BEFORE I DIE
SEHEMU YA 36
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Unayosema ni ya kweli Innocent,nina fahamika na watu wengi na wengi wananipenda sana lakini katika maelfu ya watu wanaonifahamu na kunipenda I trust only you…ni wewe pekee ambaye umeweza kusimama na mimi hata katika nyakati zile ngumu ambazo wengine hawawezi…Ahs...” Latoya akashindwa kuendelea akainama chini.Machozi yalikuwa yakimtoka.
“ Nyamaza kulia Latoya..Haya ni matatizo ya kawaida kwetu sisi wanadamu na yatakwisha Kaza moyo..” Inno akajaribu kumtia moyo
“ Innocent ,ninajitahidi sana kuvumilia na kujipa moyo lakini kuna nyakati ninajikuta nikikata tamaa na kupoteza kabisa matumaini…” akasema kwa uchungu Latoya huku machozi yakiendelea kumtoka.Innocent akaingiza mkono mfukoni na kutoa kitambaa cheupe akamsogelea Latoya karibu zaidi na kumpa
“ Wipe out all your tears..you don’t have to cry anymore..Kuyashinda majaribu yote ya dunia hii lazima uwe jasiri,usikate tamaa hata siku moja..Tears is the sign of defeat.You are powerfull and strong woman so don’t let the world defeat you Latoya..I’m here by your side and I’m going to help you ….” Akasema Innocent
ENDELEA…………………………
Latoya akakipokea kitambaa kile cha Innocent na kufuta machozi halafu akasema
“ Inno nimefarijika sana kwa maneno haya machache ya faraja uliyonitamkia.Sintalia tena..Nitasimama imara .Thank you..thank you so much.Naomba sasa nikuache nikapumzike.kama kuna kitu nitakihitaji nitakupigia simu kwa sababu siku ya kesho hatutaonana kabisa.Sintaonana na mtu yeyote.I”ll need to be alone" akasema Latoya
“ Nimefarijika sana kusikia hivyo Latoya.Pamoja na hayo naomba kabla hujakwenda kupumzika ule kwanza chakula kitakachokuwezesha kuwa na nguvu” akasema Inno.
“ hapana Innocent sihitaji chakula chochote wala kitu chochote cha kutia tumboni kwa siku ya leo na kesho.This is my way of punishing myself kwa maana hiyo sihitaji chakula chochote ” akasema Latoya.Innocent akamtazama usoni halafu akamwambia.
“ Latoya you don’t have to punish yourself..You haven’t done anything wrong.Kushinda bila kula wont help us anything.Please Latoya we’re in a hard time now and we need strength .You are so weak already kwa sababu hujala kitu toka asubuhi.If you cant do that for yourself then do it for me” akasema Innocent.Latoya akafikiri kidogo na kusema
“ For the first time in my life I’ll go out of my principles just for you Innocent.Ok you win tell Irene to bring me food “ akasema Latoya huku akitabasamu.Innocent akatoka na kumfuata Irene jikoni.
“ Ouh My God please help me to win the heart of this young man.I love him.I love him so much.Kwa ajili yake nimeweza hata kwenda nje ya kanuni zangu ” akawaza Latoya akiwa ameikunja mikono na kuiweka kifuani kwake.
“ Nina hakika Innocent ndiye yule mtu niliyekuwa nikimsubiri..Sina haja ya kusubiri hadi nitumiwe malaika aniambie kwamba Innocent ndiye kijana pekee aliyeumbwa kwa ajili yangu.Ninapokuwa karibu naye najihisi kama niko ndani ya pepo..I feel complete when I’m with him…..” akawaza Latoya halafu akakumbuka kitu na kunyong’onyea ghafla
“ Inaniuma sana kwani sintaweza kukaa na Innocent kwa muda mrefu...Siku zangu zimebaki chache sana ..It hurt so much because I have to die soon…Ouh My Gosh why I have to die ? Why so soon ?..I need much time with Innocent before I die” akawaza Latoya na matone ya machozi yakaanza kumdondoka.Innocent na Irene wakaingia mle chumbani wakiwa na chakula,wakaanda meza halafu wakala pamoja na Latoya.Baada ya kula Latoya akawaaga na kwenda chumbani kwake.
“ Innocent ahsante sana kwa jambo ulilolifanya.Nilikuwa na wasi wasi sana na afya ya Latoya.Toka nimemfahamu sijawahi kumuona akiwa dhaifu namna hii.Nashukuru kwa kumshawishi mpaka akakubali kula chakula.Kuna kitu ambacho bado hujakigundua Innocent.Latoya anakuamini kupita kiasi .Tafadhali naomba ukae naye karibu na hasa katika kipindi hiki kigumu alichonacho “ akasema Irene.Innocent hakujibu kitu alikuwa akitabasamu akachukua kikombe cha kahawa na kuelekea katika sehemu iliyokuwa ikiandaliwa kwa ajili ya wageni watakaofika msibani.
“Latoya needs someone by her side.She needs me now.I have to stay with her japokuwa si kazi rahisi lakini sina namna nyingine ya kufanya.She’s so lovely,she smiles like an angel .She needs happiness.She needs someone she can trust and she has chosen to trust me”Alikuwa akiwaza Innocent akiwa bustanini akishuhudia jukwaa likijengwa .
“Sifahamu ni kwa muda gani nitaendelea kukaa hapa kwa Latoya.May be this is my destiny.May be this is where I belong..”akawaza Innocent ,akanywa kahawa kidogo halafu akapiga hatua kuelekea ufukweni akaketi juu ya gogo la mnazi.Akaendelea kunywa kahawa yake.
“ I feel like I belong to this place.Ninahisi kama kuna kitu kinanivuta nisiondoke hapa.Kuna nguvu inayoufanya moyo wangu uwe mzito sana kila linapokuja suala la kuondoka na kumuacha Latoya.Ukiacha aina ya maisha anayoishi yaliyojaa usiri mkubwa sana , Latoya ni msichana ambaye siwezi kumfananisha na msichana mwingine yeyote .Ni msichana mzuri ambaye kuna nyakati mtu unaweza ukajiuliza mara mbili mbili iwapo ni binadamu wa kawaida au ni viumbe wale wa kiroho.Uzuri wake umepitiliza.Ni msichana mwenye roho nzuri sana,anawapenda watu wote,ana roho ya huruma,anajali utu . Latoya ana kila sifa nzuri na kama ukianza kuelezea sifa zake unaweza ukatumia siku nzima kumuelezea.Pamoja na utajiri wote alionao binti huyu ambao sina haja ya kuuchunguza ameupata wapi ,kwa nini hana furaha katika maisha yake? Kwa mujibu wa Irene ambaye amemfahamu Latoya kwa muda mrefu kidogo,anasema kwamba toka ameanza kuniona nikiwa na Latoya ,ameona mabadiliko makubwa katika maisha yake.Latoya ameonekana kuwa ni mtu mwenye furaha licha ya mambo mengi ya siri yanayomzunguka.Ametokea kuniamini kwa kiwango cha juu mno kiasi cha kuniruhusu niingie hata katika baadhi ya sehemu ambazo watu wengine hawaruhusiwi kuingia.Kwa nini Latoya ameniamini ghafla namna hii? ..” akawaza Innocent akiwa bado amekaa katika gogo la mnazi.
“Ngoja niachane kwanza na mawazo kuhusiana na Latoya na maisha yake .Ninatakiwa kuelekeza akili yangu katika kazi hii kubwa aliyonikabidhi ya kuandaa msiba wa mama yake.Watu wengi maarufu watafika ikiwamo viongozi wa serikali kwa hiyo kila kitu kinatakiwa kiende kama inavyotakiwa” Inno akainuka pale katika gogo la mnazi na kuelekea mahala linakojengwa jukwaa.
* * * *
Salamu za rambi rambi ziliendelea kumiminika toka kila pembe ya dunia kwa watu waliomfahamu Latoya.Salamu zilitoka kwa viongozi mbalimbali wa kitaifa ,viongozi wa dini ,wafanya biashara wakubwa na hata kwa watu wa kawaida ambao walionekana kuguswa sana na na msiba ule wa mama yake Latoya.Wengi walimuonea huruma binti huyu ambaye amekuwa msaada mkubwa hasa kwa watu masikini .Akina mama wengi amewawezesha kimitaji kwa kupitia taasisi zake mbili zinazohusiana na kuwakomboa akina mama kiuchumi.Vile vile amewasaidia vijana wengi kujiajiri kwa kuanzisha benki ya vijana inayotoa mikopo kwa vijana wengi. Kwa ujumla amekuwa ni msaada mkubwa hasa kwa jamii masikini.
Nyumbani kwa wazazi wake Latoya kulifurika maelfu ya watu waliohudhuria msiba ule.Msiba huu ulilitikisa jiji la Dar.Nyumbani kwa Latoya ambako ndiko mazishi yangefanyika waliruhusiwa watu maalum tu .Nje ya geti la kuingilia nyumbani hapo palijazwa maua na kadi za watu waliokuja kumpa pole Latoya kwa kufiwa na mama yake mzazi lakini hawakufanikiwa kuingia ndani .Msiba ule ulionekana kuwagusa watu wengi .
Latoya hakuonekana na mtu yeyote kwa siku nzima.Alikuwa amejifungia chumbani kwake na hakutaka kabisa kuonana na watu.Mtu pekee aliyekuwa akiwasiliana naye kwa simu ni Innocent ambaye alikuwa akimpa taarifa za maendeleo ya maandalizi ya mazishi ya mama yake.Wageni wote waliofika msibani walipokewa na Innocent ambaye ndiye aliyekabidhiwa jukumu zima la kuongoza kila kitu .Salamu zote za rambi rambi toka kwa watu mbali mbali ni yeye ndiye aliyekuwa akizipokea kwa niaba ya Latoya.Hakuna mtu aliyefahamu ni kwa nini Latoya aliamua kujifungia ndani bila kuonana na mtu yeyote.
