Simshangai Pasco wa JF tu; hapana, nawashangaa waandishi wote wa habari popote pale mlipo nchini!

Simshangai Pasco wa JF tu; hapana, nawashangaa waandishi wote wa habari popote pale mlipo nchini!

Kama nimemwelewa vizuri Faiza,anasema:Marehemu Mwangosi alienda kumvaa kamanda wa kikosi cha FFU na siyo RPC kwa uelewa wangu hawa ni watu wawili tofauti au siyo Faiza?

Hata kama ndivyo ilivyokuwa unadhani polisi walikuwa na haki ya kumuua Mwangosi?

BTW huo utetezi wa Mwangosi kumvaa kiongozi wa FFU ni upotoshaji mkubwa coz Mwangozi alikuwa anamuhoji huyo Mkuu wa FFU na sio kumvamia. Polisi waliunda zengwe ili angalau kwa 0.000001% ionekane marehemu alikuwa na kosa. Lakini hatakama marehemu angekuwa amefanya kosa kubwa kiasi gani ilitakiwa ashitakiwe na sio kuuwawa. Kwa nijuavyo mimi Polisi polisi wapo kusimamia sheria sio wao kuchukua sheria mkononi au Kutoa hukumu yakifo. Polisi hana mamlaka yakutoa hukumu.
 
Pasco yupi? Huyu ambae hana mkono? kama ni huyo yeye ni msakatonge balaa eti mayala mayala wakuzaliwa mzizima huyo si mkwele tu alianza muzilil akapewa zawadi yake kafuatia huyo msakatonge sasa yule kiongozi wao mkwele yeye atakua majivu kwenye ndege.
 
Kama nimemwelewa vizuri Faiza,anasema:Marehemu Mwangosi alienda kumvaa kamanda wa kikosi cha FFU na siyo RPC kwa uelewa wangu hawa ni watu wawili tofauti au siyo Faiza?

Hata taarifa unayoitoa ni potofu.. Wewe umeona mahali popote Mwangosi anamvaa kamanda wa FFU? Mbona wengine mnapenda kutetea ujinga na wajinga?
 
Kama nimemwelewa vizuri Faiza,anasema:Marehemu Mwangosi alienda kumvaa kamanda wa kikosi cha FFU na siyo RPC kwa uelewa wangu hawa ni watu wawili tofauti au siyo Faiza?
Na wewe unaamini hivyo? Kwamba Marehemu Mwangosi alienda kumvaa kamanda wa kikosi cha FFU? Ili iweje? mjumbe msitu, ngoja nikusaidie kidogo; bila picha kuonesha tukio, njama zilikwishapangwa na vyombo vya dola kuwabambikia kesi viongozi wa Chadema kama wahusika wakuu wa mauaji hayo. Na wapo waandishi wa habari ni kweli walishalishupalia hilo tamko la msemaji wa polisi kwamba katika harakati za kupambana na dola ni Chadema waliowatupia polisi kitu kilichosadikiwa ni bomu na kwa bahati mbaya kikamlipukia Marehemu Mwangosi.

mjumbe msitu, amini usiamini ambacho kingefuatia ni viongozi wa Chadema kukamatwa na kufunguliwa kesi ya kusababisha mauaji! Nina wasi wasi hadi leo labda wengine wao wangekuwa bado wapo jela kama si hiyo picha ikiwaonesha wauaji halisi, kikosi cha FFU. Dai kama hilo liliwahi kutolewa pale polisi walipomuuwa raia mwingine muuza magazeti mkoani Morogoro, Marehemu Ally Zona, chini ya usimamizi wa afande mwingine Faustine Shilogile siku chache tu kabla ya tukio hili la Iringa. Kama kawaida ilidaiwa ni wana Chadema waliorusha kilichasadikiwa ni risasi na kumpata Marehemu kichwani na si risasi ya moto iliyorushwa na polisi.

