Simba SC mikononi mwa UD Songo

Simba SC mikononi mwa UD Songo

Orketeemi

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
5,063
Reaction score
12,866
Wanasimba wenzangu tujiandae kisaikolojia. Dalili zipo wazi kwamba hatutaweza kuwatoa FC Platnum.

Shida kubwa ni dalili zinazoonyesha kwamba play off tutakayoangukia tutajikuta miguuni mwa UD Songo ambayo inacheza mechi yake kesho dhidi ya NAPSA , UD Songo inapewa nafasi kubwa kuitoa NAPSA.

Tupigeni magoti tusali.
 
Wanasimba wenzangu tujiandae kisaikolojia. Dalili zipo wazi kwamba hatutaweza kuwatoa FC Plutnum.
Shida kubwa ni dalili zinazoonyesha kwamba play off tutakayoangukia tutajikuta miguuni mwa UD Songo ambayo inacheza mechi yake kesho dhidi ya NAPSA , UD Songo inapewa nafasi kubwa kuitoa NAPSA.

Tupigeni magoti tusali.
Dalili Gani umeiona kuwa Simba haitaweza kuitoa FC Platinum?
 
Plutnum hasa kuanzia kiungo mpaka forward zao ni mpira wa kasi wakati Simba ina defence iliyo na wachezaj wasio na kasi.
Team yoyote duniani ktk counter attack itaonekana INA Kasi, mbona Kasi yao haikuonekana ktk Mashambulizi ya Kawaida??Ktk Mashambulizi ya kawaida walikuwa na kasi mfano wa ile inayooneshwa na Miquissone?
 
Team yoyote duniani ktk counter attack itaonekana INA Kasi, mbona Kasi yao haikuonekana ktk Mashambulizi ya Kawaida??Ktk Mashambulizi ya kawaida walikuwa na kasi mfano wa ile inayooneshwa na Miquissone?
Sawa. Lakin nakuambia Plutnum wanacheza kama Nkana na kwa kifupi Wazambia na Wazimbabwe ni walewale. Simba iliyoitoa Nkana si hii ya sasa. Hii huwez kufurukuta.
 
Sawa. Lakin nakuambia Plutnum wanacheza kama Nkana na kwa kifupi Wazambia na Wazimbabwe ni walewale. Simba iliyoitoa Nkana si hii ya sasa. Hii huwez kufurukuta.
Uliangalia game ya kwanza ya kule Zimbabwe??Uliangalia Statistics zake baada ya Game?Mbona zote ukiondoa tofauti ya goli moja zilikuwa in favour of Simba??
 
Kwani hao UD Songo kila siku ni wao tu wameandikiwa kuitoa Simba?
 
Plutnum hasa kuanzia kiungo mpaka forward zao ni mpira wa kasi wakati Simba ina defence iliyo na wachezaj wasio na kasi.
Ussain Bolt angekuwa mchezaji soka bora kabisa
 
Ni kweli kabisa Simba hii mechi haitoboi,so sad nadhan baada ya hapa,simba watajitathimini vizuri
 
Simba akifuzu hapa dhidi ya Platnum anaingia kwenye hatua ya makundi

Sasa wewe Uto hiyo taarifa ya kucheza na hao mabwana zenu ud songo sijui umedanganywa na Antonio nugaz
 
Tuna hali ngumu kiasi wanasimba wenzangu,tunapambana Mkude acheze maana ndani ya timu kuna mgogoro mkubwa sana timu imepasuka vipande vipande.

Simba nguvu 0
 
Back
Top Bottom