Saa tatu asubuhi ya siku iliyofuata Latoya akashuka toka ghorofani.Alisalimiana na watu mbali mbali waliokuwa wamefika kumpa pole na kuungana naye katika msiba ule mzito halafu akiongozana na Innocent wakaenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa kaburi na baada ya kutoa maelekezo machache wakarejea ndani.
" Innocent umefanya kazi kubwa na nzuri .Ahsante sana.Kila kitu kimekwenda kama nilivyokuwa nataka." akasema Latoya akiwa amekaa na Innocent katika chumba kidogo cha mikutano..
" Mheshimiwa waziri mkuu pamoja na viongozi kadhaa wa kitaifa watahudhuria mazishi ya mama siku ya kesho.Kinachotakiwa ni ulinzi uwe wa uhakika kwa ajili ya viongozi wetu hawa.Ratiba ya kesho itakuwa namna hivi,tutaondoka hapa nyumbani na kwenda hospitali ambako tutamchukua baba na mwili wa marehemu kisha tutaelekea nyumbani kwake.Watu wote watatoa heshima zao za mwisho kule na baada ya hapo tutaondoka na kuja hapa kwa ajili ya mazishi ya kifamilia.Hapa kutakuwa pia na zoezi la kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao hawajafanya hivyo na baadae tutamzika mama." Akasema Latoya na kisha akaagana na Innocent akaelekea chumbani kwake akajifungia.
* * * *
Hatimaye siku ya kumzika mama yake Latoya ikawadia.Wageni walioruhusiwa kuingia nyumbani kwa Latoya walianza kuwasili kuanzia asubuhi.Viongozi mbali mbali wa kitaifa walitegemewa pia kuwasili katika mazishi hayo kwa hiyo ulinzi ulikuwa mkali sana kulizunguka kasri la Latoya. Akiwa katika pilika pilika za kuhakikisha kwamba kila kitu kinakwenda sawa Innocent akapigiwa simu na Latoya na kumuomba aende mara moja katika bustani yake iliyoko juu ya jumba lake.Kwa haraka Innocent akaelekea ghorofani akiwa na wasi wasi mwingi.
Latoya alikuwa ameketi bustanini akiwa katika mavazi meusi.Alionekana ni mwenye mawazo mengi.
“ Innocent kuna jambo ambalo sikuwa nimekueleza" akaanzisha mazungumzo Latoya baada ya Innocent kufika pale bustanini.
" Mazishi ya mama yatakuwa ya kifamilia na hayatahusisha watu wengi.Ninapozungumzia familia nina maana ya baba,mimi na mtu wangu wa karibu ambaye ni sehemu ya familia yangu kwa sasa yaani wewe.Tutakaoingia katika chumba kile chenye kaburi na kumzika mama yangu ni hao watu watatu tu.Mimi wewe na baba." akasema Latoya na kumfanya Innocent ashikwe na mshangao kidogo.Latoya akaendelea
" Baada ya watu kutoa heshima zao za mwisho na jeneza kuingizwa katika chumba chenye kaburi tutaingia sisi watatu pekee.Baba atakuwa wa kwanza kutupia mchanga kaburini ishara ya kumzika mama halafu atatoka nje.Nitahitaji faragha na mwili wa mama kabla hatujaushusha kaburini.Nitafanya maombi yangu ya mwisho halafu jeneza litashuka kaburini na huo utakuwa mwisho wa mama yangu.Kuna kitu ninataka kukuomba" akasema Latoya.
" Chochote unachokitaka Latoya usisite kuomba" akasema Innocent kwa wasi wasi.
" Ninaomba wakati nikiwa faragha na mwili wa mama...uwe pembeni yangu."Akasema Latoya na kumfanya Innocent astuke akakosa neno la kusema
" Innocent , I need you more than ever today..please be by my side" akasema Latoya huku akimtazama Innocent machoni.
" I'll be there Latoya.." akajibu Innocent kwa wasi wasi.
" Thank you sasa tunaweza kuondoka " akasema Latoya kisha taratibu wakashuka tayari kwa safari ya kuelekea hospitali kuuchukua mwili wa mama yake.
Huku akisindikizwa na walinzi wake sita waliokuwa wamevalia mavazi meusi Latoya akafunguliwa mlango na kuingia katika gari lake jeusi aina ya Limousine ambalo hulitumia mara chache sana.Ndani ya gari hiyo alipanda yeye na Innocent pekee. Msafara wa kuelekea hospitali kuuchukua mwili wa marehemu ulikuwa na magari kumi na mbili yote aina ya Mercedece benz rangi nyeusi isipokuwa Limousine aliyopanda Latoya na Innocent. Taratibu msafara wa magari ukaanza kuondoka pale nyumbani kuelekea hospitali.
“ Bado siamini kama ni kweli mama yangu amefariki dunia na sintamuona tena maishani.Inaniuma sana lakini sina namna nyingine ya kufanya” akasema Latoya huku machozi yakimlenga lenga.Innocent akamuangalia na kusema
“ Latoya nafahamu ni kwa namna gani unaumia kwa msiba huu.Ninayafahamu maumivu ya kufiwa hasa na yule umpendaye .Kifo hakizoeleki hata kidogo. Tunachopaswa kufanya ni kuzidi kumuombea mama apumzike kwa amani huko aliko.Japokuwa inaumiza mioyo yetu lakini hatuna budi kumshukuru Mungu kwa kila jambo hata lile linaloumiza zaidi kwani mambo yote yanafanyika kwa mapenzi yake yeye .Nakuomba uwe na ujasiri hasa kwa siku hii ya leo..” akasema Innocent.Maneno yale ya faraja toka kwa Innocent ni kama yalikitonesha kidonda cha moyoni cha Latoya.Akainama na kuanza kulia.
“ Nyamaza kulia Latoya.You need to be strong today..Siku zote kazi ya Mungu haina makosa.Yeye hutoa na kutwaa katika muda anaoutaka yeye.Atwaapo kiumbe chake huwa hatoi salamu wala fursa ya kujiandaa.Nakuomba usilie tafadhali “ akasema Innocent huku akiogopa kumkaribia zaidi Latoya akikumbuka kilichomtokea alipotaka kumgusa Latoya..
“Ni bora kama yangekuwa ni mapenzi ya Mungu.Lakini….” Latoya akastuka akasita kuendelea akamtazama Innocent ambaye naye alikuwa amestuka .Wakatazamana
“ Sorry Innocent..I’m too emotional ndio maana wakati mwingine ninajikuta nikitamka mambo bila kujua ninaongea vitu gani” akasema Latoya huku akipangusa machozi.
“ Its ok Latoya usijali..Ninaelewa wakati ulionao ni mgumu sana.” Akasema Innocent lakini akionekana kuwa na wasi wasi baada ya kauli ile ya Latoya.
“ Kuna kitu alitaka kukisema Latoya halafu akasita .Alimaanisha nini aliposema ni bora kifo cha mama yake kingekuwa ni kwa mapenzi ya Mungu? Ina maana kifo cha mama yake si kifo cha kawaida?.Ni kifo ambacho kimegubikwa na mazingira yenye utata mwingi kwa mujibu wa mashuhuda wa namna kilivyotokea.Inaonekana Latoya anafahamu kwa kina sababu ya kifo cha mama yake .Mambo haya yanazidi kuniogopesha mno.Latoya ana siri kubwa moyoni.Nashindwa kumuelewa ni mtu wa namna gani huyu msichana.Kuna nyakati ninamuona kama si binadamu wa kawaida.Kuanzia muonekano wake na hata matendo yake vinanipa mashaka sana.Pamoja na mambo haya ya kutisha yanayomzunguka Latoya lakini najikuta siwezi kuondoka na kumuacha peke yake.Kuna nguvu ya ajabu inayonizuia nisimuache mrembo huyu.Ninaogopa sana lakini sina namna nyingine ya kufanya. Tayari amekwisha niamini na kunishirikisha katika baadhi ya mambo yake makubwa.Kwa sasa ananichukulia mimi kama rafiki na ndugu yake.Ninachotakiwa kufanya ni kujitahidi kuizoea hali hii..Kuyazoea maajabu na mauza uza ya maisha yake.Inauma sana kwa binti mrembo kama huyu kuishi maisha ya namna hii.”akawaza Innocent huku akiwa amemkazia macho Latoya.
“ Sura yake nzuri kama wale viumbe tunaowasoma katika simulizi mbali mbali za kale.Midomo yake laini.Ana sauti nzuri na tamu kama ya mtoto mdogo.Ana macho mazuri ya kuvutia.Ukija katika kifua chake ndo hutataka kuyabandua macho yako pale.Panasisimua sana.Dah..Kwa nini Msichana mzuri kama huyu ashiriki katika mambo ya miujiza ujiza kama haya? Kuna kitu ndani ya nafsi yangu kinanituma kutaka kumchunguza Latoya na kumfahamu undani wake lakini kuna sauti inanizuia nisithubutu kufanya hivyo..Ngoja kwanza nishughulikie masuala ya msiba na yakishamalizika nitajua nini nifanye.Lazima nimsaidie msichana huyu ambaye kadiri ninavyozidi kumfahamu ndivyo ninavyozidi kuyashuhudia maajabu yake na ndivyo ninavyozidi kujikuta nikiwa karibu naye zaidi.May be this is my life.This is my dest….” Innocent akastuliwa na sauti ya Latoya.
“ Innocent unawaza nini? Mbona unaniangalia hivyo? Akauliza Latoya. Innocent akafikiri kidogo na kusema.
