Mkuu Mwifwa, kwa vile hatujuani, usishadadie kuita watu njaa, ukidhani ndio wana njaa kihivyo hadi kudhani napiga vigelegele ili nineemeke kama Bashite, no way, ikitokea tukafahamiana, nadhani tutaheshimiana humu jf, msidhani kwa kila mtu uteuzi ndio big deal sana kivile!.
Kwa taarifa yako tuu, tafuta mtu wa NHC, malipo, ulizia mtu anayeitwa Pascal Andrew Mayalla ni mpangaji wa jingo la NHC ambayo ndio ofisi yangu ya PPR, jingo hilo liko mjini kati, find out nalipa kodi ya pango kiasi gani kila mwezi, ukiishajua hicho kiwango, fanya utafiti mshagara na marupurupu yote ya DC kwa mwezi ni kiasi gani, halafu uambiwe huyu mtu anautafuta u DC, for what my God?!.
Tafuta mtu wa TRA upande wa VAT, fanya search ya Tin No. ya Pascal Andrew Mayalla, find out analipa kodi kiasi gani kila mwenzi, halafu linganisha na mshahara wa DC!.
Pata mtu wa kitengo cha madinga pale TRA search Pascal Andrew Mayalla anamiliki ndinga ngapi, then zifanyie estimates kwa mshahara wa DC itamchukua mishahara ya miezi mingapi?.
Tembelea portal ya PPRA, search kampuni ya PPR imekamata tenda ngapi za kiasi gani, kabla ya ujio wa Magufuli, kisha linganisha na mshahara wa DC, upige hesabu DC atafanya kazi miaka mimgapi kufikia kiasi hicho!.
Tuheshimiane wandungu, tusidhalilishane kwa kudhani kila mtu anasaka uteuzi na hapo bado sijakueleza ninaishi wapi na maisha gani.
Paskali