Simba wadhamiria kukamilisha uwanja wao, Mo Dewji achangia Bilioni 2

Simba wadhamiria kukamilisha uwanja wao, Mo Dewji achangia Bilioni 2

Njia rahisi kwa Simba kujenga uwanja ni kuingia ubia na Kampuni duniani kote wanafanya hivyo hata kama watachangia fedha lakini at least 55% - 65% ya Bajeti itoke kwenye Kampuni hizo zingine hata wakichangia sawa

Kwa upande mwingine

kama mfumo wao wa HISA unaeleweka wangeingia DSE pale wakaweka lengo lao then watu wakanunua HISA wangefanikiwa haraka sana.
Hisa kibongo bongo zinazengua, kampuni isipokuwa na strategy ya kueleweka watu watapoteza hela kwa thamani ya hisa kushuka.
 
Nitachangia laki nasubiri utaratibu ila tungejenga uwanja mkubwa zaidi wa kuchukua watu elfu 60
Hata mimi nimekuwa na mtazamo huo maana inawezekana kabisa ili tunawe ishu ya kiwanja hadi miaka 50 ijayo ndo labda tuanze kufikiria kuongeza ukubwa wa Kiwanja
Ukitazama wanasimba milion 5 wakichanga sh 1000 kwa mwezi tu tunapata bilion 5 kwa miezi 12 itakuwa bilion 60 sasa kama wengi wanasema uwanja wa watu 30,000 unagarimu bilion 40 that means wanasima wakiweka malengo ya kuchangishana 1000 kwa mwezi uwanja wa watu elfu 60 utawachukua only two years.

We can mie natoa 50,000 kuanza we need acc tuanze kujichanga tu heri tufe tumeuona uwanja wetu mioyo yetu itafurahi sana
 
Ulimwengu wa Giza, Ulimwengu wa Mwanga.

Mashabiki wa Ua Jekundu wanaishi kwenye Dunia ya hisia,wanayatazama Mambo kichwa chini Miguu juu wapo kwenye Ulimwengu ambao Giza ni Chakula chao pendwa hawajui Vivuli vya ukweli na ukweli wenyewe

Kwasababu maamuzi yao ya msingi kuhusu maisha yanatengemea hisia zilizolala kwenye kesi ya VVIP.Kuwepo Kwao kwenye Hisia na Akili zao kuviringishwa na mgando wa fikra za kinazi kumewafanya wanaamini mnara wa Babeli ulijengwa Kwa fedha za kashata,waamini Nou Camp ilijengewa Kwa mafuta ya Vitumbua.

Pia Kufungwa Kwao minyororo ya Giza la ujinga na kutumia tumbo kutoa maamuzi ya msingi kumewafanya kuamini project ya kujenga Uwanja ni kama kukanda ngano,Waamini Samaki anaweza kupanda juu ya mti Kwa vipande vya shilingi vilivyolala mfukoni mwa waashi.

Nafikiri huu ni wakati wa kuzamisha vichwa vyao kwenye vilindi vya maji,Ni wakati ambao wanapaswa kuangalia Kila jambo kwenye Ulimwengu wa Mwanga,kwenye Ulimwengu ambao kanuni inasema kujenga Uwanja kunahitaji busara kuliko Hisia za Mtoto kunyinwa Maziwa ya VVIP.

Haya yanatokea kwasababu ya uvivu wao kufikiri na kuamua kuwa walevi wa Hisia kuliko mantiki na Ujinga mtamu umetawala pembe zote za Dunia yao iliyojaa Giza.
Unajikuta kichwa wakat umekopy kila kitu toka ig [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wakuu tukiacha siasa za maji taka za Usimba na Uyanga. Nataka nichangie huu mjadala kwa namna tofauti, kwa namna ambayo nitaiweka kidogo kisomi na hapa naomba tuache ushabiki.

1. Simba ni kampuni ambayo iko na 2 shareholders, MO and Members on the other hand. Kwa mtiririko huohuo shareholders wako na share 49% na 51% respectively.