“ Ninaumia mno moyoni kila nikikuona ukidondosha chozi.Ninataka kukuona ukiwa na uso uliojaa furaha na tabasamu siku zote.Ninajiuliza nifanye nini ili niufanye uso wako uwe na tabasamu.Napenda nikuone ukitabasamu hata nyakati zile ngumu kama hizi..” akasema Innocent.Kwa mbali Latoya akatabasamu.
“ Innocent huna sababu ya kuumiza kichwa kutafuta ni kitu gani ufanye ili nifurahi.Toka nimekufahamu umekwisha fanya mambo makubwa sana ambayo hakuna mtu ambaye angeweza kunifanyia.Umeleta tabasamu katika maisha yangu.Usoni ninaonekana ni mwenye huzuni lakini moyo wangu umejawa na tabasamu kubwa.Moyo wangu unatabasamu kwa sababu yako Innocent.Ninachokiomba toka kwako ni kitu kidogo tu,ni kuwa karibu yangu.Moyo wangu utaendelea kutabasamu milele nikiwa karibu yako.” Akasema Latoya.
“ usijali Latoya .Mimi nitakuwa karibu yako siku zote. Nitafurahi kama nitachangia japo kidogo katika furaha ya maisha yako”
“ Nashukuru sana Innocent kwa kuwa karibu yangu hasa katika kipindi hiki kigumu” Akajibu Latoya .
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………….
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 37
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Ninaumia mno moyoni kila nikikuona ukidondosha chozi.Ninataka kukuona ukiwa na uso uliojaa furaha na tabasamu siku zote.Ninajiuliza nifanye nini ili niufanye uso wako uwe na tabasamu.Napenda nikuone ukitabasamu hata nyakati zile ngumu kama hizi..” akasema Innocent.Kwa mbali Latoya akatabasamu.
“ Innocent huna sababu ya kuumiza kichwa kutafuta ni kitu gani ufanye ili nifurahi.Toka nimekufahamu umekwisha fanya mambo makubwa sana ambayo hakuna mtu ambaye angeweza kunifanyia.Umeleta tabasamu katika maisha yangu.Usoni ninaonekana ni mwenye huzuni lakini moyo wangu umejawa na tabasamu kubwa.Moyo wangu unatabasamu kwa sababu yako Innocent.Ninachokiomba toka kwako ni kitu kidogo tu,ni kuwa karibu yangu.Moyo wangu utaendelea kutabasamu milele nikiwa karibu yako.” Akasema Latoya.
“ usijali Latoya .Mimi nitakuwa karibu yako siku zote. Nitafurahi kama nitachangia japo kidogo katika furaha ya maisha yako”
“ Nashukuru sana Innocent kwa kuwa karibu yangu hasa katika kipindi hiki kigumu” Akajibu Latoya .
ENDELEA………………………..
Waliwasili hospitali ambako kulikuwa na idadi kubwa ya watu na waandishi wa habari.Askari polisi tayari walikuwepo pale kwa ajili ya kuhakikisha hakutokei aina yoyote ya fujo kutokana na idadi kubwa ya watu iliyojazana pale hospitali.Walinzi wa Latoya wakaufungua mlango wa gari lile la kifahari na akashuka akiwa ameongozana na Innocent .Waandishi wa habari na wapiga picha hawakuruhusiwa kumsogelea Latoya hata kidogo hivyo walichukua picha kwa kutumia kamera zenye uwezo wa kuchukua matukio toka mbali.Huku akiwa amezungukwa na walinzi wake Latoya akaongozwa moja kwa moja hadi ndani ya hospitali akapokelewa na mganga mkuu wa hospitali ambaye akawaongoza hadi katika chumba alimolazwa baba yake Latoya mzee Curtis.Latoya akawafanyia ishara walinzi wake wabaki mlangoni akaingia chumbani yeye na Innocent.Latoya akambusu baba yake halafu akaketi katika kiti kilichokuwa pembeni ya kitanda.Machozi yakamtoka.Mzee Curtis akainuka na kuketi kitandani
“Nyamaza kulia Latoya.Tafadhali usiendelee kulia.Jipe moyo hasa katika kipindi hiki kigumu kwetu sote.Yote haya ni mapenzi ya Mungu.Nakupenda sana mwanangu na hata mama yako anakupenda sana na ataendelea kukupenda hata huko aliko.Inauma sana lakini hatuna budi kumshukuru Mungu kwani ni yeye mwenye kutoa na kutwaa.” Akasema mzee Curtis ambaye kwa sasa hali yake ilikuwa inaendelea vizuri.
“ Baba najitahidi sana kutokutoa machozi lakini nashindwa.Nawapenda sana wazazi wangu.Nimeumia mno kwa msiba huu wa mama..” akasema Latoya.
“ Pole sana mwanangu.Hii ni mitihani ya dunia ambayo hatuna budi kuishinda.Vipi hali yako? Watu wanaonihudumia hapa hospitali waliniambia kwamba hali yako haikuwa nzuri hata kidogo.Niliogopa sana “ akasema mzee Curtis
“ Ninaendelea vizuri baba .Ni kweli nilipata wakati mgumu sana ila namshukuru Innocent ambaye muda wote amekuwa karibu yangu na kama si yeye sijui ningefanya nini .Vipi maendeleo yako? akasema Latoya
“ Mimi ninaendelea vizuri Mungu ananisaidia.Hivi sasa najisikia ni mzima wa afya ila madaktari wamenishauri niendelee kupata mapumziko ya kutosha .”
“ Usijali baba.baada ya kumaliza shughuli za msiba utakwenda kupumzika nje ya nchi ” akasema Latoya
“ Vipi kuhusu maandalizi ya mazishi ?akauliza mzee Curtis
“ tayari kila kitu kimekamilika .Mama atazikwa nyumbani kwangu .Kaburi tayari limeandaliwa.Tutauchukua mwili wa mama na kuelekea nyumbani kwake ambako watu watatoa heshima zao za mwisho halafu tutaondoka na kuelekea nyumbani kwangu ambako zitafanyika shughuli za mazishi ambayo yatakuwa ni ya kifamilia ambayo kwa sasa ni wewe,mimi na Innocent.” Akasema Latoya.Mzee Curtis hakujibu kitu akamtazama Innocent ambaye alikuwa amesimama pembeni karibu na dirisha .
“ Innocent hujambo kijana wangu? Akasema mzee Curtis na kumstua Innocent.Akasogea taratibu na kumpa mkono mzee Curtis wakasalimiana.
“ Pole sana mzee wangu kwa matatizo” akasema Innocent
“ Nimekwisha poa kijana wangu.Matatizo tumeumbiwa binadamu,ni sehemu ya maisha yetu” akajibu
Kimya kifupi kikapita halafu mzee Curtis akamwambia Latoya
“ Latoya ,kabla hatujaondoka ninaomba niongee faragha na Innocent”
Latoya akaguna kidogo na kuuliza
“ Kuhusu nini baba?
“ Its men to men talk..Just three minutes “
Latoya akafikiri kidogo kisha akainuka
“ sawa baba nitakuwa hapo nje”
“ nashukuru sana” akajibu mzee Curtis kisha akamfanyia ishara Innocent aketi kitini
“ Innocent nimeona nichukue dakika hizi chache kuongea na wewe na kuzimaliza tofauti zetu zilizojitokeza siku chache zilizopita.Najua nilikukosea kwa kukutaka ufanye kitu ambacho hukuwa tayari kufanya.Naomba unisamehe sana kwa yote yaliyotokea.” Akasema mzee Curtis.
“ Mzee hukupaswa kuniomba mimi msamaha bali mimi ndiye niliyepaswa kukuomba msamaha .Najua nilikuudhi sana siku ile.Sikupaswa kuongea namna ile mbele yako kama mzazi.Nilikukosea heshima kama mzazi wa Latoya ambaye ni rafiki yangu mkubwa.Naomba unisamehe sana mzee wangu” akasema Innocent.
“ Nilikwisha kusamehe muda mrefu kijana wangu.Sote tumekoseana na tusameheane ili tuanze upya” akasema mzee Curtis na kumpa Innocent mkono.
“ Innocent kuna jambo lingine ambalo ninataka kukuomba.”
“ Usijali mzee Curtis sema chochote ukitakacho”
“ Kwanza ninashukuru sana kwa kuwa karibu na mwanangu Latoya.Wewe ni mtu pekee ambaye anakuamini sana kwa sasa.Tafadhali nakuomba Innocent kuwa karibu naye.Wewe ni msaada mkubwa kwake.Ni mara ya kwanza nimemuona akiwa na rafiki anayemuamini kama wewe.Narudia tena kukuomba kaa karibu naye na hasa katika kipindi hiki kigumu alichonacho.Anahitaji faraja kubwa.Nitashukuru sana kama utalikubali ombi langu” akasema mzee Curtis
“ Mzee Curtis nashukuru kwa wewe na mwanao kuniamini .Latoya ni rafiki yangu amenisaidia mambo mengi na alisimama na mimi hata katika nyakati zile ngumu nilizokuwa nazo.Mimi nitakuwa naye karibu siku zote.Usihofu kuhusu hilo”
“ Nashukuru sana Innocent .Sasa naomba nijiandae ili tuweze kuondoka.”Akasema mzee Curtis.Innocent akatoka nje na kukutana na Latoya.
“ Alikuwa anakwambia nini baba? Akauliza Latoya
“ Tulikuwa tunaombana msamaha kwa yaliyotokea .Tumesameheana” akajibu Innocent
“ Good “akajibu Latoya na kuinamisha kichwa.
Baada ya dakika saba mzee Curtis akatoka mle ndani huku akitembea taratibu.Innocent akamshika mkono na kwa pamoja wakaelekea katika chumba cha kuhifadhia maiti.Tayari mwili wa mama yake Latoya ulikwisha wekwa katika sanduku zuri lenye nakshi za dhahabu .
“ Latoya uko tayari kuuona mwili wa mama? Akauliza Innocent kabla ya sanduku lile halijafunguliwa.
