kiduku, kiduku...

hahaaaaaaaaaaaaa.... yanga kweli walimbwende
 
Asante sana kwa kazi unayoifanya ya kuandika habari za timu yangu kipenzi........
 
Wachezaji Simba wajazwa mamilioni

January 14, 2011




Timu ya Simba



Uongozi wa klabu ya Simba umewapa wachezaji wa timu hiyo fedha taslimu Sh. Milioni 10 kama motisha kutokana na ushindi wa 2-0 katika mechi wao wa fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya watani wao, Yanga iliyochezwa juzi kwenye uwanja wa Amaan visiwani hapa.
Kutokana na zawadi hiyo, wachezaji wa timu hiyo sasa watagawana jumla ya Sh. Milioni 15 ambazo ni pamoja na zawadi ya Sh. Milioni 5 walizopata kwa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo ya kila mwaka.
Akizungumza na NIPASHE jana, Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu' alisema kuwa wamefurahishwa na ushindi huo na wataendelea kuwapa motisha wachezaji katika kila mechi wanazocheza ili kuwaongezea ari.
Kaburu alisema kuwa wanawataka wachezaji wao wajitume katika mazoezi ili waweze kutetea vyema ubingwa wao na kufanya vizuri katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika.
"Tumefurahi sana, tumewapa Sh. Milioni 10 na zile za zawadi zilizotolewa sasa watagawana Sh. Milioni 15," alisema Kaburu.
Katika hatua nyingine, aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Ali Juma Shamhuna, ametangaza kuwapatia wachezaji wa Simba zawadi kutokana na ushindi walioupata.
Shamhuna anatarajiwa kuwaalika wachezaji wa Simba nyumbani kwake kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam na anawatakia wakafanye vizuri katika mashindano ya kimataifa.
Mechi hiyo ya watani wa jadi ilivunja rekodi ya mapato katika uwanja wa Amaan baada ya kuingiza Sh. Milioni 27.8. Mapato hayo ni zaidi ya jumla ya mapato ya mechi mbili za nusu fainali zilizozikutanisha timu hizo kubwa nchini dhidi ya Zanzibar Ocean View na Mtibwa ya Morogoro. Mechi ya nusu fainali baina ya Simba dhidi ya Zanzibar Ocean View iliingiza Sh. Milioni 11, wakati iliyoikutanisha Yanga dhidi ya waliokuwa mabingwa watetezi, Mtibwa iliingiza Sh. Milioni 10.
Wakati huo huo, mfungaji wa Simba, Mussa Hassan ‘Mgosi', amesema kuwa kipigo walichoipa Yanga juzi ni salamu za rasharasha na kwamba mvua kamili wataipata katika mechi yao ya marudiano ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara itakayofanyika Machi 5 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mgosi ambaye alifunga goli la kwanza katika dakika ya 33 alisema kuwa wamefurahi kushinda mchezo huo na umewasaidia kuwaimarisha kuelekea katika hatua la lala salama ya ligi ya bara.
Alisema kuwa kila mchezaji amepanga kuonyesha uwezo wa juu katika mechi za ligi na vile vile kuhakikisha wanashinda pia mechi zao za michuano ya kimataifa.
"Tunashukuru Mungu tumeshinda, ni dalili njema kuwa na ligi itakuwa furaha upande wetu," alisema Mgosi ambaye aliachwa katika kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars, kutokana na kuwa majeruhi.
Aliongeza kuwa mafanikio na ushindi wa timu yao katika mechi mbalimbali walizocheza yametokana na jitihada wanazozionyesha mazoezini na wanaamini kwamba hali ikiendelea hivyo, hakuna timu itakayoweza kuwavua ubingwa wa ligi ya bara.
"Kila mchezaji Simba anauwezo wa kufanya vizuri, tunajivunia hali hii na wala hatuoni kama tumepungukiwa, tutaendelea kujiimarisha ili tuweze kuiwakilisha nchi vizuri katika mashindano ya kimataifa mwaka huu," aliongeza Mgosi aliyejiunga na Simba mwaka 2005 akitokea Mtibwa Sugar ya Manungu mkoani Morogoro.
Mwaka huu Simba itaiwakilisha nchi katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika kwa kuanza na klabu ya Elan de Mitsoudje ya Comoro na vile vile mwezi Mei itaiwakilisha Bara katika mashindano ya Kombe la Kagame yatakayofanyika visiwani hapa mwezi Mei.
Katika mchezo wa jana, Simba iliwakosa nyota wake watano ambao walikuwa katika timu ya taifa ambao ni pamoja na Juma Kaseja, Rashid Gumbo, Kevin Yondani, Juma Nyoso, Ali Shiboli huku Okwi Emmanule akiwa mgonjwa na Joseph Owino akiwa kwao Uganda akimalizia mitihani yake.
Yanga nao iliwakosa nyota wake sita walioko Stars ambao ni Nadir Haroub 'Cannavaro', Jerry Tegete, Shadrack Nsajigwa, Stephano Mwasika, Nurdin Bakari na aliyekuwa nahodha wao, Abdi Kassim ‘Babi' ambaye tayari ameuzwa katika klabu mpya ya Dom Tang Long ya Vietnam.



