Simba Sports Club achaneni na nia yenu ya kumfukuza kocha wetu Patrick Aussems kwani tutakuja kujuta na kulia akiondoka

Simba Sports Club achaneni na nia yenu ya kumfukuza kocha wetu Patrick Aussems kwani tutakuja kujuta na kulia akiondoka

Acha Kusema Vyanzo vya ndani na badala yake sema tu kwamba hii tetesi umeisikia katika ile ' Segment ' ya ' Chabo Chabo ' ya Sports Headquarters ya Efm ya leo.
Asubuhi sina muda wa kusikiliza radio,ila ndani ya simba kuna watu wangu wa karibu hapo kwahiyo baadhi ya mambo nayapata jikoni,nyie subilini redioni
 
Simba ilivurugwa na waswahili ila mzigo anataka kuangushiwa Patrick Aussems.

Ukiangalia kikosi cha simba 75% wako above 30 unategemea timu ya ushindani kwa hao veterans?

Timu imetwaa ubingwa unawaacha key players unaenda kukusanya lundo la average players na kuanza kutamba kwenye media kuwa utafanya vizuri ?

Hivi kweli Simba hawakumuona Bakary Nondo Mwamnyeto au Timothy Awany kama replacement ya Juuko Murshid badala yake wakaenda kuleta hiyo mizigo ya kibrazil na yule rasta wa Singida United ?

Hivi kweli Simba hawakumuona Allan Okello wa KCCA ya Uganda kama replacement ya Emanuel Okwi badala yake wanaenda kutuletea huyo mzee Deo Kanda na Wilker ?

Hivi Simba hawakumuona Tadeo Muwanga wa Vipers ya Uganda kama replacement ya Kotei badala yake wakaenda kutuletea Fraga asiye na uwezo wa kuhold hata mpira ?

Kama waliweza kumuona Kahata walishindwa kumuona Fred Kulembe kwenye mashindano ya Afcon kama back up ya chama na replacement ya Niyonzima?

Hivi walimsajili Ibrahim Ajib wa nini wakati hana matumizi na hana msaada wowote kwa timu kwanini wasingeweka pesa walau kwa Eliud Ambokile wa Mbeya city badala ya huyu jackal of all trades but master of none ?

Hivi Haruna Shamte na Gadiel waliwasajili wa nini wakati uwezo wao ni mdogo kwanini wasingeenda kubomoa fullback zote za Azam na kuzihamishia simba tu badala ya kuanza kuhangaika na hao wavuta bangi ?

Simba kama wanamfukuza Aussems basi watakuwa wametukosea sana sisi mashabiki wao.
Naunga mkono hoja
 
Aondoke zake hana adabu. Anaondoka kwenda kutafuta timu nyingine kihunihuni. Atuachie timu yetu. Wanakuja wenye weledi zaidi. Simba tuna pesa za Mo. Mtu akilete ujinga tunatimua tu.
Mkuu kumbe kipind kile alivyoondoka alienda kwenye mazungumzo na timu mpya???
 
Kocha kuondoka sio suluhisho kabsa, kiukweli usajili wetu haukufanywa kiweledi zaidi, mimi nachohisi itakuwa uongozi uliogopa gharama kubwa , labda kutokana na hii program ya ujenzi wa viwanja inaeza punguza ukubwa wa matumizi!! Tusubiri usajili ujao tuone nini watafanya , nategemea kuona damu changa zikiwa nyingi zaidi, vipaji maridhawa vikiwa vinatisha pale simba!! Ila ile mibrazil hapana kwakweli mimi bado sijapata ushawishi kabsaa
Wale wabrazil tumepigwa mkuu
 
Ausems ni bonge la kocha ila anatolewa tu kafara. Wakati wa usajili watu walitahadharisha hapa jamvini kuwa unapomuacha mchezaji kama Kotei, Okwi, Niyonzima unatakiwa ulete wachezaji wenye uwezo zaidi yao. Lakini viongozi walifanya walichojua wao matokeo yake wakaletwa wabrazili ambao uwezo wao ni wa kawaida sana halafu kufungwa na UD Songo, Mwadui na sare ya Prison zigo anaangushiwa Ausems.

Mo bila kuunda timu ya scounting ataendelewa kulishwa matango pori na watu wanomzunguka. Timu ya scounting inahitaji watu wanne au watano tu kutafuta vipaji ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania kwisha. Itaokoa gharama sana na dirisha la usajili likifunguliwa tayari unakuwa na wachezaji mkononi unawasainisha tu kutokana na mahitaji ya timu tena kwa gharama ndogo. Leo Simba na Yanga zinamgombania Bakari Nondo wa Coastal wakati kacheza ligi msimu uliopita. Kama kungekuwa na timu ya scounting kipaji chake kingeonekana mapema badala ya kusubiri kumuona kwenye timu ya taifa. Leo mshahara wa Wawa ukimpa nusu yake Nondo atakupa huduma iliyotukuka au nusu ya mshahara wa Deo Kanda ukampa Miraji Athumani nina hakika atafunga magoli mpaka kwa 'ugoko"

Uongozi na bodi nzima ya Simba ijitathimini yenyewe kwanza na kurekebisha usajili kwenye dirisha dogo badala ya kukimbilia kumtimua Ausems. Kwa Simba ya msimu uliopita ilihitaji tu nyongeza ya wachezaji wasiozidi wanne tu ingekuwa moto. Ilihitajika tu kipa, beki wa kati, kiungo mkabaji (mkata umeme wa ukweli) na mshambuliaji mwenye uwezo kama wa Kagere basi. Na viongozi walipaswa wajue kuwa falsafa ya Ausems ni kushambulia mwanzo mwisho kwa hiyo walihitajika walete watu wa kazi kweli kweli kuanzia mbele lakini badala yake wakaleta wachezaji wanaowajua wao halafu leo wanajitia kumtimua Ausems.

