Simba SC, klabu iliyozaliwa na Yanga SC

Simba SC, klabu iliyozaliwa na Yanga SC

Nyenyere

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
14,804
Reaction score
10,715
Ukisoma gazeti la mwanaspoti la leo mama Karume anafafanua jinsi mgogoro ndani ya Yanga ulivyopelekea kujitenga kwa baadhi ya wanachama na kuanzisha Sunderland mwaka 1936. Kisha kuitwa Simba hapo baadaye. Kweli Yanga ni baba wa soka la Tanzania.

UPDATES:

Sehemu ya hiyo habari hii hapa;

Aliyoyafanya Karume kwa Yanga

Mama Karume anasema: “Sheikh Abeid AmaniKarume alikuwa mhamasishaji mkubwa wa kuanzishwa kwa klabu ya soka ambayo sasa ndiyo hii inayoitwa Young Africans Sports Club, yaani Yanga.

“Baada ya kufanya kazi ya ubaharia iliyomwezesha kuzunguka karibu dunia nzima kwa miaka kadhaa akiwa kijana mdogo, Karume alipata uzoefu wa yaliyotokea kwenye nchi mbalimbali alizozunguka duniani na kugundua kwamba serikali za kikoloni zilipiga vita uanzishwaji wa vyama vya siasa vya wananchi wazawa, lakini zilikuwa hazipingi vyama vya kijamii kama klabu za michezo.

“Baada ya kuufahamu ukweli huo, akiwa nyumbani Zanzibar, Karume alijiunga na wenzake na kuunda klabu ya soka iliyojulikana kwa jina la African Sports Club, mwenyewe akiwa mchezaji mahiri, humo humo kwenye mikutano ya kisoka ndimo yeye na Wazanzibari wenzake walikuwa wakijadili jinsi ya kujinasua kutoka kwenye utawala wa Kisultani uliokuwa ukilindwa na Waingereza.

“Ni hayati Karume ndiye aliyehamasisha kuanzishwa kwa matawi ya hiyo African Sports ya Zanzibar na akafanikiwa kuanzishwa kwa tawi la timu hiyo jijini Dar es Salaam ambalo kwa sasa ndilo hii klabu kubwa sana ya Yanga na kule Tanga alifanikisha kuanzishwa kwa tawi jingine ambalo ni African Sports ya Tanga.

“Kumbuka kuwa kwenye miaka hiyo ya nyuma, miji ya Dar es Salaam, Bagamoyo, Pangani na Tanga ilikuwa na ukaribu sana wa kiuhusiano na miji ya visiwa vya Unguja na Pemba. Kipindi kama cha Pasaka walikuwa wakitembeleana, klabu za kule zinakuja na wakati mwingine za huku zinaenda huko.

“Baada ya kuanzishwa timu hizo tatu; Yanga ya sasa, African Sports ya Zanzibar na African Sports ya Tanga, zilitengeneza undugu wa damu kubwa mno. Zote tatu zilikuwa chimbuko la hayati Karume.

“Lakini haikuchukua muda, mwaka 1936 Yanga ikakumbwa na wimbi kali sana la migogoro, baadhi ya watu wakajitenga kutoka Yanga na kwenda kuanzisha klabu yao ambayo iliitwa Sunderland ambayo ndiyo Simba.

“Mwaka 1971, Karume aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la klabu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi. Karume alitoa mchango wake wa fedha wa kufanikisha ujenzi wa jengo hilo, hapo hapo alitoa rai kwa klabu hiyo kuachana na jina la Sunderland Sports Club lililokuwa likitumiwa na klabu hiyo hadi wakati huo.

“Hakuishia kuelekeza tu kwamba jina hilo lilikuwa haliakisi utamaduni wetu na lilikuwa mwendelezo wa mabaki ya ukoloni, bali pia alipendekeza jina linalotumika sasa na klabu hiyo nami nakumbuka waziwazi nilivyomsikia akisema kupitia Radio Tanzania Dar es Salaam, alisema ‘Achaneni na jina hilo la kikoloni la Sunderland kwani tuko Uingereza hapa? Mnaweza mkajiita Simba Mwekundu Sports Club, jina linaloeleweka na linaloendana na utamaduni wetu’.


Kwa habari zaidi soma;
http://www.mwanaspoti.co.tz/Soka/-/1799484/2144144/-/item/1/-/12344m8/-/index.html
 
Hivi kwanini mliogopa kushiriki Kombe la Mapinduzi?
 
Kwa miaka mitatu mfululizo Bwashehe?

No, unajua Yanga wanaenda kwa program. Sasa hiyo mapinduzi cup huwa haimo kwenye program zao. Kwa hali hiyo si rahisi kushiriki kwa timu inayozingatia mpangilio wa mafunzo iliyojiwekea.
 