Hata pale bomu lilipolipuka wakati wa mkutano wa Chadema pale Arusha mwaka moja baadaye, madai yalikuwa ni hayo hayo pamoja na ukweli kuwa waliojeruhiwa na wengine kupoteza maisha ni wapenzi wa Chadema. Lakini kwa hili la Marehemu Mwangosi, polisi walikosea stepu...walitoa tamko lao kabla hata ya kujua safari hii upo ushahidi unaoonesha uovu wao. Na hapa ndipo nawalaumu waandishi wa habari; walipouawa wanaharakati walikaa kimya, wakauawa wana siasa wakakaa kimya, na walipouawa wananchi wasio na hatia wakakaa kimya, hawakujua kuna siku yatawafika wao! Cha ajabu pamoja na Nyololo kuwafungua macho, wamezidi kuficha kalamu zao!
 
Mkuu Mag 3, kwanza asante kutukumbushia hili la Mwangosi japo kwa kiasi fulani umetonesha vidonda vya machungu yaliyopita, lakini pia sometimes ni muhimu kukumbushana ili follow up ya kinachoendelea iendelee kufuatiliwa kwa kupashana habari!...
  1. Kabla ya kilichokuta Daudi Mwangosi, niliwahi kuupandisha huu uzi humu,Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to Know...
Asante sana Pasco kwa maelezo murua ingawa kuna watu wanashangaa mimi kukutaja...wanauliza, kwa nini wewe na huku waandishi lukuki wamo humu! Nia yangu ilikuwa ni kufikisha tu ujumbe na nadhani japo umeweza kuwafikia wengi pamoja na hao wanaodaiwa wako humu. Naomba tu nikusahihishe kitu kimoja; ni kweli jitihada zako zilionekana humu ila mada Police Brutality in Tanzania: The World has a right to know...ilianzishwa na Mag3 tarehe 15 November, 2011 kama ifuatavyo;

[h=2]Police brutality in Tanzania, the world has a right to know![/h]
UDSM-violence.jpg



Tanzania is slowly turning into a brutal police state right in front of our own very eyes, yet we are doing nothing about it. Police brutality is slowly reaching unbearable limits as witnessed by us all day in and day out, yet we are all quiet about it. The audacity of the police force to beat and even murder innocent citizens of the republic is happening in every corner of our nation, yet there isn’t a single voice being raised in condemnation. Not even our own school children have been spared from these blood thirsty members of the police force in their quest to instill fear and intimidation, yet we all pretend like nothing is happening and look the other way.

It is high time the world is told the truth about Tanzania, it is high time the whole world learns of Tanzania’s state sponsored terrorism against its own very people. But who’s to tell the world if not us, the very people who have been a witness to all this, yet have not had the courage to do anything about it. Yes, whether we like it or not, we have been a party to these horrendous crimes against us by the very people to whom we entrusted our hopes to keep us safe. I now call upon all peace loving members of our beloved JF to join forces and expose this power hungry and corrupt regime that will stop at nothing to hang on to power at our expense.

Let us gather all evidence especially pictures and let the whole world see for themselves what we are daily going through in this land of plenty yet one of the poorest in the region. Any Tom, Dick or Harry who happens to be a Kikwete appointee can at will order the police to beat, teargas, shoot and even kill anybody, anywhere, anytime and anyhow the usual excuse being “kulinda amani “ Pictures, comrades, speak louder than words so bring them and if you cannot upload them please PM them to me ! I start with this one above !

Yaonekana mods walikuja kuunganisha mada kutoka kwa watu mbali mbali...hata hivyo tuko pamoja, vitendo vya polisi nchini ni vya kulaaniwa na wapenda amani popote pale walipo. Tumeshuhudia watoto wa chekechea wakitupiwa mabomu ya machozi, akina mama waja wazito wakirushiwa mabomu ya machozi, waalimu wakitawanywa kwa mabomu ya machozi...yaani lugha ya polisi wetu ni mabomu ya machozi, maji ya kuwasha, risasi za moto; hata pale raia wema hawana hata fimbo mkononi!
 
Last edited by a moderator:
Samahani, humu ndani mimi simjui mwandishi yeyote mwingine zaidi ya Pasco...nafikiri akipata ujumbe atanisaidia kuufikisha kwa wana taaluma wenzake.

