Simamia mwenyewe kazi zako muhimu na epuka kufanya kazi kwa simu

Simamia mwenyewe kazi zako muhimu na epuka kufanya kazi kwa simu

mlinzi mlalafofofo

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2008
Posts
725
Reaction score
1,282
Miaka fulani uko nyuma nikiwa mkoani kwangu nilishuhudia uwanja mkubwa ulio jirani yetu ukisafishwa na bdae palifanyika ujenzi matata kabisa mahala pale.

Kwa harakati zilizokuwa zinaonekana pale ni wazi walikuwa wanajenga kitu kikubwa sana km hoteli kubwa au kitu kinachofanana na hicho.

Kwa nyepesi za pale kitaani kwetu huyo mmiliki alikuwa anaishi dar, hapa nitamwita "boswadaa". sasa cha ajabu boswadaa yeye alikuwa akituma pesa tu bila yeye mwenyewe kuja kule mkoani kuona yanayoendelea kwenye saiti yake. Alikuwa na jamaa zake anaowaamini pale mkoa ndio kama wasimamizi japo nao walikuwa hawana hata huo muda wa kufika hapo saiti. sanasana kama wakija wanakuja kununua/kuchukua mifuko ya simenti ya boswadaa na kutokomea zao. Kwaiyo wale mafundi ni km walikuwa hawana mabosi wa kuwasimamia. utawala wa manyani kila mtu yupo frii afanye anavyotaka.

Ile saiti ikageuzwa kuwa sehemu ya kununua matirio hasa zile simenti zilizokuwa zinaletwa na boswadaa. mzigo ukiingizwa mlango wa mbele unatolewa kule milango ya nyuma. Wanunuzi walifurahia wakidai simenti ya boswadaa ilikuwa beichee ni sawa na bure tu.

Kila siku ile saiti ilifurika wananzengo wakivizia fursa ya kununua mzigo wa simenti wa bei chee wa boswadaa.

Sisi wengine wkt mambo haya yanafanyika hatukuwa na la zaidi la kufanya zaidi ya kusikitika na hasa kumsikitikia boswadaa na zaidi tukishangaa kwanini yeye mwenyewe haonekani saiti hata kwa masaa machache kuona maendeleo ya mradi wake. tukaganga na yetu.

Jumba lile halikuweza kukamilika na hata sasa baada ya miaka mingi kupita, jengo lile ni gofu la kucheza panya na mijusi. ndoto ya boswadaa kumiliki hotel ni km imetamatishwa, japo mjadala utabaki ni nani aliyetamatisha ndoto hizo kati ya boswadaa mwenyewe au wale aliowaamini wangeweza kumsaidia usimamizi.

Bandugu tujihadhari na huu ujenzi wa simu au usimamizi wa ndugu, jamaa na kama ni lazima basi hakikisha unapata muda wa kufika au kujua kinachoendelea saiti, maana hata wale unaowaamini wanaweza kukuangusha kama walivyomfanya huyu boswadaa.

Ujenzi huu ninaousimulia hapa haukuweza kukamilika na pengine huyo mhusika alipoteza pesa nyingi sana maana ni km alikuwa akitumbukiza pesa kwenye shimo lisilo na mwisho hadi kashindwa kusimama tena.

Wewe uliyefanya mradi ule miaka ile ktk mkoa X kama leo hii unasoma hapa jua kuwa haya ndiyo yaliyotokea kwenye mradi wako ule na wale uliowaamini kusimamia walikuwa hawasimamii na sanasana walikuwa sehemu ya kukudimiza maana nao walikuwa wateja wazuri wa simenti zako.
 
Miaka fulani uko nyuma nikiwa mkoani kwangu nilishuhudia uwanja mkubwa ulio jirani yetu ukisafishwa na bdae palifanyika ujenzi matata kabisa mahala pale.

Kwa harakati zilizokuwa zinaonekana pale ni wazi walikuwa wanajenga kitu kikubwa sana km hoteli kubwa au kitu kinachofanana na hicho.