Kama ndio hivyo basi SIMBA SC ni Mali ya MO na WANACHAMA kwa upande mwingine. Hata hivyo kama SIMBA ni kampuni na hao ni wabia wake, haitakiwi shabiki achangie kiasi fulani katika ujenzi wa ASSETS za Klabu kwa sababu shabiki akichangia ina maana unamwongezea MTAJI MMILIKI.

2. Ilitakiwa ifanyike analysis nzima juu ya gharama za ujenzi kisha gharama zile zigawanywe kwa uzito sawa na SHARES yaani kama ujenzi ni BIL 20 basi MO atapaswa kutoa Bil 9.8 na WANACHAMA Bil 10.2. Yes ni kampuni hivyo Mo hapaswi kusema watu wachangie wakati yeye ni mwanahisa na anapata INCOME through hiyo kampuni si sahihi. Kwanini aombe michango wakati kampuni ni yake kwa 49%?.

3. Watanzania wenzangu, kabla ya kurukia kitu lazima mkae chini na mtafakari kwa kina juu ya masuala haya. MO anawakosea sana Simba, na always yy hujifanya kama anasaidia lkn ukweli ni kwamba yeye ni Mwanahisa kwanini atake mashabiki wamchangie? Kama ndio hivyo basi ajitoe kuwa mmoja wa wamiliki ili watu wachangie wakijua yeyote anaweza kuwa kiongozi wa SIMBA.

4. Rai yangu kwa wapenda michezo, haki na wapenzi wa hii klabu kupaza sauti na kugundua UTAPELI wa wazi anaofanya huyu MO DEWJI.

KWA UCHACHE NAWASILISHA.
NB. Kama uelewa wako kuhusu umiliki wa makampuni ni FINYU usiquote huu mchango.
Ameshajitoa vya kutosha hadi analemewa so hatuwezi kusita katika hili eti tunamtegea never , yaani tutahakikisha tumechanga hata wachawi msimame kuturoga , hela ni zetu wewe baki na zako usichange.Na ishu ya kuwa na elimu ya makampuni hatuihitaji katika hili we are serious hadi tuuone uwanja
 
NA MIMI NITOE MAONI KUHUSU WAZO LA WANA SIMBA KUJENGA KIWANJA CHAO CHA MPIRA.

Kwanza kabisa napongeza wazo la WanaSimba kujenga kiwanja Chao Cha Mpira. Kwako Ni kwako,kwahiyo endapo watafanikiwa Basi itakuwa Ni hatua nzuri kwa Club hiyo ya Mpira Nchini Tanzania.

Lakini wazo hili ukamilishaji wake Sio wa mda mfupi Kama tunavyofikilia kabisa,hii Ni kutokana na Gharama kubwa ambazo zinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo.

Mfano,Uwanja Mkubwa kabisa wa Kabumbu nchi Tanzania Ni Uwanja wa taifa Maarufu Kama MKAPA NATIONAL STADIUM. Uwanja huu ndio Mkubwa kabisa nchini Tanzania ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki zaidi ya 60,000. Uwanja huo ulianza kutumika baada ya kukamilika mwaka 2007,na Mechi ya kwanza kuchezwa ilikuwa Kati ya SIMBA SC dhidi ya YANGA FC zote za Nchini Tanzania.

Uwanja huo ulijengwa na Kampuni ya KICHINA Kama msaada wa Serikali ya China kudumisha ushirikiano na nchi ya Tanzania.

Uwanja huo wa Mpira ujenzi wake Mpaka kukamilika Uligharimu takribani Dolla za Kimarekani Milioni 56 za kipindi hicho($ 56M). Hizo Ni sawa na Takribani Bilioni 132 za Kitanzania (Tzs 132B).

Kwa Motisha,Rais wa Club ya Simba ameahidi Kuchangia kiasi Cha Tzs 2B. Kwahiyo Kuna Naksi ya Tzs 130B ambazo wanaSimba wanatakiwa kujitoa mifukoni mwao ili kukamilisha ujenzi huo.

Kwahesabu za harakaharaka tu,tufanye Watanzania wote Milioni 58 wawe mashabiki wa SIMBA SC,na wawe tayari kuichangia Timu hiyo(Hapa tuna-ASSUME TU). Ili kukamilisha ujenzi huo kila Mtanzania atahitajika Kuchangia kiasi Cha Dola 0.9 sawa na Tzs 2,100/=.