Nikipata nafasi nitakujibu kitu kupitia PM.
Je unajua kuwa kuna kesi juu ya mhusika wa tukio la mauaji? je unajua sheria inasemaje katika kujadili suala lililoko mahakamani? sijui unataka message gani itoke. kila mtu anajua kilichotokea na wahusika ni akina nani? siyo isue ya ku blame waandishi kwamba wamezembea au kitu gani,nadhani kuna tatizo la mfumo na serikali mliyoweka madarakani ambao waandishi pekee hawawezi kubadilisha hii hali,mengine pm
 
Nikipata nafasi nitakujibu kitu kupitia PM.
Je unajua kuwa kuna kesi juu ya mhusika wa tukio la mauaji? je unajua sheria inasemaje katika kujadili suala lililoko mahakamani? sijui unataka message gani itoke. kila mtu anajua kilichotokea na wahusika ni akina nani? siyo isue ya ku blame waandishi kwamba wamezembea au kitu gani,nadhani kuna tatizo la mfumo na serikali mliyoweka madarakani ambao waandishi pekee hawawezi kubadilisha hii hali,mengine pm

Ina maana gani basi ujibu hapa kama unahitaji kum-PM mtu mmoja tu...?si mge-pm-ana huko huko...?Uzi umewekwa hapa watu wote wajadili kuelimishana kwenye chombo chetu cha habari JF.....kuna kipi cha kuficha hapa JF ambapo hata km Rais wa nchi kadokoa hapa hatumfichi tutamuita tu ni mwizi.stand up and be counted!
 
Shughuli za jeshi la polisi zinaongozwa na sheria mbalimbali. Jeshi la polisi lina mamlaka ya kisheria na linapaswa kutumia mamlaka hayo kulingana na taratibu zilizoainishwa katika sheria husika.

Polisi wanaweza kukamata, kufanya upekuzi, kushikilia, kumpeleleza mtuhumiwa, kumhoji shahidi, kufanya mahojiano na mtuhumiwa, kutawanya waandamanaji wenye nia ovu na kuhakikisha usalama wa jamii. Wanapaswa kufanya hivyo kwa kufuata taratibu na sheria na sio vinginevyo. Polisi hawawezi kufanya wapendavyo.

Sheria zinazoongoza utendaji wa Jeshi la Polisi ni:
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai inaeleza njia ambazo polisi na mahakama wanapaswa kufuata katika kuwashughulikia wahalifu. Hii ni pamoja na mamlaka ya polisi na taratibu wanazotakiwa polisi wazifuate. Mfano mmojawapo ni matumizi ya nguvu ya polisi pale anapomkamata mtuhumiwa na nguvu za polisi anapofanya uchunguzi
Sheria ya ushahidi inaeleza kwa undani kinachokubalika mahakamani kama ushahidi. Ushahidi wowote uliopatikana kwa kutumia nguvu, hauwezi kutumika kama ushahidi halali, ikibainika mahakamani kuwa ulipatikana kwa njia batili.
Sheria ya Jeshi la Polisi namba 322 (Police and Auxiliary Services Act 2002 Cap 322).

inaeleza kuhusu uendeshaji wake, nidhamu mamlaka na kazi za polisi na mambo mengine yanayolihusu jeshi la polisi. Sheria hii inasisitiza polisi kutenda haki katika utendaji wao ili kutoa mfano wa kulinda sheria na kanuni za nchi.

Hakuna mahali ambapo sheria imehalalisha wanasiasa kuwatumia Polisi kwa malengo ya kisiasa.

Matumizi yoyote mabaya ya mamlaka au uzembe katika kazi ni utovu wa nidhamu na uhalifu. Afisa wa polisi anayetenda hayo anapaswa kuchukuliwa hatua stahiki.
 
th


Huyo hapo juu ni aliyekuwa mwandishi wa habari na mwakilishi wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, mkoani Iringa, marehemu Daudi Mwangosi. Mwangosi, ambaye alikuwa pia Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), aliuawa kwa kupigwa na bomu na kusambaratisha mwili wake wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuwazuia kufungua tawi la chama hicho, katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani humo, Septemba 2, 2012

296587_4672851945587_1395901855_n.jpg


Pamoja na msemaji wa Polisi mwanzoni kukanusha askari kuhusishwa kwenye tukio la hilo la kuhuzunisha, ushahidi wa picha ulikuja kutolewa ukimuonesha polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) akimlipua Mwangosi ambaye muda huo tayari anakula kichapo kutoka kwa polisi wenzake. Polisi huyo, Pasificus Cleophace Simon (23) mwenye namba G2573 alifanya mauaji hayo mbele ya wakubwa wake akiwemo aliyekuwwa Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya RPC Michael Kamuhanda.

