Simba SC yapokwa pointi 3 dhidi ya Kagera Sukari

Simba SC yapokwa pointi 3 dhidi ya Kagera Sukari

Kagera Sugar wanaweza kuwa na kosa lakini je sheria ilizingatiwa kwa mlalamikaji alifuata sheria kuwasilisha rufaa yake?

Kama wangewasilisha kwenye muda ilo suala la kadi ya njano ndipo lingeanza kufanyiwa kazi.
Sasa huo ndio upuuzi mchezaji alikuwa na makosa au hana??? Kwanini kamati zitofautianee
 
BREAKING NEWS: TFF imetengua maamuzi ya Bodi ya Ligi kuipa pointi 3 Simba dhidi ya Kagera Stars na hakuna kukata rufaa kwani kikao kile kilikuwa batili.
[emoji36] [emoji36] [emoji36] watz tutakf n stress...kweny mpira mapichacha bongo movie matapishi mara vyeti feki mara Lipumba atuma watu wavamie....
 
Asante mwenyekiti wetu wa chama cha soka cha bukoba Jamal malinzi kwa uzalendo wako.
 
Sasa huo ndio upuuzi mchezaji alikuwa na makosa au hana??? Kwanini kamati zitofautianee

Iko hivi.

Kwa kawaida mchezaji aonekanapo na kosa ni lazima ukate rufaa. Kwenye utaratibu wa kukata rufaa kuna kanuni zake ambapo kuna muda maarumu umetengwa wa kupokea rufaa yeyote bila kuzingatia aina ya kosa lililopelekea rufaa!

Kama ukienda nje ya muda wa kuwasilisha rufaa na ukataka kulamiza rufaa yako isikilizwe kwakuwa wewe ni Simba SC au ni Yanga SC kunaondoa maana nzimaya kuwa na kanuni zinazoongoza rufaa.

swala la msingi ni rufaa kuwasilishwa nje ya muda!Hayo mengine ya kwamba hana au anayo kadi acha viongozwe na kanuni nyinginezo!

Kwakuwa hata kama alikuwa nayo kadi na wewe hukufuata sheria kwenye kuwasilisha rufaa yako unakuwa na uhalali gani wa rufaa yako kufanyiwa kazi..

Tuzingatie sheria wajameni!
 
Kagera Sugar wanaweza kuwa na kosa lakini je sheria ilizingatiwa kwa mlalamikaji alifuata sheria kuwasilisha rufaa yake?

Kama wangewasilisha kwenye muda ilo suala la kadi ya njano ndipo lingeanza kufanyiwa kazi.
Hata kama Simba waliwasilisha rufaa nje ya muda, je kuna uhalali wa Kagera Sugar kumchezesha mchezaji mwenye kadi tatu za njano?
 
Tangu lini Simba wakapata haki chini ya Tifutifu.. Wakae kimya tu
 
Back
Top Bottom