Simba Sports Club (Wekundu wa Msimbazi) | Special thread
Tatizo lako umezidi kuongea kiushabiki zaidi, hupendi kujadili soka kwa ukweli. Una ushabiki usiojali ukweli.
Wadau wazuri wa soka hawako hivyo.
Mimi tangu jana nilikwambia Simba wataponzwa na maandalizi duni hukutaka kuelewa, umejionea sasa!
Mtasingizia uzembe wa kipa na mabeki, lakin wale sio kwamba walipenda kuwa wazembe, hawakupata maandalizi mazuri ya kutosha.
Maandalizi yangekuwepo tusingekuwa hivi, lakin kwa vile wewe mbishi endelea tu.
Na hata hapa Dar mnaweza mkafungwa vile vile
sio kwamba naongea kiushabiki zaidi ,but kiukweli TP MAZEMBE sio timu ndogo inaogopeka hadi huko brazil..
but sisi tuna goli moja la ugenini kwa hiyo tunataka kuwapiga mbili bila tu na hii inawezekana kwa sababu SIMBA ni zaidi ay uijuavyo ndugu yangu
 
sio kwamba naongea kiushabiki zaidi ,but kiukweli TP MAZEMBE sio timu ndogo inaogopeka hadi huko brazil..but sisi tuna goli moja la ugenini kwa hiyo tunataka kuwapiga mbili bila tu na hii inawezekana kwa sababu SIMBA ni zaidi ay uijuavyo ndugu yangu

Hapo kwenye blue sasa ndo umeongea kama mdau halisi wa soka. Hapo kwenye pink umeongea kitu ambacho kweli kinawezekana. Ila mwishoni kwenye red ndo tatizo la mashabiki wengi wa soka hapa bongo, wazuri sana kwenye majigambo.
Nadhani unawakumbuka Enyimba FC ya Nigeria ambao walikuwa mabingwa mara mbili kama hawa TP Mazembe. Waliwafunga kwao 4 - 1 mkasema Dar inawezekana mkawapiga 3 - 0, matokeo yake hizo 3 zikawageukia nyie mkaondolewa jumla ya 7 - 2.
Ndugu unatakiwa ufahamu kwamba tunapoongelea international games tusiwe tunatambiana kama vile zinacheza Simba na Yanga. Tujifunze kuongea points ambazo zitasaidia kukuza soka letu na sisi tufikie kama walipofika Mazembe. Haya ya kusema SIMBA NI ZAIDI YA UIJUAVYO hayana msingi, hayajengi kitu, hayasaidii kuimarisha soka la Simba wala Tanzania.
Tubadilike, la sivyo tutegemee vichapo kwa timu zetu kila siku. Wale TP Mazembe bado wanapewa nafasi kubwa ya kuifunga Simba tena hata wakichezea hapa hapa Dar
 
Hapo kwenye blue sasa ndo umeongea kama mdau halisi wa soka. Hapo kwenye pink umeongea kitu ambacho kweli kinawezekana. Ila mwishoni kwenye red ndo tatizo la mashabiki wengi wa soka hapa bongo, wazuri sana kwenye majigambo.
Nadhani unawakumbuka Enyimba FC ya Nigeria ambao walikuwa mabingwa mara mbili kama hawa TP Mazembe. Waliwafunga kwao 4 - 1 mkasema Dar inawezekana mkawapiga 3 - 0, matokeo yake hizo 3 zikawageukia nyie mkaondolewa jumla ya 7 - 2.
Ndugu unatakiwa ufahamu kwamba tunapoongelea international games tusiwe tunatambiana kama vile zinacheza Simba na Yanga. Tujifunze kuongea points ambazo zitasaidia kukuza soka letu na sisi tufikie kama walipofika Mazembe. Haya ya kusema SIMBA NI ZAIDI YA UIJUAVYO hayana msingi, hayajengi kitu, hayasaidii kuimarisha soka la Simba wala Tanzania.
Tubadilike, la sivyo tutegemee vichapo kwa timu zetu kila siku. Wale TP Mazembe bado wanapewa nafasi kubwa ya kuifunga Simba tena hata wakichezea hapa hapa Dar