IMG-20120904-WA034.jpg


Mke wa Marehemu, akiwa na uchungu kufuatia kifo cha mumewe akitoa heshima zake za Mwisho siku ya mazishi. Alikuwa na imani kubwa kwamba waandishi wa habari hawangemtelekeza na kwamba kuna siku ukweli ungewekwa wazi na wahusika wote nao waonje machungu kama yaliyompata yeye na wanawe kwani silaha za kujibu mapigo kwa mwenzao wanayo.

582728_4673002029339_659749645_n.jpg



Hapo juu anaonekana Marehemu Daudi Mwangosi akihojiana na RPC Michael Kamuhanda muda mfupi kabla hajafikwa na umauti. Baadaye Michael Kamuhanda alikuja kupandishwa cheo kutoka SACP (Senior Assistant of Police) kwenda DCP (Deputy Comissioner of Police).


Sasa swali langu kwa Pasco na waandishi wote wa habari popote mliopo Tanzania, je mpo? Kama mpo vipi ile silaha yenu ya kalamu inayodaiwa kuwa kali kuliko bomu, kwa Mwangosi mmesalimu amri?
Hapo uliposema alipigwa bomu hadi mwili wake kusambaratishwa umeandika kwa kujua au bahati mbaya?
 
Hapo uliposema alipigwa bomu hadi mwili wake kusambaratishwa umeandika kwa kujua au bahati mbaya?
Heh! Hili lako ndilo tatizo la malimbukeni wanaodandia mambo wasiyoyajua...unashangaa mwili wa marehemu Mwangosi kusambaratishwa kwa bomu! Ulizaliwa lini kijana...kumbuka JF inatunza kumbukumbu na unakaribishwa kupitia mada mbali mbali zilizowasilishwa humu siku za nyuma (naona umejiunga juzi juzi, pole sana)

Kama mods wanaruhusu, ngoja nikuwekee mabaki ya mwili wa Daud Mwangosi baada ya kuuliwa na polisi wetu wa kikosi cha FFU Iringa mwezi wa September mwaka 2012.

daudi-mwangosi-remains-1.jpg


Kama unaitaka picha kubwa zaidi inayoonesha mwili ulivyosambaratishwa vipande vipande ni PM nitakutumia.
Kama si ushahidi wa picha, Chadema walikuwa wameshabambikiziwa kesi ya kuua (kumlipua mwandishi kwa bomu)
Hatun Jeshi la Polisi, tunalo genge la wauaji!​
 
Heh! Hili lako ndilo tatizo la malimbukeni wanaodandia mambo wasiyoyajua...unashangaa mwili wa marehemu Mwangosi kusambaratishwa kwa bomu! Ulizaliwa lini kijana...kumbuka JF inatunza kumbukumbu na unakaribishwa kupitia mada mbali mbali zilizowasilishwa humu siku za nyuma (naona umejiunga juzi juzi, pole sana)

Kama mods wanaruhusu, ngoja nikuwekee mabaki ya mwili wa Daud Mwangosi baada ya kuuliwa na polisi wetu wa kikosi cha FFU Iringa mwezi wa September mwaka 2012.

daudi-mwangosi-remains-1.jpg


Kama unaitaka picha kubwa zaidi inayoonesha mwili ulivyosambaratishwa vipande vipande ni PM nitakutumia.
Kama si ushahidi wa picha, Chadema walikuwa wameshabambikiziwa kesi ya kuua (kumlipua mwandishi kwa bomu)
Hatun Jeshi la Polisi, tunalo genge la wauaji!​
Nilitegemea ujibu kutokana na swali, kuwa una hakika au umeandika bahati mbaya ila cha kushangaza umeanza kwa kunishambulia japo mi huwa sina kinyongo na watu kama wewe.