CHANZO: NIPASHE
 
Mzunguko huu Ligi Kuu ulete mafanikio Send to a friend Saturday, 15 January 2011 09:00 0diggsdigg

Kocha wa timu ya simba,Patrick Phiri.

BAADA ya miezi ya mapumziko mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaanza kutimua vumbi leo katika viwanja vinne tofauti nchini nzima.

Kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga timu ya Azam itaikaribisha Kagera Sugar, wakati kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, Toto African itaikaribisha Polisi Dodoma.

Pambano lingine litakuwa kwenye uwanja wa Majimaji mkoani Ruvuma ambapo timu ya Majimaji itaikaribisha JKT Ruvu Stars na kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha, AFC itaikaribisha African Lyon.

Timu za Simba na Yanga na Mtibwa zitaanza mzunguko wa pili wiki ijayo kwa Simba kucheza na Azam, Mtibwa Sugar na Polisi Dodoma na Yanga itacheza na AFC.

Mpaka mzunguko wa kwanza unamalizika, timu ya Simba ndiyo inayoongoza Ligi Kuu ikiwa na pointi 27 wakati timu ya AFC inashika mkia ikiwa na pointi tano.

Ni takribani miezi miwili imepita tangu mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu umalizike na ligi kusimama kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa mwaka na mashindano ya kimataifa.

Tunatarajia timu zinazoshiriki Ligi Kuu zilitumia muda wa mapumziko vizuri kujiandaa kwa ajili ya mzunguko wa pili ambao unatarajiwa kumalizika April 10, 2011.

Pia, tunatarajia kushuhudia ushindani mkubwa wa timu katika mzunguko huu tofauti na tuliouona katika mzunguko wa kwanza ili kuweza kupata timu bingwa inayostahili na kupata timu zinazostahili kushuka daraja.

Tunatarajia kuona wachezaji wakionyesha vipaji vyao na kushirikiana katika timu pamoja na nidhamu ya juu kwa wachezaji, tunatarajia kuona maamuzi sahihi ya waamuzi, Tunatarajia kuona uongozi bora wa ligi hiyo kutoka TFF, tunatarajia kupata timu bora zitakazotuwakilisha katika mashindano ya kimataifa na tunatarajia mashabiki wengi watakuwa wakijitokeza kushuhudia mechi hizo.
 
Simba kusaka tiketi ya Brazil leo Send to a friend Wednesday, 19 January 2011 21:27

Clara Alphonce
SIMBA inashuka dimbani leo kucheza mchezo wa kirafiki na Atletico Paranaense ya Brazil, mchezio utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa huku ikimjaribu mchezaji wake raia wa Cameroon, Eke Cosmas.

Mchezaji huyo ambaye ni kiungo amekuja katika klabu hiyo kwa ajili ya kujaribiwa na katika mechi ya leo atakuwa ni mmoja wa wachezaji wanaotaraji kuongoza Simba kwenye mchezo huo.

