SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Ninapoona Simba wanahangaika kusajili wachezaji wa kigeni ambao ni dhahiri wanakuja kuwa wachezaji wa akiba maana namba zao tayari zina wachezaji tegemeo, naona ni matumizi mabaya ya rasilimali. Hawa wachezaji wa akiba kwa kiasi kikubwa wangekuwa ni wazawa na wale wenye uwezo wapewe nafasi timu kubwa.
Simba wangejitahidi kutafuta vijana kama 15 hivi, makocha Juma Mgunda na Selemani Matola wakapelekwa kuwasimamia na kuwaendeleza, kila mwaka timu isingeweza kukosa wachezaji 4 wenye uwezo wa kuwapandisha ngazi. Wengine wangekuwa wanauzwa ndani na nje ya nchi.
Pia changamoto za mchezaji mmoja mmoja kama ilivyo sasa kwa Denis Kibu na Habib Kyombo zingeweza kutatulika kwa kuwapeleka wachezaji wa namna hii wafanye mazoezi kwa uangalizi maalumu katika timu ya vijana kwa muda fulani. Hii itasaidia kuangalia madhaifu ya mchezaji na kuyarekebisha kabla hajarudishwa kikosini.
Ni vigumu kocha mkuu kurekebisha madhaifu ya mchezaji mmoja mmoja, hasa yale ya msingi yasiyohusiana na mfumo anaojenga wakati huo huo anahangaika kujenga mfumo ndani ya timu nzima.
Simba wangejitahidi kutafuta vijana kama 15 hivi, makocha Juma Mgunda na Selemani Matola wakapelekwa kuwasimamia na kuwaendeleza, kila mwaka timu isingeweza kukosa wachezaji 4 wenye uwezo wa kuwapandisha ngazi. Wengine wangekuwa wanauzwa ndani na nje ya nchi.
Pia changamoto za mchezaji mmoja mmoja kama ilivyo sasa kwa Denis Kibu na Habib Kyombo zingeweza kutatulika kwa kuwapeleka wachezaji wa namna hii wafanye mazoezi kwa uangalizi maalumu katika timu ya vijana kwa muda fulani. Hii itasaidia kuangalia madhaifu ya mchezaji na kuyarekebisha kabla hajarudishwa kikosini.
Ni vigumu kocha mkuu kurekebisha madhaifu ya mchezaji mmoja mmoja, hasa yale ya msingi yasiyohusiana na mfumo anaojenga wakati huo huo anahangaika kujenga mfumo ndani ya timu nzima.