Sikutegemea kama ingetokea siku na mimi nijihisi nimeambukizwa UKIMWI...

Sikutegemea kama ingetokea siku na mimi nijihisi nimeambukizwa UKIMWI...

Kamanda HAKUNA wewe ni noma..........khaaa!.............hivi muda wa kuandika haya matakataka umeutoa wapi kiongozi wangu.....................?Unatisha kuliko kirusi alichonusurika queenkami............kudadadekii wallah......kwani mtoto wa watu kakunyima nini...................mbona una hasira naye namna hii.....................au umemtongoza PM akakuchomolea nini maana hizi hasira si za kawaida......................
Heshima kwako mrembo queenkami........................maana ingekua mimi ndo namchokonoa mtu namna hii halafu asinijibu sijui ningejiona mjinga kiasi gani.....................queenkami kakudharau sana kwa kitendo chake cha kutokujibu micomenti yako.................umedharauliwa kwa kiwango cha hatari..................!

Haijalishi.............!!!???, hili ni jukwaa huru na kila mmoja anaweza kueleza jambo kutokana na alivyolichukulia, hii mada imewakilishwa kwa kuleta UNYANYAPAA kwa wanaoishi na virus vya UKIMWI, unajuaje kama na mimi ni mmojawapo; kwa kuwa wewe uko salama ndio uanzishe mada ya kujigamba na kunoyesha kwamba wengine wana nia ya kukuambukiza virus kwa makusudi. Kwa kweli sijawahi kuumizwa kwa kiwango hiki, hata hivyo najitahidi kuji-control hisia zangu.
 
UMENUSURIKA............???, usitukane mamba kabla hujavuka mto.

Wewe unataka kuwaaminisha watu hapa kwamba upo salama, ili mtu aje kukubandua bila kondomu. Lete vyeti basi............!!!???

Kwanza ulipima wapi..........???, hakuna hospital BONGO, kapime INDIA na utuletee vyeti.

Ninyi vinuka mkojo wa siku hizi, ukishaona unawanyanyasa wanaume kadhaa kwa kuwapanga foleni; mnakuwa na matusi ya rejareja sana. Juzi kuna mwenzio katukana wanaume wote wa TZ kwamba ni wachafu, wewe unawafanya waliojikuta wana virusi vya UKIMWI kwamba walitegemea kupatwa na hiyo hali, kutokana na kauli yako hii; "Sikutegemea kama ingetokea siku na mimi nijihisi nimeambukizwa UKIMWI" Kwa hiyo unafikiri waliojikuta na virusi vya UKIMWI walitegemea..........????

nahisi kuna chizi kaiba laptop ya dokta huko mirembe...........................ndo maana mrembo wa watu kakushtukia akaamua kukupotezea....................lazima utakuwa unaumwa akili......................ukitongoza demu akikataa sio kuleta hasira za kijijini....................jipange upya na mistari iliyokwenda shule....................
 
Nakubaliana na maneno yako, unachokiwaza ndio kinachokutokea hata kama ni kwa opposite side
 
Haijalishi.............!!!???, hili ni jukwaa huru na kila mmoja anaweza kueleza jambo kutokana na alivyolichukulia, hii mada imewakilishwa kwa kuleta UNYANYAPAA kwa wanaoishi na virus vya UKIMWI, unajuaje kama na mimi ni mmojawapo; kwa kuwa wewe uko salama ndio uanzishe mada ya kujigamba na kunoyesha kwamba wengine wana nia ya kukuambukiza virus kwa makusudi. Kwa kweli sijawahi kuumizwa kwa kiwango hiki, hata hivyo najitahidi kuji-control hisia zangu.

Mi nahisi umeumizwa labda ulimtongoza huyu dada akakukataa.................kama hapo ndio umecontol hisia zako sijui ukiwa hujazicontrol inakuwaje.....................huo unyanyapaa katika watu wote waliochangia wasiuone uuone wewe tu kiongozi.............taratibu swahiba.....................unajiabisha.......................
 
