GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Simba SC haishindi kwa Ubora wa Kocha wa muda Mgunda bali baada ya Viongozi baadhi wa Simba SC ambao wana DNA na Yanga SC pamoja na Matajiri wao wameshamaliza Jukumu lao walilopewa. Mpango ulikuwa ni Kwanza kuhakikisha Simba SC inadhoofishwa mbele ya Yanga SC ili iangushe Alama ( Points ) nyingi huku TFF nao pamoja na TPLB wakiwa wameshawekwa Mfukoni mwa Matajiri wasiolipa Kodi na wenye Fedha Chafu na nyingi ambazo hazina Kazi na kwa 99% tayari hilo limeshakamilika.
Hivyo baada ya sasa kile kilichokuwa kikitakiwa Kufanyika tena kwa Mafanikio makubwa kwa Timu kwenda kuwa Bingwa kwa Msimu wa Tatu mfululizo sasa Viongozi wa Simba SC ili kuwapoza Mashabiki wao na kuepuka lawama ya kukosa hata nafasi ya Pili katika NBC Premier League wanachokifanya sasa ni kuhakikisha wanacheza ile Michezo michafu ili Timu ishinde Mechi zake zilizobakia huku Mkizugwa kuwa Kocha Mgunda ni Mkombozi wa Timu na baadhi ya Mashabiki nao pamoja na Watu wa Media Wakihongwa ili wampambe Mgunda.
Kocha Benchika wala hakuwa na baya lolote la baada ya kuona Timu imejaa Uswahili na Upumbavu akaona ajivunje na awaachieni Litimu lenu. Hakuna asiyejua kuwa ili uwe Kocha wa Simba SC ni lazima uwe unaacha 10% kwa Viongozi na ukikataa kufanya hivyo wanachokifanya ni Kukuchomesha kwa Wachezaji Waandamizi ili wacheze chini ya Kiwango huku pia wakiwatafuta Waandishi wa Habari za Michezo na Wachambuzi wenye Majina na Umaaufu ili wakuseme vibaya na Kukuchafua ili uonekane hufai mbele ya Mashabiki kisha wapate sababu ya Kuachana nawe.
GENTAMYCINE mwaka 2012 nilishiriki kwa namna moja au nyingine katika hii Michezo Michafu hivyo ninachikisema hapa nakijua na nina uhakika nacho tena kwa 100% na ndiyo maana nikisema hakuna anayeniweza hapa kwa kulijua vyema Soka la Tanzania na Mauchafu yake yote na Janja Janja zake huwa namaanisha na ninajiamini kwa hilo. Niliwahi kusema na leo nasema kama FIFA au CAF au Serikali kupitia TAKUKURU ( PCCB ) wakisema wafanye Uchunguzi wa Soka la Tanzania linavyoenda nina uhakika Mpira wa Tanzania utafungiwa Milele kwani umejaa Rushwa kwa 99.999999% na Mabingwa hupatikana kwa Janja Jaja licha ya kwamba Wachezaji hutoa Jasho huko Viwanjani.
Namheshimu sana Kocha Mgunda ila najua nae hana tofauti yoyote na Makocha wa Kiswahili ( Kitanzania ) ambao wamejaa Uswahili Uswahili na Majungu 24/7 mbele ya Makocha Wageni na hata Wachezaji wa Kigeni baadhi ambao hawatoi 10% Kwao. Hakuna lolote jema au jipya alifanyalo Kocha Mgunda isipokuwa anasafishia Nyota yake kwa muda na Uongozi ( ambao unamwona Tambala la Dekio ) ili tu Kutuliza Mashabiki Mambumbu wa Simba SC ( nami GENTAMYCINE nikiwemo ) huku Wao sasa wakiendelea Kuzihonga Timu Pinzani ili zikubali Kufungwa na kuonekane kuwa baada ya Kocha Mkuu Kuondoka yuko anayeweza zaidi.
Namalizia kwa kusema hiki wanachokinya sasa Yanga SC kwa haya yote niliyoyaelezea hapa hata Simba SC nasi tulikifanya Kipindi tulipokuwa Mabingwa kwa Miaka ile Mitatu mfululizo tukisaidiwa na Utawala wa Nchi ambao ulikuwa unaipenda Simba SC na hata Tajiri yetu nae akawa anapata Jeuri na Nafuu ya Kodi. Hivyo hata hivi sasa Yanga SC nao wanapita mule mule ilikopita Simba SC huku nao wakifaidika na Utawala wa sasa ambao una Vinasaba vingi vya Kuwapenda wao ( Yanga SC ) lakini pia hata Tajiri yao nae ( kama ilivyokuwa kwa Tajiri yetu ) nae ana ukaribu mno na Utawala hivyo wana Simba SC tutulie tu kwani Kutesa huwa ni kwa zamu.
