Simba wadhamiria kukamilisha uwanja wao, Mo Dewji achangia Bilioni 2

Hisa kibongo bongo zinazengua, kampuni isipokuwa na strategy ya kueleweka watu watapoteza hela kwa thamani ya hisa kushuka.
 
Nitachangia laki nasubiri utaratibu ila tungejenga uwanja mkubwa zaidi wa kuchukua watu elfu 60
Hata mimi nimekuwa na mtazamo huo maana inawezekana kabisa ili tunawe ishu ya kiwanja hadi miaka 50 ijayo ndo labda tuanze kufikiria kuongeza ukubwa wa Kiwanja
Ukitazama wanasimba milion 5 wakichanga sh 1000 kwa mwezi tu tunapata bilion 5 kwa miezi 12 itakuwa bilion 60 sasa kama wengi wanasema uwanja wa watu 30,000 unagarimu bilion 40 that means wanasima wakiweka malengo ya kuchangishana 1000 kwa mwezi uwanja wa watu elfu 60 utawachukua only two years.

We can mie natoa 50,000 kuanza we need acc tuanze kujichanga tu heri tufe tumeuona uwanja wetu mioyo yetu itafurahi sana
 
Unajikuta kichwa wakat umekopy kila kitu toka ig [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ameshajitoa vya kutosha hadi analemewa so hatuwezi kusita katika hili eti tunamtegea never , yaani tutahakikisha tumechanga hata wachawi msimame kuturoga , hela ni zetu wewe baki na zako usichange.Na ishu ya kuwa na elimu ya makampuni hatuihitaji katika hili we are serious hadi tuuone uwanja
 
NA MIMI NITOE MAONI KUHUSU WAZO LA WANA SIMBA KUJENGA KIWANJA CHAO CHA MPIRA.

Kwanza kabisa napongeza wazo la WanaSimba kujenga kiwanja Chao Cha Mpira. Kwako Ni kwako,kwahiyo endapo watafanikiwa Basi itakuwa Ni hatua nzuri kwa Club hiyo ya Mpira Nchini Tanzania.

Lakini wazo hili ukamilishaji wake Sio wa mda mfupi Kama tunavyofikilia kabisa,hii Ni kutokana na Gharama kubwa ambazo zinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo.

Mfano,Uwanja Mkubwa kabisa wa Kabumbu nchi Tanzania Ni Uwanja wa taifa Maarufu Kama MKAPA NATIONAL STADIUM. Uwanja huu ndio Mkubwa kabisa nchini Tanzania ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki zaidi ya 60,000. Uwanja huo ulianza kutumika baada ya kukamilika mwaka 2007,na Mechi ya kwanza kuchezwa ilikuwa Kati ya SIMBA SC dhidi ya YANGA FC zote za Nchini Tanzania.

Uwanja huo ulijengwa na Kampuni ya KICHINA Kama msaada wa Serikali ya China kudumisha ushirikiano na nchi ya Tanzania.

Uwanja huo wa Mpira ujenzi wake Mpaka kukamilika Uligharimu takribani Dolla za Kimarekani Milioni 56 za kipindi hicho($ 56M). Hizo Ni sawa na Takribani Bilioni 132 za Kitanzania (Tzs 132B).

Kwa Motisha,Rais wa Club ya Simba ameahidi Kuchangia kiasi Cha Tzs 2B. Kwahiyo Kuna Naksi ya Tzs 130B ambazo wanaSimba wanatakiwa kujitoa mifukoni mwao ili kukamilisha ujenzi huo.

Kwahesabu za harakaharaka tu,tufanye Watanzania wote Milioni 58 wawe mashabiki wa SIMBA SC,na wawe tayari kuichangia Timu hiyo(Hapa tuna-ASSUME TU). Ili kukamilisha ujenzi huo kila Mtanzania atahitajika Kuchangia kiasi Cha Dola 0.9 sawa na Tzs 2,100/=.

Swali,je Watanzania wote Ni Mashabiki wa Simba? Jibu Ni Hapana.