Kwa nyepesi za pale kitaani kwetu huyo mmiliki alikuwa anaishi dar, hapa nitamwita "boswadaa". sasa cha ajabu boswadaa yeye alikuwa akituma pesa tu bila yeye mwenyewe kuja kule mkoani kuona yanayoendelea kwenye saiti yake. Alikuwa na jamaa zake anaowaamini pale mkoa ndio kama wasimamizi japo nao walikuwa hawana hata huo muda wa kufika hapo saiti. sanasana kama wakija wanakuja kununua/kuchukua mifuko ya simenti ya boswadaa na kutokomea zao. Kwaiyo wale mafundi ni km walikuwa hawana mabosi wa kuwasimamia. utawala wa manyani kila mtu yupo frii afanye anavyotaka.

Ile saiti ikageuzwa kuwa sehemu ya kununua matirio hasa zile simenti zilizokuwa zinaletwa na boswadaa. mzigo ukiingizwa mlango wa mbele unatolewa kule milango ya nyuma. Wanunuzi walifurahia wakidai simenti ya boswadaa ilikuwa beichee ni sawa na bure tu.

Kila siku ile saiti ilifurika wananzengo wakivizia fursa ya kununua mzigo wa simenti wa bei chee wa boswadaa.

Sisi wengine wkt mambo haya yanafanyika hatukuwa na la zaidi la kufanya zaidi ya kusikitika na hasa kumsikitikia boswadaa na zaidi tukishangaa kwanini yeye mwenyewe haonekani saiti hata kwa masaa machache kuona maendeleo ya mradi wake. tukaganga na yetu.

Jumba lile halikuweza kukamilika na hata sasa baada ya miaka mingi kupita, jengo lile ni gofu la kucheza panya na mijusi. ndoto ya boswadaa kumiliki hotel ni km imetamatishwa, japo mjadala utabaki ni nani aliyetamatisha ndoto hizo kati ya boswadaa mwenyewe au wale aliowaamini wangeweza kumsaidia usimamizi.

Bandugu tujihadhari na huu ujenzi wa simu au usimamizi wa ndugu, jamaa na kama ni lazima basi hakikisha unapata muda wa kufika au kujua kinachoendelea saiti, maana hata wale unaowaamini wanaweza kukuangusha kama walivyomfanya huyu boswadaa.

Ujenzi huu ninaousimulia hapa haukuweza kukamilika na pengine huyo mhusika alipoteza pesa nyingi sana maana ni km alikuwa akitumbukiza pesa kwenye shimo lisilo na mwisho hadi kashindwa kusimama tena.

Wewe uliyefanya mradi ule miaka ile ktk mkoa X kama leo hii unasoma hapa jua kuwa haya ndiyo yaliyotokea kwenye mradi wako ule na wale uliowaamini kusimamia walikuwa hawasimamii na sanasana walikuwa sehemu ya kukudimiza maana nao walikuwa wateja wazuri wa simenti zako.
Watanzania kwa jumla wana roho mbaya hata awe ndugu yo hata kuharibia uta umweke ofisini kwako, hawana huruma na mali ya mtu .......bahati mbaya mwenye pesa hana mda mwenye mda hana pesa
 
Akiwepo John kitalumba ,akiwa rafiki yangu wa utotoni ila jamaa tuliyeshibana Sana wakati wa makuzi yetu .
John akaondoka kwenda ughaibuni baada ya elimu ya upili ,mawasiliano na yeye yakawa hafifu kila siku iendayo kwa nuumba .

Basi mzazi wa kiume wa rafiki yangu huyu akatangulia mbele za haki ,msibani nikabahatika kukutana na rafiki yangu tena.

Nikaani msiba na salamu za mbali atokako rafiki nikazipokea ,siku chache akakwea pipa kurudi ughaibuni ,akamwambia dada yake wa kumtangulia ati nitume hela juma lijalo ujenge kaburi la baba Ila naomba ujenge liendane na hadhi ya baba .