wewe ndugu yangu kwanza ni timu gani
 
wewe ndugu yangu kwanza ni timu gani

Mkuu Ivuga
Mimi hata nikisema nashabikia mpinzani mkubwa wa Simba ktk soka la Tanzania, yaani Yanga bado si kitu.
Yanga wametolewa kizembe sana, kijinga mno. Lakin nao sio kwamba wamependa, bali maandalizi yao pia yalikuwa ZERO.
Unajua ndugu yangu mimi nimechoka sana kuona kila mwaka tunaingia international games tukiwa MAHUTUTI.
Tuna soka la kujipa matumaini na kuongea sana mdomoni kuliko kujiandaa kitaalamu. Wakati mwingine tunafanya hata yale mambo ya giza ili kupata ushindi. Katika hali hii kweli tunategemea kufika kokote jamani, hata kama itokee Simba wameitoa TP Mazembe?? Huko mbele kuna Kano Pillars ya Nigeria, kuna Esperence ya Tunisia . . . . au tunataka tuwatoe Mazembe tu basi, tuanze kuwaringishia Yanga kwamba tumetoa mabingwa wa afrika na namba mbili wa dunia???
Utajisikiaje kama siku moja Simba au Yanga wachukue ubingwa na afrika wakapata nafasi ya kucheza na Barcelona, Man utd, Real Madrid, AC Milan, Liverpool n.k.???? Huoni hayo ndio yatakuwa maujiko ya kweli???
Tulipanue basi soka letu lisikike mpaka kule Brazil akina Sao Paolo na wenzake waanze kubabaika wakisikia jina la Simba au Yanga.
Tufanye maandalizi, tujenge Football schools za watoto, tuwape lishe za uhakika, tuwatunze halafu tuone kama hao akina Mazembe watatusumbua tena, hata wakija mara 6 mfululizo kama tuna viwango na utaalamu wa uhakika, wala hatuna wasiwasi, tunawachezesha kiduku tu. Lakin saa hizi wao ndo wanatuchezesha ikibinda nkoi, ndombolo ya solo, nzawisa, na inde monii
 
mkuu CPU umeongea maneno yenye nguv sana ..... Nitarudi badae kidogo.
 
Simba yaanza vibaya Send to a friend Sunday, 20 March 2011 20:55 0diggsdigg


ochan%20mazembe.jpg
Kiungo wa Simba, Patrick Ochan akichanja mbuga jana kwenye Uwanja wa Kenya katika mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika. TP Mazembe ilishinda mabao 3-1. Picha/Majuto Omary

Majuto Omari, Lubumbushi
MABINGWA wa Tanzania, Simba wameanza vibaya kampeni yao ya kusaka kufuzu kuingia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka TP Mazembe.
Vigogo hao wa Afrika walifanikiwa kupata mabao ya mapema kupitia kwa Patou Kabangu, Amia Ekanga na Alain Kaluyituka Dioko kabla ya mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi kuifungia Simba bao pekee kwa mkwaju wa penalti.

Mazembe wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani walifanikiwa kupata bao la kuongoza dakika 11, kupitia kwa Patou Kabangu kabla ya Ekanga kupachika bao la pili katika dakika ya 27 kwa shuti la mbali lililomshinda kipa Juma Kaseja na kujaa wavuni na kuwafanya mabingwa hao wa Afrika kwenda mapumziko wakiwa mbele 2-0.

Simba ilianza kipindi cha pili kwa kasi na kufanya mashambulizi kadhaa katika dakika ya 59, 62 hata hivyo washambuliaji wake Emmanuel Okwi, Mbwana Samatta na Mussa Mgosi hawakuwa makini kwenye umaliziaji.

Mabeki wa Simba waliokuwa makini kwa muda wote kumlinda Kaluyituka walijisahau na kumwacha nyota huyo wa Congo kuipatia Mazembe bao la tatu katika dakika ya 70, baada ya kupokea pasi ya Ekanga, ambapo kabla ya kufunga alimlamba chenga Haruna Shamte na kupiga kulia kwa kipa Juma Kaseja na kuamsha shangwe kubwa kwa mashabiki waliokuwa wamefurika uwanjani.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Okwi aliifungia Simba bao la kufutia machozi dakika ya 76 kwa mkwaju wa penalti baada ya kipa wa Mazembe, Robert Kidiaba kumuangusha kwenye eneo la hatari na mwamuzi kuamuru ipigwe penalti ambayo ilifungwa na Emmanuel Okwi mwenyewe.

Zikiwa zimebaki dakika tisa mpira kumalizika, Kaseja alifanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na Kaluyituka aliyeunganisha vizuri kona ya Rainford Kalaba ambaye alikuwa akiisumbua ngome ya Simba.

Akizungumzia mchezo huo kocha wa Simba, Patrick Phiri alifurahi jinsi wachezaji wake walivyoweza kujituma na kupata bao moja ugenini ambapo alisema ni matokeo mazuri.