“ Niko tayari Innocent” akajibu latoya na taratibu sanduku likafunguliwa.Mama yake Latoya alionekana ni kana kwamba amelala usingizi.
Latoya akanyoosha mkono na kuuweka usoni pa mama yake.Baada ya dakika kama tatu akautoa mkono na sanduku likafungwa na kuingizwa katika gari maalum lililokuwa nje ya jengo.Latoya akagoma kupanda katika gari lenye maiti ya mama yake alilotakiwa kupanda yeye na baba yake. Hakutoa sababu kwa nini hakutaka kupanda gari lile .Mzee curtis akapanda katika ile mercedece benzi iliyokuwa na maiti ya mke wake akiwa na mmoja wa walinzi wa Latoya.Huku akisindikizwa na walinzi wake Latoya na Innocent wakaingia katika gari walilopanda wakati wakija hospitali na safari ya kuelekea nyumbani kwa wazazi wa Latoya ikaanza.
Ndani ya gari Latoya alikuwa anamiminikwa na machozi.
“ She’s crying..I can hear her…My mother isn’t dead..she’s not dead but I cant save her” akasema Latoya huku akilia.Innocent akastuka sana kwa kauli ile ya Latoya.
“ Latoya tafadhali usilie.kaza moyo” Innocent akajaribu kumbembeleza Latoya baada ya kumuona akidondosha machozi.
“ Innocent let me cry..nina uchungu mkubwa sana ..ninaumia sana moyoni kila nikiisikia sauti yake.She’s crying and I cant help her….”akasema Latoya huku akilia.innocent akastuka na kuuliza
“ Latoya nani analia? ..Innocent akauliza kwa mshangao.
Latoya akastuka kama mtu aliyekurupushwa usingizini…
“ What ! No body is crying..No body….”akasema Latoya na kuzidi kumchanganya Innocent.
Innocent akazidi kuingiwa na wasi wasi mwingi,akamtazama Latoya ambaye alikuwa ameinama akilia.
“ Kuna nyakati ninashindwa kumuelewa huyu Latoya hasa kutokana na matendo yake na maneno ambayo amekuwa akiyatamka .Pale mwanzo alisema kwamba kifo cha mama yake hakikuwa kifo cha kawaida.Hivi sasa amejisahau na kusema tena kwamba anaisikia sauti ya mama yake akilia.Nilipomuuliza akastuka kama mtu aliyekuwa usingizini na kuanza kuniuliza tena nani anayelia..Whats going on here? ..Innocent akazama katika lindi la mawazo.
“ Nimejiingiza katika mambo mazito sana .Nakumbuka ndoto niliyoota wazee wawili wakinionya kwamba nimeingia katika mambo mazito nisiyoyafahamu na wakanitahadharisha niwe makini .Sasa nimeanza kuamini maneno yao.Huku mahala nilikoingia ni kugumu na kuna mambo ya ajabu ajabu mno.Pamoja na yote yanayoendelea ya ajabu ajabu na ya kushangaza bado najikuta siwezi kuondoka na kumuacha Latoya peke yake.Kuna nguvu inayonizuia kufanya hivyo. Latoya ananigusa sana moyo wangu.Kila nikimuona najikuta nikijisikia tofauti na hata mawazo ya kuondoka na kumuacha yanatoweka.” Akawaza Innocent huku akimtazama Latoya ambaye bado alikuwa ameinama.
“Bado ni msichana mdogo kuingia katika mambo makubwa kama haya.Siwezi kumuacha.Lazima nimsaidie kwa kadiri nitakavyoweza.Siwezi kukubali msichana mzuri namna hii aishi maisha kama haya.lazima nitafute namna ya kumuondoa katika maisha ya namna hii na kumrudisha katika ulimwengu wa kawaida.”
“ Innocent “ akasema Latoya na kumstua Innocent katika mawazo aliyokuwa nayo.
“ Naam Latoya” akaitika Innocent
“ Unawaza nini? Akauliza Latoya
“ mambo ya kawaida tu Latoya “ akajibu Inno
“ Najua unawaza mambo mengi sana kuhusu mimi.Naomba tafadhali usiwaze lolote kuhusiana na mimi.Naomba unichukulie mimi kama Latoya msichana wa kawaida.Kwa siku hizi chache ulizokaa nami najua umekutana na mambo mengi ambayo kwako wewe si ya kawaida.I can see in your eyes you are very scared .Nafahamu umeogopa sana.Ninachokuomba ,usiogope hata kidogo.Maisha yangu ya ndani ni magumu sana na ninaomba uyavumilie.” Akasema Latoya kwa sauti ndogo.Innocent akakohoa kidogo na kusema
“ Latoya wewe ni rafiki yangu mkubwa na siwezi kukuficha kitu.Ni kweli baada ya kuingia katika jumba lako nimekutana na maisha Fulani ya tofauti kidogo na yale ambayo nimeyazoea kuishi ,kwa hiyo kwa siku za mwanzo nilipata shida sana lakini kwa sasa nimekwisha yazoea. “ akasema Innocent
“ nashukuru sana Innocent. It means a lot to me. ” akasema Latoya
“ Usinishukuru Latoya.Ni wajibu wangu kufanya hivi. Kwa hiyo kama rafiki yako nitajitahidi siku zote kuwa karibu nawe na kukufanya uwe ni mwenye furaha na tabasamu daima” maneno yakazidi kumtoka Innocent.
“ Innocent nashindwa hata niseme nini kwa maneno hayo uliyoyaongea.Ni maneno mazito sana na yameufanya moyo wangu ujawe na furaha kubwa na kunisahaulisha kwa muda machungu ya kufiwa na mama yangu .Nashukuru sana Innocent sina neno la kusema zaidi ya ahsante” akasema Latoya huku uso wake ukionyesha dhahiri furaha aliyokuwa nayo baada ya maneno yale ya Innocent.
“Nilikuwa na wasi wasi mwingi pengine Innocent angeweza kuondoka kutokana na maisha ya pale kwangu ambayo ni tofauti na maisha aliyoyazoea.This is the man I’ve been waiting to see before I die..This is my man.Sasa moyo wangu una amani kwani nina imani nimemuona mtu niliyekuwa nikimsubiri kwa hamu kwa muda mrefu.” Akawaza Latoya akiwa ameinama.
Msafara ule mkubwa wa magari ya kifahari ,uliokuwa ukiongozwa na pikipiki ya askari wa usalama barabarani ulisababisha foleni kubwa jijini wakati ukielekea nyumbani kwa wazazi wa Latoya. Watu wengi walijitokeza barabarani kuushuhudia msafara uliobeba maiti ya mama wa Latoya msichana mdogo lakini tajiri mkubwa.Wengi walikuwa wameguswa sana na msiba huu na walimuonea huruma sana Latoya ambaye alikuwa ni kipenzi cha wengi. Katika barabara walizopita wengi wa akina mama walikuwa wakipunga mikono yao ishara ya kumuaga mama mzazi wa kipenzi chao Latoya.
Hatimaye msafara ule ukafika katika mtaa waliokuwa wakiishi wazazi wa Latoya. Watu walikuwa ni wengi mno.Magari hayakuruhusiwa kuingia katika mtaa ule kutokana na uwingi wake hiyo yakatafutiwa eneo la kuegeshwa ili kuacha nafasi kwa waombolezaji waliokuwa wamekusanyika kwa maelfu. Ni gari nne tu ambazo ziliruhusiwa kuikaribia nyumba ya wazazi wa Latoya .Gari iliyobeba maiti gari ya Latoya na gari mbili za walinzi wake ndio pekee ziliruhusiwa kuegeshwa mbele ya nyumba ile. Vilio vikaanza upya baada ya gari lenye maiti kuwasili pale nyumbani.Walinzi wa Latoya wakashuka kwa haraka katika magari yao na kulizunguka gari la Latoya.Baada ya dakika kama tatu hivi mlango wa gari ile ya kifahari ukafunguliwa na Latoya akashuka akiwa ameongozana na Innocent.Baada ya Latoya kushuka garini mlango wa gari lililobeba maiti ukafunguliwa na taratibu jeneza lililokuwa limenakshiwa kwa dhahabu likaanza kushushwa na walinzi sita waliokuwa wamevalia suti nyeusi na kuliweka katika meza maalum ya magurudumu.Innocent akamshika mkono mzee Curtis baba yake Latoya na kwa pamoja wakiwa nyuma ya jeneza lililokuwa likisukumwa na walinzi ,wakaanza kutembea kuelekea ndani mahala ambako shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa marehemu zingefanyika.Eneo lote lilitawaliwa na vilio vya akina mama .Watu kadhaa walikuwa wakianguka na kupoteza fahamu baada ya kulishuhudia jeneza lenye mwili wa mama yake Latoya likiingizwa ndani.Watu wa huduma ya kwanza walikuwa wamejipanga vyema kuwahudumia watu waliopatwa na matatizo ya kuanguka na kupoteza fahamu.Hali ya mahali hapa ilikuwa ni ya simanzi kubwa sana.Mama huyu alikuwa kipenzi cha wengi.
