m2kutu
Senior Member
- Apr 5, 2014
- 125
- 101
Wasalaam wadau wa sports, ningependa kujua mechi ya marudiano kati ya Gendarmerie na Simba Sc itaonyeshwa live kupitia channel gani kwan Azam tv wamesema hatoweza kuirusha hii mechi.
Natanguliza shukran zangu kwenu wadau.
UPDATES
Simba imesonga mbele katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuifunga Gendarmerie bao 1-0, ikiwa na ushindi wa jumla ya mabao 5-0.
Klabu ya Simba Sc,imefanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Gendarmerie ya Djibout, katika mchezo wa marudiano.
Simba imefanikiwa kupata bao hilo kupitia mshambuluaji wake Mganda Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 55 ya kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo Simba inafuzu katika hatua hii ya awali kombe la Shirikisho barani Afrika kwa jumla ya bao 5-0.
Katika mchezo wa awali uliofanyika hapa chini katika dimba la Taifa-Jijini Dar es salaam, Simba walifanikiwa kupata ushindi wa bao 4-0.
Baada ya matokeo hayo Simba itakutana na Al-Masry ya Misri iliyopokea kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa Green Buffaloes.
Pamoja na kufungwa bao 2-1 Al- Masry ilifanikiwa kupata ushindi wa bao 4-0 katika mchezo wa awali na kufanikiwa kusonga mbele kwa jumla yabao 5-2.
Kikosi cha Simba SC kilichoanza leo kilikuwa; Aishi Manula, Nicholas Gyan, Asante Kwasi, Juuko Murshid, Yussuph Mlipili, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya, James Kotei, Jonas Mkude, Emmanuel Okwi na Muzamil Yassin
Natanguliza shukran zangu kwenu wadau.
UPDATES
Simba imesonga mbele katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuifunga Gendarmerie bao 1-0, ikiwa na ushindi wa jumla ya mabao 5-0.
Klabu ya Simba Sc,imefanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Gendarmerie ya Djibout, katika mchezo wa marudiano.
Simba imefanikiwa kupata bao hilo kupitia mshambuluaji wake Mganda Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 55 ya kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo Simba inafuzu katika hatua hii ya awali kombe la Shirikisho barani Afrika kwa jumla ya bao 5-0.
Katika mchezo wa awali uliofanyika hapa chini katika dimba la Taifa-Jijini Dar es salaam, Simba walifanikiwa kupata ushindi wa bao 4-0.
Baada ya matokeo hayo Simba itakutana na Al-Masry ya Misri iliyopokea kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa Green Buffaloes.
Pamoja na kufungwa bao 2-1 Al- Masry ilifanikiwa kupata ushindi wa bao 4-0 katika mchezo wa awali na kufanikiwa kusonga mbele kwa jumla yabao 5-2.
Kikosi cha Simba SC kilichoanza leo kilikuwa; Aishi Manula, Nicholas Gyan, Asante Kwasi, Juuko Murshid, Yussuph Mlipili, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya, James Kotei, Jonas Mkude, Emmanuel Okwi na Muzamil Yassin