"Mabao mawili ya kwanza ni makosa ya kiuchezaji, hauwezi kumlaumu mtu, tunasubiri nyumbani, tumegundua uzuri wao na sisi tutahakikisha tunashinda na kusonga mbele,"alisema Phiri.Alisema,"Mazembe siyo timu ya kutisha sana kama unavyoisikia, umeona jinsi tulivyoshambulia, naamini tukiwa nyumbani tutafanya vizuri zaidi," alimaliza Phiri kwa matumaini makubwa.

Simba iliingia raundi ya pili ya mashindano hayo ya klabu bingwa barani Afrika baada ya kuichapa Elan de Mitsoudje ya Comoro mabao 4-2.

Kikosi cha Simba
Juma Kaseja, Haruna Shamte, Amir Maftar, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, Jerry Santo, Amri Kiemba, Patrick Ochan, Emmanuel Okwi, Mbwana Samatta na Mussa Mgosi.
Akiba
Ally Mustapha, Juma Jabu, Meshack Abel, Ally Shiboli, Nico Nyagawa, Rashid Gumbo, Shika Mkina.
 
Wajipa matumaini kwa Simba kuitoa TP Mazembe Send to a friend Monday, 21 March 2011 20:24 0diggsdigg


phirisimba.jpg
Kocha wa Simba Patrick Phiri

Waandishi Wetu
BAO la mkwaju wa penalti lililofungwa na mshambuliaji Emmanuel Okwi limewapa matumaini wadau wa soka nchini kiasi cha kuanza kuamini Simba inaweza kuwafungasha virago mabingwa wa Afrika, TP Mazembe kwenye mchezo wa marudiano mwezi ujao.

Mabingwa hao wa Afrika walipata ushindi wa mabao 3-1 kwenye mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliochezwa mjini Lubumbashi DR Congo juzi.

Wakizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana wadau hao walieleza hisia na ushauri wao kwa Simba kama inataka kutimiza azma hiyo.

Beki wa zamani wa Yanga, Willy Martin 'Gari Kubwa' amemtaka kocha Patrick Phiri kuifanyia marekebisho safu yake ya ulinzi kabla ya mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo.

"Sababu kubwa iliyofanya Simba kufungwa mabao 3-1 kwenye mchezo huo ni safu yake ya ulinzi kujisahau na kutoa mwanya kwa wapinzani wao kupata mabao mawili ya haraka.

"Kukosa umakini na kuzubaa kwa safu ya ulinzi ya Simba ndiko kulikosababisha timu hiyo kufungwa mabao ya haraka," alisema Martin.

"Nafikiri kwa sasa inamlazimu mwalimu (Phiri) kuifanyia marekebisho safu hiyo kabla ya mchezo wa marudiano kwa siku hizi chache zilizosalia," aliongeza.

Mshambuliaji na nahodha msaidizi wa Simba, Mussa Hassan Mgosi aliwatoa hofu wapenzi wa soka nchini na kusema kuwa Mazembe ni timu rahisi tofauti na walivyowachukulia awali.

Alikiambia kituo kimoja cha redio jana kuwa uwezo wa kuwafunga mabao Mazembe mabao 2-0 kwenye mchezo wa marudiano wiki mbili upo."Hatimaye tumewaona Mazembe ni wa kawaida sana tofauti na nilivyowachukulia mwanzo kabla ya kukuatana nao, uwezo wa kuwafunga hata mabao 2-0 tunao," alisema Mgosi.

"Mwanzoni ni sisi tulijichanganya kwenye ulinzi, lakini nawahakikishia Watanzania kwamba mchezo wa marudiano lazima waondoke na mabao si chini ya mawili," alisisitiza Mgosi ambaye alikuwa nahodha katika mchezo huo.

Naye Okwi aliyefunga bao hilo la kufutia machozi alisema kufungwa kwao kulitokana na wapinzani wao kuwazidi uzoefu pamoja na kutumia vyema nafasi walizopata.

Alisema wapinzani wao walitumia nafasi walizopata na kufunga mabao na ndio sababu walipata idadi hiyo ya magoli na kuongeza kuwa pia uzoefu wa kucheza miche zo mingi ya kimataifa imechangia ushindi huo.

Alisema kiujumla mchezo huo ulikuwa mgumu na wenye ushindani mkubwa kufuatia wapinzani wao kuwa nyumbani, lakini akaongeza kuwa Mazembe ni timu ya kawaida na yenye kucheza mpira wa kawaida.

