Simba na yanga nani ana washabiki wengi?

Simba na yanga nani ana washabiki wengi?

only83

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2010
Posts
5,343
Reaction score
2,527
...Wana JF nimekuwa nikipata shida kujua kati ya hizi timu kubwa za soka la BONGO yaani SIMBA na YANGA nani anawashabiki wengi hapa Tanzania na other East Africa countries.......? Mwenye data kamili plz tujuzeni!!!
 
Mkuu hili swali ni ngumu kupata data za uhakika sijawahi kusikia sensa ya mashabiki, najua club zenyewe zina idadi ya wanachama wao but kwa mashabiki huwezi!
 
Ni yanga africa ndio wana mashabiki wengi kuliko wengine,fanya utafiti ktk mitaa kama mitatu karibu na unapoishi utaujua ukweli huu,napia kilapenye mikusanyiko yawatu ulizia utaona kuwa yanga inakaribu 60% ya mashabiki tzania.
 
Simba imeanza kupendwa miaka ya 2000+ yanga ilipendwa sana miaka ya tisini.
 
Hivi inakuwa kuwaje hadi Mtanzania halisi, USISHABIKIE YANGA?. Yanga yenye historia ya karibu kabisa na jitihada za uhuru wa nchi hii...
Yanga ambayo rangi zake mbili zipo pia kwenye bendera ya Taifa. Hivi kweli kuna mtu hashabikii Yanga?
 
Ila wanachama wengi wa SIMBA ni waarabu

Hii inaweza ikawa imesababishwa na waanzilishi wa timu hizi...maana wana historia wanadai kuwa Simba ilianzishwa na watoto wa mabwanyenye na ikaitwa sunderland kipindi hicho...baada ya watoto wa kiafrika kuona wanatengwa na watoto wa mabwanyenye wakaamua waanzishe timu yao wakaipa jina Dar Young Africans......
 
Simba imeanza kupendwa miaka ya 2000+ yanga ilipendwa sana miaka ya tisini.

Kumbe we bado bwamdogo sana! Tangu ikiitwa Sunderland na Young african sport we unasema miaka ta tisini na buku mbili!?????
 
Wanajamii kama nitakosea mtanikosoa ila kwa kweli kupata idadi kami ni ngumu sana ila nimewahi kufanya utafiti wa hali ya juu saana katika hili la nani ana wapenzi (wanachama)mashabiki wengi kati ya Simba Sport club 'wekundu wa Msimbazi au Dar Young african 'YANGA'Nimebahatika kutembelea na kuishi mikoa na wilaya nyingi za Tanzania bara na visiwani isipokuwa Mkoa wa Katavi tu kwa takwimu yangu isiyo rasmi mikoa yote ya Bara isipokuwa Dodoma,Tanga na Singida ndio Simba inaongoza kwa 60% Lakini iliobaki Yanga wako mbali sana mfano Kagera,Kigoma,Mbeya,Arusha,Mtwara Tabora Mara Hata Pwani wanaweza kufikia hata 70%Mpaka 75% iliyobakia Yanga wanavuna mashabiki wengi tu hata 65% kama Kilimanjaro,Moro,DSM,Shinyanga,Manyara,Iringa,Rukwa,Mwanza,Lindi na Ruvuma upande wa Tanzania visiwani Unguja Yanga wanaongoza kwa wingi ila kwa Pemba wanaweza kulingana au Simba kuzidi kwa thuluthi kadha pia Yanga wana mashabiki lukuki Uganda na maeneo kadha ya pwani ya Kenya. Mombasa,Malindi na lamu. Huenda Yanga wakawa na Mashabiki kwa 40%kwa eneo zima la Afrika mashariki Utafiti huu nimeufanya kati wilaya karibu zote katika mikoa nilio orodhesha hususani katika Viwanja vya Soka. Mara nyingi zinapocheza timu hizo mbili au zikija kupambana na timu za Mikoa hiyo
 
...Wana JF nimekuwa nikipata shida kujua kati ya hizi timu kubwa za soka la BONGO yaani SIMBA na YANGA nani anawashabiki wengi hapa Tanzania na other East Africa countries.......? Mwenye data kamili plz tujuzeni!!!