Afisa Habari wa Simba, Clifford Ndimbo alisema jana kuwa mchezaji huyo yuko katika majaribio kwani alitua nchini wiki iliyopita na endapo atafaulu majaribio hayo watabaki naye mpaka kwenye usajili wa msimu ujao.

Endapo Cosmas atafuzu majaribio yake, atawaweka mashakani wachezaji viungo wawili wa kimataifa ambao ni Hilal Echessa, Jerry Santo pamoja na mkongwe, Mohamed Banka.

Simba inaingia dimbani leo ikiwa na mawazo ya kwenda Brazil kwa ajili ya kuweka kambi baada ya Mkurungezi wa timu ya African Lyon, Rahma Kharoos ambaye ndio aliyeileta timu hiyo kutoka Brazil kuiahidi Simba kuipeleka nchini humo lakini endapo tu, itashinda mchezo wa leo.

Hata hivyo, mechi ya leo itakuwa na hamasa kubwa baada ya mkurugenzi huyo kuruhusu mashabiki kuingie bure baada ya kuona viti vikiwa tupu katika mchezo dhidi ya Yanga juzi kutokana viingilio walivyoweka kuwa vikubwa.

Meneja wa Simba, Innocent Njovu alisema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na mpaka sasa wachezaji majeruhi katika timu ya Simba ni Uhuru Seleman na Emmanuel Okwi.

Alisema huenda kocha wao Patrick Phiri akawatumia wachezaji waliokuwepo katika timu ya taifa nchini Misri waliojiunga na wenzao jana au asiwatumie na kuwachezesha wale waliokuwepo.

Katika hatua nyingine, klabu ya Yanga imelalamikia maamuzi ya mratibu wa ziara ya Wabrazil hao, Rahma kuwa haikuwatendea haki kwa kuruhusu mashabiki kuingia bure kwenye mechi ya Simba wakati wao walicheza viti vikiwa wazi.

Yanga ilipambana na Wabrazil hao na kufungwa mabao 3-2 kwenye uwanja huo, katika mechi iliyokuwa na mashabiki kiduchu kabla ya mratibu huyo kutoa ofa kwa Simba kwa mashabiki wake kuingia bure na endapo itashinda, Simba itakwenda Brazil.
source:mwananchi
 
Simba kuwafuata Wacomoro Jan. 26

WAWAKILISHI wa Tanzania katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba ya jijini Dar es Salaam wanatarajiwa kuondoka nchini Januari 26 kwenda nchini Comoro kwa ajili ya mechi yao ya kwanza dhidi ya Elan de ya huko.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jana, kikosi cha Simba kilitarajiwa kuingia kambini rasmi jana jioni katika Hoteli ya Lamada iliyopo jijini Dar es Salaam tayari kujiweka sawa na michuano hiyo na ile ya Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara.
Simba imekuwa katika maandalizi ya michuano hiyo tangu mwishoni mwa mwaka jana, ilipokwenda kuweka kambi visiwani Zanzibar, sambamba na kucheza mechi kadhaa za kirafiki na timu za ndani na nje ya nchi.
Aidha, katika maandalizi yake, Simba ilishiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani humo iliyofikia tamati Januari 12 na kufanikiwa kutwaa ubingwa baada ya kuwafunga mahasimu wao wa jadi, Yanga kwa mabao 2-0.
Mabingwa hao wa Bara, iwapo watawatoa Wacomoro hao watakutana na vigogo vya soka barani Afrika, TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Katika hatua nyingine, Simba leo inatarajiwa kushuka katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kucheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya timu inayodaiwa kuchakachuliwa ya vijana wanaodaiwa kuwa ni U-20 wa Atletico Paranaense ya nchini Brazil.
 
Eti Simba wakishinda wanapewa offer ya kwenda kutrain Brazil for two weeks, hawa jamaa wajanja sana maana wanajua ushindi kwa Simba ni ndoto
 
Eti Simba wakishinda wanapewa offer ya kwenda kutrain Brazil for two weeks, hawa jamaa wajanja sana maana wanajua ushindi kwa Simba ni ndoto

umegundua hii janja ya nyani eeh?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…