Siku yako ya kwanza ku drive highways ilikuwaje?

luangalila

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2014
Posts
6,346
Reaction score
6,928
Wadau uzi wa ku share experience yako kwa mara ya kwanza ku drive high ilikuwaje.

Kwangu binafsi ilikuwa shida sana katika ku overtake yaani nilikuwa naogopa sana ila nilikuwa nikukuta road iko open nilikuwa speed sanaa 80Km/h nakumbuka nilikuwa na drive Mazda.
 
Nilikua natoka Dar kwenda Mtwara, nikiwa na toyota voltz-mannual gia (na kila siku nawaambia naiuza hamtakiπŸ˜’
πŸ˜’) nilienjoi sana nilivokua naomba njia kwa kutumia indiketa halafu naruhusiwa, mwingine ananiambia subir then ananiruhusu asee nilikua napata furaha sana, mwingne ananiwashia taa kuniambia punguza mwendo trafiki mbele, na mwingne ananiuliza namjibu hahaha aiseee nilikua najiona ndio baaasi tena maisha nimeshayamaliza hapo sihitaji kingine.... ilikua Novemba 2014!
 
Hiyo barabara nimepita juzi kurudi DAR aisee sasahivi haifai maana ina mabonde ya kufa mtu tena kama mtu mgeni na hiyo njia ni hatari Sana hasa waendeshaji Magari madogo..
 
Hiyo barabara nimepita juzi kurudi DAR aisee sasahivi haifai maana ina mabonde ya kufa mtu tena kama mtu mgeni na hiyo njia ni hatari Sana hasa waendeshaji Magari madogo..
Yah uko sahihi mkuu, ukishavuka daraja la mkapa pale vinaanza viraka viraka ambavyo vinaondoa kabisa ladha ya Safari...Dereva mgeni awe makini
 
Business as usual...

Muhimu umakini na kama huijui barabara tembea mwendo wa kawaida at least 80kph iwe max limit...
 
Speed limit ni 100 km/hr yaani 70 ilikuwa ngumu kuifikia halafu wasiwasi ile mbaya usukani nimeukumbatia πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ baada ya kuwa mjuzi sasa kuna siku nilikuwa nateleza 160 km/hr uzuri ni kwamba madreva wanashirikiana ili kuvunja sheria sikustuka mpaka mmoja wa passengers kuniuliza BAK unataka kupaa!? πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…