Kwa mwendo wa taratibu sana jeneza lenye mwili wa marehemu likiwa juu ya meza maalum ya magurudumu likaingizwa ndani huku Latoya ,baba yake mzee Curtis na Innocent wakifuatia nyuma.Kwaya mbali mbali zilikuwa zikitumbuiza waombelezaji kwa nyimbo za maombolezo.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 38
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Baada ya dakika kama tatu hivi mlango wa gari ile ya kifahari ukafunguliwa na Latoya akashuka akiwa ameongozana na Innocent.Baada ya Latoya kushuka garini mlango wa gari lililobeba maiti ukafunguliwa na taratibu jeneza lililokuwa limenakshiwa kwa dhahabu likaanza kushushwa na walinzi sita waliokuwa wamevalia suti nyeusi na kuliweka katika meza maalum ya magurudumu.Innocent akamshika mkono mzee Curtis baba yake Latoya na kwa pamoja wakiwa nyuma ya jeneza lililokuwa likisukumwa na walinzi ,wakaanza kutembea kuelekea ndani mahala ambako shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa marehemu zingefanyika.Eneo lote lilitawaliwa na vilio vya akina mama .Watu kadhaa walikuwa wakianguka na kupoteza fahamu baada ya kulishuhudia jeneza lenye mwili wa mama yake Latoya likiingizwa ndani.Watu wa huduma ya kwanza walikuwa wamejipanga vyema kuwahudumia watu waliopatwa na matatizo ya kuanguka na kupoteza fahamu.Hali ya mahali hapa ilikuwa ni ya simanzi kubwa sana.Mama huyu alikuwa kipenzi cha wengi.
Kwa mwendo wa taratibu sana jeneza lenye mwili wa marehemu likiwa juu ya meza maalum ya magurudumu likaingizwa ndani huku Latoya ,baba yake mzee Curtis na Innocent wakifuatia nyuma.Kwaya mbali mbali zilikuwa zikitumbuiza waombelezaji kwa nyimbo za maombolezo
ENDELEA………………………..
Latoya ,baba yake na Innocent wakaenda kuketi katika jukwaa lililokuwa limeandaliwa maalum kwa ajili yao.Nyuma yao walikuwepo ndugu kadhaa wa karibu wa marehemu akiwemo mjomba wake Latoya.Hakuna ndugu yeyote aliyemsalimu Latoya.Kila aliyekuja alikuwa akimsalimu mzee Curtis pekee.Innocent aliyekuwa amekaa pembeni ya Latoya akaliona hilo na kumuomba Latoya asijali wala kuhuzunika kwa kitendo cha yeye kubaguliwa kupewa salamu za pole na ndugu zake.
Shughuli ilifunguliwa kwa ibada ya misa toka kwa askofu msaidizi wa jimbo kuu la Dar es salaam mhashamu Leonard tubarua. Katika mahubiri yake aliwakumbusha watu kujiweka tayari muda wowote kwani kifo hakipigi hodi.Vile vile aliwaasa watu kumtegemea zaidi Mungu na kuachana na imani potofu hasa sehemu kama hizi za misiba.Aliyasema haya kwa sababu alikwisha sikia minong’ono ya watu kwamba kifo cha mama yake Latoya hakikuwa cha kawaida.Kilitawaliwa na mazingara mengi.
Baada ya ibada ile ya misa kumalizika kikafuata kipindi cha watu kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu .Jeneza lenye nakshi za dhahabu likafunguliwa na watu wa kwanza kutoa heshima zao za mwisho ni mume na watoto wa marehemu.Mzee Curtis akiwa ameongozana na mwanae Latoya na Innocent wakasimama katika jeneza lile kwa muda halafu wakaondoka na kuwaachia nafasi ndugu wengine nao watoe heshima zao za mwisho.Lilikuwa ni zoezi gumu sana na akina mama wengi walianguka na kupoteza fahamu.
Pamoja na kwamba tayari alikwisha kuwa mtu mzima sana lakini mama yake Latoya bado sura yake iliendelea kung’aa na ule uzuri wake wa asili haukutoweka.Ndani ya jeneza alikuwa ametulia kana kwamba amelala usingizi.Mikono yake ilikuwa kifuani mwake na alionekana kama amepumzika.Vilio vingi vikasikika.Watu walimlilia mama huyu hadi sauti zikakauka.Vilio vile vikamchoma sana Latoya .Alisikia uchungu mkubwa na mara akaanza kusikia maumivu makali mno katika mgongo wake na kwa mbali akaanza kuhisi kama nguvu zinaanza kumuishia.Akauma meno kwa uchungu.
“ouh My Gosh..Not now…Ouh No..Its coming..Not here..Not here infront of all these people” akasema kimoyomoyo Latoya halafu akamgeukia Innocent.
“ Innocent nishike mkono nipeleke katika gari langu” akasema Latoya na bila kuuliza chochote Innocent akamshika mkono wakaondoka kwa mwendo wa haraka kuelekea katika gari la Latoya huku wakifuatiwa nyuma na walinzi wa Latoya.Innocent akawa na wasi wasi mwingi.
Latoya akawafanyia ishara walinzi wake wafungue mlango wa gari halafu akaingia ndani.
“ Innocent naomba asiingie mtu yeyote ndani ya gari.I need a privacy” Akaamuru Latoya na kuufunga mlango.Maumivu yakaongezeka na kuwa makali zaidi.Macho yake yakaanza kuona giza.
“ Ouh My Gosh.i’m going down again……”akasema Latoya na kuanguka chini .
* * * *
Msafara wa mheshimiwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ukawasili katika kasri la Latoya.Ulinzi ulikuwa wa kutosha sana.Mheshimiwa waziri mkuu aliiwakilisha serikali katika mazishi ya mama wa Latoya binti mdogo ambaye anasemekena ndiye tajiri mkubwa nchiniTanzania na afrika Bilionea huyu mdogo amekuwa na mchango mkubwa sana katika miradi mbalimbali ya maendeleo hususani katika masuala ya afya.Amekuwa akisaidia katika ujenzi wa hospitali na zahanati nchini.Latoya amekuwa ni mfadhili mkuu wa mamia ya wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi kila mwaka kwa matibabu baada ya kushindikana kutibiwa hapa nchini.Amekuwa mstari wa mbele katika kusaidia huduma ya afya ya mama na mtoto kwa kutoa vifaa vya kujifungulia na kuboresha wodi za wazazi katika hospitali zote za mikoa na wilaya.Katika upande wa uchumi amewasaidia maelfu ya akina mama na vijana kujiwezesha kiuchumi kwa kuwapatia mikopo yenye riba nafuu kupitia benki zake mbili. Latoya amekuwa mfadhili mkubwa wa elimu kupitia mfuko wake wa kusaidia elimu vjijini.Amesaidia katika ujenzi wa shule kubwa na nzuri zenye vifaa vya kutosha ikiwamo waalimu.Kiujumla mchango wake kwa taifa ni mkubwa sana na hivyo kuwa mmoja wa watu wanaotambuliwa na serikali kwa mchango wao mkubwa.
Mheshimiwa waziri mkuu akapokelewa na Stevie mtu maalum aliyekuwa akipokea wageni na kuongozwa hadi jukwaani.Vikundi mbali vya kwaya vilikuwa vikindelea kuimba nyimbo za maombolezo .Wageni mbali mbali waliendelea kuwasili nyumbani kwa Latoya kwa ajili ya mazishi.Wengi wa wageni waliofika hapa ni viongozi wa serikali wageni toka nje ya nchi matajiri wakubwa wa ndani na nje ya nchi pamoja na watu wake wa karibu.
Kwa mujibu wa ratiba ,ilipangwa shughuli ya mazishi ianze saa saba za mchana lakini mpaka saa nane na nusu bado shughuli haikuwa imeanza.Ikamlazimu Stevie ambaye ndiye aliyeachiwa jukumu zima la kusimamia shughuli zote za nyumbani kwa Latoya ampigie simu Innocent ili kufahamu nini kilichokuwa kinaendelea kule nyumbani kwa wazazi wa Latoya kilichosababisha wawe nje ya ratiba.
“Stevens kuna jambo limetokea hapa “ akasema Innocent baada ya kupokea simu ya Stevens.
“ Jambo gani limetokea Innocent” akauliza Steve lakini Innocent hakujibu kitu.
“ Innocent jambo gani limetokea huko ? akauliza tena Steve.
“ Steve nitakupigia baada ya muda mfupi..Kuna jambo zito hapa limetokea.” akasema Innocent kwa wasiwasi na kukata simu.Steve kijasho kikamtoka.
Steve aliingiwa na wasi wasi mwingi.Kauli ile ya Innocent kwamba kuna jambo limetokea ikampa wasi wasi mkubwa.Akatoa kitambaa na kujifuta jasho.
“ Nini kimetokea ? akajiuliza Stevie bila kupata jibu.
“ Tuko nje ya ratiba na wageni wa kitaifa wana majukumu mengine.Nitawaambia kitu gani ? akazidi kuwaza Stevie.Hali ile ilimchanganya sana kichwa chake.Akaingia ndani akatafakari kidogo na baada ya kama dakika tano hivi akaelekea moja kwa moja jukwaani akachukua kipaza sauti na kuiomba kwaya iliyokuwa ikitumbuiza isimame kwa muda.
“ Ndugu zangu waombolezaji,bado tunaendelea kuusubiri mwili wa marehemu uweze kufika hapa na shughuli za mazishi ziweze kufanyika.Kwa mujibu wa ratiba yetu inavyoonyesha ni kwamba baada ya kuuchukua mwili wa marehemu toka hospitali ,utaelekea moja kwa moja nyumbani kwa marehemu ambako itafanyika ibada na shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu.Baada ya zoezi hilo kumalizika mwili utaletwa hapa kwa ajili ya watu wengine nao kutoa heshima zao za mwisho halafu yatanyika mazishi ambayo yatakuwa ni ya kifamilia. Narudia tena kwamba mazishi yatakuwa ni ya kifamilia tu kwa hiyo watakaoingia katika chumba atakamozikiwa mpendwa wetu ni familia ya marehemu tu.Tunaomba kama wewe si mwana familia usiingie katika sehemu ya kuzikia.Kwa mujibu wa taarifa nilizopokea muda si mrefu ni kwamba kumejitokeza idadi kubwa ya watu wanaotoa heshima zao za mwisho nyumbani kwa marehemu kwa hiyo tunaomba tuendelee kuwa wavumilivu .Baada ya zoezi hilo kukamilika nyumbani kwa marehemu ,mwili utaletwa hapa na sisi tutapata nafasi ya kuuaga. Tuendeleeni kuliwazika kwa nyimbo za maombolezo toka katika vikundi mbali mbali vya kwaya.” Akasema stevie halafu akashuka jukwaani.
