SIMBA SC, baada ya kumfunga Yanga zile TANO, sasa hivi ni lazima tukubali hili !

Hapo Aboubacar Yousouf ndie mchezaji pekee wa kimataifa wa yanga ambae hastahili kuwapo kwenye kikosi chetu.
 
Nakubaliana na mleta mada kwa kiasi flani. Yanga ni bora kuliko simba kwa sasa na hasa msimu huu hilo lipo wazi. Illa hata kwa msimu uliopita walikuwa kiwango sawa walizidiana kwenye mbinu za nje ya uwanja. Illa yanga kwa mpira wa afrika ni bado sana. Na hassa ukizingatia timu nyingi za afrika magharibi mpira wao ulishuka kwa sababu za machafuko ya siasa kama wa Misri Morocco Tunisia na Nigeria na wengineo. Ilikuwa ni fursa nzuri timu mmojawapo za tz angalau kufika nusu fainali za makombe afrika. Illa wenzetu sasa wanarudi taratibu na wameanza kujenga timu zao za vilabu na taifa. Al Ahly ya 2010 - 2012 au huko nyuma yanga wangepigwa nyingi tu. Leo Al Ahly ipo kwenye kujijenga na kinachosikitisha hassa sio yanga wala simba ni Azam wana killa kitu pesa uwanja n.k. illa sijui wanafanya nini wameajiri wana yanga na simba mno ndio inawagharimu watafute viongozi mahiri toka nje waache uswahili hii timu itafika mbali. Kwa msimu huu mi ni simba illa yanga ni bora. simba lazima ijichunguze la sivyo sio timu ya ushindani pale.
 
Chini ya utawala wa Malinzi na genge lake pale TFF, hata Simba Sc wasajili kikosi bora cha dunia bado mambo hayataweza kubadilika.

Na kadiri Malinzi anavyoendelea kuendekeza mapenzi yake kwa Yanga Sc ndivyo soka letu linavyozidi kudidimia ...
 
mtoa mada nakupongeza sana kwa kuwe ukweli ulivyo na kuacha porojo za usimba na uyanga...Nakumbuka miaka ya 90 kukikuwa na wafadhiri wa hizi timu
Simba alikuwepo Azim Dewji na wenzake nitanikuu maneno ya Azim wwakati wanaifunga Club Sports Villa ya Uganda katika fainal ya CLub bingwa ya Africa Mashariki na kati alisema ikiwa timu ya ukanda huu tumeifunga fainal ya michezo yetu katika kanda yetu na hii timu(Villa) wamefika fainal ya kombe la CAF kwanini na sisi tusifike fainal. Alitengeneza timu na mwaka 1993 timu ya Simba walifika Fainal ya Kombe la CAF.


Kwa upande wa Yanga alikuwepo mfadhiri anaeitwa Marehemu Abbas Gulamali...mwaka 1991 wakati Simba wanabeba kombe la club bingwa Africa Mashariki ..Simba walimualika katika sherehe za kulipeleka kombe Ikulu kwa Raisi Ali Hassan Mwinyi....Na nukuu maneno aliyeyasema Mh Raisi na ahdi mwakani na mimi nitakuja kukuletea kombe hapa Ikulu..kilichotokea mwaka uliofuata Yanga aliungia fainal na Simba akafungwa lakini 1993 alitimiza ndoto yake ya kupeleka kombe Ikulu..huu ndio utani na majigambo yanayotakiwa kwa sisi wapenzi wa mpira
 
Ukweli mchungu. Mtu mwenye maono kama mleta maada hawezi kukubalika na watu waliokalia unazi unaopofua kutafakari kwao.

Sio siri Yanga inafanya vizuri lakini Azam ilitakiwa ifanye vizuri zaidi kwa uwekezaji wao kwenye timu. Kuna mahali kuna kasoro Azam. Mojawapo ni kumrudisha Stewart Hall. Walimtimua ili timu iende mbele lakini wamekula matashi yao kwa kumrudisha. Baada ya kumtimua Omog, afadhali wangempa mzawa timu wakati wakitafuta kocha mwingine mwenye kiwango zaidi.

Yanga, Azam na Simba zikiwa bora, bila shaka timu ya taifa itakuwa nzuri zaidi.
 
Chini ya utawala wa Malinzi na genge lake pale TFF, hata Simba Sc wasajili kikosi bora cha dunia bado mambo hayataweza kubadilika.

Na kadiri Malinzi anavyoendelea kuendekeza mapenzi yake kwa Yanga Sc ndivyo soka letu linavyozidi kudidimia ...

Akili za kushiikiwa na akina Manara hizi!
 
Mamluki huwa hawakosekani kila sehemu.
Mkuu acha hizo. Mimi nawafahamu mashabiki wa Simba pamoja na viwango vyao vya ushabiki. Huwezi kudai eti barafuyamoto ni mamluki pale Simba, huyu ni shabiki wa kufa na kuzikana na Simba. Kwa kifupi yeye ni mnazi wa Simba kuliko hata wewe. Kilichokusukuma useme ni mamluki ni ukweli aliouandika.

Pole sana, endelea kuamini kuwa Yanga inabebwa huku wenzako tunapiga boli bila kuangalia uso wala makunyanzi.
 
Ubishi m
Angalau kwa kipi walichofanikiwa mkuu kuwatoa apr, kufungwa goli dk za mwisho na waarabu au kutolewa klabu bigwa n kwenda shirikisho ndo angalau.?
wingine shida Tu wametinga name bora shirikisho
 
Mpira umetushinda mpaka Website na App ya simba sc hazifanyi kazi sasa.

Nadhani club yetu imeishiwa punzi idara zote.
 
Kiusajili Yanga walilamba dume,ila kimpira bado wako chini sana.Hawastahili kusifiwa.
 
Sina la kuongeza maana umeandika ukweli.
 
kwanini usiwaambie yanga wamuuzie timu manji wakati anaihudumia kila kitu wewe kama umetumwa namo nenda kaombe kazi kwenye zile bajaj zake zinazopiga kelele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…