Mi nahisi umeumizwa labda ulimtongoza huyu dada akakukataa.................kama hapo ndio umecontol hisia zako sijui ukiwa hujazicontrol inakuwaje.....................huo unyanyapaa katika watu wote waliochangia wasiuone uuone wewe tu kiongozi.............taratibu swahiba.....................unajiabisha.......................

Labda wewe ndio wale ambao mpo kwenye mtandao kwa kusudi la kutafuta wanawake, kwa hiyo katika hali yoyote ile wewe utakuwa tayari. Hapa JF kumekuwa na tabia ya watu kutokubali mawazo ya tofauti, kwanini unilazimishe kuelewa mada kama wewe ulivyoelewa, kama uliona hakuna UNYANYAPA ulipaswa kujibu kwa hoja na sio kuanza kusema eti namtongoza, hivi kumbe kuna wanaume bado wanatongoza wanawake, maana kwa hali ilivyo sasa, wanawake ndio wanatongoza wanaume.
 
Labda wewe ndio wale ambao mpo kwenye mtandao kwa kusudi la kutafuta wanawake, kwa hiyo katika hali yoyote ile wewe utakuwa tayari. Hapa JF kumekuwa na tabia ya watu kutokubali mawazo ya tofauti, kwanini unilazimishe kuelewa mada kama wewe ulivyoelewa, kama uliona hakuna UNYANYAPA ulipaswa kujibu kwa hoja na sio kuanza kusema eti namtongoza, hivi kumbe kuna wanaume bado wanatongoza wanawake, maana kwa hali ilivyo sasa, wanawake ndio wanatongoza wanaume.

kamanda unajua maana ya kujibu hoja wewe?.......................hebu rudia kusoma matakataka yako uliyomuandikia binti wa watu halafu uone wewe na yeye nani mnyanyapaaji......................kuwa na mawazo tofauti inakubalika..............lakini kumwita mtoto wa watu kahaba,malaya aliyejificha kwenye ukristu..........kinuka mkojo.............na kumwambia ameathirika yuko hapa kutafuta wakumwambukizwa inakufanya wewe ndio mnyama na mnyanyapaaji namba moja...................Kama kutumia lugha hiyo ndio kujibu hoja basi wewe utakuwa chizi........................wape hi washikaji zako hapo mirembe.......................!
 
bibie upo.....................?......... sweetlady.Pole queenkami...............hili dude linatisha asikwambie mtu.............unaweza kufa kwa presha.............!Ila hongera kwa kupima................na kukuta uko fresh..............Sasa kuwa makini zaidi ukicheza kizembe zembe tu hadithi inabadilika...................................!
Nipo father-xmas tena bukheri wa afya.......ukinijuza uzima wako ntafurahi zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Hello Wapendwa.

Kuna mahala fulani huwa ninasafiri kwenda mara kwa mara kufuatilia mambo ya kibiashara.Huko mahala ninaposafiri huwa kuna mama yangu mkubwa anaishi huko lakini siku zote huwa nashukia hotelini.Kila nikifika huwa nampigia simu mama mkubwa na pia najitahidi kwenda nyumbani kwake kumsalimia lakini mama mkubwa analalamika kuwa ni vizuri siku nikiwa huko japo siku moja moja nilale nyumbani kwake.

Mama yangu mkubwa nimuathirika wa UKIMWI,sio kwa kumuhisi bali kwa kinywa chake alimweleza mama yangu,pia hataki kutumia hizi dawa za kurefusha maisha hivyo amekonda sana na ana mapele na vidonda na majipu vinamtokea kila mara.

Siku moja nikiwa huko nikaamua kwenda kulala nyumbani kwa mama mkubwa wangu japo ana chumba kimoja,nilipofika nikakuta kidole chake kimoja cha mkononi kimeoza kwa kidonda chenye usaha,mwenyewe akanambia eti kuna mdudu akiingia kwenye kucha kidole ndo kinakua hivyo.