Dada mtu akubali na hela ikatumwa ,yapata hela nyingi baada ya kuigeuza kutoka kwenye dollar Ila dada hakuona ajizi akaila kwa kuweka starehe mbele ,kwa walioshuhudia wanasema hakikuwepo kiwanja dada hakufika kufurahia .

Ni mwaka Jana mwezi Kama huu ,rafiki yangu John amefariki kwa presha baada ya kutoka safari ya mbali Ila matarajio ya alichofanya kukuta hayakuwa vile alivyowaza na mbaya ni pale alipoiweka Imani iliyo dhabiti kwa dadaye pasina Shaka hata asiwaulize ndugu wengine kuwa kulikoni huko kwenye kaburi la baba .


Ni hayo kwa leo ,ahsanteni .

Historia hii inatukumbusha na kutufundisha kuwa usimuamini yeyote hapa duniani .

Asubuhi njema ndugu zangu .
 
Miaka fulani uko nyuma nikiwa mkoani kwangu nilishuhudia uwanja mkubwa ulio jirani yetu ukisafishwa na bdae palifanyika ujenzi matata kabisa mahala pale.

Kwa harakati zilizokuwa zinaonekana pale ni wazi walikuwa wanajenga kitu kikubwa sana km hoteli kubwa au kitu kinachofanana na hicho.

Kwa nyepesi za pale kitaani kwetu huyo mmiliki alikuwa anaishi dar, hapa nitamwita "boswadaa". sasa cha ajabu boswadaa yeye alikuwa akituma pesa tu bila yeye mwenyewe kuja kule mkoani kuona yanayoendelea kwenye saiti yake. Alikuwa na jamaa zake anaowaamini pale mkoa ndio kama wasimamizi japo nao walikuwa hawana hata huo muda wa kufika hapo saiti. sanasana kama wakija wanakuja kununua/kuchukua mifuko ya simenti ya boswadaa na kutokomea zao. Kwaiyo wale mafundi ni km walikuwa hawana mabosi wa kuwasimamia. utawala wa manyani kila mtu yupo frii afanye anavyotaka.

Ile saiti ikageuzwa kuwa sehemu ya kununua matirio hasa zile simenti zilizokuwa zinaletwa na boswadaa. mzigo ukiingizwa mlango wa mbele unatolewa kule milango ya nyuma. Wanunuzi walifurahia wakidai simenti ya boswadaa ilikuwa beichee ni sawa na bure tu.

Kila siku ile saiti ilifurika wananzengo wakivizia fursa ya kununua mzigo wa simenti wa bei chee wa boswadaa.

Sisi wengine wkt mambo haya yanafanyika hatukuwa na la zaidi la kufanya zaidi ya kusikitika na hasa kumsikitikia boswadaa na zaidi tukishangaa kwanini yeye mwenyewe haonekani saiti hata kwa masaa machache kuona maendeleo ya mradi wake. tukaganga na yetu.

Jumba lile halikuweza kukamilika na hata sasa baada ya miaka mingi kupita, jengo lile ni gofu la kucheza panya na mijusi. ndoto ya boswadaa kumiliki hotel ni km imetamatishwa, japo mjadala utabaki ni nani aliyetamatisha ndoto hizo kati ya boswadaa mwenyewe au wale aliowaamini wangeweza kumsaidia usimamizi.

Bandugu tujihadhari na huu ujenzi wa simu au usimamizi wa ndugu, jamaa na kama ni lazima basi hakikisha unapata muda wa kufika au kujua kinachoendelea saiti, maana hata wale unaowaamini wanaweza kukuangusha kama walivyomfanya huyu boswadaa.

Ujenzi huu ninaousimulia hapa haukuweza kukamilika na pengine huyo mhusika alipoteza pesa nyingi sana maana ni km alikuwa akitumbukiza pesa kwenye shimo lisilo na mwisho hadi kashindwa kusimama tena.

