Simuelewi Baba Mkwe wangu

Simuelewi Baba Mkwe wangu

Nimeshangazwa na baba mkwe wangu kuniangalia kwa ukali kila ninapo kutana nae iwe nyumbani kwangu au kwake.

Nimeoa binti yake na mahali nimelipa lakini mpaka leo sijajua kwanini hunionyesha sura ya aina hiyo. Nahisi kama si ukarimu wa mama mkwe wangu ningempiga stop kuja kwangu maana hii ni dalili ya uchawi. Akimuona mwanae anafurahi sana lakini akiniona tu unakua mkinywa mwenye sura ya ukauzu

Hata nilipompa ujauzito binti yake kabla sijamuoa mzee aliwahi kuniambia namtaka mwanae ili nipate ahueni ya kimaisha, lakini sikuwahi kumuomba hata chumvi huyu mzee mwenye mwenye tuhela twa tia maji tia maji.

Mtoto wake na mama mkwe wananipenda sana lakini dingi kauzu dagaa kama mwarabu fighter nipeni ushauri wazee au nimkate kidevu.



By mdau mmoja hapa Dar

Huyo ndo Baba Mkwe! Unamzarau ila kamsomesha mwanae ambaye anakusaidia Na Mshahara wake!
 
Labda umeoa nyumba ndogo yake maana wazee wa karne hii wanakula binti zao.
Ongea na mkeo taratibu juu ya tabia hiyo ya babake labda kuna kitu kimejificha.
 
Kuna umuhimu gani wa kukutana na Baba Mkwe wako mara kwa mara.??
Kutana nae kwa ishu maalum na sio kuzoeana.

Sisi nyumbani ukiwa barabarani ukamuona Baba Mkwe /Mama Mkwe kwa mbali, mmoja wenu ubadilisha njia ili mladi msikutane.
 
Huenda alikua anajitafunia mtoto wake
 
Jikngeze, huyo mzee anaona huna hadhi ya kuwa na mwanae

Alitaka mwanae aoelewe na mtu aliye toka familia yenye status.

Anakuona tuu dunga dunga, yaani play boy unamchezea mwanae na siku si nyingi utamuacha

Hata na hivyo hawez kukutambulisha mbele za watu kuwa ww ni mume wa mwanae
 
Tatizo linaonekana ni kuwa wewe itakua unalelewa na Binti yao ,, chakufanya tafuta pesa ukitoboa ukawa na mkwanja kuliko Binti yao watakuheshimu laa sivyo hawawezi kukuheshimu
 
Tatizo linaonekana ni kuwa wewe itakua unalelewa na Binti yao ,, chakufanya tafuta pesa ukitoboa ukawa na mkwanja kuliko Binti yao watakuheshimu laa sivyo hawawezi kukuheshimu

Hapana naprovide kila kitu mkuu i mean everything
 
Huyo nenda naye kikauzu kama anavyofanya ipo siku uzalendo utamshinda atafunguka tu.
Hili ndio la msingi, wakwe wa dizaini hio ni kuwakazia tu mwanzo mwisho, tena kama una mazoea ya kumpigia simu kumsalimia achana nayo, akishapata wajukuu wawili watatu utamuona anabadilika mwenyewe.
Muhimu jitahidi kila unapohisi anakukwaza we potezea, ila ikifia usiku ukiwa na binti yake unalipa kisasi cha babamkwe.
 
Back
Top Bottom