* * * *
Bado Innocent aliendelea kuwa na wasi wasi kuhusu hali ya Latoya ilivyobadilika ghafla.
“ Latoya anasumbuliwa na nini? Mbona hali yake imebadilika ghafla? Akawaza Innocent bila kupata jibu.Bado aliendelea kusimama nje ya gari lile akiwa na walinzi wa Latoya. Japokuwa alijitahidi asiweze kuonyesha wazi wazi woga aliokuwa nao miguu yake ilikuwa ikimtetemeka.Alihisi uoga Fulani ambao hakujua ulitokana na nini.
Muda ulizidi kuyoyoma bila ya Latoya kutoka ndani ya ile gari.Taratibu idadi ya watu waliokuwa wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu ikaanza kupungua.Innocent jasho likaendelea kumtoka.
“ Itakuwaje iwapo watu watamaliza kutoa heshima zao za mwisho na latoya hajatoka ndani ya gari? Ametoa amri asiingie mtu yeyote ndani ya gari lake.Tutawezaje kumtaarifu kwamba shughuli ya kutoa heshima za mwisho imemalizika? Anafanya nini ndani ya gari? …Innocent akazidi kuumiza kichwa kwa maswali ambayo hayakuwa na majibu.
Hatimaye watu wakamaliza kutoa heshima zao za mwisho na jeneza likafungwa kuashiria kwamba shughuli ile imemalizika.Mapigo ya moyo wa Inno yakaanza kwenda mbio.Hakujua angeieleza nini hadhira ile iliyokusanyika.
Mjomba wa Latoya akamfuata Innocent .Alipomuona anakuja akahisi kuchanganyikiwa.Hakujua angempa jibu gani.
“ Kijana shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu zimemalizika.Nini kinafuata? Akauliza mjomba wa Latoya.
“Kinachofuata sasa hivi ni kuelekea nyumbani kwa Latoya ambako ndiko maziko yatafanyika.” Akajibu Innocent
“ Latoya yuko wapi ?
Inocent hakujibu kitu kitu akamfuata mlinzi mmoja wa Latoya akamnong’oneza kitu sikioni halafu akamuomba mjomba waongozane kuelekea jukwaani.
“ Wakati maandalizi ya kuelekea nyumbani kwa mtoto wa marehemu yanafanyika naomba uruhusu vikundi vya kwaya viendelee kuwaliwaza waombolezaji kwa nyimbo za faraja.” Innocent akamwambia muongoza shughuli halafu akashuka jukwaani.
“ Latoya anafanya nini ndani ya gari ? Itakuaje iwapo muda unazidi kusonga na hajatoka mle garini? Nitawaeleza nini watu iwapo watataka kufahamu mahala alipo Latoya? Innocent akazidi kuumia kichwa kwa maswali ambayo hakupata majibu yake.Ghafla simu yake ikaita.Kwa haraka akaitoa na kutazama mpigaji alikuwa ni Stevie.
“ Innocent vipi hali ya huko? Bado shughuli zinaendelea? Akauliza Stevie baada ya Inno kupokea simu
“Stevens kuna jambo limetokea hapa “ akasema Innocent
“ Jambo gani limetokea Innocent” akauliza Steve lakini Innocent hakujibu kitu.
“ Innocent jambo gani limetokea huko ? akauliza tena Steve.
“ Steve nitakupigia baada ya muda mfupi..Kuna jambo zito hapa limetokea.” akasema Innocent kwa wasiwasi na kukata simu akasimama akatafakari na mara simu yake ikaita tena.Katika kioo cha simu ,lilionekana jina la Latoya.Haraka haraka Inno akaipokea huku akihema..
“ Hallo Latoya” akasema Innocent
“ Nini kinaendelea Innocent? Akauliza Latoya kwa sauti ya chini sana.
“ Kwa sasa shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu zimemalizika na tunakusubiri wewe pekee ili tuweze kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwako kwa mazishi..” Akasema innocent
“ Innocent naomba uruhusu safari ianze kuelekea nyumbani.One more thing…” akasema Latoya halafu akanyamaza kidogo na kuendelea.
“ You will drive this car.” Latoya akatulia tena kidogo.Alikuwa akiongea kana kwamba alikuwa katika maumivu makali mno.
“ Innocent wakati ukiendesha usijaribu kutaka kuangalia nyuma.Dont do that please..” akanyamaza tena akagugumia kwa maumivu kisha akasema
“ Tukifika nyumbani ,ingiza gari moja kwa moja ndani katika maegesho yangu halafu shuka na ukanisubiri chini sebuleni.Naomba ufanye kama ninavyokuagiza Innocent” akasema Latoya.
“ Sawa Latoya nitafanya kama ulivyosema” akajibu Innocent.Alishukuru kwa kuongea na Latoya lakini kwa upande mwingine alikuwa na wasi wasi mwingi sana .
“ Nimesikia Latoya akigugumia kwa maumivu. Ana matatizo gani? Lazima kuna kitu kinamsumbua.Maisha ya Latoya yamezungukwa na fumbo gumu.Japokuwa ninajitahidi kuwa karibu naye lakini kuna nyakati ninamuogopa sana hata kumsogelea.Nakumbuka juzi niliposikia kama mkono wangu umepitiwa na umeme nilipotaka kuupeleka mgongoni mwake.Siyo siri kuishi karibu na Latoya kunataka uvumilivu mkubwa sana.Kwa nini amesema nisijaribu kuangalia nyuma ya gari? Kuna nini kinaendelea huko nyuma? Dah maisha haya yananipa wakati mgumu sana lakini sina namna nyingine ya kufanya itanibidi nifanye kama anavyotaka kwa sababu mimi ndiye mtu anayeniamini sana kwa sasa." akawaza Innocent halafu akarejea jukwaani akaongea kidogo na mzee Curtis na maandalizi ya kuelekea nyumbani kwa Latoya yakaanza.Jeneza Likapakiwa katika gari na magari yakajipanga tayari kwa kuondoka.Zoezi hili liliamsha vilio toka kwa akina mama.Baada ya kila kitu kuwa tayari,Innocent akachukua funguo za gari na kuingia akaketi katika usukani kisha akavuta pumzi ndefu.Hakuwahi kuendesha gari kama hili lakini akajipa moyo na kuliwasha.Hakuthubutu kutazama nyuma kama alivyokuwa ameamriwa na Latoya japokuwa kulikuwa na kioo cheusi ambacho dereva hawezi kuona kinachotokea nyuma. Taratibu msafara wa magari ukaanza kuondoka pale nyumbani kwa marehemu na kuacha vilio vingi.Innocent alikuwa akitiririkwa na jasho
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………..
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 39
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Nakumbuka juzi niliposikia kama mkono wangu umepitiwa na umeme nilipotaka kuupeleka mgongoni mwake.Siyo siri kuishi karibu na Latoya kunataka uvumilivu mkubwa sana.Kwa nini amesema nisijaribu kuangalia nyuma ya gari? Kuna nini kinaendelea huko nyuma? Dah maisha haya yananipa wakati mgumu sana lakini sina namna nyingine ya kufanya itanibidi nifanye kama anavyotaka kwa sababu mimi ndiye mtu anayeniamini sana kwa sasa." akawaza Innocent halafu akarejea jukwaani akaongea kidogo na mzee Curtis na maandalizi ya kuelekea nyumbani kwa Latoya yakaanza.Jeneza Likapakiwa katika gari na magari yakajipanga tayari kwa kuondoka.Zoezi hili liliamsha vilio toka kwa akina mama.Baada ya kila kitu kuwa tayari,Innocent akachukua funguo za gari na kuingia akaketi katika usukani kisha akavuta pumzi ndefu.Hakuwahi kuendesha gari kama hili lakini akajipa moyo na kuliwasha.Hakuthubutu kutazama nyuma kama alivyokuwa ameamriwa na Latoya japokuwa kulikuwa na kioo cheusi ambacho dereva hawezi kuona kinachotokea nyuma. Taratibu msafara wa magari ukaanza kuondoka pale nyumbani kwa marehemu na kuacha vilio vingi.Innocent alikuwa akitiririkwa na jasho
ENDELEA…………………………….
Hatimaye msafara uliobeba mwili wa marehemu ukawasili nyumbani kwa Latoya.Gari lile la Latoya ambalo lilikuwa linaendeshwa na Innocent likaingia moja kwa moja ndani hadi katika maegesho yanayotumiwa na Latoya pekee.kama alivyokuwa ameamriwa ,Inno akazima gari na kushuka akafunga mlango na kuondoka kuelekea sebuleni .Maiti ilishushwa toka garini na kuwekwa kwanza sebuleni wakisubiri Latoya ashuke chini.Baada ya dakika kama kumi na tano hivi Latoya akashuka akiwa katika mavazi mengine kabisa tofauti na yale aliyokuwa amevaa.Bila kupoteza muda jeneza lenye mwili wa mama yake likaanza kupelekwa mahala ambao shughuli za kuuaga mwili wa mwarehemu zingefanyika.Latoya ,baba yake mzee Curtis na Innocent walikuwa wakilifuata kwa nyuma.Walipofika jukwaani wakachukua nafasi zao na shughuli zikafunguliwa kwa maombi maalum.Baada ya maombi Innocent akasoma historia ya marehemu na kisha zikafuata salamu za rambi rambi toka kwa serikali ,watu binafsi na mashirika .Mheshimiwa waziri mkuu alitoa salamu za serikali na kuelezea namna serikali na wananchi kwa ujumla walivyoguswa na msiba ule.Baada ya kumaliza kutoa salamu za serikali,zikafuata salamu toka kwa watu mbali mbali na wawakilishi wa mashirika mbali mbali.