Tulikula kisha tukapiga story hadi usiku mwingi kisha sababu alikua ana magodoro mawili nikamwomba anitandikie godoro mim nilale chini.

Wakati anatandika shuka kwenye hilo godoro kwa bahati mbaya kile kidole chake chenye kidonda kikanichoma mguuni hadi pakakatika hadi damu ikanitoka halafu ule usaha wake ukabakia juu ya hapo aliponikata na kucha yake.Niliogopa sana,cha ajabu yeye hata hakuonesha mshituko,ila mimi niliogopa hadi sikuweza hata kupata usingizi.Kesho yangu nikarudi hotelini kwangu nikiwa na mawazo ya kuwa labda virusi vimenipata.Nilimaliza shughuli zangu huko nikasafiri kurudi nilipotoka lakini wiki mbili tokea aliponikata na kucha nilikuwa na mawazo sana lakini baadae nikasahau.

Kwa kawaida mimi ni mtu mwenye kinga imara,ni kwa miaka mingi sijawahi kuumwa kitu chochote zaidi ya mafua,tena hata mafua yenyewe sio mara kwa mara.Kama baada ya mwezi na nusu hivi tokea nilipokatwa na kucha nikapata mafua makali yaliyoambatana na homa kali na maumivu ya kichwa,nikaanza tena kukumbuka lile tukio,nikaanza kuhisi labda nimeshaathirika,wakati mwingine najipa moyo kuwa ni mafua ya kawaida maana hata kama kuathirika inaweza kuchukua hata miaka mingi bila kuona dalili.

Miezi michache baadae nikasafiri kwenda Ulaya,wiki moja tu tokea nifike nikaanza kupiga chafya mfululizo halafu pua ilikua inawasha ajabu hadi ikawa nyekundu na jicho moja likawa linatoa machozi hasa nikiwa nje natembea,mawazo tena ya kukatwa na kucha yakarudi kwa kasi,safari hii nikawa sina uhakika kabisa kuwa mimi ni muathirika au la maana tokea nizaliwe sijawahi kupatwa na hali kama hii,baada ya kupiga chafya kila dakika kwa wiki nzima mfululizo nikaamua kwenda hospitali,nikaambiwa nina allergy ya polen,daktari akasema kwa vile kilikua kipindi cha summer hewa imechafuka kwa polen inayotokana na maua yaliyopo kila mahala,ila nikashangaa maana home kwangu nina maua ya kila aina na sijawahi kupata hiyo hali,rohoni nikazidi kuogopa kuwa huenda nimeathirika kwa kukatwa na kucha.

Siku nyingine tena ghafla nikaanza kuwashwa na kuvimba mwili,yaani bila kujua sababu nilikuwa nawashwa kuanzia utosini hadi kwenye unyayo halafu nikiamka ngozi imevimba na kuwa nyekundu,kwenda hospitali nikambiwa eti kuna matunda nilikula ambayo nina allergy nayo,kweli kuna vitunda fulani nilikula,lakini nilizidi kuogopa kuwa haya mauza uza labda yanatokana na kukatwa na lile kucha.

Siku nyingine tena nikala viazi na samaki halafu usiku nikaamka tumbo likawa linaniuma sana kisha nikaanza kuendesha,kila dakila nikawa naenda chooni kwa siku mbili kisha likapoa.

Nikaona kukata mzizi wa fitina acha nikapime,kabla ya kukatwa na kucha nilikua nina uhakika kuwa sina ukimwi,niliamini kama mtu hujawahi kusex,wala kuongezewa damu,sindano nilichomwa nikiwa mtoto,wala sishirikiani na mtu vitu vya kukata hivyo chance ya kuwa na UKIMWI ni ndogo.

Kabla ya kwenda kupima nilisali nikamuomba Mungu kuwa kama kuna kirusi chochote kilichojipenyeza mwilini mwangu siku ile nilipokatwa na kucha la muathirika kife kwa jina lake lenye nguvu kupita majina yote.
Majibu yangu yakaja kuwa mim sio muathirika.