Je,Mashabiki wa Simba Ni Kiasi gani? Mashabiki wa Simba Nchi nzima Ni Milioni 10 lakini wenye uwezo wa Kuchangia kutokana na ushabiki wao kindakindani Ni Watu Laki moja TU. Kwamaana hiyo Kati ya hao watu Laki moja,kila Mmoja atahitajika Kuchangia kiasi Cha Tsh 1,218,000 (Milioni moja Laki Mbili na Elfu 18). Je hapo vepee? Jibu Ni haiwezekani.

Kwahiyo Simba watulie tu,Kama MO anataka Simba iwe na Uwanja wake na anaipenda Simba kweli Basi kwanini asizame mfukoni akachomoa Tsh 132B akajenga Uwanja? Utajiri wa MO Dewji Ni Zaidi ya Tsh 3500B (Trillion Tatu na Nusu)

Ukichukua utajiri wa MO ukatoa gharama za Uwanja Ni sawa na aliyechota kikombe Cha Maji kutoka Baharini,Bahari haiwezi kuathirika kabisa.

3,500B-132B= 3,368B. Yaani anabaki na Tzh Trillion Tatu na Billion miatatu na sitini na nane.

Ushauri

MO aache kuwakamua Masikini wanaSimba ili kutimiza ndoto zake.

Antony Linken
 
NA MIMI NITOE MAONI KUHUSU WAZO LA WANA SIMBA KUJENGA KIWANJA CHAO CHA MPIRA.

Kwanza kabisa napongeza wazo la WanaSimba kujenga kiwanja Chao Cha Mpira. Kwako Ni kwako,kwahiyo endapo watafanikiwa Basi itakuwa Ni hatua nzuri kwa Club hiyo ya Mpira Nchini Tanzania.

Lakini wazo hili ukamilishaji wake Sio wa mda mfupi Kama tunavyofikilia kabisa,hii Ni kutokana na Gharama kubwa ambazo zinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo.

Mfano,Uwanja Mkubwa kabisa wa Kabumbu nchi Tanzania Ni Uwanja wa taifa Maarufu Kama MKAPA NATIONAL STADIUM. Uwanja huu ndio Mkubwa kabisa nchini Tanzania ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki zaidi ya 60,000. Uwanja huo ulianza kutumika baada ya kukamilika mwaka 2007,na Mechi ya kwanza kuchezwa ilikuwa Kati ya SIMBA SC dhidi ya YANGA FC zote za Nchini Tanzania.

Uwanja huo ulijengwa na Kampuni ya KICHINA Kama msaada wa Serikali ya China kudumisha ushirikiano na nchi ya Tanzania.

Uwanja huo wa Mpira ujenzi wake Mpaka kukamilika Uligharimu takribani Dolla za Kimarekani Milioni 56 za kipindi hicho($ 56M). Hizo Ni sawa na Takribani Bilioni 132 za Kitanzania (Tzs 132B).

Kwa Motisha,Rais wa Club ya Simba ameahidi Kuchangia kiasi Cha Tzs 2B. Kwahiyo Kuna Naksi ya Tzs 130B ambazo wanaSimba wanatakiwa kujitoa mifukoni mwao ili kukamilisha ujenzi huo.

Kwahesabu za harakaharaka tu,tufanye Watanzania wote Milioni 58 wawe mashabiki wa SIMBA SC,na wawe tayari kuichangia Timu hiyo(Hapa tuna-ASSUME TU). Ili kukamilisha ujenzi huo kila Mtanzania atahitajika Kuchangia kiasi Cha Dola 0.9 sawa na Tzs 2,100/=.

Swali,je Watanzania wote Ni Mashabiki wa Simba? Jibu Ni Hapana.

Je,Mashabiki wa Simba Ni Kiasi gani? Mashabiki wa Simba Nchi nzima Ni Milioni 10 lakini wenye uwezo wa Kuchangia kutokana na ushabiki wao kindakindani Ni Watu Laki moja TU. Kwamaana hiyo Kati ya hao watu Laki moja,kila Mmoja atahitajika Kuchangia kiasi Cha Tsh 1,218,000 (Milioni moja Laki Mbili na Elfu 18). Je hapo vepee? Jibu Ni haiwezekani.

