Kocha wa hiko kikosi alikuwa Marehemu Bruno Metsu.
Hapo kikosini nawakumbuka golikipa Tony Silva, Captain Aliou Cisse ambaye kwasasa ndiye kocha mkuu wa kikosi hiko, pia Ferdinand Coly huyo jamaa mwenye rasta.
Kiungo matata kabisa aliyestafu mpira mapema kutokana na matatizo ya moyo, Khalilu Fadiga mwenye jezi namba 10.
Pia kuna Salif Diao namba 15, Henry Camara mwenye namba 7, Beki ya kulia Omar Daf mwenye namba 2.
El Hadji Diouf mwenye 11, na Papa Bouba Diop mwenye 19 ambaye aliwagunga Ufaransa kwenye mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia.
Pia walifungwa na Cameroon katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya mwaka 2002 kwa mikwaju ya penati.
Miaka ya 2000 ilikuwa ni wakati mzuri kama mshabiki wa soka kufatilia soka kutokana na uwepo wa kikosi kama hiki.
Ahsante mtoa mada kwa kutukumbusha mbali.
cc:
Guasa Amboni