Nilichojifunza ni kuwa ukiruhusu ubongo wako uamini unaumwa kweli utakuletea vimagonjwa vya ajabu ajabu kusuport imani yako maana kipindi nilichokua naogopa nilipatwa hadi na vichomi ila nilipoambiwa sina UKIMWI hata sikujua vilipotelea wapi.

Pole sana na hongera kwa kutokuwa muathirika...siku nyingine ukipatwa na tumbo la kuendesha chemsha maji ya chumvi (chumvi kiasi) halafu kunywa glass moja kama unaendelea basi baada ya masaa sita unaweza kunywa glass nyingine ya maji ya chumvi....mara nyingi glass mbili zinatosha kabisa lakini unaweza kunywa ya tatu baada ya masaa mengine sita hapo utaona nafuu kubwa sana.

 
nadhani hali ya kujihisi ni ya kawaida haswa kama umepoteza mechi za mchangani siku za karibuni.....ila baada ya huo upepo kupita (kama wasemavyo viongozi wa chama kijani) unasahau na kendelea na hamsini zako.

Observation: mshauri mama mkubwa atumie dawa za kuongeza maisha na kula lishe bora aipukane na vidonda. Pia nasikia kuna truvada siku hizi, sijui kama imeanza kazi....

Pili: kitendo cha kwenda kulala nane chaonyesha kabisa hapo hamna unyanyapaa kama baadhi ya wachangizi walivyodai.

Tatu: hongera kwa kigori....mswati anawatafuta sana, ukipata safari ya huko unaweza mtembelea 🙂!
 
Shigongo fanya story writer search utapata wengi sana..............

Sitaki kuamini kuwa ukucha umekukata tena wenye kidonda mpaka damu itoke???

Story zingine bana mmmmmhhhhhhhhhhhhhh kama naona nakosa connection vileee???
 
Jinsi ulivyowasilisha ujumbe wako ni dhahiri kwamba wewe unajiona ni bora kuliko wale walioadhirika, mbona JF siku hizi sio MA-GREAT THINKER, mtu anawasilisha upumbavu kama huu na wengine wakawa wana-support. Naomba utambue wewe unayejiita queenkami wanadamu kabla hajafa hajaumbika na uelewe kwamba kuna magonjwa yanayowatesa wanadamu zaidi ya hiyo hali ya UKIMWI ambayo wewe ndio unaona kwamba ni tishio na wakati kuna watu wanaishi miaka na miaka na maisha yanaenda, wewe uliumwa mafua tu na ukaanza kufa kihoro. Kamuulize SAJUKI, atakueleza kwamba kuna magonjwa yanatesa wanadamu zaidi ya hivyo ujuavyo. Nakusikitikia kwamba una hatari ya kupoteza maisha mapema zaidi kwani utakufa kwa ugonjwa wa KIHORO, yaani kitu kidogo tu kitakusumbua na hofu iliyotawala maisha yako ndio itakayokumaliza. Unahitaji kubadili mtazamo........!!!!???? else...............?????

Aisee we ni israel mtoa roho? mbona dada katoa yaliyo moyoni mwake na imekua fundisho lake.usipende kuangalia kila kitu negatively utakuwa na upungufu wa maji mwilini
 
bibie upo.....................?......... sweetlady.

Pole queenkami...............hili dude linatisha asikwambie mtu.............unaweza kufa kwa presha.............!
Ila hongera kwa kupima................na kukuta uko fresh..............Sasa kuwa makini zaidi ukicheza kizembe zembe tu hadithi inabadilika...................................!

Thanx father xmas.
Ni kweli ukitaka kujua jinsi hii kitu inavyotisha ni pale utakapokua unajihisi unao.
Habari ya kwako lakini?
 
