Simbachawene: Kupata kitambulisho cha NIDA siyo mwarobaini wa kutokuulizwa uraia wako

Kwa maneno ya waziri maana yake suala la uraia wa mtu ni open ended question, hata uwe na aina gani ya ID muda wowote tunaweza kurudi tena kwenye swala la uraia.
Huyo akili zake na Ndugaye hazina tofauti
 
Kwa nchi za wenzetu Simbachawene angepaswa kujiuzulu leo leo. Huo ni UPUMBAVU wa hali ya juu kwa kuwa Tanzania kabla ya vitambulisho vya NIDA ni sawa na Watanzania BAADA ya vitambulisho vya NIDA.

Ni upotevu wa Fedha za walipa Kodi wa Tanzania
Jiwe alikuwa anaweka watu wasiyo hitaji kutumia elimu na weledi ili wasimuhoji
 
Labda sawa lkn alikipataje?!!
 
Basi visitishwe kwasababu vinafuja pesa zetu za sis walipa kodi
Kea kweli katoa tafsiri nzuri,ni wengi wangekuwa wakidhani kuwa na hicho kitambulisho kumehalilisha uraia wao.
 
Point yake nini sasa hapa?! Kwamba mtu apewe kwanza halafu ataulizwa badae kuhusu uhalali wa uraia wake nchini?! Kwanini asiulizwe kwanza kabla ya kupewa icho kitambulisho?! Haoni ni upotevu wa pesa za serikali na kutokujipanga vizuri kwenye huo mchakato?!
 
Hii kama siyo kitambulisho serekali inachezea kori zetu
 
Ki ukweli hivi vitambulisho vya NIDA, watu wengi tu ambao sio raia wa Tz, wanavyo na hii ni kutokana na utaratibu mbovu/rushwa.wakitaka hili zoezi lije liwe lenye manufaa waliyokusudia wangeanzisha utaratibu pale mtoto tu anapozaliwa kinaandaliwa na kupewa hapo hapo.sio haya mtu anakuwa mtu mzima ndio akifuatilie.
 
Hii nchi ina watu wa Ajabu sana.
 
Sasa kitambulisho cha taifa utampaje Tu kila MTU bila kumuhoji.yaani umpe alafu baadae ndo uje umuulize utaifa wake?
Tatizo ni jinsi uteuzi wake ulivyofanywa ndiyo shida inaanzia hapo
 
Mbona Mussa Assad alishawaongolea watu sampuli hii siku nyingi kuwa vilaza wapo wengi🤣🤣
 
Huyu simbachawene na yale mamiwani yake ni kama ana mtindio wa ubongo.
 
Kwahiyo Kitambulisho cha Kupigia Kura ndicho kimachomtambulisha Mtanzania au na chenyewe Wanapewa hadi Wakimbizi?
 
Viongozi wasiojua Taifa linataka nini ndio waliojaa kwenye baraza la Mawaziri.

Kabisa mkuu. Anamalizia kwa kusema mtu atanyang’anywa ikigundulika sio raia!! Hapo hapo akisema vitambulisho vhivo vinatolewa kwa raia, wakimbizi na wakazi wahamiaji.

Yaani tunakuwaje na watu wa namna hii wakiongoza?? Hiki ni kitambulisho cha utaifa. Huo mchakato tofauti hata hausemi na unaishia kupewa utambulisho kinaitwaje hasemi pia!!
 
Acha kuspin amesema Vitambulisho vya URAIA hutolewa kihalali hata kwa Wahamiaji wakazi na Wakimbizi.
 
Kule uhamiaji watu wanaenda kufanya nini ili wapate kitambulisho hiki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…