Kwahiyo Simba watulie tu,Kama MO anataka Simba iwe na Uwanja wake na anaipenda Simba kweli Basi kwanini asizame mfukoni akachomoa Tsh 132B akajenga Uwanja? Utajiri wa MO Dewji Ni Zaidi ya Tsh 3500B (Trillion Tatu na Nusu)

Ukichukua utajiri wa MO ukatoa gharama za Uwanja Ni sawa na aliyechota kikombe Cha Maji kutoka Baharini,Bahari haiwezi kuathirika kabisa.

3,500B-132B= 3,368B. Yaani anabaki na Tzh Trillion Tatu na Billion miatatu na sitini na nane.

Ushauri

MO aache kuwakamua Masikini wanaSimba ili kutimiza ndoto zake.

Antony Linken
 
Shida yetu Simba iwe na uwanja wake tu mengine ya anamiliki nani bakini nayo ninyi yaani mimi nishindwe kutoa elfu 10 eti kisa itakuwa ni kumtajirisha Mo kwa kitu ambacho uwepo wake tu utakuwa furaha kwetu , TUTACHANGA tu maadam sio dhambi mbele za Mungu
 
Ushauri mzuri ila umeshapiga hesabu za ikiwa mashabik watatoa sh 1000 na wawe 5000 kwa miezi 12?
 
Muwe waelewa , aliyeanzisha hoja hii ni Magori sasa unamlaumu vipi Mo kukubaliaba na Magori watu wachange?
 
Ha ha haaa kweli maisha yako kasi sana, hawa si walikuwa wakiibeza Yanga kipindi kile? Ngoja tuone
 
Unawakatisha tamaa watu ila inawezekana niambie

Watu milion 5 wakichangia sh 1000 kila mmoja kwa mwezi itakuwa sh ngapi kisha izidishe mara miezi 36 yaani miaka 3 uone uwanja unakamilika au la
 
Watachanga wachache mwanzo juhudi za ujenzi ndy zitakazo ongeza idadi ya wachangiaji.
 
Unawakatisha tamaa watu ila inawezekana niambie

Watu milion 5 wakichangia sh 1000 kila mmoja kwa mwezi itakuwa sh ngapi kisha izidishe mara miezi 36 yaani miaka 3 uone uwanja unakamilika au la
Hesabu za makaratasi hizo boya wewe.. nani achangie buku kila mwezi? We unadhani watu MIL 5 ni mchezo eeh.

Jezi zenyewe zinazouzwa hazifiki hata 200k afu upate watu Mil 5 wa kuchangia kila mwezi. Uelewa wako ni finyu sana, kama una familia basi watoto wako wameridhi hayo maradhi.

We ukitoka Buza huko asubuhi umevaa Blauzi yako unadhani wote wanapenda mpira kichaa kwa namna hiyo?

We umepewa maelezo namna gani mmiliki anapaswa kuwa. We ushawahi sikia CHELSEA INACHANGISHWA, AU MAN UTD, AU MAN CITY? Timu ikiwa katika mfumo wa KAMPUNI huwezi changisha watu tena maana kuna watu tayari wameweka mitaji yao na wanakuwa wamiliki.

Kwa akili hizi mtapigwa mchakae. Sijui humo kichwani umejaza wadudu gani.
 
Uwanja wa azam uligharimu shingapi?
Tzs 24B. Fedha zote zilitoka mfukoni mwa BAKHERESA. Makapuku wa Simba hawawezi kuchanga 22B Tzs. Historia inakataa,Hakuna Rambirambi(Michango) bongo iliyowahi kufikia hicho kiasi.
 
Utopolo mbona umeshituka baada ya kusikia simba wanataka kujenga uwanja, kwa kifupi tumeshaamua haturudi nyuma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…