Pole sana queenkami, umenikumbusha rafiki yangu mmoja aliwahi kupatwa na mkasa unaokaribia kufanana na wako na kiukweli aliponea tundu la sindano, wakati mwingine watu huwa wanaugua kwa makosa...ni bora wewe ulipata hata huo ujasiri wa kwenda kupima mwingine angeamua kubaki kama alivyo kwa kuhofia majibu atakayokutana nayo.....
sweetlady asante dear.
chukualia mfano unaambukizwa kwa style kama hii yangu halafu unajifanya mcha Mungu hivi ukiwaambia watu kuwa sijaupatia kwenye zinaa watakuelewa kweli?au si ndio utaonekana chui kwenye ngozi ya kondoo..
Mimi mpaka naamua kwenda kupima mawazo yangu kwa asilimia kubwa yalishawishika kuwa ninao hivyo nikaona bora nikapime ili kama ni dozi nianze mapema kabla sijaanza kutokwa na mapele na kukonda hadi watu wakaanza kunishangaa.
Mpendwa wangu ukiwa katika hali hii ya kujihisi unao ni mateso yaani tumuombeni Mungu atuepushe.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana na hongera kwa kutokuwa muathirika...siku nyingine ukipatwa na tumbo la kuendesha chemsha maji ya chumvi (chumvi kiasi) halafu kunywa glass moja kama unaendelea basi baada ya masaa sita unaweza kunywa glass nyingine ya maji ya chumvi....mara nyingi glass mbili zinatosha kabisa lakini unaweza kunywa ya tatu baada ya masaa mengine sita hapo utaona nafuu kubwa sana.


Asante BAK
Nitaizingatia hiyo tiba siku nikipatwa tena na hilo tatizo asante sana.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
nadhani hali ya kujihisi ni ya kawaida haswa kama umepoteza mechi za mchangani siku za karibuni.....ila baada ya huo upepo kupita (kama wasemavyo viongozi wa chama kijani) unasahau na kendelea na hamsini zako.

Observation: mshauri mama mkubwa atumie dawa za kuongeza maisha na kula lishe bora aipukane na vidonda. Pia nasikia kuna truvada siku hizi, sijui kama imeanza kazi....

Pili: kitendo cha kwenda kulala nane chaonyesha kabisa hapo hamna unyanyapaa kama baadhi ya wachangizi walivyodai.

Tatu: hongera kwa kigori....mswati anawatafuta sana, ukipata safari ya huko unaweza mtembelea 🙂!


Asante Mkuu wehoodie.
Nitamwambia maza amshauri ndugu yake na kumpa elimu juu ya umuhimu wa hilo maana kwa kweli anahitaji hizi dawa ila kusema ukweli kwa vile mimi hajaniambia yeye mwenyewe naogopa kuanza kumwambia hayo mambo ila kwa mama ni sawa sababu mama mkubwa wangu alimwambia mama hilo tatizo lake.
Kuhusu kumnyanyapaa sio kweli na wala siwezi kufanya hivyo sababu hata mimi nikiwa katika hali hiyo sitafurahia watu waninyanyapae.
 
Last edited by a moderator:
Shigongo fanya story writer search utapata wengi sana..............

Sitaki kuamini kuwa ukucha umekukata tena wenye kidonda mpaka damu itoke???

Story zingine bana mmmmmhhhhhhhhhhhhhh kama naona nakosa connection vileee???

Mpendwa Dena Amsi hata mimi sio kila kitu kinachosemwa huwa ninakiamini hivyo sikushangai jinsi ambavyo hujaniamini.
Haya yamenitokea mimi,kwangu mimi huu ni ukweli na sioni sababu ya kujikakamua ili kukufanya uniamini.
 
Last edited by a moderator:
kamanda unajua maana ya kujibu hoja wewe?.......................hebu rudia kusoma matakataka yako uliyomuandikia binti wa watu halafu uone wewe na yeye nani mnyanyapaaji......................kuwa na mawazo tofauti inakubalika..............lakini kumwita mtoto wa watu kahaba,malaya aliyejificha kwenye ukristu..........kinuka mkojo.............na kumwambia ameathirika yuko hapa kutafuta wakumwambukizwa inakufanya wewe ndio mnyama na mnyanyapaaji namba moja...................Kama kutumia lugha hiyo ndio kujibu hoja basi wewe utakuwa chizi........................wape hi washikaji zako hapo mirembe.......................!