Kwa kutaka kupata jibu kirahisi aanzisha thread ili wana JF Wapige kura mkuu utaona idadi ya kura kwa kuanzia Weka wewe kura yako wengine watafuatia mwisho wa siku tutahesabu na kupata twakimu ya wana jamii wote maana hakuna asiye kuwa mpenzi wa timu hizo mbili nchini otherwise labda ukimuliza kuhusu Yanga au Simba akujibu ndio Mmea gani au mboga gani Yanga! Simba wa Mikumi au Serengeti Dr. Slaa Yanga Freema Mbowe Yanga Samwel sitta Simba Sumaye simba Malecela Simba Ali H Mwinyi Yanga Ben mkapa Yanga Lipumba Yanga Sharif hamad Simba Shein Yanga Nyerere na karume walikuwa Yanga wa kutupwa Tuendele ... JK ni
 
Kumbe we bado bwamdogo sana! Tangu ikiitwa Sunderland na Young african sport we unasema miaka ta tisini na buku mbili!?????

mkuu mimi najua yanga ya maulidi dilunga lakini yanga ya lunyamila, ilipendwa na waganda!(hii inamaanisha miaka ya 90 yawezekana yanga ilipendwa hadi nje ya tanzania!
 
Makamba ni Simba
Kapuya pia Simba
Zitto kabwe?
Mrema Simba
Salim Ahmed salim Simba
Tuendele... Mizengo pinda?
 
Yanga wako juu, hata sioni vipi unaweza kuiwalinganisha na mapaka, vimburu wale! lol
 
Ukiangalia uasilia wa uanzilishi wa hizi timu utagundua Yanga wanaweza wakawa na mashabiki wengi zaidi Tanzania
 
Nchi hii ni kubwa. Hapa huwezi pata jibu la moja kwa moja.Labda ufanye, tena si utafiti wa kuchukua sample tu, ni lazima ufanye sensa nyumba moja baada ya nyingine na uhakikishe unapunguza kwa kiwango kikubwa cha watu wanaoachwa na sensa hiyo.Hii inahitaji fedha nyingi. Pia haina tija kwani ukishajua then itasaidia nini? Kwa upande wa wanachama ni rahisi kwani unaweza kwenda katika ofisi husika, japokuwa napo unaweza kuambulia patupu, kwani utunzaji wa kumbukumbu ktk vilabu hivi ni very poor, labda siku hizi. Kwa ujumla katika hili, usifanye ushabiki tu katika kutoa majibu.
 
Yanga inawashabiki na wapenzi wengi zaidi kuliko Simba hapa nchini, NI KWELI WAARABU & WAHINDI WENGI NI SIMBA.
 

Hii inaweza ikawa imesababishwa na waanzilishi wa timu hizi...maana wana historia wanadai kuwa Simba ilianzishwa na watoto wa mabwanyenye na ikaitwa sunderland kipindi hicho...baada ya watoto wa kiafrika kuona wanatengwa na watoto wa mabwanyenye wakaamua waanzishe timu yao wakaipa jina Dar Young Africans......

Niliwahi kusikia Simba ilitokea ubavuni mwa Yanga (yaani kuna waliojitoa Yanga kwenda kuazisha Sunderland), kama ilivyokuwa Pan African (Yanga), Red Star (Simba). Kuna mwenye data atumwagie hapa jamvini? Ingawa bado haitasaidia kujua ipi yenye mashabiki wengi!
 
Kwa kutaka kupata jibu kirahisi aanzisha thread ili wana JF Wapige kura mkuu utaona idadi ya kura kwa kuanzia Weka wewe kura yako wengine watafuatia mwisho wa siku tutahesabu na kupata twakimu ya wana jamii wote maana hakuna asiye kuwa mpenzi wa timu hizo mbili nchini otherwise labda ukimuliza kuhusu Yanga au Simba akujibu ndio Mmea gani au mboga gani Yanga! Simba wa Mikumi au Serengeti Dr. Slaa Yanga Freema Mbowe Yanga Samwel sitta Simba Sumaye simba Malecela Simba Ali H Mwinyi Yanga Ben mkapa Yanga Lipumba Yanga Sharif hamad Simba Shein Yanga Nyerere na karume walikuwa Yanga wa kutupwa Tuendele ... JK ni

Njia hii ya kura sidhani kama itasaida, maana kwa ushabiki tu watu watapiga hata mara 100000000000000000000000000, ili mradi tu timu yake ionekane inaongoza kwa kuwa na mashabiki weeeeengiiii!!
 
Back
Top Bottom