Sikutegemea kama ingetokea siku na mimi nijihisi nimeambukizwa UKIMWI...

Sikutegemea kama ingetokea siku na mimi nijihisi nimeambukizwa UKIMWI...

Aaagh.....!
Yaani we Qk ni msanii, title ya thread ilinifanya niogope kuisoma toka nlipoiona mara ya kwanza!
Leo nipo eneo hapa nimeona ngoja nijitose kuisoma, basi nimeisoma roho ipo juu juu tu hadi kufika mwisho ndo nimepumua lol,
so kumbe mtoto hujaathirika!
Haya furaha iwe nawe, ila duu umepitia wakati mgumu sana kiakili,
kwa kweli i can imagine what u ve been thru!

Pole kwa hofu jouneGwalo.

Sasa wewe kichwa cha habari tu kinakutia hofu pata picha mimi ilikuaje wakati sina uhakika kuwa ni neg au positive.
Ni wakati mgumu asikwambie mtu,sasa naelewa umuhimu wa watoa ushauri nasaha maana kama hauko jasiri huwezi kwenda kupima kitu ambacho kinazidi mateso ya kisaikolojia.
UKIMWI umechukua taji la kutisha japo kuna magonjwa mengine yanatisha zaidi kama cancer na mengineyo ila ukimwi ni habari nyingine jamani.Mungu atuondolee hili janga jamani linatisha.
 
Last edited by a moderator:
Mpaka mwili umeni sisimka! Pole sana QK..
Be careful na huyo aunt yako. Watu wengine hawachelewi kukuchana na viwembe kusudi akuhamishie gonjwa.. Dunia hii jamani!
 
Hello Wapendwa.

Kuna mahala fulani huwa ninasafiri kwenda mara kwa mara kufuatilia mambo ya kibiashara.Huko mahala ninaposafiri huwa kuna mama yangu mkubwa anaishi huko lakini siku zote huwa nashukia hotelini.Kila nikifika huwa nampigia simu mama mkubwa na pia najitahidi kwenda nyumbani kwake kumsalimia lakini mama mkubwa analalamika kuwa ni vizuri siku nikiwa huko japo siku moja moja nilale nyumbani kwake.

Mama yangu mkubwa nimuathirika wa UKIMWI,sio kwa kumuhisi bali kwa kinywa chake alimweleza mama yangu,pia hataki kutumia hizi dawa za kurefusha maisha hivyo amekonda sana na ana mapele na vidonda na majipu vinamtokea kila mara.

Siku moja nikiwa huko nikaamua kwenda kulala nyumbani kwa mama mkubwa wangu japo ana chumba kimoja,nilipofika nikakuta kidole chake kimoja cha mkononi kimeoza kwa kidonda chenye usaha,mwenyewe akanambia eti kuna mdudu akiingia kwenye kucha kidole ndo kinakua hivyo.

Tulikula kisha tukapiga story hadi usiku mwingi kisha sababu alikua ana magodoro mawili nikamwomba anitandikie godoro mim nilale chini.

Wakati anatandika shuka kwenye hilo godoro kwa bahati mbaya kile kidole chake chenye kidonda kikanichoma mguuni hadi pakakatika hadi damu ikanitoka halafu ule usaha wake ukabakia juu ya hapo aliponikata na kucha yake.Niliogopa sana,cha ajabu yeye hata hakuonesha mshituko,ila mimi niliogopa hadi sikuweza hata kupata usingizi.Kesho yangu nikarudi hotelini kwangu nikiwa na mawazo ya kuwa labda virusi vimenipata.Nilimaliza shughuli zangu huko nikasafiri kurudi nilipotoka lakini wiki mbili tokea aliponikata na kucha nilikuwa na mawazo sana lakini baadae nikasahau.

Kwa kawaida mimi ni mtu mwenye kinga imara,ni kwa miaka mingi sijawahi kuumwa kitu chochote zaidi ya mafua,tena hata mafua yenyewe sio mara kwa mara.Kama baada ya mwezi na nusu hivi tokea nilipokatwa na kucha nikapata mafua makali yaliyoambatana na homa kali na maumivu ya kichwa,nikaanza tena kukumbuka lile tukio,nikaanza kuhisi labda nimeshaathirika,wakati mwingine najipa moyo kuwa ni mafua ya kawaida maana hata kama kuathirika inaweza kuchukua hata miaka mingi bila kuona dalili.

