Kwa jinsi nilivosearch mtandaoni, nimegundua kuwa mechi ya gendarmerie vs Simba haitoonyeshwa na channel yoyote ile iwe Tanzania au Djibouti.
Hii inatokana na nchi mwenyeji kuwa na muamko hafifu wa mchezo wa soka na pia hawana technology ya kutosha kuweza kurusha mechi hii. Kwa mfano hiyo channel ya taifa iitwayo RTD tv ambayo ndo ilikuwa tegemeo kubwa la wadau wengi kuwa wangerusha hii gemu ni ya hovyo sana bora hata TBC 1.
Hivyo wadau tufuatilie tu matokeo kupitia live scores tu, kuhusu mdau aliesema tusubiri ABOOD tv pia atakuwa amefeli kwa sababu na wao wanategemea wapate mawasiliano kutoka channel za Djibouti.
Ni hayo tu wadau wa sports..