MIEZI SITA MILIONI SITINI.
Namba 6 yenye utata.
✍️Miezi 6 iliyopita Simba SC ilianzisha kampeni ya kuchangia Uwanja.
✍️ Imechukua miezi 6 hesabu kuwekwa bayana.
✍️Milioni 60000000 zimechangwa kwa miezi SITA ikiwa ni Sawa na uwiano wa Milioni 10 kwa Mwezi.
✍️Wale watu wa kukokotoa tusaidiane kidogo: Tukichukua tu kiasi Cha buku kama kiwango Cha chini Cha mchango kwa waliochangia Mimi nikiwemo, basi Ina maaana ni Simba SC Ina mashabiki elfu sitini TU ambao Ndio waliochangia.KWELI? Sasa si afadhali kutengeneza mechi ya bonanza na Timu Moja Afrika mashariki,kuifanyia promo mechi hiyo na kuujaza Uwanja kwa kiingilio Cha 5000 tu utakuwa umekusanya 5000×60000=300,000,000(milioni mia tatu) ukitoa gharama za uwanja na gharama za timu alikwa unaweza ukabakia na Milioni 240,000,000 ambayo kwa hesabu tuliyopewa na klabu yetu leo basi tunahitaji miaka 6 kuchangia milioni mia tatu achilia mbali bilioni 30 zanazihitajika kujenga Uwanja. Je si tutahutaji miaka 60 Tena ya uhuru?
✍️Vipi na zile bilioni mbili (2,000,000,000) alizoahidi mdhamini wetu kuwa ameweka katika kuendeleza mchango huu uwanja? Mbona hazikujumuishwa katika taarifa ya Leo? Au Mimi sikuelewa? Au hatupaswi kuhoji?
✍️Kwa hiyo mnataka kutuaminisha kuwa Simba hii iliyo na wapenzi wengi iwe ni watu elfu 60000 tu ndio wamechangia? NATAFAKARI.
✍️Itoshe kusema majibu hayakujitosheleza na haikuwa na haja ya kulizungumzia hili. TUMEPIGWA.
✍️Kwanini kusiwepo na update ya Kila Mwezi kuhusu zoezi lile ikawa unapata ujumbe kila unapochangia kuwa 'Mchango wako umefikia mtu wa....au namba.....)? NAWAZA KIMOYOMOYO
Kama ilivyo kwa simba hata kwa Yanga endapo utaratibu itakuwa ni huu wa kuficha taarifa za makusanyo hasa kutoka kwa wanaochangia basi NANI ZAIDI itageuka na kuwa ZAIDI NI NINI Mbona mchango umedorora?