Simba wamecheza chini ya kiwango, kuna kitu

Lwanga, mkude na bwalya ni viungo wakabaji wote walicheza mechi moja ona sasa


Lyanga ni typical kiungo mkabaji, mkude vivyo hivyo expect bwalya ambaye anaweza kuchezesha

Jana walizidiwa mbinu tu
 
Wakat simba amemiliki mpira kwa 68% na kaizer 32..kumbe ndo kucheza chini ya kiwango?
Uwezo wa kusoma na kujua makosa ya mpinzani unamwadhibia hapo hapo

Ndo maana hao jamaa walijaribu kuposses dkk kama 3 hivi wakaamua kuacha kuwaachia Simba mpira wao wakaanza kupiga counter attack tu huku wakiziba mashimo yao
 
Exactly
 
Aina hii ya watanzania ndio wanatufanya tuonekane mazezeta. Kwa hiyo wachezaji Chelsea nao wamehongwa na GSM jana. Amka ndugu. Nani kakwambia Simba ndio klabu bora Afrika hadi isifungwe na Kaizer Chiefs? Tunatia Aibu.
 
Sijamtetea Kapombe kwa lolote alilokosea, nilichokataa ni kumwangushia kumba bovu peke yake.
Nakubaliana na wewe katika masuala yafuatayo;
1.Ni kweli Simba ina shida kubwa ya beki wa kati. Mabeki wake wote wawili hawajui wafanye nini na mipira inayokatisha na huu ni ugonjwa wao siku hadi siku.
2.Simba ina tatizo la kiungo mzuiaji. Thadeo ni kiungo mkabaji ndo maana kwenye matukio ya kukaba/kunyang'anya utamuona mara nyingi akicheza faulo akicheza tackle nk lkn kuzuia mashambulizi imekuwa ngumu kwake hususan timu inapozidiwa.
3.Kuwa na aina moja pekee ya uchezaji hili nimelifafanua vizuri kwenye comment yangu. Simba ni Simba wakati wote. Wakati katika soka ni kosa kubwa kudhani ukiwa mkali na ikakusaidia siku moja basi unatakiwa kuwa mkali siku zote. Kuna kipindi unahitajika kuwa mpole, mkarimu, mkimya nk.
 
Hii meti inaitwa nganganna ujinyeee.

Simba huwa wanawahadaa timu nyingi huwa wanacheza 5:4:1 au5:3:2 wakiwa hawana mpira wakipata mpira

Mawinga ambao siyo typical Frans ambao ni chama na mosq wakipata mpira huwa wanaganda wanaanza kuchezza pasi fupi fupi wanaubana uwanja wakifosi kupita katikati

Huku wakiwaachia mabeki wa pembeni kupanda ambao huwapa mipira ya pasi na kuupanua uwanja Kwa ghafla na kuubana kwa ghafra hujikuta wamecheza 3:2:5 au 3:1:6 mpaka 2:1:7 na kusababisa timu pinzani kufanya makosa na kiadhibu


Sasa jama walicheza 4:3:3 walipokuwa na mpira wakaswith to 6:2:2 mfumo ambao haumo kabisa kwenye kanuni za soka
Walipokuwa na mpira walitunia mipira mirefu kwa mshambuliaji upande wa kapombe wakijua huko ndo week zaidi Kwa kuwa hakuna mtu anayeweza kuwa fit sehemu zote mbili yaani kushambulia na kujilinda , walishamsima kapombe kuwa magoli mengi huwa anatengeneza yeye hivyo hawezi kuwa mzuri sana kikuba wakamfanyia suprise

Na coach alivoona pia junior na yeye anambwembwe za kupanda akamtoa haraka kiungo mkabaji akaingiza mshambuliaji kuhakikisha zimbwe hapandi, jamaa alipoingia akaenda kucheza 9 hapo sasa 4&5 ya Simba zikapata pancha kabisa
 
Hapana mechi ya Kaizer Vs Simba mbinu za Simba ziligonga mwamba.
Wapo wachezaji baadhi walioonyesha mapungufu lakini bado sio sababu ya kutoa lawama kupita kiasi, socer ni mchezo wa makosa.

