Jabali la Siasa
JF-Expert Member
- Jul 10, 2020
- 2,823
- 2,466
===
Mr Daniel Jilala mwenye umri wa miaka 43 ambaye ni katibu wa chama cha msingi cha Ushirika AMCOS,
Mkazi wa kijiji cha Sulu wilaya ya Maswa mkoani Simiyu amekutwa amejinyonga kwa kamba kwenye mti jana jioni Mei27, 2022,
Bwana Jilala ameacha ujumbe wa simu( sms) aliomtumia mmoja wa afisa wa TAKUKURU ulioshiria kuwa ni muhanga wa opareshen inayoendeshwa na RC Kafulila wa Mkoani Simiyu,
RC David Kafulila ameanzisha operesheni hii ili kusafisha uozo ndani ya vyama Ushirika,
Mtakumbuka oparesgen hii ina baraka za Rais Samia Suluhu Hassan,
Simu ya marehemu imekutwa na ujumbe aliomtumia kwa mmoja wa maofisa TAKUKURU wilaya Maswa mwenye namba 0622591912 uliosomeka
" NIMEAMUA KUJIUA KWASABABU SIJASAIDIWA , NAOMBWA RUSHWA KILA SIKU NA AFISA USHIRIKA BUDODI KUWA ANAWAPELEKEA TAKUKURU MKOA LAKINI SIONI MATUMAINI YA SUALA LANGU NA INAELEKEA NITAFUNGWA, SASA SIONI SABABU KUISHI KWANI SIJUI WANANGU WATAISHIJE IKIWA NITAFUNGWA"
April 4, 2022 akigawa pikipiki Dodoma kwa maofisa ugani nchi nzima tukio lilioandaliwa na wizara ya Kilimo,
Rais Samia Sukuhu Hassan alimwelekeza Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mhe David Kafulila kuendelea kudhibiti wizi wa pembejeo za pamba na michezo michafu kwenye vyama vya ushirika na Ushirika..
" Nakuagiza Kafulila, endelea kuwakaba, najua wapo ambao mliowafungulia mpaka kesi za uhujumu uchumi kwa wizi wa madawa ya pamba. Nasisitiza endelea kuwakaba wezi wa pembejeo na ushirika wote tena kwa hatua kali mpaka wazijue rangi zangu" aliagiza Rais Samia Suluhu Hassan,
Katika utekelezaji huo RC Kafulila aliwaondoa maofisa ushirika wote ngazi ya wilaya na kuelekeza wapangiwe kazi zingine wilayani kwani ni sehemu ya madhaifu ya usimamizi wa ushirika na hujuma kwa wakulima pamba.
Mpaka sasa vyama vya msingi 182 kati ya 335 vimefanyiwa uchunguzi na TAKUKURU ambapo nyingi zimerejesha fedha ama za wakulima au wanunuzi na kubaki AMCOS 37.