Kwangu mimi Ausems atabaki kuwa bonge la kocha kwani ukilinganisha matokeo anayoyapata mpaka sasa na kikosi kilichosajiliwa anajitahidi sana inabidi apongezwe sio kutimuliwa.
Hizi comments nataman Mo na bodi members wapite wasome mawazo yetu
 
Kocha aende zake, kimbinu anazidiwa na makocha wengi tu wa kitanzania. Kocha gani unafungwa nje ndani na timu kama Kagera Sugar, ina maana mechi ya kwanza hukujifunza.

Unacheza na Prison haijafungwa hata mechi moja, unashindwa kujua kwanini hawafungwi, mimi nafanyaje ili niwafunge.

Huyo kocha wenu is tactically inept, huwezi kumlinganisha na Leschante.

Hiyo timu mnayoidharau mkimpa kocha makini m'bongo tu itapiga mpira mkubwa sana. Huwa nasema hata akipewa dogo Matola Simba itakuwa moto tu maana anaujua mpira na ana mbinu za mpira.

Kuna wachezaji vijana wadogo kama akina Mlipili wanasugua benchi week in week out, unashindwa kuwapa mechi wakaanza kuwareplace akina Wawa na Nyoni.

Unafanya rotation ila top class goalkeeper Kakolanya anasugua benchi kila mechi, una mpango gani na keeper hodari kama Kakolanya ambae alicheza na Simba yote na hawakumfunga.

Get that coach out of Simba, as a matter of urgency!!
Mkuu una dharau prison na kagera sugar? Unafaham timu zinazocheza na simba uwa zinajiandaa na kukamia all 90mins?
 
Asubuhi sina muda wa kusikiliza radio,ila ndani ya simba kuna watu wangu wa karibu hapo kwahiyo baadhi ya mambo nayapata jikoni,nyie subilini redioni

Acha Upuuzi na katika Lugha adhimu ya Kiswahili hatuna neno ' Subilini ' kama ulivyoandikana neno sahihi ni ' Subirini ' sawa? Ungekuwa na tabia ya Kusikiliza Redio usingekuwa unakosea hivi na kuonekana ni wa hovyo hovyo.
 
Alifanya hivyo baada ya kumuona ni effective zaidi kwenye defence na attack tofauti na Mkude na Mzamiru ambao wote ni defence midfielders.

Kapombe anafanya vitu viwili kwa usahihi uwanjani lateral movement na vertical movements

Anauwezo mkubwa kwenye battle za one against one kuliko Mzamiru.

Passing accuracy yake iko juu kuliko Mzamiru au Ndemla ambao ndiyo walikuwa viungo wajuu baada ya Kotei kurudishwa kucheza kama defender.

Anaweza kuwin aerial duels zaidi kuliko Mzamiru kulingana na height yake.

Lechantre was right.
Sawa nazikubali sababu ulizoeleza zinazohalalisha Kapombe kuahamishwa namba na Lechantre. Lakini mimi binafsi sikubali falsafa ya kupaki basi. Simba ya Lechantre ilikuwa inaboa sana kuitazama kwani walikuwa wanacheza kujilinda muda wote haijalishi wanacheza taifa au mikoani, wanacheza na Yanga au Ndanda. Habari ya kwenda mpirani kuangalia square pass dakika tisini na kushuhudia kagoli kamoja sio kabisa. Mpira ni magoli mtu anapigwa tatu, nne au akikaa vibaya hata tano kabisa.
 
Ulipomtaja huyo Masoud Djuma Irambona ndiyo nimekuona ' Mpuuzi ' kabisa na kumbe huijui Simba SC na yaliyokuwa yakiendelea kati ya Wachezaji wa Simba SC na huyo Kocha wako ambayo kwa bahati mbaya siyo ya Kimaadili kwa Mimi kuweza Kuyaanika hapa ila Watu wa Mpira na Watoto wa Mjini tunayajua na ndiyo maana tulipiga Kelele zetu ili aondolewe mapema kabla hali haijawa mbaya na nashukuru Uongozi ulitusikia na ukaachana nae.
Gents kwenye post yangu #41 nimesema hii Simba hata ukimpa MATOLA atafanya vizuri sana maana 'dogo' yupo vizuri tactically.

Naona kama uongozi wa Simba wamenisikia inawezekana 'dogo' akaifundisha Simba.

Hapo ndipo utakapoona mpira unaopigwa na Simba. Anazijua vizuri sana timu za bongo na sio za bongo tu lakini huwa anafanyia research timu pinzani kabla ya mchezo na kujua yeye acheze vipi kukabiliana nao.

sio kocha wenu Aussems yeye alikuwa ana approach game kichwa kichwa bila kujua anacheza na timu ya namna gani.
 
Matola hana class B ya CAF unataka akafundishe club kubwa kama simba ?
Gents kwenye post yangu #41 nimesema hii Simba hata ukimpa MATOLA atafanya vizuri sana maana 'dogo' yupo vizuri tactically.

Naona kama uongozi wa Simba wamenisikia inawezekana 'dogo' akaifundisha Simba.

Hapo ndipo utakapoona mpira unaopigwa na Simba. Anazijua vizuri sana timu za bongo na sio za bongo tu lakini huwa anafanyia research timu pinzani kabla ya mchezo na kujua yeye acheze vipi kukabiliana nao.

sio kocha wenu Aussems yeye alikuwa ana approach game kichwa kichwa bila kujua anacheza na timu ya namna gani.
 
Kocha kafurushwa,haya sasa wale wa kuzira anzeni kutoa tamko.Hahahaa
 
Back
Top Bottom