Simba wasusie hela ya goli ya mama

Dabil

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2021
Posts
6,823
Reaction score
15,293
Mama alitangaza goli moja sh mil 10. Bila kusema kwamba hiyo hela ni timu ikishinda tu, baada ya kuona simba imeshinda magoli mawili Msigwa akatangaza hela ni timu ikishinda tu.

Tunajua mama ni Yanga ndo maana amegoma kutoa hela kwasababu simba haikushinda. Mashindano mengine yapo huo ni udhalilishaji Kwanza mil 10 hela gani kwa timu kama Simba.

Ingekuwa vizuri hata kwenye mashindano yoyote simba ikishinda wasiende kupokea hiyo hela wapuuzie tu.

Unasema unanunua goli halafu hukuweka vigezo baadaye unasema hawakushinda.
 
Alishasema timu ikishinda tu. Hahahaha 🤣🤣🤣🤣🤣🤣.
 
Shikamoo manaraa wenye akili ni mtu bee tu.......
Raisi ....yanga...no brain
Msigwaa..yanga no brain

Ela zenu mpeni skuduuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Unataka kusema kuwa Mama Samia ameahidi kuwa hata Al Ahly wangeshinda goli 3 kwa 2 mama angegawa pesa kwa Simba kwa hayo magoli mawili aliyopata pamoja na kufungwa kwao?
 
Usimsingizie Msigwa!! Usimlishe maneno!! Pesa za simba sh 20M ziko pale pale!! Mama hawezi kujidhalilisha kiasi hicho!!
Msigwa simlishi maneno amehojiwa na ameshaongea na clip ipo kina kitenge wameweka insta
 
Msigwa alisema na akarudia mara mbili mbili. Simba ikishinda, Simba ikishinda, kila goli mama atatoa 10M, zingatia neno ikishinda! Sasa labda tuanzie hapo, Simba imeshinda!!?[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Unataka kusema kuwa Mama Samia ameahidi kuwa hata Al Ahly wangeshinda goli 3 kwa 2 mama angegawa pesa kwa Simba kwa hayo magoli mawili aliyopata pamoja na kufungwa kwao?
Yanga kwenye mechi na USM alger ahadi ilikuwa kama hiyo endapo yanga akishinda mechi kila holi milioni kadhaa, yanga akabanduliwa 2-1 kwa mkapa na bado akapewa hela
 
Yanga kwenye mechi na USM alger ahadi ilikuwa kama hiyo endapo yanga akishinda mechi kila holi milioni kadhaa, yanga akabanduliwa 2-1 kwa mkapa na bado akapewa hela
Kama ilikuwa hivyo basi kuna tatizo hapo, kuna kupata goli na kushinda. Sasa hapo ni kupata goli na sio kushinda
 
Mbona hata msimu uliopita utaratibu ulikuwa ni huo huo!! Sioni sababu ya kususia hizo pesa kama ina mashiko. Uzuri bado mna nafasi ya kwenda kushinda ugenini kwenye mechi ya marudiano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…