Tujipange vema haya mashindano ya CAF Simba tutacheza tena kwa misimu mingi ijayo kwasababu Simba kwa sasa ndo mwenye hati miliki ya ubingwa wa VPL kwa zaidi ya misimu kadhaa mbele.
 
Jana makosa ni yaleyale ya siku zote.
Sijui kwanini wachezaji wetu ( ligi za amateur mpaka premier) hawawezi kucheza mipira ya juu. Ni tatizo la kitaifa.
 
Simba walikaa wiki 2 bila kucheza mechi yoyote, mwili unapunguza utimamu wake ajabu wapanga ratiba wa hapa kwetu
 
Kama kawaida. Hilo lilijulikana,sisi ni wabongo hatuwezi kukosa visingizio.
 
Aisee..we jamaa nakushangaa Sana..sasa mikataba waliyoisain na Simba juzi juzi tukaononyeshwa ni uwongo!? Aliyekwambia kusian Pre contract kuwa unapewa pesa hapo hapo nani!? Embu acha ujuha Basi shekhe
 
Juzi Man United walipochapwa 4-2 na Liverpool nao walihongwa. Waswahili ni waswahili tu hamkosi sababu mkishatembezewa kichapo.

Hii ndio tabu ya mpira wa kuchezea kwenye vyombo vya habari ya akina Haji Manara, Simba mpira mdogo hata hapo wamefika tu baada ya timu nyingi kuwa off form.

Simba hii ya sasa haiwezi kufikia hata robo ya kiwango cha akina Athumani Mambosasa, Shaban Baraza, Mohammed Kajole, Athumani Juma, Aloo Mwitu, Omar Shaban Gumbo, Willy Mwaijibe, Haidari Abeid, Adam Sabu, Abdallah Kibadeni, Abbas Dilunga na Saad Ally.

Hiyo ndio ilikuwa Simba original iliyofika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika mwaka 1974 na kutolewa kwa matuta na Ghazil Mehalla El-Mehalla El-Khubra ya Misri.

Mpira waliokuwa wakicheza hao jamaa na huu wa Ulaya tunaotizama kwenye runinga leo, hauna kabisa tofauti na enzi hizo kulikuwa hakuna mambo ya marefa kubeba timu kama ilivyo leo.

Kwa ile Simba ya akina Kibadeni hii Kaizer Chiefs ingepigwa nane hapo hapo South Africa. Hawa wachezaji wa sasa ni wa maslahi tu kwa mpira hawana lolote.
 
Ni kwel ni muda wa kujipanga upya aina faida kuwa na wachezaj weng alaf wote aina moja na pia kama mchezaj amecheza simba alaf umr na kiwango kikashuka ni vzur kutafuta mbaya hii ya kuwakumbatia kisa walicheza kwa mafanikio kila cku tutakua na kaz ya kujipanga upya tokea msimu huu unaanza simba ina tatzo na namba 9 mwenye maono ambae nafas mbil au 3 atatumia moja mfano wale jamaa namba tisa wao sio kwamba alipata nafas zaid ya tano ila izo alizopata alizitumia na ili jambo nililiona mapema ata kama mech za ligi wachezaj weng wa simba sio watu wa kutumia nafas ata ktk lig kwa hatua kama iz ni lazma ufungwe timu ambazo zinaenda robo kwenda nusu ni atar kama utakua na wachezaj ambao wafunge bas lazma wapate nafas nne au tano ni rais kuishia apa ,wana kaz ya kufanya kuongeza wachezaj watatu au wanne wenye viwango ambao moja kwa moja waingia ktk kikos cha kwanza mpra una pesa lkn kwanza tumia pesa ,kuna muda naona viongoz kama wanauchukulia poa mpra mfano angalia baada ya kufka makund walipewa pesa kwa ajir ya kuongeza nguvu walichofanya wanakijua wao, mfano mwngne ambao unaonyesha viongoz kuna sehem wanachukulia mpra kawaida ktk usafir wamatumia bas la kawaida ni karbu miaka kum apa katikat wamepata pesa na mikataba ming tu ya maana kama wangekua makin wangefanya jambo ambalo nitakumbukwa mfano kuuboresha uwanja wao au kupata usafir wa maana kuliko kununua bas ambalo alipishan sana na la zaman tunataka kuwekeza ktk mpra ila kuna uoga na kutojiamin
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…