TANZIA Simpasa Eliakim, Mwenyekiti wa kamati ya haki za Bunge 2000-2005 afariki dunia

TANZIA Simpasa Eliakim, Mwenyekiti wa kamati ya haki za Bunge 2000-2005 afariki dunia

Mlendamboga

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2011
Posts
667
Reaction score
338
IMG-20200525-WA0023.jpg

Aliyekuwa mbunge wa Mbozi Magharibi na baadaye jimbo hilo kubadilishwa na kuitwa Momba Miaka ya 1995-2005 Eliakim Simpasa amefariki majira ya saa 7 mchana leo hii katika hospitali ya Mkoa wa Songwe.

Simpasa ambaye aliongoza kamat ya Haki, maadili na Madaraka ya Bunge atakumbukwa namna alivyokuwa kinara wa kuita watu bungeni wakahojiwe pale walipokuwa wakijaribu kugusa mhimili wa Bunge.

Miongoni mwa walioitwa mbele ya kamati ya Simpasa kama walivyoiita watu ni pamoja na Mama Terry, Uongozi wa ITV na Radio one pale mijadala ya kipindi alichoshiriki mama Terry kugusia namna utendaji wa bunge ulivyokuwa hauwaridhishi wananchi, lakini kamati hiyo haikuridhishwa na uendeshaji wa kipindi hicho na kuwaita kuhojiwa.

Simpasa aliangushwa kwenye kiti cha ubunge na Dr Luka Siame 2005-2010, na baadaye jimbo hilo likachukuliwa na Silinde kwa vipindi viwili.

======

UPDATES:

Mwili utasafirishwa kesho trh 26~5~2020 saa 3:00 Asubuhi kutoka vwawa kuelekea Kapele, na mazishi yatakuwa keshokutwa.
 
View attachment 1459584
Aliyekuwa mbunge wa Mbozi Magharibi na baadaye jimbo hilo kubadilishwa na kuitwa Momba Miaka ya 1995-2005 Eliakim Simpasa amefariki majira ya saa 7 mchana leo hii katika hospitali ya Mkoa wa Songwe.

Simpasa ambaye aliongoza kamat ya Haki, maadili na Madaraka ya Bunge atakumbukwa namna alivyokuwa kinara wa kuita watu bungeni wakahojiwe pale walipokuwa wakijaribu kugusa mhimili wa Bunge.

Miongoni mwa walioitwa mbele ya kamati ya Simpasa kama walivyoiita watu ni pamoja na Mama Terry, Uongozi wa ITV na Radio one pale mijadala ya kipindi alichoshiriki mama Terry kugusia namna utendaji wa bunge ulivyokuwa hauwaridhishi wananchi, lakini kamati hiyo haikuridhishwa na uendeshaji wa kipindi hicho na kuwaita kuhojiwa.

Simpasa aliangushwa kwenye kiti cha ubunge na Dr Luka Siame 2005-2010, na baadaye jimbo hilo likachukuliwa na Silinde kwa vipindi viwili.
View attachment 1459583
Rip Simpasa!
 
RIP hii corona kwanini inawamaliza chama tawala ?

Toka maktaba : makubwa aliyoyafanya kwa wananchi wa Momba mkoa wa Songwe Tanzania ni kuwaasa CCM kuwa maendeleo hayana chama waache kubagua !
Tuweke itikadi za siasa kando kwa Maendeleo-CCM
JUMANNE , 1ST MAR , 2016
Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Momba mkoani Songwe kimewataka madiwani wa halmashauri ya wilaya kujenga umoja na mshikamano pasipo kubaguana kutokana na itikadi za vyama.



Mombaa.JPG

Kikao cha balaza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Momba
Mwenyekiti wa CCM wilayani humo Eliakim Simpasa ametoa nasaha hizo kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Momba kilichokuwa maalumu kwajili ya kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017.
Simpasa amesema kuingizwa kwa itikadi za vyama katika utoaji maamuzi ya halmashauri kunaweza kusababisha mambo ya msingi kukwama na hivyo kusababisha wanancho kutonufaika na vipaumbele wanavyoviibua kwenye maeneo yao.
Amewataka madiwani hao kuwa mfano wa kuigwa na halmashauri nyingine kwa kufanya kazi kwa umoja kwakuwa nyumba wanayojenga ni moja hivyo hakuna haja ya kugombania fito.
Simpasa pia amesema ushirikiano baina ya madiwani na wataalamu wa halmashauri ni jambo muhimu kwakuwa pande hizo mbili zinategemeana katika utekelezaji wa majukumu wenye tija kwa jamii zinazoitumikia.
Amesema tabia ya madiwani kujenga ukuta kati yao na watendaji ndiyo chanzo cha kuzorota kwa maendeleo ya halmashauri kwakuwa wakati madiwani wakipanga kuwaazimia watendaji, wao watakuwa wakipanga kukwamisha mikakati inayowekwa na vikao vya baraza. Source : Tuweke itikadi za siasa kando kwa Maendeleo-CCM | East Africa Television
 
Back
Top Bottom