Miezi michache baadae nikasafiri kwenda Ulaya,wiki moja tu tokea nifike nikaanza kupiga chafya mfululizo halafu pua ilikua inawasha ajabu hadi ikawa nyekundu na jicho moja likawa linatoa machozi hasa nikiwa nje natembea,mawazo tena ya kukatwa na kucha yakarudi kwa kasi,safari hii nikawa sina uhakika kabisa kuwa mimi ni muathirika au la maana tokea nizaliwe sijawahi kupatwa na hali kama hii,baada ya kupiga chafya kila dakika kwa wiki nzima mfululizo nikaamua kwenda hospitali,nikaambiwa nina allergy ya polen,daktari akasema kwa vile kilikua kipindi cha summer hewa imechafuka kwa polen inayotokana na maua yaliyopo kila mahala,ila nikashangaa maana home kwangu nina maua ya kila aina na sijawahi kupata hiyo hali,rohoni nikazidi kuogopa kuwa huenda nimeathirika kwa kukatwa na kucha.

Siku nyingine tena ghafla nikaanza kuwashwa na kuvimba mwili,yaani bila kujua sababu nilikuwa nawashwa kuanzia utosini hadi kwenye unyayo halafu nikiamka ngozi imevimba na kuwa nyekundu,kwenda hospitali nikambiwa eti kuna matunda nilikula ambayo nina allergy nayo,kweli kuna vitunda fulani nilikula,lakini nilizidi kuogopa kuwa haya mauza uza labda yanatokana na kukatwa na lile kucha.

Siku nyingine tena nikala viazi na samaki halafu usiku nikaamka tumbo likawa linaniuma sana kisha nikaanza kuendesha,kila dakila nikawa naenda chooni kwa siku mbili kisha likapoa.

Nikaona kukata mzizi wa fitina acha nikapime,kabla ya kukatwa na kucha nilikua nina uhakika kuwa sina ukimwi,niliamini kama mtu hujawahi kusex,wala kuongezewa damu,sindano nilichomwa nikiwa mtoto,wala sishirikiani na mtu vitu vya kukata hivyo chance ya kuwa na UKIMWI ni ndogo.

Kabla ya kwenda kupima nilisali nikamuomba Mungu kuwa kama kuna kirusi chochote kilichojipenyeza mwilini mwangu siku ile nilipokatwa na kucha la muathirika kife kwa jina lake lenye nguvu kupita majina yote.
Majibu yangu yakaja kuwa mim sio muathirika.

Nilichojifunza ni kuwa ukiruhusu ubongo wako uamini unaumwa kweli utakuletea vimagonjwa vya ajabu ajabu kusuport imani yako maana kipindi nilichokua naogopa nilipatwa hadi na vichomi ila nilipoambiwa sina UKIMWI hata sikujua vilipotelea wapi.

Pole sana mamie,
Dah, umenikumbusha miaka ya nyuma niliwahi kuugua hofu ya kuwa nimeathirika. kiukweli nilipungua uzito niliwaza sana. basi kulikuwa na doctor mmoja hivi rafiki yangu, nikamfuata nikamweleza kuwa ninaumwa, basi akaniuliza naumwa nini? nikamwambia naumwa hofu ila naogopa kupima. kama mjuavyo madakrati wana mbinu nyingi za kuwashauri wagonjwa wao, basi akanambia mimi nitakupima malaria, typhoid, VDRL na magonjwa mengine yote ila HIV sitakupima mpaka utakapoamua mwenyewe. basi c nikatoa damu kwa hiyari ili kupima kwanza magonjwa mengine....... Lahaula, kumbe yeye alikwenda kupima na HIV bila KUNAMBIA. alivyomaliza kupima hivyo vipimo vingine akanambia kuwa hauna magonjwa yoyote yale na pia HIV status yako ni NEGATIVE. nilifurahi sana na kujiona nimezaliwa upya.... baada ya muda nikaenda tena kucheck kwenye hosp. nyinge pia majibu yakawa NEGATIVE. Ushauri unaweza ukawa na hofu ukaugua ugua kumbe huna HIV ila ni magonjwa ya kawaida tu hata kama ungekuwa huna HIV ungeugua lakini kwa sababu una hofu utafikiri kuwa umeshaathirika. ni vymea kujua status yako mapema kuliko kubaki na assumption...........
 
