Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 33 KATI YA 50
?Mh! Kweli mtu hawezi kuona tatizo lake, Latifa wewe hukulala na Big siku ile ukarudi kesho yake mchana? Bora hata mimi nimerudi asubuhi,? akasema Lilian kwa kujiamini.
Wakacheka tena.
Lilian akaamua kuingia bafuni, akaoga haraka kisha akatoka na kujitupa kitandani.
?Sitaki usumbufu leo, hata darasani sitakwenda, nahitaji kupumzika siku nzima ya leo,? akasema Lilian.
?Sawa mama, umesomeka!? Lucy ndiye aliyejibu.
Lilian akavuta shuka, kama vile alikuwa amelala usiku. Akajitahidi kuvuta usingizi.
***
WIKI MOJA BAADAYE
Lilian hakuamini macho yake, aliendelea kukaza macho yake kwenye kioo cha simu yake ili kupata uhakika wa alichokuwa akikiona, lakini bado kiliendelea kuwa vilevile.
Namba iliyokuwa ikimpigia ndiyo iliyomchanganya Lilian. Namba ya mpenzi wake Edo ya nchini Tanzania.
?Mh! Inamaana Edo yupo Bongo?? akajiuliza.
Alijiuliza sana, lakini baadaye akagundua maswali yake yasingekuwa na maana kama asingepokea simu na kuujua ukweli. Mara moja akabonyeza kitufe cha kupokea.
?Haloo,? akaita Lilian.
?Surprise! Surprise!? akasema Edo.
?Baby really?? akauliza Lilian.
?Yeah baby, nipo jijini Dar es Salaam,? akasema Edo kwa furaha.
?Uko wapi nikufuate mpenzi wangu??
?Ha! Ha! Ha! Huo ni wimbo wa Ray C! Sikia nipo hapa chuoni.?
Lilian alihisi kuzimia!
KWA sekunde kadhaa alibaki amesimama ameduwaa kabisa, bila kujua cha kufanya. Hakujua kama alikuwa na furaha au huzuni. Hakuna alichojua kuhusu tukio lile! Furaha ya Edo kuja na huzuni ya kuja kumtibulia penzi lake jipya kwa Pam!
Edo kuwa Tanzania, tena chuoni! Lilikuwa jambo kubwa na la kushtukiza kuliko kawaida. Alibaki hewani, akavuta pumzi ndefu sana kisha akazishusha taratibu kabisa.
Edo alikuwa amemchanganya sana.
?Baby are sure?? akauliza Lilian.
?Yes baby, kwani nina utani na wewe?? akasema Edo.
?Najua huna, uko maeneo gani sasa??
?Kwani wewe uko wapi??
?Utawala.?
?Hata mimi pia nipo hapa Utawala.?
Lilian akazidi kuchanganyikiwa. Kama ni mshtuko ulikuwa wa kipekee kabisa kuwahi kutokea katika maisha yao ya kimapenzi.
?Hebu geuka, angalia upande wa kituoni, kuelekea Survey!? akasema Edo.
Lilian akafanya hivyo!
Hakuamini!
Edo alikuwa amesimama upande wa pili. Ghafla Lilian akataka kuvuka barabara, Edo akamwonyesha ishara kwamba asifanye hivyo. Akatulia kwa muda, kisha Edo akavuka na kumfuata.
Walirukiana na kukumbatiana kwa nguvu. Kwa zaidi ya dakika mbili walikuwa wameng?ang?aniana bila kuachiana. Walikuwa na mengi ya kuongea.
?Mambo baby?? Lilian alimwambia Edo akijitoa kifuani mwake.
?Poa.?
Tayari macho ya Lilian yalikuwa yameshajaa machozi kila kona. Hakutegemea kabisa kukutana na Edo muda ule, ingawa kichwani mwake alikuwa na mawazo sana na mpenzi wake mpya Pam.
?Umependeza sana mpenzi,? akasema Lilian.
?Hata wewe pia mama, umependeza mpaka kidogo nikusahau!?
Wakacheka sana!
?Kwa nini umekuwa bonge hivyo? Unakula nini?? Edo akauliza tena.
?Kama kawaida, vyakula vya hapa chuoni si unavijua!?
Walizungumza mengi, mwisho Edo akamwambia Lilian watoke waende kwenye hoteli aliyofikia. Lilian hakubisha, alikubali haraka sana.
?Tusubiri daladala hapa,? akasema Lilian.
?No! Nimekuja na teksi.?
?Sawa, wapi sasa??
?Tabata.?
?Sawa.?
Wakavuka barabara, Edo akampigia simu dereva ambaye alikuwa ameegesha kwenye maegesho, muda mfupi baadaye, gari aina ya Toyota Corolla liliegesha mbele yake. Edo akasogea na kufungua mlango wa siti za nyuma.
?Karibu malkia wangu,? akasema Edo akiachia tabasamu mwanana.
?Ahsante mfalme wangu!?
Wakacheka!
Baada ya Lilian kuingia ndani ya gari, alifuata Edo ambaye alibamiza mlango kwa nguvu. Dereva akawasha gari na kuliondoa kwa kasi.
