Simba wamalize tofauti zao, migogoro haitawasaidia

Simba wamalize tofauti zao, migogoro haitawasaidia

King Jody

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2022
Posts
1,834
Reaction score
3,456
Ni wakati wa kumaliza tofauti zenu baada ya kufungwa na mtani wenu kwa idadi ya mabao mengi {1-5} Maisha lazima yaendelee, haikuwepo sababu ya msingi kumtimua kocha Robertinho mzee wa Objective football, Takwimu zinaonesha amepoteza mechi moja tu tangu ajiunge nanyi kama Head coach.

-Hakuna haja ya kuwatuhumu wachezaji kuihujumu timu, Kubalini mlizidiwa na mpinzani wenu [Yanga} ambaye yupo kwenye ubora kuwazidi kwa sasa, Huo ndiyo ukweli {kitakwimu}

Kumbukeni kuna michuano ya kimataifa inawasubiri, Msiangalie mlipojikwaa, angalieni mlipodondoka,
Kumbukeni kuna watu wanapenda kuwaona mkiendelea na migogoro ambayo kimsingi haina afya kwenye tasnia na mustakabali wa soka letu.

Simameni imara kwa ajili ya kuimarisha timu yenu, kumtafuta mchawi nani ni kujipotezea muda.

Nawatakia kila la heri watani zangu.
 
Msimu huu kwenye mashindano ameisimamia SIMBASC michezo 11 ya ndani na nje ya nchi ..

Ligi kuu NBC
Mtibwa 2-4 SimbaSC
DodomaFC 0-2 SimbaSC
SimbaSC 3-0 COASTAL UNION
Tz Prison 1-3 SimbaSC
SingidaFG 1-2 SimbaSc
SimbaSc 2-1 Ihefu FC
SimbaSC 1-5 YangaSC

MICHUANO YA CAF CHAMPIONS LEAGUE & AFRICAN FOOTBAL LEAGUE ..

POWER DYANAMO 2 - SIMBASC 2
SIMBASC 1-1 POWER DYNAMO

SIMBASC 1-1 AL AHLY EGYPT
AL AHLY EGYPT 2-2 SIMBASC


Katika mechi kumi na moja ni mbili tu hakuruhusu goli na nyingine zote alikuwa anavuja.

Kocha anabebwa na falsafa na si kwa matukio kama ilivyokuwa kwa Robertanho wa mchongo.
 
Migogoro itaisha vipi wakati promo kibao wakati wa usajili halafu yanaletwa magarasa . Onana aliposajiliwa Ahmed Ally alisema "tumeleta mtu hatari akitua tu Tanzania umeme unakatika"
Na kweli ulikatika November 05, Sim5a.
 
Siku mashabiki wakiweka mgomo kutokwenda uwanjani ndipo Viongozi watakuwa serious.
 
Back
Top Bottom