Pole sana mamie,
Dah, umenikumbusha miaka ya nyuma niliwahi kuugua hofu ya kuwa nimeathirika. kiukweli nilipungua uzito niliwaza sana. basi kulikuwa na doctor mmoja hivi rafiki yangu, nikamfuata nikamweleza kuwa ninaumwa, basi akaniuliza naumwa nini? nikamwambia naumwa hofu ila naogopa kupima. kama mjuavyo madakrati wana mbinu nyingi za kuwashauri wagonjwa wao, basi akanambia mimi nitakupima malaria, typhoid, VDRL na magonjwa mengine yote ila HIV sitakupima mpaka utakapoamua mwenyewe. basi c nikatoa damu kwa hiyari ili kupima kwanza magonjwa mengine....... Lahaula, kumbe yeye alikwenda kupima na HIV bila KUNAMBIA. alivyomaliza kupima hivyo vipimo vingine akanambia kuwa hauna magonjwa yoyote yale na pia HIV status yako ni NEGATIVE. nilifurahi sana na kujiona nimezaliwa upya.... baada ya muda nikaenda tena kucheck kwenye hosp. nyinge pia majibu yakawa NEGATIVE. Ushauri unaweza ukawa na hofu ukaugua ugua kumbe huna HIV ila ni magonjwa ya kawaida tu hata kama ungekuwa huna HIV ungeugua lakini kwa sababu una hofu utafikiri kuwa umeshaathirika. ni vymea kujua status yako mapema kuliko kubaki na assumption...........

Woow nimeipenda mbinu ya huyo daktari.
Amekusaidia sana maana kama sio hivyo ungeendelea kuugua ukimwi wa kuhisi.
Ila angekuta Positive nadhani asingekwambia,ila negative ni habari njema.
Ila ukiambiwa huna unajiona tajiri si tajiri,yaani ni raha tupu.
Pole kwa hofu uliyopata charminglady.
 
Last edited by a moderator:
pole sana..............ILA MI LAZIMA NITAJITENDA NA WAGONJWA WA UKIMWI,NITAWANYANYAPAA
 
pole na hayo ndio maisha kihoro ndio kinaua watu wengi tupimeni tujue afya zetu na tutaishi kwa amani sana
 
Pole sana kwa mawazo, mawazo ya aina hiyo yalishamfanya ndugu yangu mmoja aumwe mpaka basi, kisa shugamami lake la siri lilikufa na ngoma watu walikuwa wanasema but yeye kumbe alikuwa safi kabisa, na umalaya alipunguza vibaya mno, kuna waathirika ambao mawazo ndio yanayozidi kuwadhoofisha zaidi kuliko hata unyanyapaa, just mtu anatakiwa kuchukulia poa, kula balance diet na kurefresh mind yake kwa vitu ambavyo ni fun, or ni hobbies zake, but asifanye mazoezi magumu sana, yatamchosha mno
 
siku hizi hakuna kupima tena, ukimwi haupo ndugu zangu,
 
Hello Wapendwa.

Kuna mahala fulani huwa ninasafiri kwenda mara kwa mara kufuatilia mambo ya kibiashara.Huko mahala ninaposafiri huwa kuna mama yangu mkubwa anaishi huko lakini siku zote huwa nashukia hotelini.Kila nikifika huwa nampigia simu mama mkubwa na pia najitahidi kwenda nyumbani kwake kumsalimia lakini mama mkubwa analalamika kuwa ni vizuri siku nikiwa huko japo siku moja moja nilale nyumbani kwake.

Mama yangu mkubwa nimuathirika wa UKIMWI,sio kwa kumuhisi bali kwa kinywa chake alimweleza mama yangu,pia hataki kutumia hizi dawa za kurefusha maisha hivyo amekonda sana na ana mapele na vidonda na majipu vinamtokea kila mara.

Siku moja nikiwa huko nikaamua kwenda kulala nyumbani kwa mama mkubwa wangu japo ana chumba kimoja,nilipofika nikakuta kidole chake kimoja cha mkononi kimeoza kwa kidonda chenye usaha,mwenyewe akanambia eti kuna mdudu akiingia kwenye kucha kidole ndo kinakua hivyo.

Tulikula kisha tukapiga story hadi usiku mwingi kisha sababu alikua ana magodoro mawili nikamwomba anitandikie godoro mim nilale chini.

Wakati anatandika shuka kwenye hilo godoro kwa bahati mbaya kile kidole chake chenye kidonda kikanichoma mguuni hadi pakakatika hadi damu ikanitoka halafu ule usaha wake ukabakia juu ya hapo aliponikata na kucha yake.Niliogopa sana,cha ajabu yeye hata hakuonesha mshituko,ila mimi niliogopa hadi sikuweza hata kupata usingizi.Kesho yangu nikarudi hotelini kwangu nikiwa na mawazo ya kuwa labda virusi vimenipata.Nilimaliza shughuli zangu huko nikasafiri kurudi nilipotoka lakini wiki mbili tokea aliponikata na kucha nilikuwa na mawazo sana lakini baadae nikasahau.

Kwa kawaida mimi ni mtu mwenye kinga imara,ni kwa miaka mingi sijawahi kuumwa kitu chochote zaidi ya mafua,tena hata mafua yenyewe sio mara kwa mara.Kama baada ya mwezi na nusu hivi tokea nilipokatwa na kucha nikapata mafua makali yaliyoambatana na homa kali na maumivu ya kichwa,nikaanza tena kukumbuka lile tukio,nikaanza kuhisi labda nimeshaathirika,wakati mwingine najipa moyo kuwa ni mafua ya kawaida maana hata kama kuathirika inaweza kuchukua hata miaka mingi bila kuona dalili.

