Simba bado tu haijamtimua Pablo?

Simba bado tu haijamtimua Pablo?

Moshi25

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2022
Posts
2,555
Reaction score
4,118
Hivi kwa mpira mbovu ilionao Simba kwasasa, Mashabiki kuugua magonjwa ya moyo na wengine hadi kulazwa kwa magoli ya kideoni ya wananchi, mashabiki wa Simba kupiga makonde wananchi wanapowatania vibanda umiza,mashabiki wa Simba kushindwa kuvaa jezi zao mitaani kwa kuona aibu ya kuwa wabovu, Simba kuwa na viungo na washambuliaji butu, Simba kupasuliwa na Yanga kila mechi ya watani.

Simba kulazimisha wachezaji waliopasuka kina Kibu kuendelea kucheza kwa kukosekana kikosi kipana, Simba kukosa viporo vya kuchukulia ubingwa, Simba kukosa makombe yote msimu huu, Simba kukosa mganga nguli kama watani wao , Simba kushindwa kuhonga marefa, Simba wachezaji kukosa pumzi ya kukaba kwa bidii mda wote kama wale wa Yanga, Wachezaji Simba kuhangaika kuvaa hereni uwanjani badala ya kumkaba Mayele, Simba kutolewa ligi ya mabingwa na shirikisho.

Je nani alaumiwe?

Je MO Dewji atuachie timu yetu?
Je benchi la ufundi limeishiwa sera?
Je Simba haina mganga?
Je Matola ni tatizo pia?
Je CEO amefeli?
Je Msemaji mpya hajafanikiwa kama Manara?
Je Pablo bado ni kocha anaefaa?
Je wachezaji wamechoka?
Je usajili ni mbovu?
Je kuna fitna toka Yanga?
Je Simba wameishiwa mpunga?

Wananchi tujadili bila mhemko!
 
Kwani alipewa muda wa kusajili wachezaji anao wahitaji?
 
Nabi gani? yule wa Pumzi ya Moto fc ya Mbagala inayokipiga Ndondo kapu au Professor Nabi wa Yanga?, mbona kama nishavutiwa hivi? mjomba nitumie video wasapu!
Nabi huyo huyo
 
Alipowasili kuna gazeti moja liliandika "heading" moja matata sana..... " Kwa kocha huyu vilio Simba sasa basi". Sasa ikawa kinyume chake. Natamani hilo gazeti lingeandika tena..... " kwa kocha huyu vilio Simba vimekuwa tele"....
 
Back
Top Bottom