"Ukweli wenzetu walijipanga zaidi na walitumia nafasi ndogo walizopata katika kuhakikisha wanashinda,tulijitahidi kadri ya uwezo wetu kwani tulifahamu fika tunacheza na timu gani, wao wana uzoefu mkubwa wa kucheza mechi nyingi za kimataifa kitu ambacho kimechangia ushindi huo,"alisema Okwi.

Aidha, Okwi alisema bado wana nafasi nzuri ya kusonga mbele endapo watatumia vyema uwanja wao wa nyumbani na kuhakikisha wanashikamana na kushinda na kuahidi kuwa watajipanga kitimu zaidi ili kushinda mchezo wa marudiano.

Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage ambaye aliongoza msafara wa kwenda Lubumbashi alisema Mazembe si timu ya kutisha sana kama inavyopewa sifa na wameikuta tofauti na sifa zinazotajwa.

Alisema kuwa timu yake (Simba) ina uwezo mkubwa wa kushinda kwa mabao tena zaidi ya mawili katika mchezo wa marudiano.

Alisema kuwa wamefungwa mchezo wa awali kutokana na makosa ambayo wachezaji waliyafanya hasa upande wa mabeki zaidi katika kipindi cha kwanza.Mechi haikuwa ngumu sana na hata matokeo hayafanani na jinsi tulivyocheza, tunaamini kuwa mchezo wa pili ambao tutautumia uwanja wa nyumbani, tutafanya vyema,î alisema Rage.

ìHata wao wameshangaa na hasa mchezo wa kipindi cha pili, tuliwabana sana na kupata bao muhimu kwetu, tunaamini tutafanya vyema, alisema.Katibu Mkuu wa Yanga, Celestine Mwesingwa alisema jana kuwa Simba ni klabu ya Tanzania hivyo matokeo mabaya ni ya Watanzania wote.

"Tumesikitishwa na kipigo cha watani zetu hasa ukizingatia kule walikuwa wanawakilisha taifa, ushauri wangu ni kwamba wajiande mapema kwa mechi ya marudiano.

"Jambo la kushukuru ni kwamba walipata bao moja ugenini, hivyo kitu muhimu ni wafanye maandalizi ya uhakika tena mapema badala ya kujisahau na kuona nyumbani itakuwa mechi rahisi halafu matokeo yake wakafungwa tena,"alisema Mwesingwa.

Alisema kuwa kiuhalisia TP ni timu bora, lakini mbinu inayoweza kuisaidia Simba na hatimaye kushinda mchezo wa marudio ni wachezaji kujituma kwa nguvu, akili zao zote.

*Calvin Kiwia, Sosthenes Nyoni,Jessca Nangawe na Majuto Omary, Lubumbashi
 
TP Mazembe: Simba imetushika pabaya
6219.jpg
Kikosi cha timu ya TP Mazembe kilichoiangamiza timu ya SimbaMICHAEL MOMBURI
SIMBA imewashika pabaya TP Mazembe. Mabingwa hao watetezi wa Afrika wamekiri kuwa bao la Emanuel Okwi hawakulitarajia na limewavurugia mahesabu.

Mazembe ilishinda mabao 3-1 dhidi ya Simba Jumapili iliyopita mjini Lubumbashi kwenye Uwanja wa Kenya ambapo timu hizo zitarudiana Aprili 2 jijini Dar es Salaam huku Simba ikihitaji kushinda mabao 2-0.

Msemaji wa Mazembe, Jean Sidwe aliiambia Mwanaspoti jana Jumatatu kutoka Lubumbashi kwamba Simba iliwabana sana na hawakutarajia.

�Simba ilicheza mpira sana muda wote, sema sisi tulifanya makosa ya kizembe kuruhusu bao moja, tumewapa faida na kufanya mchezo wa marudiano kuwa mgumu kwetu huko Dar es Salaam,�alisema Sidwe.

�Tulitakiwa kushinda mabao mengi zaidi ya hayo tuliyopata halafu tusiruhusu goli ili mambo yawe rahisi na tulikuwa tunaweza kufanya hivyo, lakini mpira ndivyo ulivyo inabidi kujipanga sana kwa mechi ya marudiano.�

�Simba wameonyesha kiwango cha juu, lolote linaweza kutokea kwenye mchezo wa marudiano, lakini tutajipanga vizuri tunajua cha kufanya na tumewaona, Simba vizuri,�alisisitiza.

Rais wa Mazembe, Moise Katumbi amewaambia wachezaji kwamba; �Tunahitaji kupambana kufa na kupona kama tunataka kombe hilo kwa mara nyingine.�

Kocha wa Mazembe, Lamine Nd�iaye amekiambia kituo kimoja cha redio mjini Lubumbashi kwamba mchezo wa Simba ni wa kasi lakini wachezaji wake wana uwezo wa kuwakabili na kusonga mbele.