Haya nakuomba chukua haya Madini yangu GENTAMYCINE uwe nayo kwani hutoweza kuyapata Kwingineko kokote Oky?
Hivyo baada ya sasa kile kilichokuwa kikitakiwa Kufanyika tena kwa Mafanikio makubwa kwa Timu kwenda kuwa Bingwa kwa Msimu wa Tatu mfululizo sasa Viongozi wa Simba SC ili kuwapoza Mashabiki wao na kuepuka lawama ya kukosa hata nafasi ya Pili katika NBC Premier League wanachokifanya sasa ni kuhakikisha wanacheza ile Michezo michafu ili Timu ishinde Mechi zake zilizobakia huku Mkizugwa kuwa Kocha Mgunda ni Mkombozi wa Timu na baadhi ya Mashabiki nao pamoja na Watu wa Media Wakihongwa ili wampambe Mgunda.
Kocha Benchika wala hakuwa na baya lolote la baada ya kuona Timu imejaa Uswahili na Upumbavu akaona ajivunje na awaachieni Litimu lenu. Hakuna asiyejua kuwa ili uwe Kocha wa Simba SC ni lazima uwe unaacha 10% kwa Viongozi na ukikataa kufanya hivyo wanachokifanya ni Kukuchomesha kwa Wachezaji Waandamizi ili wacheze chini ya Kiwango huku pia wakiwatafuta Waandishi wa Habari za Michezo na Wachambuzi wenye Majina na Umaaufu ili wakuseme vibaya na Kukuchafua ili uonekane hufai mbele ya Mashabiki kisha wapate sababu ya Kuachana nawe.
GENTAMYCINE mwaka 2012 nilishiriki kwa namna moja au nyingine katika hii Michezo Michafu hivyo ninachikisema hapa nakijua na nina uhakika nacho tena kwa 100% na ndiyo maana nikisema hakuna anayeniweza hapa kwa kulijua vyema Soka la Tanzania na Mauchafu yake yote na Janja Janja zake huwa namaanisha na ninajiamini kwa hilo. Niliwahi kusema na leo nasema kama FIFA au CAF au Serikali kupitia TAKUKURU ( PCCB ) wakisema wafanye Uchunguzi wa Soka la Tanzania linavyoenda nina uhakika Mpira wa Tanzania utafungiwa Milele kwani umejaa Rushwa kwa 99.999999% na Mabingwa hupatikana kwa Janja Jaja licha ya kwamba Wachezaji hutoa Jasho huko Viwanjani.
Namheshimu sana Kocha Mgunda ila najua nae hana tofauti yoyote na Makocha wa Kiswahili ( Kitanzania ) ambao wamejaa Uswahili Uswahili na Majungu 24/7 mbele ya Makocha Wageni na hata Wachezaji wa Kigeni baadhi ambao hawatoi 10% Kwao. Hakuna lolote jema au jipya alifanyalo Kocha Mgunda isipokuwa anasafishia Nyota yake kwa muda na Uongozi ( ambao unamwona Tambala la Dekio ) ili tu Kutuliza Mashabiki Mambumbu wa Simba SC ( nami GENTAMYCINE nikiwemo ) huku Wao sasa wakiendelea Kuzihonga Timu Pinzani ili zikubali Kufungwa na kuonekane kuwa baada ya Kocha Mkuu Kuondoka yuko anayeweza zaidi.
Namalizia kwa kusema hiki wanachokinya sasa Yanga SC kwa haya yote niliyoyaelezea hapa hata Simba SC nasi tulikifanya Kipindi tulipokuwa Mabingwa kwa Miaka ile Mitatu mfululizo tukisaidiwa na Utawala wa Nchi ambao ulikuwa unaipenda Simba SC na hata Tajiri yetu nae akawa anapata Jeuri na Nafuu ya Kodi. Hivyo hata hivi sasa Yanga SC nao wanapita mule mule ilikopita Simba SC huku nao wakifaidika na Utawala wa sasa ambao una Vinasaba vingi vya Kuwapenda wao ( Yanga SC ) lakini pia hata Tajiri yao nae ( kama ilivyokuwa kwa Tajiri yetu ) nae ana ukaribu mno na Utawala hivyo wana Simba SC tutulie tu kwani Kutesa huwa ni kwa zamu.
Haya nakuomba chukua haya Madini yangu GENTAMYCINE uwe nayo kwani hutoweza kuyapata Kwingineko kokote Oky?