Simba kuukatia tamaa ubingwa ni kosa kubwa sana

Simba kuukatia tamaa ubingwa ni kosa kubwa sana

BANDOKITITA

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2022
Posts
1,484
Reaction score
2,852
Kuanzia kikosi alochopanga kocha hadi uchezaji na hatimae draw ni dhahiri Simba walikuwa wameshakata tamaa ya ubingwa mwaka huu 2023. Hili ni kosa kubwa sn wamefanya.

Hata mwaka jana walikata tamaa mapema na kumalizia mechi zao ilimradi kwa kutoa sare nk bila kujua kuwa hata wapinzani wao wanaweza kupoteza. Hata wapinzani wao walipopata sare ilikuwa too late to come back.

Hili nalo limejitokeza msimu huu tena, na baadae watakuja kujilaumu wenyewe pindi wapinzani wao nao watakapopoteza au ku draw na km ilivyokuwa msimu uliopita itakuwa too late to come back.

Naona wao wameona wapeleke ugali wao kombe la FA hapo J2 na wataulia mboga hapo Mkwakwani siku ya fainali. Siyo mbaya ila haina afya wa wapenzi wao.

Pole sn wanasimba, timu yenu leo imehitimisha hisia za mbio za ubingwa. Jipangeni kwa msimu mpya kwa hapa biashara imeisha. Kesho bila hiyana Yanga watatangaza ubingwa baada ya ushindi.

Tukutane msimu Mpya.
 
Sisi kama lunyasi tunahamishia nguvu ASF (LOOSER) [emoji123][emoji123][emoji123]
 
Sio kuukatia tamaa ubingwa ndio uwezo wao ulipoishia. Kocha kaiga kafanya rotation kanyolewa. Kweli wamekufa kiume
Mkuu umenichekesha sana sasa huyo kocha alifanya rotation ya wachezaji ili iweje labda manake unapumzisha wachezaji wakiwa wanahitajika kwenye game kubwa na za ushindani sasa hawa wanapumzika ili iweje.
 
Mkuu umenichekesha sana sasa huyo kocha alifanya rotation ya wachezaji ili iweje labda manake unapumzisha wachezaji wakiwa wanahitajika kwenye game kubwa na za ushindani sasa hawa wanapumzika ili iweje.
Akili mtu wangu Robertinho amezingua leo
 
Simba tunakombe la robo fainali linatutosha
 
Back
Top Bottom