Hapo kwenye picha askari wanaonekana wame-concentate na kitu kingine kabisa na sio hayo mabaki, nitafsirie hapo maana ni kama hawayaoni (hakuna mabaki)

Pia nitumie tu hiyo picha nyingine na ukimaliza nami nitakwambia nilishiriki vipi hadi kuchimba kaburi lake na kuaga mwili.
 
Mtoa post acha ukuda, kama hoja ni kuuliwa basi wazanzibar walishauliwa sana miaka ya nyuma hadi leo na cjakusikia kusema chochote, sasa ni zamu yenu watanganyika kulinywesha jini ccm damu ya watanganyika acha kulalamika.
  1. Historia yangu na haraka niliwahi kuiweka hapa [h=3]Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar[/h]
    Ni mimi ndie nilyepiga zile picha za vurugu za 1996 kule Zanzibar, na nilishikwa kuswekwa ndani kituo cha Mwembe Madema nikiwa na Ali Saleh na Khalfani Saidi akiwa mpiga picha wa gazeti la Majira. Nikanyang'wa kamera ya DV, polisi wakaniambia niwaonyeshe picha nilizopiga, nikawaambia sijapiga picha!. Wakaichukua kamera kuipeleka TVZ, Mungu bariki, TVZ walikuwa bado wako VHS, DV hawajui, wakairudisha na kuthibitisha hakuna picha!. Nikafukuzwa Zanzibar under escort. Kufika bara, jioni mimi mwenyewe nikatangaza vurugu za Zanzibar na picha juu!. Ulimwengu ukaona!. Picha hizo zilipelekea Kituo cha DTV na Gazeti la Majira kupigwa marufuku Zanzibar!.
    Pia ni mimi niliyetangaza zile vurugu za Mwembechai nikiwa in a line of fire!.
    Hivyo kutangaza police brutality sikuanza jana!.
Natumaini, umenipata.
Paskali
 
th

Huyo hapo juu ni aliyekuwa mwandishi wa habari na mwakilishi wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, mkoani Iringa, marehemu Daudi Mwangosi. Mwangosi, ambaye alikuwa pia Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC), aliuawa kwa kupigwa na bomu na kusambaratisha mwili wake wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuwazuia kufungua tawi la chama hicho, katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani humo, Septemba 2, 2012



296587_4672851945587_1395901855_n.jpg

Pamoja na msemaji wa Polisi mwanzoni kukanusha askari kuhusishwa kwenye tukio la hilo la kuhuzunisha, ushahidi wa picha ulikuja kutolewa ukimuonesha polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) akimlipua Mwangosi ambaye muda huo tayari anakula kichapo kutoka kwa polisi wenzake. Polisi huyo, Pasificus Cleophace Simon (23) mwenye namba G2573 alifanya mauaji hayo mbele ya wakubwa wake akiwemo aliyekuwwa Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya RPC Michael Kamuhanda.



IMG-20120904-WA034.jpg

Mke wa Marehemu, akiwa na uchungu kufuatia kifo cha mumewe akitoa heshima zake za Mwisho siku ya mazishi. Alikuwa na imani kubwa kwamba waandishi wa habari hawangemtelekeza na kwamba kuna siku ukweli ungewekwa wazi na wahusika wote nao waonje machungu kama yaliyompata yeye na wanawe kwani silaha za kujibu mapigo kwa mwenzao wanayo.



582728_4673002029339_659749645_n.jpg


Hapo juu anaonekana Marehemu Daudi Mwangosi akihojiana na RPC Michael Kamuhanda muda mfupi kabla hajafikwa na umauti. Baadaye Michael Kamuhanda alikuja kupandishwa cheo kutoka SACP (Senior Assistant of Police) kwenda DCP (Deputy Comissioner of Police).

