitwa rural agricultural economy maarufu kama YELLOW BOOK kwa waliosoma SUA wataelewa, basi picha moja ilikua imebandikwa ukutani ikapulizwa upepo ikadondoka chini jamaa kule mbele akiwa na maiki alisema "what is that, ooh the picture drop down without becouse" basi tulicheka sana
Kitabu cha profesa Mlambiti..
[emoji2] [emoji2]
 
Siku ya kwanza kuongea kiingereza ilikua kwenye interview ubalozi wa uingereza wakati naomba viza ya kwenda huko. Ndio nimetoka kumaliza form 6 tu,yani bora ningefanyiwa interview na blacky mwenzangu kuliko bibi yule wa kizungu.
Mpaka kesho huwa najiuliza niliongea nini lakini sikumbuki.
 
duuh ipyax so ulipewa viza kwa huruma tu! hataree naona bibi wa kizungu akaona ngoja nimtoe tu huyu dogo asije kunifia hapa na broken yake.
 
Sitasau siku moja Chuoni..Madam mmoja Aitwae Jibrea akanichagua from no where 'go and write a word kitunguu in English...kumbukaa.Ni Degree Na Ni.Mwalimu Wa English kwa miaka 10 Na nakijuaa ...hatarii nikajikuta nnaandika Union..Na kwa mbwembwe nikachoraa...sasa nikashangaa Watu wanaguna..basi ile kujaa akachaguliwa Dada mwingine mwenye Mbwembwe kujifanya Amesomea International schools Ndo kunirekebisha Onion...Rohoo iliniumaaa sababu Najuaa ila sijuii Ni shetani Gani alinigusa... Hatujakaa sawa Madam akamwinua Dada mwingine aitwae Gift 'come in Front' akaenda kufikaa..Chuo blackboard Ni zile za kufungua Na kupandisha Na kushushaa.(hope mnazijua)basi...sasa kwa kuwa Madam alitaka yule dada Aandike kitu Na Ni mfupi ubao ulipandishwa Ukawa juu...Akamwambia 'pull the blackboard..Down!!!.. Dada kaganda..,akarudia kwa msisitizo with high pitch..Dada still aliganda. Ghafra tukiwa tunachangaa what happened to her...Akapiga Magoti...heee! Madam akarudia tena..sasa kumbe lilee neno Down Ndo alilipata Na akadhani Kuna jambo kakosea Ndo Lecturer anampa Adhabu..sasa Mara akawa anatambaa huku akimfuata Madam..wkt huo Darasa kwa kuwa walijua hajaelewa walichekaa saaana..thing which made her to cry Loudly..... just thing about that A University student...Kiinglish Ni Noumer..Dada yule Baada ya incident ile hakukaa Darasani Japo kipindi Ndo iilikuwa kina anza Aliondoka kwa Huzuni kuubwa..swali jje t ungekuwa tunatumia lugha yetu kama Wachina jje t ungekuwa Tunaumbukaa mpaka wengine wanakimbilia chuoni wkt Wa kupresent..Mara ivi..OMG!!
 
e1b0d8cdf40d3e72b7c99bfdee3852e8.jpg
1464373238118.jpg
 
Back
Top Bottom