Zoezi la salamu lilipomalizika,likafuata zoezi la kuuaga mwili wa marehemu .Kama ilivyofanyika nyumbani kwa marehemu,Latoya,baba yake mzee Curtis na Innocent walikuwa wa kwanza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu halafu akafuata mheshimiwa waziri mkuu ,viongozi wengine wa serikali,mabalozi na watu wengine nao wakafuatia.Kila aliyekuwa akipita mbele ya jeneza na kutoa heshima zake za mwisho kwa marehemu alitakiwa kuwapa mkono wa pole wafiwa akianzia na mzee curtis,Latoya na mwisho Innocent.Wakati zoezi lile likiendelea kijana mmoja mzungu aliyekuwa amenyoa upara akatoa heshima zake kwa mwili wa marehemu lakini utoaji wake wa hesima za mwisho ukamstua kidogo Latoya .Akamuangalia yule kijana kwa makini sana mwili ukamsisimka.Alipotoa heshima zake za mwisho yule kijana akatembea taratibu hadi walipokuwa wamekaa familia ya marehemu na kuanza kutoa mkono wa pole kwa mzee Curtis. halafu akampa mkono Latoya.Mwili wake wote ukatetemeka.Macho ya Latoya yalitua katika vidole vya yule kijana.Katika kidole kimojawapo alikuwa amevaa pete ya rangi ya fedha ambayo ilikuwa na alama ya x katikati iliyokuwa ikitoa miale ya kama ya moto.Hakuna aliyekuwa akiiona miale ile mikali ya moto iliyotolewa na ile pete zaidi ya Latoya pekee.
" Huyu ndiye " Latoya akasikia sauti ikimwambia.Akahisi kuchanganyikiwa.
Kijana yule ambaye alikuwa amevaa miwani myeusi alikuwa akitabasamu.Latoya akamuagalia kijana yule kwa macho ya wasi wasi sana.Alionyesha mstuko wa dhahiri.Innocent aliyekuwa amekaa pembeni ya Latoya akagundua namna Latoya alivyokuwa amestuka baada ya kumuona yule kijana.Taratibu akautoa mkono wa Latoya toka katika mkono wa yule kijana .Latoya alionekana kuishiwa nguvu.Alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
" Ouh My Gosh ! why so soon? I need more time to be with Innocent.Ninampenda kwa moyo wangu wote.I've seen the guy but I'm not ready yet..I cant do that now..." Latoya akaomba kimoyomoyo
" Nitafanya kila ninaloweza hadi nihakikishe ninakuwa na Innocent katika muda huu mfupi niliobaki nao.Yule kijana ndiye Brandon.Miaka saba iliyopita niliambiwa kwamba nitakutana na kijana aitwaye Brandon msibani.Leo imetimia.Kumuona Brandon ni ishara kwamba nimebakiwa na muda mchache sana.No I cant let that happen that fast.I must fight ."Latoya akawaza .Alikuwa amenyong'onyea sana.
Zoezi la kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu liliendelea lakini Latoya alionekana kama aliyechanganyikiwa.Alikuwa amebadilika ghafla baada ya kumuona yule kijana.Ni Innocent pekee aliyeweza kuyaona mabadiliko yale ya ghafla kwa Latoya.
“ Kitu gani kimemfanya Latoya akabadilika ghafla namna hii ? Mara tu baada ya kumuona yule kijana alibadilika ghafla akawa ni kama mtu aliyepigwa na butwaa akabaki akimshangaa .Yule kijana ni nani? Halafu mbona kila alipomtazama Latoya alikuwa anatabasamu? Kuna kitu kinachoendelea hapa si bure.Yule kijana lazima atakuwa ana uhusiano fulani na Latoya.Inawezekana akawa ni mpenzi wake ? I need to find out “ akawaza Innocent huku akijaribu kuangaza angaza kama angeweza kuona mahala alikokaa yule kijana lakini hakuweza kumuona kutokana na idadi kubwa ya watu.
Zoezi la heshima za mwisho likamalizika na kilichofuata kwa mujibu wa ratiba ilikuwa ni mazishi ambayo yangefanywa na familia pekee.Muongoza shughuli akamuomba Innocent ambaye alikuwa ni kama msemaji wa familia atoe ufafanuzi wa namna mazishi yale yatakavyofanyika.
“ Ndugu waombolezaji,kwa niaba ya familia na kwa ruhusa niliyopewa na familia ya mzee Curtis ninaomba niwataarifu kwamba mazishi yatakuwa ni ya kifamilia tu ikimaanisha mume wa marehemu ,watoto na kama kuna mtu mwingine ambaye wao watapenda aungane nao katika mazishi hayo watamchagua na atajiunga nao.Tunaomba kama hujaru……..” Innocent akastuka kidogo na kunyamaza mara alipomuona yule kijana aliyemstua Latoya.Alikuwa akitabasamu kama kawaida yake.
“ Tunaomba “ akaendelea Innocent
“ Kama hujaruhusiwa na familia ya marehemu kuingia katika mahala atakakozikwa marehemu basi usisogee mahala hapo.Narudia tena watakaoingia katika chumba chenye kaburi ni familia ya marahemu na wale tu ambao watakuwa wamechagulia na familia hii .Baada ya mazishi watu wote mtaruhusiwa kuweka mashada ya maua juu ya kaburi la mpendwa wetu “ akasema Innocent .Walinzi sita wa Latoya ambao kwa siku hii walikuwa na jukumu moja tu la kukaa pembeni ya jeneza ,wakiwa wamevalia sare maalum ambazo ni suti nyeusi wakalifunga jeneza lile zuri lenye nakshi za dhahabu na kisha wakasimama pembeni yake wakisubiri amri.Latoya akasimama,akifuatiwa na mzee Curtis halafu Innocent.Walinzi wale wakaanza kulisukuma jeneza lile kulipeleka katika chumba ambacho kulikuwa na kaburi. Vilio vya chini chini vikasikika toka kwa baadhi ya wanawake waliohudhuria msiba ule.
Hatimaye wakafika katika chumba ambacho ndani yake kuna kaburi.Ni chumba ambacho kilikuwa na uzuri wa namna yake.Ilikuwa ni sehemu iliyotengenezwa kwa ustadi wa ajabu sana.Walinzi wa Latoya wakasimama mlangoni Innocent akawafanyia ishara waingize jeneza ndani.Wakaliingiza ndani ,wakalitoa juu ya kile kitanda maalum wakaliweka juu ya vyuma vilivyokuwa juu ya kaburi.Innocent akawafanyia ishara watoke nje halafu mle ndani akabaki yeye,Latoya na mzee Curtis.Kwa pamoja wakalisogelea jeneza na kisha Latoya akaanza kufanya maombi.Baada ya maombi yale,akamuomba Innocent ausogeze mchanga uliokuwa karibu.Akamuomba mzee Curtis achote kidogo na kuurushia juu ya jeneza lile kama ishara ya kumzika rasmi mke wake . Bila ubishi mzee Curtis akachota mchanga na kuutupia juu ya jeneza halafu Latoya akamuomba atoke nje.Mzee Curtis hakutaka kubishana na mwanae,akageuka na kuanza kutoka Innocent akamshika mkono na kumsaidia akatoka na kukaa nje ya kile chumba.
“ Innocent sasa ni wakati wangu wa kumzika mama na ninaomba uwe pembeni yangu.Naomba chochote utakachokiona humu kibaki kuwa siri yako.Nimekuamini na nina imani utatunza uaminifu huo” akasema Latoya.Innocent akatikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na Latoya lakini alikuwa akitetemeka kwa ndani.
“Naomba ulifungue jeneza” akasema Latoya.Innocent huku mikono ikimtetemeka akalifungua jeneza.Latoya akaweka mikono yake yote miwili katika paji la uso la mama yake halafu akaanza kuongea maneno ambayo Innocent hakuyaelewa.Alikuwa akiongea huku amefumba macho na katika mashavu yake kulionekana michirizi ya machozi.Aliendelea kuongea yale maneno yake na mara kikatokea kitu cha ajabu ambacho nusura kimfanye Innocent atimue mbio.Uso wake uliloa jasho na mwili ukazidi kumtetemeka.
Mwili wa mama yake Latoya ulikuwa ukitetemeka mle ndani ya jeneza kadiri Latoya alivyokuwa akiongea yale meneno yake.
“ Ouh Mungu wangu haya ni maajabu gani yanatokea? Mama yake Latoya si ameshakufa sasa mbona anatingishika ndani ya jeneza? Anaonekana ni mtu aliye hai kabisa. She’s not dead..She’s alive .Ouh Mungu wangu niepushe na mauza uza haya makubwa.” Akaomba Inno
“Latoya si mtu wa kukaa naye karibu hata kidogo.Ni mtu hatari sana na ninahisi anahusika kwa namna fulani na kifo cha mama yake .Kifo chake ni kama kimezungukwa na mazingira yasiyoeleweka .Hapana kwa hali hii sintaendelea tena kuwa karibu naye. Huyu si mtu wa kuwa naye karibu hata kidogo.Mambo anayoyafanya sijawahi kuyaona na hayafai hata kuyazungumza kwa watu.Lakini nitawezaje kumuacha wakati nimekwisha muahidi kwamba nitakuwa naye siku zote? Latoya ameniamini kupita hata baba yake mzazi.Ouh Mungu wangu naomba unisaidie.Niko katika wakati mgumu sana..” akawaza Innocent
Ndani ya jeneza uso wa mama yake Latoya ulionekana kama ukiwa na jasho.Bado Latoya alikuwa akiongea katika lugha ambayo Inno hakuielewa. Inno alikuwa anatetemeka mwili mzima kwa mambo aliyoyaona.Latoya akaifungua vifungo nguo aliyokuwa amevaa mama yake halafu akatoa kitu kidogo kama kisu toka ndani ya koti lake jeusi akakata kidogo sehemu ya bega na kwa mshangao damu ikachuruzika.Inno aliona ni kama mazingaombwe fulani. Alikuwa anatetemeka mwili mzima kwa maajabu yale.