JERRY SANTO
�Mazembe ni wazuri kwenye kucheza krosi lakini katika hawatishi sana, ndio maana uliona tulikuwa tunawamudu na tulisukuma mashambulizi, ni timu ambayo inafungika kabisa na tunaweza kufanya hivyo hapa Dar es Salaam.

�Tunachopaswa kufanya ni kuongeza umakini kila idara na kucheza kwa malengo, tunawaweza,�alisisitiza kiungo huyo, Mkenya wa Simba jana Jumatatu.

PATRICK KATALAY
Mshambuliaji huyo mpya wa DC Motema Pembe, alisema ;

�Nimesikitika sana kusikia Simba imefungwa mabao 3-1,
niliwaambia mapema kwamba dakika 20 za kwanza Mazembe watakuja kwa kasi, wawazuie. Kilichotokea ndiyo kile kile Patou Kabangu na Ekanga wamefunga magoli mawili ndani ya dakika 21.�

�Naamini Simba inaweza kuifunga Mazembe mabao 2-0 hapo Dar es Salaam, wakomae sana kwenye ulinzi na kujiamini, Simba wakiwa Dar es Salaam wanakuwa wakali sana naamini wataweza kuwatoa. Wawe makini ndani na nje ya uwanja kuanzia leo hii.�

Uongozi wa Simba ulisema kuwa matokeo ya uwanjani si ya kutisha na walicheza vizuri na kwamba wanachofanya sasa ni kupanga mikakati ya mchezo wa marudiano.
 
Okwi: Tutawamaliza Mazembe
6222.jpg
Mfungaji wa bao Simba dhidi ya TP Mazembe Emmanuel OkwMICHAEL MOMBURI
MFUNGAJI wa bao pekee la Simba dhidi ya TP Mazembe mjini Lubumbashi, Emmanuel Okwi amewaambia mashabiki wa timu hiyo; �Msiogope TP Mazembe wataondoka tu.� Simba ilifungwa mabao 3-1.

Okwi, ambaye aliwasili na kikosi cha Simba jijini Dar es Salaam saa sita usiku wa kuamkia jana Jumatatu, aliondoka tena jana mchana kwenda Uganda kujiunga na timu ya Taifa inayocheza na Guinea Bissau, Jumamosi ijayo ugenini.

Simba inahitaji kushinda mabao 2-0 jijini Dar es Salaam ili kusonga mbele, mabao ambayo Okwi anaamini kwamba yatapatikana lakini watahitaji kuweka ukuta wa chuma kwenye mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika itakayochezwa April 2, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

�Nimegundua Mazembe wametuzidi uzoefu tu, si timu ya kutisha kama inavyoelezwa ila ni wazuri sana pembeni, wanatumia mawinga na kusababisha madhara ndio maana hata ukiangalia bao zao zimetokea huko pembeni,�alisema Okwi, ambaye alijiunga na Simba akitokea Villa ya Uganda.

�Tuliwashtukia ndio maana tukawadhibiti kipindi cha pili, lakini naamini kwamba ndoto yangu ya kuwaondoa kwenye mashindano itatimia, tunachotakiwa ni kutoruhusu bao lolote Dar es Salaam na tuwafunge hayo mawili hata zaidi.

�Tunaweza, tutafanya kazi kubwa na naomba mashabiki wawe nyuma yetu kila sekunde tutawafunga Mazembe, wasitukatishe tamaa watusapoti kwa nguvu zote kuanzia maandalizi mpaka siku ya mchezo.�

�Akili ya kila mchezaji ni ushindi na tuko kwenye uwanja wetu wa nyumbani tuna kila sababu, tuungane tufanye kazi.

Yanga watuunge mkono kwani Simba ni timu ya Tanzania, kuisapoti Mazembe hakuwasaidii na hata wakitugeuka sisi tutacheza soka uwanjani tutawalazimisha watukubali.

�Naamini makelele ya wapinzani uwanjani hayasaidii, kinachotakiwa ni umakini wetu wachezaji uwanjani ndani ya dakika 90, tunajua tunachotakiwa kufanya na mashabiki wanataka nini.�
 
Wakuu hebu tupeni matarajio ya gemu na kagera sugar kesho....tutashinda?? Phiri amerudi??.....Mungu ibariki SIMBA
 
Half time Simba 0 na Kagera Sugar 0.....
wanabana tu lakini wataachia.......
 
Back
Top Bottom