Mkuu, kuhusu Mavugo.. Vital'o wameongeza dau maradufu tofauti na makubaliano ya awali.. Ila kuna binadamu anaitwa Danny Lyanga toka Daring Motema Pemba a.k.a DC Motema Pembe ameshatua kuziba pengo la Mavugo.
Danny Lyanga ni nani?
- Kazaliwa 28/07/1991 (miaka 24) jijini Arusha
-Baada ya kucheza soka kwa kiwango cha juu kabisa mitaani, msimu wa 2010/2011 akiwa na miaka 19 tu, alitua timu ya Arusha FC na kuingia moja kwa moja 1st eleven, ambapo rekodi yake ya kutupia magoli ni ile ile kama ya Mavugo.. Mechi moja, Goli moja au zaidi
-Kutokana na kuonesha kiwango bora msimu uliofuata alitua Coastal Union, ambapo alicheza misimu miwili. Msimu wake wa mwisho alitupia goli 7, na goli la mwisho kufunga lilikua katika uwanja wa Mkwakwani dhidi ya timu yako (Azam FC) na gemu iliisha 1-1.. Na siku hiyo Ndala wakatangaza ubingwa wakiwa na mechi mbili mkononi.
-Msimu ukiofuata, alijiunga DC Motema Pembe.. na hii ni baada ya kuzipiga chini Simba, Ndala na Azam.
- Msimu uliopita, mkataba wake umeisha.. Hivyo anatua Simba SC akiwa huru.
KARIBU SANA SIMBA SC.. Mshambuliaji hatari, Danny Lyanga.