Nakumbuka ile Mechi na Raja, nilikuwa na kuongozi mmoja wa Simba pale Element Hotel akawa ananiambia maneno haya haya. Kuwa tumewafanyia umafia wa hali ya juu, kuamzia airport hadi kwenye Mahoteli. Tumeungana na Yanga kuwafanyia wageni Umafia maana Yanga alikuwa na Mgeni TP Mazembe na sasa hawana sehemu ya Kulala kwani Hotel zote Nyota 5 za hapa Town wamesema hawana nafasi zimejaa. Jamaa alijitamba sana nami nilimuamini na nikawa nawashirikisha wenzangu kwenye majukwaa yetu ya kikazi huku nikisindikiza picha nilizopiga na Chama na wengine.
Ila kilichowakuta wakati wa Mechi, mlikiona wenyewe. Jiandaeni uwanjani na sio hizo blah blah za nje.