Simba Sport Club: Taarifa kwa umma

Simba Sport Club: Taarifa kwa umma

hapana mkuu arsenal wamefunga kwa mkono sekunde ya mwisho hakuna alieng'oa kiti wakat tambwe amefunga kwa mguu.
 
Dah! janga la Kitaifa hili.😵😵😵

SIMBA SPORTS CLUB
DAR ES SALAAM
2-10-2016

TAARIFA KWA UMMA



Na mwisho klabu itoe malalamiko yake kwa Waziri wa mambo ya nchi,Mh Mwigulu Nchemba.

Waziri huyu bila shaka amesahau majukumu yake yake ya kazi na kugeuka kiongozi wa klabu ya Yanga.

Tunajua ni haki yake kuwa na mapenzi kwa klabu aliyoichagua.lakini vitendo vyake anavyovifanya vinaacha maswali mengi kuliko majibu.ukizingatia nafasi yake kama Waziri mwenye dhamana ya kuongoza Wizara nyeti.


Itakumbukwa majuzi waziri huyu alifanya ziara Mkoani Morogoro kuzungumza na vikosi anavyoviongoza.
Na inajulikana pia Refarii wa mchezo wa jana Martin Sanya ni mwajiriwa wa Jeshi la Magereza mkoani Morogoro


Sote tulishuhudia Jana Mwigulu alishangilia goli la hovyo la mwajiriwa wake Sanya.

Pia waziri huyu alitoa kauli tata kuwa angetamani siku moja klabu inayoshangilia wapinzani wa Yanga wakipigwa mabomu ya machozi na Askari wa jeshi la Polisi.
Kauli hii aliitoa wakati wa sherehe za kukabidhi zawadi kwa timu zilizoshinda msimu uliopita zilizoandaliwa na wadhamini wa ligi.kampuni ya Vodacom.


Tunajiuliza yale mabomu ya jana pale Uwanja wa Taifa ndio utekelezaji wa maagizo ya boss Mwigulu?



IMETOLEWA NA
KLABU YA SIMBA

SIMBA NGUVU MOJA
 
Nilikuwepo vyumbani pale Uwanja wa Taifa ( Nina Access ya kuingia kokote) vyumba vyote vilipuliziwa dawa sio vyumba vya Simba pekee.

Walipoingia Taifa Simba waligawana vyumba vya kuingia, kulikuwa na makundi matatu tofauti na kundi moja liliingia dressing room ya kawaida ya siku zote, lingine likaenda chumba pembeni ya vyoo vya Press Room.
 
His taharifa kweli imetoka kwenye taasisi kubwa kweli Kama simba camini
 
kulalamikia goli la mkono ni ushamba.magoli ya mkono wamefunga tangu akina maradona,thiery henry kwenda world cup2010.
 
Simba bhana, sasa goli la mguu nyie mnasema la mkono...mm niliona mpira ulitulizwa kifuani akiwa juu akageuka, huenda mpira ukapitia ktk mkono lakini ukatua mguuni...akamhadaa golikipa...akafunga kirahisi...goli safiiii...
Tatizo nini Simba??, bao la mapema tofauti na matarajio yenu,? Au Mtoa roho Tambwe kuwatungua ...isije ikawa hasira tu maana dah hilo Goli limeuma watu balaaa
 
Hawa mikia wakiwakilisha nchi inaweza kutokea aibu has a matokeo yakiwa mabaya kwao wanaweza kung'oa viti vya ndege. Tahadhari kwa ndege zetu hahahaaa
 
taarifa gani unaweka ktk....mimi ni simba lakini taarifa haina mashiko
 
Aisee lile goli hata marefa wa ulaya ningewashida kujua kama c goli maana hata wale mabeki wawili waliokua wanamkaba tambwe hawajaona kama tabwe ameshika zaidi alieona kwa ufasaha ni kipa na ndo alinyoosha mkono haraka kuonyesha kwamba tambwe ameshika ule mpira!
 
Aisee lile goli hata marefa wa ulaya ningewashida kujua kama c goli maana hata wale mabeki wawili waliokua wanamkaba tambwe hawajaona kama tabwe ameshika zaidi alieona kwa ufasaha ni kipa na ndo alinyoosha mkono haraka kuonyesha kwamba tambwe ameshika ule mpira!
Mabeki waliona ndio maana walisimama
 
Sawa goli la Tambwe ni sahihi,je vp kuhusu goli la Ajibu?
mkuu tambua mpira ni mchezo wa makosa, probability ya kutokea kwa makosa ktk mechi yapo, Goli la Ajib lipo sahihi kwa mtazamo wangu ila ni makosa ya marefa kukataa na ni kawaida ktk soka
 
Jamaani naomba msaada kidogo mnijuze kam ni kweli taarif kama hii inatoka kwenye klabu ya ligi kuu
 
Walipe kwanza,kimoja tu wamang'oa viti!!!!!!!?????
 
No Offense. Ila hii barua ipo kama imeandikwa na BIG RESULT NOW vile.
 
Back
Top Bottom