Siku ya viwango na ubora barani Afrika

Siku ya viwango na ubora barani Afrika

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
SIKU YA VIWANGO NA UBORA BARANI AFRICA

Dar es Salaam - Tanzania
Tarehe 29/03/2024

Shirika la Viwango Tanzania TBS limeadhimisha Siku ya Viwango na Ubora Barani Africa kwa Nchini Tanzania Katika Makao Makuu ya shiriki hilo JIJI DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa TBS nchi Bwana Athumani Yusufu Ameeleza Dhamira ya TBS ni kuendelea kumuwezesha Mlaji Kupata Haki yake ya Msingi ya Kupata Bidhaa bora zenye viwango

Mgeni RASMI katika Maadhimisho hayo Mh Hassan Bomboko Mkuu wa wilaya ya Ubungo Ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam aliwaeleza washiriki wa kongamano hilo kwamba Katika Kipindi cha Miaka Mitatu ya Dr Samia Suluhu Hassan Shirika la TBS limeimarika zaidi kwa Kufanya Kazi Kubwa katika Kuhakikisha Mlaji anapata Bidhaa zenye kuzingatia Viwango na Ubora, lkn Pia Mh Rais Dr Samia Suluhu Hassan amewezesha wafanya biashara wadogo na wakati Kuingiza Bidhaa zao katika Soko shindani zikiwa zimepewa Utambulisho wa TBS kwa kupimwa ubora na Viwango kwa Gharama za Serikali

Aidha DC Bomboko amewataka TBS kuendelea kuwekeza Katika Tekinolojia ili utendaji kazi wao uendane na kasi kubwa ya Mabadiliko katika Tekinolojia ili kuweza kushindanisha Bidhaa za ndani katika Masoko ya Kimataifa
IMG-20240330-WA0067(2).jpg
IMG-20240330-WA0066(2).jpg
IMG-20240330-WA0069(2).jpg

Kazi Iendelee
 
Habari kama hiyo wangejaa ila CAG amewatibulia.
Nchi hii jamani
 
Back
Top Bottom