Simba tuache kulialia. Kanuni ya mpira ni kushinda mechi zako


Kwamba pts za Yanga kule dhidi ya Geita ilikua halali? Utakua una matatizo. Kama Yanga ni bora ipate kweli kwa kuonesha uwezo halali na siyo janja ya bahasha( tiGO pesa, maneno ya mashabiki wao wenyewe)
 
Hakuna timu mbovu mzee Komaeni na uongozi wenu.
Management ikipuyanga huku Chini wanaungua
 
Kwamba pts za Yanga kule dhidi ya Geita ilikua halali? Utakua una matatizo. Kama Yanga ni bora ipate kweli kwa kuonesha uwezo halali na siyo janja ya bahasha( tiGO pesa, maneno ya mashabiki wao wenyewe)
Hizi bahasha ni zipi? si muwe mnaleta ushahidi hapa ?

Cha muhimu we shinda mechi zako sio unaboronga alafu unategemea timu nyingine zikupambanie!!
 
Na wewe screenshot hii msg yangu, Simba anachukua ubingwa NBC Pr Lg this season, mark my words
Labda kwa kuliiba ila kwa matokeo ya uwanjani hawezi abadani.
 
Ukweli ndio huu, timu ambayo wapinzani wako wanachukua pointi tatu, halafu wewe ukikutana nayo unaondoka na pointi moja ya kuipigania inabidi kujitafakari sana..

Hii ligi yetu tunakimbizana sana, ukishindwa kuchukua pointi tatu kwa timu za kawaida, basi lazima uwe na uwezo wa kuzichukua tatu kwa Yanga na Azam, kinyume na hapo, kama Azam nae anakupiga, ukweli ubingwa usahau.
 
Kawaida ya mwizi akishukiwa uwa anajitoa yeye siyo mwizi, anawasingizia wenzake.

Kwa kifupi sisi Nganda FC ndio wanunuaji wa mechi na haswa ubingwa tuliochujua mfulululizo ni kwa njia ya ngawira
 
Si mpo Club bingwa CAF ,mtakuwaje na timu mbaya maana wenzetu humu ndicho wanacho jitambia.
 
Simba Cha muhimu we shinda mechi zako sio unaboronga alafu unategemea timu nyingine zikupambanie!!
 
Well said bro..Bravo
 
Nadhani haujamuelewa mleta mada mkuu, anachosema ni kwamba mashabiki wa Simba waache kulalamika kuwa team hasimu wao ananunua mechi badala yake wakomae washinde zao maana mpira wa miguu ni kushinda mechi zako.

Simba ni kweli matatizo yapo hata kama team imefuzu makundi, Team imetangaza juzi kocha wa makipa na fitness coach huoni kama ni tatizo Hilo team kukaa muda mrefu bila fitness coach?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…