Simba & Yanga Special Thread

Simba & Yanga Special Thread

Yanga - Juzi, Jana, Leo na Kesho.....
Yanga ni level nyingine Simba watasubiri sana
muwe na akiba ya maneno. inamaana hata historia ya mechi zilizopita na hii hii yanga ya sasa (hapa najumuisha mechi zote za ndani(vpl) na zile za kimataifa, hamwezi kucalculate mkaona kwamba probility ya kushinda game ijayo ni almost non(0.002..)??)
probability={Number
of favorable outcomes}/
{Total number of possible
outcomes}
muache kelele maana aibu inawaijieni!
 
Simba haijadai pont za mezani, bali ni Yanga, kama huna habari uliza, maana wengine mnafuatilia mechi ya Simba na yanga tu basi.
Hahaha we chopeko kweli,kwa taarifa yako mi sio ndezi kwenye sports kama wewe,huna uwezo wa kufanana na Mimi kwenye hiyo idara,hebu nipe mfano halisi lini na wapi yanga alipewa ushindi wa mezani?kisha uje uniambie kwanini msimu uliopita simba na stend mechi ilichezwa dk 101 kule shinyanga?
 
Wakuu nitakuwa nawawekea hapa kila kinachojiri kutoka kambi mbili za timu hizi zikijiandaa na mechi kali ya tarehe 1.
 
14517566_1281909241851606_6567984784771585369_n.jpg
 
VIINGILIO VYA MECHI KATI YA YANGA VS SIMBA.

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limetangaza viingilio vya mchezo wa 'Watani wa Jadi' Simba na Yanga wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara utakaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi Octoba mosi.

Simba inakutana na watani wao wakiwa vinara wa ligi baada ya kushinda Michezo mitano na kutoka sare mmoja huku Yanga wakishinda mitatu, kutoka sare mmoja na kupoteza mmoja.

Afisa Habari wa TFF Alfred Lucas amevitaja viingilio hivyo kuwa VIP A ni sh 30,000 VIP B & C sh 20,000 na mzunguko utakuwa sh 7,000.

Mashabiki watakaotaka kushuhudia mtanange huo uwanjani watatakiwa kutumia tiketi za Kielectoniki ambazo ndiyo pekee zitakazowezesha kuutazama mchezo huo ambao unaziba mianya yote ya kuingia bila kulipa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni ya Selecom ambao ndiyo wasimamizi wa tiketi hizo Galus Runyeta alisema tiketi hizo zitaanza kuuzwa kuanzia kesho katika vituo mbali mbali jijini hapa.

Baadhi ya vituo hivyo ni Vituo vya mafuta vya Total, Village Supermarket, Vituo vya mafuta ya Puma, Samaki Samaki, Buguruni Sheli, Mlimani City, Sinza Africa Sana na Uwanja wa Taifa.

Aidha Galus amewataka mashabiki wa timu hizo kununua tiketi mapema kuanzia kesho katika vituo tajwa ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza siku ya mtanange huo.
 
Yanga akifungwa na Simba nafuta akaunti ya Jf lol
 
Simba team, funga vyura hao
Nimejifunza kuwa katika mechi za watani, mashabiki wanaokuwa over ambitious ndio wale timu yao hufungwa. Kwa ilivyo kwa sasa hakuna ubishi Simba SC wako over ambitious wakicheza mpira kwenye midomo yao na kujivunia timu ambayo hawana uhakika nayo.

Kwa kuzingatia rekodi za nyuma, Yanga tayari imeshashinda maana haichezi mpira wa mdomoni.

Mwenye kutamba na atambe sana lakini matokeo ya mwisho ni Yanga 2-0 Simba.

Salaam kwa watani Simba Sc kutoka kwa vijana wa Jangwani Yanga africa

Simba kapakatwa.png


Bye bye, tuonane hapa jamvini Oktoba Mosi, 2016.
 
Back
Top Bottom