Swali,je Watanzania wote Ni Mashabiki wa Simba? Jibu Ni Hapana.

Je,Mashabiki wa Simba Ni Kiasi gani? Mashabiki wa Simba Nchi nzima Ni Milioni 10 lakini wenye uwezo wa Kuchangia kutokana na ushabiki wao kindakindani Ni Watu Laki moja TU. Kwamaana hiyo Kati ya hao watu Laki moja,kila Mmoja atahitajika Kuchangia kiasi Cha Tsh 1,218,000 (Milioni moja Laki Mbili na Elfu 18). Je hapo vepee? Jibu Ni haiwezekani.

Kwahiyo Simba watulie tu,Kama MO anataka Simba iwe na Uwanja wake na anaipenda Simba kweli Basi kwanini asizame mfukoni akachomoa Tsh 132B akajenga Uwanja? Utajiri wa MO Dewji Ni Zaidi ya Tsh 3500B (Trillion Tatu na Nusu)

Ukichukua utajiri wa MO ukatoa gharama za Uwanja Ni sawa na aliyechota kikombe Cha Maji kutoka Baharini,Bahari haiwezi kuathirika kabisa.

3,500B-132B= 3,368B. Yaani anabaki na Tzh Trillion Tatu na Billion miatatu na sitini na nane.

Ushauri

MO aache kuwakamua Masikini wanaSimba ili kutimiza ndoto zake.

Antony Linken
 
NA MIMI NITOE MAONI KUHUSU WAZO LA WANA SIMBA KUJENGA KIWANJA CHAO CHA MPIRA.

Kwanza kabisa napongeza wazo la WanaSimba kujenga kiwanja Chao Cha Mpira. Kwako Ni kwako,kwahiyo endapo watafanikiwa Basi itakuwa Ni hatua nzuri kwa Club hiyo ya Mpira Nchini Tanzania.

Lakini wazo hili ukamilishaji wake Sio wa mda mfupi Kama tunavyofikilia kabisa,hii Ni kutokana na Gharama kubwa ambazo zinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo.

Mfano,Uwanja Mkubwa kabisa wa Kabumbu nchi Tanzania Ni Uwanja wa taifa Maarufu Kama MKAPA NATIONAL STADIUM. Uwanja huu ndio Mkubwa kabisa nchini Tanzania ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki zaidi ya 60,000. Uwanja huo ulianza kutumika baada ya kukamilika mwaka 2007,na Mechi ya kwanza kuchezwa ilikuwa Kati ya SIMBA SC dhidi ya YANGA FC zote za Nchini Tanzania.

Uwanja huo ulijengwa na Kampuni ya KICHINA Kama msaada wa Serikali ya China kudumisha ushirikiano na nchi ya Tanzania.

Uwanja huo wa Mpira ujenzi wake Mpaka kukamilika Uligharimu takribani Dolla za Kimarekani Milioni 56 za kipindi hicho($ 56M). Hizo Ni sawa na Takribani Bilioni 132 za Kitanzania (Tzs 132B).

Kwa Motisha,Rais wa Club ya Simba ameahidi Kuchangia kiasi Cha Tzs 2B. Kwahiyo Kuna Naksi ya Tzs 130B ambazo wanaSimba wanatakiwa kujitoa mifukoni mwao ili kukamilisha ujenzi huo.

Kwahesabu za harakaharaka tu,tufanye Watanzania wote Milioni 58 wawe mashabiki wa SIMBA SC,na wawe tayari kuichangia Timu hiyo(Hapa tuna-ASSUME TU). Ili kukamilisha ujenzi huo kila Mtanzania atahitajika Kuchangia kiasi Cha Dola 0.9 sawa na Tzs 2,100/=.

Swali,je Watanzania wote Ni Mashabiki wa Simba? Jibu Ni Hapana.

Je,Mashabiki wa Simba Ni Kiasi gani? Mashabiki wa Simba Nchi nzima Ni Milioni 10 lakini wenye uwezo wa Kuchangia kutokana na ushabiki wao kindakindani Ni Watu Laki moja TU. Kwamaana hiyo Kati ya hao watu Laki moja,kila Mmoja atahitajika Kuchangia kiasi Cha Tsh 1,218,000 (Milioni moja Laki Mbili na Elfu 18). Je hapo vepee? Jibu Ni haiwezekani.

