Sikutegemea nilichokikuta ukweni

Sikutegemea nilichokikuta ukweni

Yaani ukute alishachakazwa sana huku kitaa halafu wanataka wakuuzie wewe.....achana naye mwanangu.

mimi sio muhumini wa maswala ya ndoa ila ikitokea nataka kuoa basi mahali mwisho laki 5....sijaona manzi wa kumtolea 1milion huku kitaa bado
 
Uislamu raha sana kwenye jambo kuoa moja mahari ni ya mwanamke yeye ndio anataja anataka nini kama seti ya sahani sawa kama mkeka wa kuswalia sawa ... Jambo la kuzika na jambo la kuoa limefanywa rahisi na la haraka mno .
Pole mkuu lipa hiyo mahari mambo ya mila ya ajabu ajabu waachie wenyewe
Hilo is not about dini is about jamii anayotoka muhusika.
wengine hawakulipa mahari, wengine mahari mwanamke alijilipia na si waislam. Familia nyingine ni wasomi kabisa walikataa mahari.
So inategemea unaenda kuchumbia wapi na familia ya muhusika ikoje
 
Wakuu habari za muda huu.

Kijana wenu nina umri wa miaka 28. Baada ya kuona kwamba sasa yanifaa kuwa na mwenzangu wa kuishi nae basi nikachukua jukumu la kwenda kwao kujitambulisha na kufahamika rasmi ili basi niishi nae kihalali kabsa
Kipato changu sio kikubwa sana hvo nikawa nimejiwekea kias flan kama mahari (million 1) nikamwambia mwenzangu kwamba hima hima kaongee na mama kama ataweza kuongea na mzee bc mahari isizidi hapo.

Mwenzang akanifata na kunijulisha kwamba mzee amekubal lkn anaomba angalau basi iwe 1.5 ili waweze kugawana nyumban na baadhi ya ndugu kwakuwa natambua kwamba mahari huwa haiishi (baada ya kuelezwa na wakubwa wangu) bc nilikubali kulipa hyo 1.5 lkn kwa malipo ya kidogo kidogom.

Jana kwa neema ya Mungu ndugu na familia yangu wakaongozana hadi kwao na mwenzang kwa ajili ya kutoa kishika uchumba na pia kulipa nusu ya mahali tuliyokubaliana. Baada ya kufika huko ndugu zangu hawakuamin walichokutana nacho huko ambacho ht mm mpk sasa siamin bado.

Mahari wamekuta ni million 4 na mahitaji kama koti la babu na vitu vingine jumla million 2 yan TOTAL ni million 6.

Kwa bahati mbaya sikuwepo ila laiti kama ningekuwepo bc ningewaomba ndugu zangu turudi nyumban
Nimesikitishwa sana na kilichotokea jana japo ndugu wamenishauri nisioneshe nia ya kukataa kuendelea na binti huyo lakini naona kabisa sitoweza najiona nikimuacha na kuendelea na maisha yangu
Ukweni wamenionesha rangi halisi kwamba kwao pesa ndio kipaumbele kikubwa kulko upendo.

Roho imeniuma sana nimejitoa vitu vingi sana ukweni kabla ya cku ya jana malipo yake ni mahari ya kukomoana kiasi hiki.

Wakuu naombeni faraja zenu na ushauri wenu nifanye nini katika swala hili.

Natanguliza shukran🙏
Familia zote civilized huwa haziwekagi mahari kubwa za kukomoa au wameona wakunyime mke..
 
Ninesoma replies nyingi nimegundua wengi humu wanalalamika maari kubwa kwa sababu hawana kazi au wanapitia maisha magumu

Mimi ni mchaga kutoka Rombo, nimeoa mmasai. Ni haki ya mzaszi kutaka maharishi ya mwanae, Leo anakuja lofa mmoja na shida zake analalamika kuwa mahari ni kubwa.

Nililipa million 4 na sikulalamika. Fair kabisa

Jifunzeni kuheshimu tamaduji za wengine na wanawake mnaowaoa. Unakuja jamaaa linanunua malaya kwa mwaka linatumia zaidi ya hiyo mahari aliyotajiwa huku linalalama kuwa maharishi ni nyingi

Juzi nimetoka kumkemea mtu kazulimiwq lako na nane na baba mkwe anatangaza kila kona. Mwanaume unatakiwa kuvunga kitu kama hicho unamezea sio kulia kulia lia

Kifupi mwanaume hutakiwi kulia lia umeshindwa kulipa maharishi. Kama umeshindwa pita na njia zako sio kulia kulia au kulaumu wake, AIBU
Hahaaaa watu wenye pesa bwana
 
Back
Top Bottom