Simba msitafute kocha mpya kipindi hiki, mtakurupuka tena.

Simba msitafute kocha mpya kipindi hiki, mtakurupuka tena.

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Hakuna kocha mzuri asiyekuwa na timu ya kuifundisha, na hakuna timu bora inaweza kuachana na kocha na mchezaji bora katikati ya msimu labda kwa dau kubwa la kufa mtu. Simba haina fedha ya kubwa ya kuzinyanganya timu bara wachezaji na makocha wao bora kabla ya mwisho wa msimu. Hamna haja ya kutafuta mwalimu mpya sasa badala yake watumieni Cadena, Matola, Mgunda na Julio kwa pamoja hadi mwisho wa msimu, mtaona maajabu ambayo hamkuyatarajia. Bila Simba tamu hakuna Yanga tamu.
 
Hakuna kocha mzuri asiyekuwa na timu ya kuifundisha, na hakuna timu bora inaweza kuachana na kocha na mchezaji bora katikati ya msimu labda kwa dau kubwa la kufa mtu. Simba haina fedha ya kubwa ya kuzinyanganya timu bara wachezaji na makocha wao bora kabla ya mwisho wa msimu. Hamna haja ya kutafuta mwalimu mpya sasa badala yake watumieni Cadena, Matola, Mgunda na Julio kwa pamoja hadi mwisho wa msimu, mtaona maajabu ambayo hamkuyatarajia. Bila Simba tamu hakuna Yanga tamu.
lazima wamtafute ili wapate kisingizio wakishuka daraja mwisho wa msimu
 
Shida yetu wabongo tunaujua Sana mpira wa Miguu,,tuna uchambua na kuuchamba Haswa!!
 
lazima wamtafute ili wapate kisingizio wakishuka daraja mwisho wa msimu
Ni mhemuko tu kumtimua kocha kipindi hiki. Kocha kaonekana hajui na timu inacheza vizuri kwakuwa tu Yanga inacheza vizuri baaasi!! Kama yanga isingekuwa inacheza vizuri simba ingeonekana inacheza vizuri.
 
Ni mhemuko tu kumtimua kocha kipindi hiki. Kocha kaonekana hajui na timu inacheza vizuri kwakuwa tu Yanga inacheza vizuri baaasi!! Kama yanga isingekuwa inacheza vizuri simba ingeonekana inacheza vizuri.
mabadiliko katika soka na siasa za tanzania huchochewa zaid na hisia, mihemko na ghadhabu baada ya kuboronga. Tunakua na kupiga hatua, ila kwa mwendo wa polepole sana
 
wachambuzi wetu wanachambua mpira kuzisaidia timu zao wanazozishabikia, yaani wanachezea timu zao nje ya uwanja kwa kutumia midomo yao na kusahau kuwa mpira unachezwa kiwanjani tu baasi! Wachambuzi wa mpira wa kweli ni wachache sana, wasiozidi 3 nchini, na bahati mbaya mmoja (kashasha) keshakufa.
 
Kina Jose M, Rafa B na wengineo si makocha wabaya ila unaweza wakuta sokoni kwa kuachwa na timu sababu ya kufanya vibaya.
 
Bongo hakuna jobless, wote ni wachambuzi wa football
kulala na njaa kupenda. Hata hivyo, simba hawana uongozi madhubuti, ona sakata la Sakho linaishusha thamani simba na utetezi wa kijinga
 
Back
Top Bottom