Kwahiyo Simba watulie tu,Kama MO anataka Simba iwe na Uwanja wake na anaipenda Simba kweli Basi kwanini asizame mfukoni akachomoa Tsh 132B akajenga Uwanja? Utajiri wa MO Dewji Ni Zaidi ya Tsh 3500B (Trillion Tatu na Nusu)

Ukichukua utajiri wa MO ukatoa gharama za Uwanja Ni sawa na aliyechota kikombe Cha Maji kutoka Baharini,Bahari haiwezi kuathirika kabisa.

3,500B-132B= 3,368B. Yaani anabaki na Tzh Trillion Tatu na Billion miatatu na sitini na nane.

Ushauri

MO aache kuwakamua Masikini wanaSimba ili kutimiza ndoto zake.

Antony Linken
 
Wewe ni kilaza, pitia hoja zako zote kila uelimishwapo kuhusu SIMBA unajaza mafua kichwani. SIKIA MO NI MMILIKI HALALI WA SIMBA KWA 49% na WANACHAMA WANAMILIKI 51% Kwahiyo KAMA ILIVYO AZAM AMBAPO BAKHRESA ANAMILIKI KWA 100% NA SIMBA INAMILIKIWA KWA 49% NA MO. HIVYO NI JUKUMU LAKE KUJUA GHARAMA ZA UWANJA NA KISHA AKAE YEYE NA WANACHAMA WAGAWANE KULINGANA NA UBIA WAO AMBAO NI 51% KWA 49%.

Unapochangia kitu tuliza akili yako na acha ushabiki wako wa kimpira usio na maana.
Kwa mfano wewe ukichangia hiyo pesa na UWANJA UKAJENGWA hujui kuwa UTAKUWA MALI YA MO KWA 49%?? kwa maana itakuwa ni ASSET ya SIMBA?
Sasa kwanini atake mchangie wakati anajua wazi kuwa yeye ni mmiliki? Anataka tumpe mtaji aongezee kwenye mtaji wa AWALI?
Shida yetu Simba iwe na uwanja wake tu mengine ya anamiliki nani bakini nayo ninyi yaani mimi nishindwe kutoa elfu 10 eti kisa itakuwa ni kumtajirisha Mo kwa kitu ambacho uwepo wake tu utakuwa furaha kwetu , TUTACHANGA tu maadam sio dhambi mbele za Mungu
 
Kwa bajeti nzuri na kubwa duniani kote, Viwanja hutumia mpaka miaka minne au mitano kukamilika, vile vya kuanza kabisa chini! Hivyo unahitaji resource za kutosha sana, maana kuchanga tu Watu watachoka

Klabu nyingi duniani zimeingia ubia na Makampuni makubwa katika ujenzi wa Viwanja vyao kisha kukubaliana suala la mapatano kuhusu malipo

Mfano Atletico Madrid baada ya kuvunja Vicente Calderon na kujenga uwanja mpya chini ya udhamini wa Kampuni ya wachina wakakubaliana kwenye naming rights

Uwanja unaitwa METROPOLITANO ila kutokana na sababu za kibiashara unaitwa WANDA METROPOLITANO, hii Wanda ni Kampuni ya Kichina

Hivyo Simba wanaweza kuingia ubia na Kampuni moja Tajiri, jumlisha na pesa yao wakapata uwanja mzuri, wa kisasa na wenye kuingiza hata Mashabiki 30,000 sio mbaya sana

Ni ukweli mchungu kuwa huwezi kusimamisha uwanja wa hadhi ya Simba kwa michango tu mfukoni, bali kumeza vidonge vichungu vya kukopa, kuingia ubia na Kampuni Ili kufanikisha!

