Simba Sports Club (Wekundu wa Msimbazi) | Special thread
Ni wakati sasa timu zetu zikubali kuwa mpira wa sasa huwezi kushinda kwa kutegemea kamati ya ufundi.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Tanzania tuna laana jana yanga 2-0 leo simba nayo imefungwa 2-0 kwa mtazamo wangu cjui kama tutafika ..
 
Wale warwanda wamepiga pasi 75 wakati simba wakiwa wanautafta kwa tochi, walikua simba wanaombea walau penart1 ila ikawa refa yupo makini sana,. Pole mabingwa wa urafiki cup
 
walisema Chaka la Simba Nguruwe hawalali...asa
leo Nguruwe wamelala na kubinuka Salakasi
mchana kweupeee
 
Oooooh! Taifa kubwa haya ndo mambo gani sasa unafanya? I am angryyyyyyyyyyyyyyyyyyyyy!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
waganda waliizidi simba.Wangefunga hata matano

Mechi ya jana ingekuwa inahitaji mtu kufunga magoli mengi ili kuvuka kwenda hatua nyingine nafikiri jana Wale watoza ushuru wa Uganda ilikuwa watulipie kile kipigo cha penalt 3 na magoli mawili walichotupiga Simba,jamaa walikuwa better zaidi.
 
Mabingwa wa kombe la ujirani simba sports club, leo imetota kwa mabao 2-0
mbele ya watoza ushuru wa uganda (ura). Ni kilio kingine kwa mashabiki wa
simba na yanga..siku zote mwenzio akinyolewa nawe tia maji.:a s 465:

Nimejaribu kuzichambua timu zote mbili Yanga na Simba ktk mechi zao za ufunguzi ktk kombe la Kagama 2012 na huu ndio MTAZAMO wangu

YANGA

Haikuwa ktk kiwango kizuri kama timu, lakini bado kwa mchezaji mmoja mmoja walijitahidi. Imeonekana kubadilisha style ya mpira wake kutoka kukimbiza, ku-force na hivyo kutumia nguvu nyingi na kuinyima timu pinzani utulivu. Kwa mechi ya juzi, Yanga ilicheza mchezo wa taratibu na utulivu lakini Atletico waliivuruga kwa kucheza mpira wa pasi za uhakika na kasi. Na ilivyo ni kwamba Yanga imebadilisha zaidi ya nusu ya wachezaji wake kwenye kikosi cha kwanza cha msimu uliopita kwa hiyo bado "chemistry" baina yao haijachanganya.

Na hili lilionekana karibu na mwishoni wa mchezo ambapo wachezaji wa Yanga waliamua kila mtu kucheza kivyake kwa nguvu kubwa nadhani ili kuwafurahisha mashabiki lkn hali ilizidi kuwa mbaya.

Kitu kingine nilichokiona ni kwamba Yanga haikuwafahamu kabisa wapinzani wao, na hivyo haikufanyia mazoezi udhaifu wa Athletico. Na hii ni tatizo kubwa kwa timu zetu za Tanzania kwa kuingia kichwa kichwa ktk mashindano bila kufanya home works za nguvu hasa kwa timu zile zinazoonekana kutokuwa na majina makubwa.

Wasiwasi wangu ni kwamba, nafasi ya Yanga kuvuka nusu fainali inatia shaka ukizingatia upya wa kocha, upya wa kikosi na kutengeneza timu wakati mashindano yanaendelea hasa ukuzingatia kuwa timu nyingi za nje kama URA na APR zinaonekana ziko vizuri.. Lakini hakuna lisilowezekana.

SIMBA

Simba katika mechi yake ya kwanza imecheza vizuri lakini haijafikia ubora wake. Inaendelea na style yake ile ile ya kupitishia mashambulizi yake kupitia upande wa kushoto ambako kwa mechi ya jana ulikuwa ndio eneo dhaifu kuliko yote. Kasi na uwezo binafsi wa wachezaji Danny Mrwanda na Abdallah Juma haujafikia au haukuwa sawa na ubora wa Okwi.

Vile vile pamoja na kuwa na kikosi kilichokaa pamoja kwa muda lakini ingizo la wachezaji wapya zaidi ya 4 katika kikosi cha kwanza limeonekana kuiyumbisha timu kwa kiasi fulani hasa katika namna ya kushambulia ambako wachezaji wa Simba walikuwa wanakwenda kwa kasi tofauti na wakiwa ama mbali mbali sana ama wakati mwingine kujikuta wako pamoja wakigombania kufunga.

Kama ilivyo kwa Yanga, bado nao Simba walioonekana kutokuwa wamefanya homework za kutosha kwa wapinzani wao URA ambayo ina nidhamu kubwa ya kimchezo hasa kwenye ulinzi na ushambuliaji. Hawakuwa na tamaa ya kuishambulia Simba kwa nguvu hata pale Simba walipoonekana kupoteza mwelekeo badala yake walicheza kwa utulivu, kumiliki mpira na kuziba njia.