Aisee we ni israel mtoa roho? mbona dada katoa yaliyo moyoni mwake na imekua fundisho lake.usipende kuangalia kila kitu negatively utakuwa na upungufu wa maji mwilini

Wakuu father-xmas na mkuu The secretary msameheni mkuu HAKUNA bure,honestly mi nimeishia kumuonea huruma tu.

Anyway,wakuu mimi nilichojifunza ni kwamba,hapa JF kuna watu hutawaona kamwe wakichangia posts zako,huwa wana watu wao ambao wakiweka thread hata iwe ya aina gani watacoment positevely.
Sawa siku watu hawa ukiwaona kwenye thread yako hata iwe ya aina gani lazima watachangia negatively.
So kwa vile mimi nishajua hilo huwa watu wa aina hii hawanisumbui maana tayari nishajijengea akilini kuwa chochote nitakachosema aidha watasema ni uongo au watatafuta jinsi ya kukosoa.
Yaani ni kama vile wao tu ndio wenye haki ya kuweka nyuzi zinazofaa kusupotiwa ila watu kama kina queenkami tukiweka uzi ni aidha hawatachangia au watachangia coments zenye lengo la kukufanya uonekane mpuuzi ili wao tu ndio wabaki wakionekana wa maana.
Kwa hiyo wakuu nawaomba mrelax hawa ni wenzetu na siku zote watakuwepo na siku zote watapinga thread za kina queenkami.
 
Hello Wapendwa.

Kuna mahala fulani huwa ninasafiri kwenda mara kwa mara kufuatilia mambo ya kibiashara.Huko mahala ninaposafiri huwa kuna mama yangu mkubwa anaishi huko lakini siku zote huwa nashukia hotelini.Kila nikifika huwa nampigia simu mama mkubwa na pia najitahidi kwenda nyumbani kwake kumsalimia lakini mama mkubwa analalamika kuwa ni vizuri siku nikiwa huko japo siku moja moja nilale nyumbani kwake.

Mama yangu mkubwa nimuathirika wa UKIMWI,sio kwa kumuhisi bali kwa kinywa chake alimweleza mama yangu,pia hataki kutumia hizi dawa za kurefusha maisha hivyo amekonda sana na ana mapele na vidonda na majipu vinamtokea kila mara.

Siku moja nikiwa huko nikaamua kwenda kulala nyumbani kwa mama mkubwa wangu japo ana chumba kimoja,nilipofika nikakuta kidole chake kimoja cha mkononi kimeoza kwa kidonda chenye usaha,mwenyewe akanambia eti kuna mdudu akiingia kwenye kucha kidole ndo kinakua hivyo.

Tulikula kisha tukapiga story hadi usiku mwingi kisha sababu alikua ana magodoro mawili nikamwomba anitandikie godoro mim nilale chini.

Wakati anatandika shuka kwenye hilo godoro kwa bahati mbaya kile kidole chake chenye kidonda kikanichoma mguuni hadi pakakatika hadi damu ikanitoka halafu ule usaha wake ukabakia juu ya hapo aliponikata na kucha yake.Niliogopa sana,cha ajabu yeye hata hakuonesha mshituko,ila mimi niliogopa hadi sikuweza hata kupata usingizi.Kesho yangu nikarudi hotelini kwangu nikiwa na mawazo ya kuwa labda virusi vimenipata.Nilimaliza shughuli zangu huko nikasafiri kurudi nilipotoka lakini wiki mbili tokea aliponikata na kucha nilikuwa na mawazo sana lakini baadae nikasahau.

Kwa kawaida mimi ni mtu mwenye kinga imara,ni kwa miaka mingi sijawahi kuumwa kitu chochote zaidi ya mafua,tena hata mafua yenyewe sio mara kwa mara.Kama baada ya mwezi na nusu hivi tokea nilipokatwa na kucha nikapata mafua makali yaliyoambatana na homa kali na maumivu ya kichwa,nikaanza tena kukumbuka lile tukio,nikaanza kuhisi labda nimeshaathirika,wakati mwingine najipa moyo kuwa ni mafua ya kawaida maana hata kama kuathirika inaweza kuchukua hata miaka mingi bila kuona dalili.

