Simiyu: Mkuu wa Wilaya ya Busega: Nimepigwa mawe wakati wa Maandamano, tumewakamata Watu 108

Simiyu: Mkuu wa Wilaya ya Busega: Nimepigwa mawe wakati wa Maandamano, tumewakamata Watu 108

Mwenyekiti anadai alitoa taarifa na wakaambiwa wasubiri viongozi kutoka wilayani....mkuu wa wilaya anasema hajui lolote, dah
 
Kuna kitu kinaendelea..hao wananchi mpaka wamefanya kitu kama hicho lazima kuna jambo....Inashangaza sana kiongozi anasema hana taarifa...yajao yanatisha sana...
 
Failed state, unakamata vipi watu 108, hayo ni matumizi mabaya ya resources za nchi.

Jeshi la polisi acheni uvivu, jikiteni katika kufanya uchunguzi na kubaini wahusika haswa ni kina nani, acheni kurahisisha mambo
 
Wakati baadhi ya Wananchi wakikiri kuwa kuna Watu kadhaa wanahofiwa kufariki kutokana na kupigwa risasi na Polisi wakijaribu kuwatawanya kwenye maandamano yaliyofanywa na Wananchi huko Busega Mkoani Simiyu leo, imethibitika kuwa Mkuu wa Wilaya ya Busega Faiza Salim pamoja na Maofisa wengine wamejeruhiwa kwa mawe na Wananchi hao.


@AyoTV_ imeelezwa kuwa Wananchi walimrushia Mkuu huyo wa Wilaya mawe wakati akiwasogelea kwa nia ya kuwasikiliza ambapo hawakutaka Kiongozi huyo kufanya chochote na kuanza kumrushia mawe yaliyopelekea kujeruhiwa kwenye ubavu na mgongoni huku Maofisa wengine aliokuwa ameambatana nao ambao ni Kamanda wa Zimamoto Simiyu na Kaimu Afisa wa TAKUKURU Simiyu wakijeruhiwa kichwani na kupelekea kushonwa nyuzi.


Kwa sasa hali zao zinaendelea vizuri na wameruhusiwa kwenda nyumbani baada ya kupata matibabu.


Wananchi wa Busega waliandamana leo hadi Kituo cha Polisi baada ya kuchoshwa na kushamiri kwa matukio ya Watoto wao kupotea katika eneo la Lamadi bila Polisi kuchukua hatua za kuridhisha kudhibiti matukio hayo. #MillardAyoUPDATES


View: https://x.com/millardayo/status/1826314931727466877?t=QgmZBVl1PdkVwqECySfnXA&s=19
 
Akizungumzia maandamano yaliyotokea Lamadi, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, Faiza Salim amesema athari zilizotokea baadhi ya Viongozi kushambuliwa kwa kupigwa mawe akiwemo yeye (Faiza).

Amesema kwa muda wa miezi minne aliyokuwa katika nafasi hiyo hajapata taarifa ya Watoto kupotea. Amesema “Mabomu ya machozi yamepigwa kwa kuwa walizuia magari yote, wameharibu Miundombinu, maduka... Mamlaka hatuwezi kukubali hilo.”

Kuhusu taarifa za Waandamanaji kupoteza maisha, amesema “Sijapokea taarifa kama kuna mtu amekufa, inawezekana yapo majeraha madogo, baadaye tukimaliza oparesheni tutatoa taarifa kamili, mpaka sasa tumewakamata Wtu 108 na tunawapeleka Mahakamani.”

Pia Soma ~ Simiyu: Wananchi wavamia Kituo cha Polisi wakidai kuna matukio mengi ya Watoto kupotea

Kuna mwanzo wa ngoma..hapo DC
 
Jeshi la polisi lichukulie hilo suala kwa uzito,wananchi wameghadhibika,wanalipa kodi ili walindwe wao na mali zao,halafu watoto wanapotea.
Walishuhgulikie hilo suala kwa weledi.
 
Akizungumzia maandamano yaliyotokea Lamadi, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, Faiza Salim amesema athari zilizotokea baadhi ya Viongozi kushambuliwa kwa kupigwa mawe akiwemo yeye (Faiza).

Amesema kwa muda wa miezi minne aliyokuwa katika nafasi hiyo hajapata taarifa ya Watoto kupotea. Amesema “Mabomu ya machozi yamepigwa kwa kuwa walizuia magari yote, wameharibu Miundombinu, maduka... Mamlaka hatuwezi kukubali hilo.”

Kuhusu taarifa za Waandamanaji kupoteza maisha, amesema “Sijapokea taarifa kama kuna mtu amekufa, inawezekana yapo majeraha madogo, baadaye tukimaliza oparesheni tutatoa taarifa kamili, mpaka sasa tumewakamata Wtu 108 na tunawapeleka Mahakamani.”

Pia Soma ~ Simiyu: Wananchi wavamia Kituo cha Polisi wakidai kuna matukio mengi ya Watoto kupotea
Wangekukata na kichwa kabisa
 
Kuna msemo unasemaga no sweet without sweat,kama unataka mabadiriko lazima kuyatafta kwa nguvu maana demokrasia imeshindwa.

Hapo anasema tangu afike huko hajawahi kuletewa kesi ya kupotea kwa mtoto? Tuseme hao watu wamerukwa na akili mpaka wafanye fujo zisizo na tijan?
Yeye kama district commissioner lazima awajibike siyo kila siku anakuja na ngonjera za kukanusha wakati watoto wanapotea,

Kama umeletewa hizo kesi mara nyingi lakini hakuna la maana umefanya kwanini wasichukue Sheria?
Hilo nalo ni neno.
 
Akizungumzia maandamano yaliyotokea Lamadi, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, Faiza Salim amesema athari zilizotokea baadhi ya Viongozi kushambuliwa kwa kupigwa mawe akiwemo yeye (Faiza).

Amesema kwa muda wa miezi minne aliyokuwa katika nafasi hiyo hajapata taarifa ya Watoto kupotea. Amesema “Mabomu ya machozi yamepigwa kwa kuwa walizuia magari yote, wameharibu Miundombinu, maduka... Mamlaka hatuwezi kukubali hilo.”

Kuhusu taarifa za Waandamanaji kupoteza maisha, amesema “Sijapokea taarifa kama kuna mtu amekufa, inawezekana yapo majeraha madogo, baadaye tukimaliza oparesheni tutatoa taarifa kamili, mpaka sasa tumewakamata Wtu 108 na tunawapeleka Mahakamani.”

Pia Soma ~ Simiyu: Wananchi wavamia Kituo cha Polisi wakidai kuna matukio mengi ya Watoto kupotea
Washughulikiwe wote waliotaka kuvamia Polisi,kukiteka na kuchukua sheria mkononi
 
Back
Top Bottom