?Mh! Kweli mtu hawezi kuona tatizo lake, Latifa wewe hukulala na Big siku ile ukarudi kesho yake mchana? Bora hata mimi nimerudi asubuhi,? akasema Lilian kwa kujiamini.
Wakacheka tena.
Lilian akaamua kuingia bafuni, akaoga haraka kisha akatoka na kujitupa kitandani.
?Sitaki usumbufu leo, hata darasani sitakwenda, nahitaji kupumzika siku nzima ya leo,? akasema Lilian.
?Sawa mama, umesomeka!? Lucy ndiye aliyejibu.
Lilian akavuta shuka, kama vile alikuwa amelala usiku. Akajitahidi kuvuta usingizi.
***
WIKI MOJA BAADAYE
Lilian hakuamini macho yake, aliendelea kukaza macho yake kwenye kioo cha simu yake ili kupata uhakika wa alichokuwa akikiona, lakini bado kiliendelea kuwa vilevile.
Namba iliyokuwa ikimpigia ndiyo iliyomchanganya Lilian. Namba ya mpenzi wake Edo ya nchini Tanzania.
?Mh! Inamaana Edo yupo Bongo?? akajiuliza.
Alijiuliza sana, lakini baadaye akagundua maswali yake yasingekuwa na maana kama asingepokea simu na kuujua ukweli. Mara moja akabonyeza kitufe cha kupokea.
?Haloo,? akaita Lilian.
?Surprise! Surprise!? akasema Edo.
?Baby really?? akauliza Lilian.
?Yeah baby, nipo jijini Dar es Salaam,? akasema Edo kwa furaha.
?Uko wapi nikufuate mpenzi wangu??
?Ha! Ha! Ha! Huo ni wimbo wa Ray C! Sikia nipo hapa chuoni.?
Lilian alihisi kuzimia!
KWA sekunde kadhaa alibaki amesimama ameduwaa kabisa, bila kujua cha kufanya. Hakujua kama alikuwa na furaha au huzuni. Hakuna alichojua kuhusu tukio lile! Furaha ya Edo kuja na huzuni ya kuja kumtibulia penzi lake jipya kwa Pam!
Edo kuwa Tanzania, tena chuoni! Lilikuwa jambo kubwa na la kushtukiza kuliko kawaida. Alibaki hewani, akavuta pumzi ndefu sana kisha akazishusha taratibu kabisa.
Edo alikuwa amemchanganya sana.
?Baby are sure?? akauliza Lilian.
?Yes baby, kwani nina utani na wewe?? akasema Edo.
?Najua huna, uko maeneo gani sasa??
?Kwani wewe uko wapi??
?Utawala.?
?Hata mimi pia nipo hapa Utawala.?
Lilian akazidi kuchanganyikiwa. Kama ni mshtuko ulikuwa wa kipekee kabisa kuwahi kutokea katika maisha yao ya kimapenzi.
?Hebu geuka, angalia upande wa kituoni, kuelekea Survey!? akasema Edo.
Lilian akafanya hivyo!
Hakuamini!
Edo alikuwa amesimama upande wa pili. Ghafla Lilian akataka kuvuka barabara, Edo akamwonyesha ishara kwamba asifanye hivyo. Akatulia kwa muda, kisha Edo akavuka na kumfuata.
Walirukiana na kukumbatiana kwa nguvu. Kwa zaidi ya dakika mbili walikuwa wameng?ang?aniana bila kuachiana. Walikuwa na mengi ya kuongea.
?Mambo baby?? Lilian alimwambia Edo akijitoa kifuani mwake.
?Poa.?
Tayari macho ya Lilian yalikuwa yameshajaa machozi kila kona. Hakutegemea kabisa kukutana na Edo muda ule, ingawa kichwani mwake alikuwa na mawazo sana na mpenzi wake mpya Pam.
?Umependeza sana mpenzi,? akasema Lilian.
?Hata wewe pia mama, umependeza mpaka kidogo nikusahau!?
Wakacheka sana!
?Kwa nini umekuwa bonge hivyo? Unakula nini?? Edo akauliza tena.
?Kama kawaida, vyakula vya hapa chuoni si unavijua!?
Walizungumza mengi, mwisho Edo akamwambia Lilian watoke waende kwenye hoteli aliyofikia. Lilian hakubisha, alikubali haraka sana.
?Tusubiri daladala hapa,? akasema Lilian.
?No! Nimekuja na teksi.?
?Sawa, wapi sasa??
?Tabata.?
?Sawa.?
Wakavuka barabara, Edo akampigia simu dereva ambaye alikuwa ameegesha kwenye maegesho, muda mfupi baadaye, gari aina ya Toyota Corolla liliegesha mbele yake. Edo akasogea na kufungua mlango wa siti za nyuma.
?Karibu malkia wangu,? akasema Edo akiachia tabasamu mwanana.
?Ahsante mfalme wangu!?
Wakacheka!
Baada ya Lilian kuingia ndani ya gari, alifuata Edo ambaye alibamiza mlango kwa nguvu. Dereva akawasha gari na kuliondoa kwa kasi.