Miezi michache baadae nikasafiri kwenda Ulaya,wiki moja tu tokea nifike nikaanza kupiga chafya mfululizo halafu pua ilikua inawasha ajabu hadi ikawa nyekundu na jicho moja likawa linatoa machozi hasa nikiwa nje natembea,mawazo tena ya kukatwa na kucha yakarudi kwa kasi,safari hii nikawa sina uhakika kabisa kuwa mimi ni muathirika au la maana tokea nizaliwe sijawahi kupatwa na hali kama hii,baada ya kupiga chafya kila dakika kwa wiki nzima mfululizo nikaamua kwenda hospitali,nikaambiwa nina allergy ya polen,daktari akasema kwa vile kilikua kipindi cha summer hewa imechafuka kwa polen inayotokana na maua yaliyopo kila mahala,ila nikashangaa maana home kwangu nina maua ya kila aina na sijawahi kupata hiyo hali,rohoni nikazidi kuogopa kuwa huenda nimeathirika kwa kukatwa na kucha.

Siku nyingine tena ghafla nikaanza kuwashwa na kuvimba mwili,yaani bila kujua sababu nilikuwa nawashwa kuanzia utosini hadi kwenye unyayo halafu nikiamka ngozi imevimba na kuwa nyekundu,kwenda hospitali nikambiwa eti kuna matunda nilikula ambayo nina allergy nayo,kweli kuna vitunda fulani nilikula,lakini nilizidi kuogopa kuwa haya mauza uza labda yanatokana na kukatwa na lile kucha.

Siku nyingine tena nikala viazi na samaki halafu usiku nikaamka tumbo likawa linaniuma sana kisha nikaanza kuendesha,kila dakila nikawa naenda chooni kwa siku mbili kisha likapoa.

Nikaona kukata mzizi wa fitina acha nikapime,kabla ya kukatwa na kucha nilikua nina uhakika kuwa sina ukimwi,niliamini kama mtu hujawahi kusex,wala kuongezewa damu,sindano nilichomwa nikiwa mtoto,wala sishirikiani na mtu vitu vya kukata hivyo chance ya kuwa na UKIMWI ni ndogo.

Kabla ya kwenda kupima nilisali nikamuomba Mungu kuwa kama kuna kirusi chochote kilichojipenyeza mwilini mwangu siku ile nilipokatwa na kucha la muathirika kife kwa jina lake lenye nguvu kupita majina yote.
Majibu yangu yakaja kuwa mim sio muathirika.

Nilichojifunza ni kuwa ukiruhusu ubongo wako uamini unaumwa kweli utakuletea vimagonjwa vya ajabu ajabu kusuport imani yako maana kipindi nilichokua naogopa nilipatwa hadi na vichomi ila nilipoambiwa sina UKIMWI hata sikujua vilipotelea wapi.

1. Mtu haambukizwi ukimwi. Anaambukizwa virusi. Jifunze tofauti ya HIV na AIDS.
2. Ukipima kuna aina tatu za majibu: una virusi, huna au "hali ya isiyotoa hakika ya yoyote kati ya hayo'.Pima zaidi ya mara moja ikiwezekana kwa vipimo tofauti.
3. Acha unyanyapaa wa maneno na vitendo.

BTW: nini lengo la hii post yako?
 
hii inanikumbusha stor moja ya nyoka, kunguru na binadam...nyoka alikuwa anabishana na kunguru kwamba mara nyngi kinachomuua bnadam ni HOFU na sio kingne. Ubish ulkuwa mkubwa ikabid wafanye zoez moja kuhakikisha, ikawa hivi...nyoka na kunguru wakajfcha kwenye majan bnadam alpopta nyoka akamgonga bnadam kwenye mguu halaf akajfcha, kunguru akatoka kwa kelele, bnadam alpomwona ni kunguru hofu ikaisha akaendelea na safar...wakarudia zoez lao kwa kubadlshana, wakati huu kunguru akamgonga bnadam mguuni, akajfcha, nyoka akatoka akikimbia eneo lile na bnadam akamuona kilichofata nadhan jibu unalo...pole sana Qk
 
Poleni sana kwa hayo majaribu ila naamini mungu aliwapigania kwa sabu ya nia yenu njema.
Mimi nahisi kwa maisha ya sasa mtu kujua status yake ni jambo la msingi sana...
 
Hichi kitu babu aliniambia kuwa imani huleta ugonjwa ila sikuamini ila leo nimeamini kwa mfano huu
 
Back
Top Bottom