Miezi michache baadae nikasafiri kwenda Ulaya,wiki moja tu tokea nifike nikaanza kupiga chafya mfululizo halafu pua ilikua inawasha ajabu hadi ikawa nyekundu na jicho moja likawa linatoa machozi hasa nikiwa nje natembea,mawazo tena ya kukatwa na kucha yakarudi kwa kasi,safari hii nikawa sina uhakika kabisa kuwa mimi ni muathirika au la maana tokea nizaliwe sijawahi kupatwa na hali kama hii,baada ya kupiga chafya kila dakika kwa wiki nzima mfululizo nikaamua kwenda hospitali,nikaambiwa nina allergy ya polen,daktari akasema kwa vile kilikua kipindi cha summer hewa imechafuka kwa polen inayotokana na maua yaliyopo kila mahala,ila nikashangaa maana home kwangu nina maua ya kila aina na sijawahi kupata hiyo hali,rohoni nikazidi kuogopa kuwa huenda nimeathirika kwa kukatwa na kucha.

Siku nyingine tena ghafla nikaanza kuwashwa na kuvimba mwili,yaani bila kujua sababu nilikuwa nawashwa kuanzia utosini hadi kwenye unyayo halafu nikiamka ngozi imevimba na kuwa nyekundu,kwenda hospitali nikambiwa eti kuna matunda nilikula ambayo nina allergy nayo,kweli kuna vitunda fulani nilikula,lakini nilizidi kuogopa kuwa haya mauza uza labda yanatokana na kukatwa na lile kucha.

Siku nyingine tena nikala viazi na samaki halafu usiku nikaamka tumbo likawa linaniuma sana kisha nikaanza kuendesha,kila dakila nikawa naenda chooni kwa siku mbili kisha likapoa.

Nikaona kukata mzizi wa fitina acha nikapime,kabla ya kukatwa na kucha nilikua nina uhakika kuwa sina ukimwi,niliamini kama mtu hujawahi kusex,wala kuongezewa damu,sindano nilichomwa nikiwa mtoto,wala sishirikiani na mtu vitu vya kukata hivyo chance ya kuwa na UKIMWI ni ndogo.

Kabla ya kwenda kupima nilisali nikamuomba Mungu kuwa kama kuna kirusi chochote kilichojipenyeza mwilini mwangu siku ile nilipokatwa na kucha la muathirika kife kwa jina lake lenye nguvu kupita majina yote.
Majibu yangu yakaja kuwa mim sio muathirika.

Nilichojifunza ni kuwa ukiruhusu ubongo wako uamini unaumwa kweli utakuletea vimagonjwa vya ajabu ajabu kusuport imani yako maana kipindi nilichokua naogopa nilipatwa hadi na vichomi ila nilipoambiwa sina UKIMWI hata sikujua vilipotelea wapi.

Bado ulikosea sana, unaishi wka sandakalawe.......na wasomi wengi sana wana matatizo HAWAJUI ukimwi, ila wanadhania wanaujua!!

ulichotakiwa kufanya

1. Nenda hospitali haraka within 72 hours upate kinga, hii ina itwa PEP-post exposure prophylaxis ! hakuna cha kusali wala cha nini

Vijidudu vya HIV huchukua masaa 72 kuingia kwenye cell ambako vitaishi siku zote, ukiweza kuvizuia visifike huko basi wewe mzima PEP inafanyanya hivyo

Kwa watoto wa mjini Septrin inatumika kama PEP!!! ha ha ha
 
Nashauri mkapime tena ukizingatia kwamba kuna vipimo vya VVU havikufikia viwango vya TBS ndio maana hata matokeo ya Samunge yalikuwa tata (msitishike lakini)!
 
Back
Top Bottom