Pia Simba wajiandae kusacrifice kipindi cha miaka hadi mitano ya kufanya vibaya uwanjani kwasababu watashindwa kufanya vizuri ktk masoko ya usajili wa wachezaji bora wenye gharama kwasababu ya Pesa nyingi imeelekezwa kwenye ujenzi wa uwanja

Waitishe Mkutano Mkuu wa dharura kukubaliana, kujenga uwanja ni Uamuzi wa hasira, sasa ni hatari sana kufanya maamuzi ingali na hasira, hivyo kuzifanya hasira ziwe rasmi wanapaswa kuitisha Mkutano Mkuu wakubaliane, kwenye faida na hasara pia
Ushauri mzuri ila umeshapiga hesabu za ikiwa mashabik watatoa sh 1000 na wawe 5000 kwa miezi 12?
 
Naona kwa mbali unaanza kuelewa. Iko hivi mkataba wowote una VOID ikiwa uko nje ya sheria mama (Company act) kwa vyovyote vile gharama za ujenzi wa UWANJA lazima ziendane sawa na kiwango cha uwekazaji.

Hakuna shortcut kwenye kuongoza hizi kampuni mkuu. Mo arudi tena akae na wanahisa wenzake (WANACHAMA) watafute VALUER wajue gharama nzima ya ujenzi kisha kila upande uchangie kulingana na HISA ZAKE.

Kubwa zaidi upande wa wanachama ndio ulipaswa utoke uombe wanachama wake kuchangia maana ndio upande wao ma sio MO aombe watu wachangie akijua wazi ni JUKUMU lake kutoa 49% ya gharama.
Muwe waelewa , aliyeanzisha hoja hii ni Magori sasa unamlaumu vipi Mo kukubaliaba na Magori watu wachange?
 
Ha ha haaa kweli maisha yako kasi sana, hawa si walikuwa wakiibeza Yanga kipindi kile? Ngoja tuone
 
Hapana , sidhani kama ni jukumu lake kigharamia 49%za ujenzi wa uwanja. Uwanja una gharama Sana za ujenzi. Hao wanachama Wana buku buku tu. Haiwezi kufika huko. Labda wajenge kama chamazi. Ila kama uhuru au taifa. Nguzo moja ya uwanja tu unakuta imelamba mamilioni ya pesa. Dawa ni kukopa tu.
Unawakatisha tamaa watu ila inawezekana niambie

Watu milion 5 wakichangia sh 1000 kila mmoja kwa mwezi itakuwa sh ngapi kisha izidishe mara miezi 36 yaani miaka 3 uone uwanja unakamilika au la
 
Watachanga wachache mwanzo juhudi za ujenzi ndy zitakazo ongeza idadi ya wachangiaji.
 
Unawakatisha tamaa watu ila inawezekana niambie

Watu milion 5 wakichangia sh 1000 kila mmoja kwa mwezi itakuwa sh ngapi kisha izidishe mara miezi 36 yaani miaka 3 uone uwanja unakamilika au la
Hesabu za makaratasi hizo boya wewe.. nani achangie buku kila mwezi? We unadhani watu MIL 5 ni mchezo eeh.

Jezi zenyewe zinazouzwa hazifiki hata 200k afu upate watu Mil 5 wa kuchangia kila mwezi. Uelewa wako ni finyu sana, kama una familia basi watoto wako wameridhi hayo maradhi.

We ukitoka Buza huko asubuhi umevaa Blauzi yako unadhani wote wanapenda mpira kichaa kwa namna hiyo?

We umepewa maelezo namna gani mmiliki anapaswa kuwa. We ushawahi sikia CHELSEA INACHANGISHWA, AU MAN UTD, AU MAN CITY? Timu ikiwa katika mfumo wa KAMPUNI huwezi changisha watu tena maana kuna watu tayari wameweka mitaji yao na wanakuwa wamiliki.

Kwa akili hizi mtapigwa mchakae. Sijui humo kichwani umejaza wadudu gani.
 
Uwanja wa azam uligharimu shingapi?
Tzs 24B. Fedha zote zilitoka mfukoni mwa BAKHERESA. Makapuku wa Simba hawawezi kuchanga 22B Tzs. Historia inakataa,Hakuna Rambirambi(Michango) bongo iliyowahi kufikia hicho kiasi.
 
Utopolo mbona umeshituka baada ya kusikia simba wanataka kujenga uwanja, kwa kifupi tumeshaamua haturudi nyuma.
 
Back
Top Bottom