Simba yamtupia virago KOPUNOVIC,yamleta mbelgiji PIET DE MOL!!!

Simba yamtupia virago KOPUNOVIC,yamleta mbelgiji PIET DE MOL!!!

Mkuu...Kuna kipindi Yanga ilienda kuweka Kambi Moshi ikashindwa kulipia hoteli wakawa wanadaiwa hadi kushikiliwa gari lao

Labda uwe mgeni wa soka la simba na Yanga

Hizi timu hua migogoro inahama toka upande mmoja kwenda mwingine

Kabla ya Manji ...Yanga kuna wakati ilikua inalia njaa

Jumatano, 28 Desemba 2011

WACHEZAJI YANGA NJAA KALI, PESA HAKUNA.


Wachezaji Yanga walia njaa



Yangaazamground%288%29.jpg


Timu ya Yanga​
Ikiwa inakabiliwa na ushindani mkali katika kampeni yake ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na pia mashindano ya Klabu Bingwa Afrika, programu za mazoezi ya Yanga inashindwa kutekelezeka kikamilifu kutokana na wachezaji wake kutopata mishahara yao ya miezi miwili.Mishahara hiyo ambayo wachezaji wanadai ni ya mwezi Novemba na Desemba, ambao umeambatana na sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.
Kwa mujibu wa habari ambazo gazeti hili imezipata ni kwamba mbali na wachezaji hao, pia wafanyakazi wengine walioajiriwa na klabu hiyo hawajalipwa kwa muda wa miezi mitatu sasa.
Chanzo hicho kiliongeza kuwa hali hiyo ya ukata imechangia mambo mengi kutofanyika kama ilivyotarajiwa ikiwemo kuvurugika kwa programu ya mazoezi.
"Hali ni mbaya, klabu haina pesa, mambo mengi hayafanyiki kama ilivyokusudiwa, tunajaribu kufanya kila linalowezekana ili kutatua tatizo hili linalotukabili," alisema mmoja wa viongozi wa Yanga ambaye hakutaka jina lake litajwe.
Aliongeza kuwa kukosekana kwa fedha kutoka kwa aliyekuwa mfadhili wao na mapato madogo ya mlangoni yaliyokuwa yakipatikana katika mechi za mzunguko wa kwanza wa ligi ndio sababu nyingine iliyofanya klabu yao ikose fedha za kujiendesha.

Mambo yaliyonipa raha kwenye hiyo habari uliyoleta
1. Yanga ni ya kimataifa kitambo kumbe
2. Wapo wachezaji walikuwa first eleven 2011 mpaka leo wapo first elven duh
 
Kwa hili nawaunga mkono viongozi, pale hatukuwa na kocha.

Kaka katavi suala hapo wameshindana maslahi,lakin kopunovic bonge la kocha.tatizo kopunovic anataka mshahara mkubwa wakat mtu mzima alijisemea kuwa simba hali ni mbaya ya kiuchumi.
 
Hivo James siang'a aliendaga wap?

Mkuu, "mtalaamu" James Aggrey Siang'a yupo nchini kwao akiwa katika hali isiyo nzuri.. kwani anasumbuliwa na kisukari pia kakatwa mguu mmoja. Kazi anayofanya sasa ni kupiga tempo ya kufundsha soka mara moja moja katka akademi na shule mbali mbali nchini Kenya.
 
Mkuu, "mtalaamu" James Aggrey Siang'a yupo nchini kwao akiwa katika hali isiyo nzuri.. kwani anasumbuliwa na kisukari pia kakatwa mguu mmoja. Kazi anayofanya sasa ni kupiga tempo ya kufundsha soka mara moja moja katka akademi na shule mbali mbali nchini Kenya.

Hivi Simba imemchangia kiasi gani kwa ajili ya matibabu yake?
 
Hivi Simba imemchangia kiasi gani kwa ajili ya matibabu yake?

Sifahamu ni kwa kiasi gani Simba Sc imemsaidia... ila..

Siang'a alishafundisha timu ya taifa lake.. lakini mpaka sasa serikali yake haina habari nae.

Siang'a alishafundsha Mtibwa, Kagera, nadhani na Moro United akiwa Tanzania bila kusahau timu kadhaa za nchini kwake.. lakini zote hizo hazina habari nae.

Jambo la msingi ni hizi timu kukaa pamoja na kuona zinamsaidiaje, japo si lazima.
 
Kocha huyu anasubiri nini au hawana pesa ya kocha mpya
 
Back
Top Bottom