Sasa swali langu kwa Pasco na waandishi wote wa habari popote mliopo Tanzania, je mpo? Kama mpo vipi ile silaha yenu ya kalamu inayodaiwa kuwa kali kuliko bomu, kwa Mwangosi mmesalimu amri?
Wanabodi,
Leo ni siku ya kimataifa ya uhuru wa habari, kila mwaka sisi waandishi huwa tunakutana mahali kwa siku 2 na kujadili mambo mbalimbali kuhusu uhuru wa habari, na katika mkusanyiko huo, serikali, vyama vya habari na Taasisi za habari hutoa matamko kede kede kuhusu uhuru wa habari, lakini kwa mwaka huu, kufuatia janga la Corona, hakuna maadhimisho yoyote rasmi ya kukutana, ila nilitegemea wizara ya habari, vyama vya habari na mashirika na Taasisi za habari zitoe matamko mbalimbali.

Bado sijabahatika kuona tamko lolote!, ila usikute zile speech huwa zinaandaliwa kwa ajili ya presentations kwenye kongamano hotelini, safari na per diem!, leo hakuna safari, no trip, no per diem, no hotel gathering, hivyo this time hata speech tuu hakuna?!.

Nawatakia waandishi wenzangu, maadhimisho haya ya kimya kimya, nawashauri wale wafadhili mbalimbali wa tukio hili, kwa vile hatukusafiri, wala kula na kulala hotelini, then naomba hao wafadhili watutumie tuu hizo per diem, tutahama majumbani mwetu na kuhamia hotelini 3 days kisha tutatoa matamko.

Paskali
 
Wanabodi, kwa vile kesho nitakuwa na Waziri wa Habari, Dr. Harrison Mwakyembe tukijadili kuhusu sekta ya Habari, nikipata muda pia nitaulizia kuhusu issue hii ya kihabari, ila na wewe, kama una swali lolote, liulize hapa

Una Swali Lolote kwa Waziri wa Habari, Dk. Harrison Mwakyembe?, Atakuwa Live Star TV, Kuzungumzia Sekta ya Habari na Janga la Corona, Uliza Chochote! - JamiiForums
P.
Muulize kwanini mke wa askari aliyehukumiwa kwa mauaji ya mwangosi alipatiwa ajira kujikimu na maisha kwakuwa mumewe yupo jela na mke wa mwangosi hajapatiwa ajira
 
Sasa swali langu kwa Pasco na waandishi wote wa habari popote mliopo Tanzania, je mpo? Kama mpo vipi ile silaha yenu ya kalamu inayodaiwa kuwa kali kuliko bomu, kwa Mwangosi mmesalimu amri?​
Mkuu Mag3, the pen is mightier than the sword kwa nchi ambazo jamii kubwa ni literates wanasoma maandishi, lakini kwa jamii iliterate kama yetu, the pen doesn't matter much, hivyo baada ya kuwa a pen pusher for more than 30 years, nimegundua pen doesn't matter much, hivyo sasa nimeamua mazima ndani ya ngoma tuicheze na kuleta mabandiko from within.
Hivyo kuna hili jambo langu naomba uungwaji mkono wako lifanikiwe niingie mitaa hii nikasaidie kutokea huku
P
 
. leo hii kuna mwandishi gani mwenye ujasiri kama aliokuwa nao marehemu stan katabalo wa gazeti la mfanyakazi miaka ya mwanzo ya tisini?
Mkuu Grand Jury, waandishi wenye ujasiri huo kama wa Stan Katabalo, tupo, ila zama zimebadilika, kila zama na zama zake!. Kama sisi waandishi wote wa habari wenye ujasiri kama wa Stan Katabalo na wote tukafanya kama Stan, nani angebaki kuuliza maswali kama yale ya Kiti Moto?. Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama... wengine tumechagua ile ama ya pili ndio maana leo tupo!.
Paskali
 
Mkuu Grand Jury, waandishi wenye ujasiri huo kama wa Stan Katabalo, tupo, ila zama zimebadilika, kila zama na zama zake!. Kama sisi waandishi wote wa habari wenye ujasiri kama wa Stan Katabalo na wote tukafanya kama Stan, nani angebaki kuuliza maswali kama yale ya Kiti Moto?. Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama... wengine tumechagua ile ama ya pili ndio maana leo tupo!.
Paskali
Kwahiyo wewe ni mwandishi wa habari mwoga!?
 
Back
Top Bottom