Siku ya vijana duniani

Siku ya vijana duniani

Binti 1

Member
Joined
Dec 1, 2018
Posts
30
Reaction score
65
Mawazo ya kuwepo kwa siku ya kimataifa ya vijana yalitolewa mnamo mwaka 1991 na vijana waliokusanyika mjini Vienna nchini Austria kwa ajili ya kipindi cha kwanza cha jukwaa la dunia la vijana la mfumo wa umoja wa mataifa.

Kwa mara ya kwanza, Umoja wa Mataifa ulisherehekea mwaka wa kimataifa wa vijana mnamo mwaka 1985 ambapo mwaka 1999, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha tarehe 12/Agosti kuwa siku ya kimataifa ya vijana ambayo ilisherehekewa kwa marea ya kwanza mwaka 2000.

Siku ya vijana duniani husherehekewa ikiwa na lengo la kutambua na kusherehekea juhudi za vijana katika masuala mbalimbali kama wadau wa jamii ya kimataifa. Siku hii pia hutumika kuwahamasisha vijana kushiriki katika masuala mbalimbali ili kuleta mabadiliko chanya katika jamii zao.

Kama hilo halitoshi, siku hiyo pia hutumika kwa ajili ya kutoa uelewa kwa jamii na kupaza sauti kuhusiana na changamoto mbalimbali zinazoiwagusa vijana ikiwemo ajira, afya, elimu na ushiriki wa vijana katika ngazi mbalimbali za uongozi.

Kila mwaka huwa kuna kauli mbiu tofauti tofauti kwa ajili ya kusherehekea siku hii ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni "Mshikamano wa vizazi: Kuunda Ulimwengu kwa Vizazi zote" ikiwa na lengo la kuhamasisha na kuimarisha ushiriki wa vizazi vyote katika kufikia malengo endelevu yaliyowekwa yaliyowekwa na umoja wa mataifa mwaka 2015.
 
Ji
Kwani kijana anaanza miaka mingapi na mwisho ni ngapi?
Jibu ni kazi kutoa,maana unakuta mtu kama ni age ya kina Zzk,January Makamba,Ridhiwani Kikwete,Nnape,Mchengerwa n.k wanaitwa vijana,ukigugo,unaambiwa 18-35,inachanganya kwakweli.
 
Kijana ni namna unavyojiona wewe kwa mfano mimi hapa nina miaka 78 ila bado najiona kijana nguvu nazo,muonekano safi akija mama namnyandua vizuri.
 
Ji

Jibu ni kazi kutoa,maana unakuta mtu kama ni age ya kina Zzk,January Makamba,Ridhiwani Kikwete,Nnape,Mchengerwa n.k wanaitwa vijana,ukigugo,unaambiwa 18-35,inachanganya kwakweli.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Watu hawataki uzee...
 
Kwenye hii siku hata vijana wa hovyo tunaruhusiwa ama ni kijana yupi kalengwa.
 
Niliudhuria leo youth Forum pale M city kulikuwa na mada na wachangia mada mbali mbali ambao walizungumzia issues za kuwa shirikisha vijana ktk programs mbali mbali za vijana zinazo gusa maisha yao
 
Ngoja tuone... Inasemekana siku hizi kuna vijana wa hovyo...
 
Back
Top Bottom