Kama nilivyosema hapo juu Simba bado wana kikosi kizuri na kinachoweza kushindana kama watarudi darasani kuyafanyia kazi makosa ya jana na kusoma wapinzani kabla ya mechi. Ni ngumu kutabiri chochote kwao lakni wanapaswa kujua hawana cha kujitetea maana wamecheza mechi nyingi za kujipima nguvu na wamekuwa na kocha kwa muda sasa.

Naomba kuwasilisha.
 
Nimejaribu kuzichambua timu zote mbili Yanga na Simba ktk mechi zao za ufunguzi ktk kombe la Kagama 2012 na huu ndio MTAZAMO wangu

YANGA

Haikuwa ktk kiwango kizuri kama timu, lakini bado kwa mchezaji mmoja mmoja walijitahidi. Imeonekana kubadilisha style ya mpira wake kutoka kukimbiza, ku-force na hivyo kutumia nguvu nyingi na kuinyima timu pinzani utulivu. Kwa mechi ya juzi, Yanga ilicheza mchezo wa taratibu na utulivu lakini Atletico waliivuruga kwa kucheza mpira wa pasi za uhakika na kasi. Na ilivyo ni kwamba Yanga imebadilisha zaidi ya nusu ya wachezaji wake kwenye kikosi cha kwanza cha msimu uliopita kwa hiyo bado "chemistry" baina yao haijachanganya.

Na hili lilionekana karibu na mwishoni wa mchezo ambapo wachezaji wa Yanga waliamua kila mtu kucheza kivyake kwa nguvu kubwa nadhani ili kuwafurahisha mashabiki lkn hali ilizidi kuwa mbaya.

Kitu kingine nilichokiona ni kwamba Yanga haikuwafahamu kabisa wapinzani wao, na hivyo haikufanyia mazoezi udhaifu wa Athletico. Na hii ni tatizo kubwa kwa timu zetu za Tanzania kwa kuingia kichwa kichwa ktk mashindano bila kufanya home works za nguvu hasa kwa timu zile zinazoonekana kutokuwa na majina makubwa.

Wasiwasi wangu ni kwamba, nafasi ya Yanga kuvuka nusu fainali inatia shaka ukizingatia upya wa kocha, upya wa kikosi na kutengeneza timu wakati mashindano yanaendelea hasa ukuzingatia kuwa timu nyingi za nje kama URA na APR zinaonekana ziko vizuri.. Lakini hakuna lisilowezekana.

SIMBA

Simba katika mechi yake ya kwanza imecheza vizuri lakini haijafikia ubora wake. Inaendelea na style yake ile ile ya kupitishia mashambulizi yake kupitia upande wa kushoto ambako kwa mechi ya jana ulikuwa ndio eneo dhaifu kuliko yote. Kasi na uwezo binafsi wa wachezaji Danny Mrwanda na Abdallah Juma haujafikia au haukuwa sawa na ubora wa Okwi.

Vile vile pamoja na kuwa na kikosi kilichokaa pamoja kwa muda lakini ingizo la wachezaji wapya zaidi ya 4 katika kikosi cha kwanza limeonekana kuiyumbisha timu kwa kiasi fulani hasa katika namna ya kushambulia ambako wachezaji wa Simba walikuwa wanakwenda kwa kasi tofauti na wakiwa ama mbali mbali sana ama wakati mwingine kujikuta wako pamoja wakigombania kufunga.

Kama ilivyo kwa Yanga, bado nao Simba walioonekana kutokuwa wamefanya homework za kutosha kwa wapinzani wao URA ambayo ina nidhamu kubwa ya kimchezo hasa kwenye ulinzi na ushambuliaji. Hawakuwa na tamaa ya kuishambulia Simba kwa nguvu hata pale Simba walipoonekana kupoteza mwelekeo badala yake walicheza kwa utulivu, kumiliki mpira na kuziba njia.

Kama nilivyosema hapo juu Simba bado wana kikosi kizuri na kinachoweza kushindana kama watarudi darasani kuyafanyia kazi makosa ya jana na kusoma wapinzani kabla ya mechi. Ni ngumu kutabiri chochote kwao lakni wanapaswa kujua hawana cha kujitetea maana wamecheza mechi nyingi za kujipima nguvu na wamekuwa na kocha kwa muda sasa.

Naomba kuwasilisha.
Watu kama nyie ndo mnatakiwa kuwa mnakuja mara kwa mara kwenye jukwaa la michezo, umejitahidi, analysis yako ni nzuri ingawa kuna watu watakupinga.
 
Back
Top Bottom