Wewe uliyefanya mradi ule miaka ile ktk mkoa X kama leo hii unasoma hapa jua kuwa haya ndiyo yaliyotokea kwenye mradi wako ule na wale uliowaamini kusimamia walikuwa hawasimamii na sanasana walikuwa sehemu ya kukudimiza maana nao walikuwa wateja wazuri wa simenti zako.
Pesa za kutuma unayemtuma hana uchungu nazo.

Ndio Maana wahindi wanakuwa wakali sana
 
Ni mwaka Jana mwezi Kama huu ,rafiki yangu John amefariki kwa presha baada ya kutoka safari ya mbali Ila matarajio ya alichofanya kukuta hayakuwa vile alivyowaza na mbaya ni pale alipoiweka Imani iliyo dhabiti kwa dadaye pasina Shaka hata asiwaulize ndugu wengine kuwa kulikoni huko kwenye kaburi la baba .
John ni mtu wa hovyo amefariki kwa kukuta kaburi halijajengwa? Ni hilo tu au hilo kaburi lilikuwa na jambo?
 
Watanzania kwa jumla wana roho mbaya hata awe ndugu yo hata kuharibia uta umweke ofisini kwako, hawana huruma na mali ya mtu .......bahati mbaya mwenye pesa hana mda mwenye mda hana pesa
Si kila Mtanzania ni mjinga wa kuharibu eneo lake la kulia
 
John ni mtu wa hovyo amefariki kwa kukuta kaburi halijajengwa? Ni hilo tu au hilo kaburi lilikuwa na jambo?
John rafiki yangu wa udogoni ,akiwa na mwili mdogo Sana kiasi kuwa ungetuona pasina Shaka ungeniita Mimi mkubwa Sana kwake kumbe abadani umri ulikuwa sawa .

Baada ya kufika ughaibuni ni dhahiri vyakula vyenye asili ya watu weupe vilimkubali Sana .
Basi John Kawa na mwili mkubwa ila walau nipatapo muda wa kujuliana hali hakusita kunijulisha hali ya afya yake kuwa Sasa imezorota .

Hivyo alipoliona kaburi la baba yake mzazi halijawa vile alivyotarajia alafu pia ukichanganya na ugonjwa basi ikawa Kama njia ya kumwondosha rafiki yangu .

Karibu tena ndugu .
 
Wewe uliyefanya mradi ule miaka ile ktk mkoa X kama leo hii unasoma hapa jua kuwa haya ndiyo yaliyotokea kwenye mradi wako ule na wale uliowaamini kusimamia walikuwa hawasimamii na sanasana walikuwa sehemu ya kukudimiza maana nao walikuwa wateja wazuri wa simenti zako.
Kwa hio Pesa zangu walikua wanazipiga?
 
Watanzania kwa jumla wana roho mbaya hata awe ndugu yo hata kuharibia uta umweke ofisini kwako, hawana huruma na mali ya mtu .......bahati mbaya mwenye pesa hana mda mwenye mda hana pesa
Yaani hatari sana
 
Watanzania wengi wanafanana kitabia hawana uaminifu na hawana huruma na pesa za watu, japo kuna waandilifu hususani wakina dada zetu na wale wanaume wenye hofu ya Mungu.
Sio kweli uaminifu ni moyo tu wa mtu, Mimi nimewahi kusimamia ujenzi wa nyumba ya mtu, pia nimewahi kusimamia ujenzi wa kanisa moja la RC, unajua mafundi usipowasimamia wao wanaweka weka tu mradi wamalize kazi sababu wanasema kuna kazi zinataka utumie akili na hapo hapo utumie nguvu, hii ya mtu binafsi ilikua ni kwenye kufanya decorations na kufanya finishing za hapa na pale km kuweka tiles na vinginevyo jamaa waliokuja kuweka milango wakaweka milango ovyoovyo milango haijachongwa vizuri inaburuza tiles mpaka inakwangua nikawaambie wang'oe waiweke vizuri kisha waiweke upya, kumbuka Mimi sio mwenye nyumba ila naona mapungufu ya mafundi sasa imagine wangekua wenyewe na ubaya wa mafundi akimaliza akaondoka umemlipa ndio imetoka hio
 
Back
Top Bottom