demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
STRAIKA mpya wa Yanga na kipenzi cha walio mashabiki wa Simba SC, Ibrahim Ajibu, tangu asajiliwe kutoka Simba hakuwahi kuzungumza lolote, lakini juzi Jumanne jamaa aliamua kufunguka na kutamka kauli ambayo Simba wakiisikia lazima wanune.
Ajibu amesema tangu atue ndani ya kikosi chake kipya, amekuwa mtu mwenye amani, akifurahia maisha na amewaahidi mashabiki wa Yanga mambo mazuri.
Straika huyo aliyeifungia Simba mabao 26 katika Ligi Kuu Bara kwa misimu mitatu aliyoichezea akiwa tegemeo, alisema anajisikia faraja kubwa kuwa Yanga na kwamba kuna mazuri yanakuja.
Ajibu anacheza nafasi ya ushambuliaji lakini sifa yake kubwa ni unyumbulikaji yaani ana uwezo wa kuuchezea mpira anavyotaka, pia ana uwezo wa kutembea uwanjani anavyotaka jambo ambalo ndiyo linalowafanya makocha wengi kumtumia kama straika namba mbili.
Mchezaji huyo kipenzi cha mashabiki, amesema: “Nahisi tofauti, tangu nimejiunga na Yanga nimekuwa mtu mwenye amani na ninafuraha, nashukuru tunaishi vizuri na wachezaji wenzangu na wananipa ushirikiano wa kutosha.
“Kwa ujumla nina furaha na imani yangu kazi nitakayofanya itakuwa nzuri, ninachowaahidi mashabiki ni mambo mazuri kuhakikisha Yanga inafanikiwa, huwa sipendi kuzungumza maneno mengi, wasubiri nitakachokifanya uwanjani, kikubwa nahitaji ushirikiano.”
Ajibu ndani ya kikosi cha Yanga amekabidhiwa jezi namba 10 iliyokuwa inavaliwa na Matheo Anthony na anatarajia kuanza kung’aa pale msimu mpya wa Ligi Kuu Bara utakapoanza mwezi ujao.
Ajibu amesema tangu atue ndani ya kikosi chake kipya, amekuwa mtu mwenye amani, akifurahia maisha na amewaahidi mashabiki wa Yanga mambo mazuri.
Straika huyo aliyeifungia Simba mabao 26 katika Ligi Kuu Bara kwa misimu mitatu aliyoichezea akiwa tegemeo, alisema anajisikia faraja kubwa kuwa Yanga na kwamba kuna mazuri yanakuja.
Ajibu anacheza nafasi ya ushambuliaji lakini sifa yake kubwa ni unyumbulikaji yaani ana uwezo wa kuuchezea mpira anavyotaka, pia ana uwezo wa kutembea uwanjani anavyotaka jambo ambalo ndiyo linalowafanya makocha wengi kumtumia kama straika namba mbili.
Mchezaji huyo kipenzi cha mashabiki, amesema: “Nahisi tofauti, tangu nimejiunga na Yanga nimekuwa mtu mwenye amani na ninafuraha, nashukuru tunaishi vizuri na wachezaji wenzangu na wananipa ushirikiano wa kutosha.
“Kwa ujumla nina furaha na imani yangu kazi nitakayofanya itakuwa nzuri, ninachowaahidi mashabiki ni mambo mazuri kuhakikisha Yanga inafanikiwa, huwa sipendi kuzungumza maneno mengi, wasubiri nitakachokifanya uwanjani, kikubwa nahitaji ushirikiano.”
Ajibu ndani ya kikosi cha Yanga amekabidhiwa jezi namba 10 iliyokuwa inavaliwa na Matheo Anthony na anatarajia kuanza kung’aa pale msimu mpya wa Ligi Kuu Bara utakapoanza mwezi ujao.