Simbachawene: Kati ya majambazi 10 wanaokamatwa, 3 wanatoka gerezani

Simbachawene: Kati ya majambazi 10 wanaokamatwa, 3 wanatoka gerezani

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1625484443477.png

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema katika operesheni ya kuwasaka majambazi inayoendelea nchini kati ya majambazi kumi wanaokamatwa mitaani, watatu wanatoka gerezeni.

Amesema kuwafunga majambazi hao hakusaidii sana kwa sababu wanarudi mitaani na kuendelea kufanya uhalifu wa aina mbalimbali pamoja na kuwaua watu wenye haki, hivyo watatafuta namna nyingine ambayo watamalizana na majambazi hayo.

Waziri Simbachawene amezungumza hayo katika Kata ya Pwaga, Jimbo la Kibakwe, Wilayani Mpwapwa, katika ziara yake inayoendelea ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake, ambapo amesema licha ya kuwa wamemalizana na majambazi hayo lakini bado Jeshi la Polisi linaendelea na operesheni ya kuwasaka itakayo kamilika Julai 28, mwaka huu.

Aidha, Waziri Simbachawene alisema wanaohusika na uhalifu ni watu wanaotoka katika jamii, wananchi wanawajua, ili kudhibiti matukio ya uhalifu wananchi hao wanapaswa kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kuwafichua wanaofanya uhalifu huo katika sehemu wanazoishi.

Alisema Jeshi la Polisi haliwezi kuwa na askari kila mahali ni jukumu la wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa ajili ya usalama wao kwa kutoa taarifa sahihi juu ya uhalifu na wahalifu, lakini pia kwa kushiriki katika ulinzi pamoja na Jeshi la Polisi na ndiyo tunaita ulinzi shirikishi.

PIA SOMA:
- Waziri Simbachawene: Majambazi yamenyamazishwa kimyakimya nchini, msako wabakaji, waporaji waendelea
 
Amesema kuwafunga majambazi hao hakusaidii sana kwa sababu wanarudi mitaani na kuendelea kufanya uhalifu wa aina mbalimbali pamoja na kuwaua watu wenye haki, hivyo watatafuta namna nyingine ambayo watamalizana na majambazi hayo.
Ile mbinu aliyowaachia Mwendazake imewashinda!
 
Ndugu yako akipotea kwa muda mrefu wekeni matanga
 
Kwa maana hiyo asilimia kubwa ya majambazi hawajawahi kwenda jela
Pertinent observation! Yaani asilimia 70% ya majambazi hawajawahi kufungwa gerezani. Haya juhudi za kuwakamata na kuwafunga ziendelee.
 
Yuko RPC mmoja wa zamani Alfred Gewe,. Huyu mwamba alikua hacheki na nyani.
Sijui Yuko wapi huyu kiongozi mstaafu
 
Aisee, jambazi wanamwachia!! Hawa ni kuuwa tu hakuna cha huruma hapo....wameshauwa wangapi huko nyuma n then mnawaachia kweli!! Au wakusingiziwa?
 
Nadhani pengine ameremba maneno tu, labda atakuwa anamaanisha, wizi mkubwa mkubwa unafanywa na wafungwa(majambazi waliokatwa na kuhukumiwa tayari), wakipiga maela ya watu benki kwa michongo ya washika mpini, wanarudi zao kiotani, mtatafuta weeee, hola.

Kwahiyo sasa, wale waliokamatwa tukioni pengine ndo wamebainika kuwa kati ya 10, 3 tayari ni wafungwa, hapo utakuta naye anatuuliza, wanatokaje tokaje gerezani kuja kufanya kazi maalum?
 
Back
Top Bottom