Hivi kwanini mliogopa kushiriki Kombe la Mapinduzi?

Yanga hatukuogopa kushiriki isipokuwa Simba wasio na akili kama Wagalatia wanadhani kwamba eti tuliogopa kushiriki. Kwa Simba mapinduzi ni nafasi yao ya mwisho, Yanga tuna majukumu ya CECAFA na CAF.
 
Ukisoma gazeti la mwanaspoti la leo mama Karume anafafanua jinsi mgogoro ndani ya Yanga ulivyopelekea kujitenga kwa baadhi ya wanachama na kuanzisha Sunderland mwaka 1936. Kisha kuitwa Simba hapo baadaye. Kweli Yanga ni baba wa soka la Tanzania.

Kama YANGA ni Mama wa SIMBA Baba yake nani???

Achana na porojo hizo wewe..... angetuambia Kabla ya Simba mpinzani halisi wa YANGA alikuwa nani..? na kama hakuwepo YANGA ilikuwa inacheza mpira peke yake?
 
Nyuma mbona mlikuwa mnakubali kugawa? Mechi ya mwisho ya Fainali ya Mapinduzi mlipofungwa na Simba...ndo mkaamua Kususa sio?
Hamjui kuwa Ushindi wetu wa leo hautanoga?
 
Wangepeleka timu tu... Jangwani ilikuwa vipande vipande maana wasingeachwa... kama si 5 ingekuwa 8...
 
Yanga hatukuogopa kushiriki isipokuwa Simba wasio na akili kama Wagalatia wanadhani kwamba eti tuliogopa kushiriki. Kwa Simba mapinduzi ni nafasi yao ya mwisho, Yanga tuna mjukumu ya CECAFA na CAF.

Mzee Akilimali aliwakataza eti?
 
Mzee Akilimali aliwakataza eti?

Ee Mwenyezi Mungu hadi lini utaruhusu hawa jamaa waendelee kututukana na kukebehi timu yetu? Walikuwa kimya muda mrefu, wameibuka baada ya mtani jembe. Dua yangu kwako ni kuruhusu KCC wapate goli moja tu jioni hii ili kumaliza hizi kelele, asante Bwana kuwa umesikia dua ya mtumishi wako Makoye Matale, amina.
 
Last edited by a moderator:
Ee Mwenyezi Mungu hadi lini utaruhusu hawa jamaa waendelee kututukana na kukebehi timu yetu? Walikuwa kimya muda mrefu, wameibuka baada ya mtani jembe. Dua yangu kwako ni kuruhusu KCC wapate goli moja tu jioni hii ili kumaliza hizi kelele, asante Bwana kuwa umesikia dua ya mtumishi wako Makoye Matale, amina.

hiyo dua iombee yanga leo wanacheza na tax drivers wa uturuki
 
Last edited by a moderator:
Kama YANGA ni Mama wa SIMBA Baba yake nani???

Achana na porojo hizo wewe..... angetuambia Kabla ya Simba mpinzani halisi wa YANGA alikuwa nani..? na kama hakuwepo YANGA ilikuwa inacheza mpira peke yake?

Soma historia kijana, unadhani watu walikaa tu chini wakapanga kuanzisha Yanga na Simba ili ziwe pinzani? Simba ni mtoto aliyemwasi mzazi wake. Ndio maana tunawachukulia kama watoto tu na hoja zenu za ajabu ajabu. Mzazi ni mzazi tu.
 
hebu nipe historia yanga ilianzishwa mwaka gani na simba ilianzishwa mwaka gani,yaani historia toka wakati wa ukoloni.
 
hebu nipe historia yanga ilianzishwa mwaka gani na simba ilianzishwa mwaka gani,yaani historia toka wakati wa ukoloni.

Ya Simba ipo tayari hapo juu 1936. Umeiona?
 
nimeiona basi nipe ya Yanga.

Ok. Yanga ilianzishwa mapema mwaka 1935. Mwaka mmoja baadaye kukatokea mgogoro ndani ya klabu na ndipo Simba ikajimega 1936
 
Ok. Yanga ilianzishwa mapema mwaka 1935. Mwaka mmoja baadaye kukatokea mgogoro ndani ya klabu na ndipo Simba ikajimega 1936

nipe source ya kuaminika!

kwahiyo inaonyesha upinzani wao umenzia baada wengine kusaliti na kujitoa?au upinzani wa jadi ulikuja kutokea baadaye sana
 
duuh ile dozi ya goli 5 bado inawasumbua Ndala....polen sana na harakati zetu za kutafuta hauwen
 
Back
Top Bottom