“ Help me Jesus !! ..akasema Innocent kwa sauti ndogo huku akihisi kama shati lake linaloa jasho.
Latoya akachukua damu kidogo kwa kidole chake akaipaka katika paji lauso la mama yake na kuandika herufi XXII halafu akailamba kidogo damu ile.
“ Innocent mshike mama sehemu za miguuni.Naomba ukandamize kwa nguvu “ akasema Latoya ambaye jasho jingi lilikuwa linamtoka.Innocent akakandamiza sehemu za miguu kama alivyotakiwa na Latoya halafu Latoya akaanza kuongea tena ile lugha yake isiyoeleweka.Mama yake akaanza kutikisika mle ndani ya jeneza kana kwamba anataka kutoka.Inno alizidi kutetemeka na kuogopa.Hakuwahi kuona kwa macho yake mambo kama haya.Ilikuwa ni kama anaangalia filamu lakini hii haikuwa filamu bali ni kitu cha kweli alichokuwa akikishuhudia kwa macho yake.
Ghafla chumba kikaanza kujaa moshi mweupe mithili ya wingu zito.Innocent akazidi kuogopa.Moshi ule mweupe ambao haukuwa kama ule moshi wa kawaida ambao huumiza macho ukakifunika chumba chote kiasi kwamba hakuweza kuona kitu chochote halafu akaanza kuhisi kama jeneza lile likitikisika kwa nguvu akajikuta akisukumwa na kuanguka pembeni. Baada ya dakika tatu moshi ule ukaanza kupotea na mara chumba chote kikarudi katika hali yake ya kawaida.Latoya bado alikuwa amesimama pembeni ya jeneza la mama yake akiwa amefumba macho huku midomo yake ikimtetemeka . Innocent akahisi kama miguu yake haina nguvu ya kuinuka pale alipokuwa amekaa .Bado mwili ulikuwa unamtetemeka.
“ naogopa hata kumkaribia Latoya.Huyu si binadamu wa kawaida.“ akawaza Inno akimuangalia Latoya kwa macho ya woga.Bado alikuwa amesimama akiongea maneno yake yale ya ajabu ajabu .Akageuza shingo na kumtazama Innocent aliyekuwa kimya akimuangalia kwa uoga,akamfanyia ishara ainuke pale chini na asogee katika jeneza.Inno akainuka na kulikaribia lile jeneza akakutana na kioja kingine ambacho kilimfanya atake kukimbia.Jeneza lilikuwa tupu.Maitiya mama yake Latoya haikuwemo ndani yake.Mwili ukamtetemeka akamuangalia Latoya kwa wasi wasi akashindwa aseme nini.
“ Funga jeneza” akasema Latoya na Innocent akalifunga jeneza lile.
“ Shusha jeneza chini” akasema Latoya akimuelekeza Innocent alishushe jeneza lile chini kaburini.
Inno akafyatua kidude fulani kilichokuwa pembeni ya kaburi na taratibu jeneza likaanza kushuka chini huku Latoya akiongea maneno katika ile lugha yake anayoijua mwenyewe.Jeneza liligusa sakafu ya kaburi halafu Latoya akachukua mchanga kidogo akaumwagia ndani ya kaburi lile akamuamuru na Innocent naye afanye kama alivyofanya yeye.
“ Innocent kazi imekwisha.Tayari nimemzika mama yangu.Chochote ulichokiona humu ndani itabaki siri yako.Usithubutu kumweleza mtu yeyote yule.Kwa sasa simamia mafundi waweze kulifunika kaburi hili lakini asitokee yeyote atakayethubutu kuingia ndani ya kaburi..” akasema latoya.Innoent akaitika kwa kichwa ishara kwamba amekubaliana na maagizo yale .Latoya akatoka ndani ya kile chumba akaongozana na mzee Curtis wakarejea tena katika sehemu yao ya kukaa. Kilichofuata ikawa ni chakula na vinywaji huku kwaya mbali mbali zikiendelea kuimba nyimbo za maombolezo.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………………..
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 40
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Funga jeneza” akasema Latoya na Innocent akalifunga jeneza lile.
“ Shusha jeneza chini” akasema Latoya akimuelekeza Innocent alishushe jeneza lile chini kaburini.
Inno akafyatua kidude fulani kilichokuwa pembeni ya kaburi na taratibu jeneza likaanza kushuka chini huku Latoya akiongea maneno katika ile lugha yake anayoijua mwenyewe.Jeneza liligusa sakafu ya kaburi halafu Latoya akachukua mchanga kidogo akaumwagia ndani ya kaburi lile akamuamuru na Innocent naye afanye kama alivyofanya yeye.
“ Innocent kazi imekwisha.Tayari nimemzika mama yangu.Chochote ulichokiona humu ndani itabaki siri yako.Usithubutu kumweleza mtu yeyote yule.Kwa sasa simamia mafundi waweze kulifunika kaburi hili lakini asitokee yeyote atakayethubutu kuingia ndani ya kaburi..” akasema latoya.Innoent akaitika kwa kichwa ishara kwamba amekubaliana na maagizo yale .Latoya akatoka ndani ya kile chumba akaongozana na mzee Curtis wakarejea tena katika sehemu yao ya kukaa. Kilichofuata ikawa ni chakula na vinywaji huku kwaya mbali mbali zikiendelea kuimba nyimbo za maombolezo.
ENDELEA……………………
Wakati zoezi la chakula likiendelea Innocent alikuwa akiwasimamia mafundi kutoka kampuni ile iliyotengeneza kaburi la mama yake Latoya katika kulifunika.Alikuwa amekaa pembeni ya chumba kile kilichokuwa na nakshi za kuvutia sana akiwa na mawazo mengi mno.Alichokiona leo kilimstua sana..
“ Ndani ya kaburi hili kumuwekwa jeneza tupu.Mwili wa mama yake Latoya haupo.Umekwenda wapi? ..akajiuliza Inno bila kupata jibu.jasho jingi likaendelea kumtiririka.
“ Latoya ni mtu wa namna gani ? Nimeshindwa kumuelewa ni kiumbe wa namna gani.Naogopa hata kumsogelea . Ni mtu hatari sana na maisha yake yametawaliwa na mambo ya kutisha sana.Lazima nijitoe katika maisha haya haraka iwezekanavyo.Ili niwe salama ,lazima nikae mbali naye.Japokuwa ameniamini kupita watu wote,sina namna nyingine zaidi ya kuyaokoa maisha yangu zaidi ya kuondoka wakati bado nina nafasi.” Akawaza Innocent.
“ Tatizo nimekwisha zijua siri zake.je atakubali kuniachia niende zangu? Nadhani hiyo ndiyo itakuwa mbaya zaidi na inaweza hata kumpandisha hasira akaamua kuniua kabisa kwa sababu hataki siri zake zijulikan.Sikutegemea kama siku moja ningeingia katika maisha kama haya.” Akaendelea kuwaza Inno huku mafundi wakiendelea kulifunika kaburi.
Shughuli ya kulifunika kaburi la mama yake Latoya ilichukua kama saa moja hivi kisha watu wakaruhusiwa kuingia na kuweka mashada ya maua.Muda wa nusu saa kaburi lote lilikuwa limefunikwa na maua hata likashindwa kuonekana.Wakati zoezi lile la uwekaji wa maua likiendelea Latoya alikuwa akisalimiana na watu mbali mbali ambao walikuja kumpa pole.Wakati akisalimiana nao mara akatokea tena yule jamaa aliyemfanya astuke wakati wa kutoa heshima za mwisho. Latoya akastuka tena alipomuona akamshika mkono na kumuongoza wakaelekea ndani.
Zoezi la uwekaji wa mashada ya maua likakamilika na baadhi ya watu wakataka kuanza kuondoka akiwemo mheshimiwa waziri mkuu.Inno akamtafuta Latoya lakini hakumuona.Walinzi wake wakasema kwamba alikuwa ameelekea ndani ya nyumba akiwa ameongozana na kijana mmoja .
“ lazima atakuwa ni yule yule kijana aliyemfanya akastuka muda ule.Huyu kijana ni nani ? I must find out” akawaza Inno huku akipiga hatua kuelekea ndani. Katika chumba kidogo ambacho Latoya huwa anakitumia kwa maongezi ya faragha mlango haukuwa umefungwa Inno akajitokeza na kusikia kama watu wakibishana.Akatega sikio na kuisikia sauti ya Latoya.
“ Brandon siko tayari kwa sasa…Utalazimika kunisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari.Nina jambo kubwa na la msingi sana ambalo lazima nilitimize kwani ni ahadi niliyojiwekea mimi mwenywe kuitimiza kabla sijafa.Kwa namna yoyote ile lazima niitimize ahadi hiyo..” Akasema Latoya kwa sauti ya ukali
“ Nitasubiri kwa muda gani Latoya ? Sina muda zaidi wa kuendelea kusubiri. Muda wangu umefika…” akasema yule kijana
“ Brandon utanisikia na kufuata nitakavyokwambia.Lazima usubiri na hiyo ni amri na si ombi.Nasem…………..” Latoya hakumalizia sentensi yake akasikia mlango unagongwa.Alikuwa ni Innocent.wote wawili wakastuka sana.
“ Innocent ! akasema Latoya kwa mstuko.
“ How long have you been here at the door? Akauliza Latoya.
“ Ndiyo nakuja sasa hivi Latoya..kwani vipi? Akauliza Inno
“ Nothing’ akajibu Latoya.
“ So this is Innocent ? akauliza Brandon huku akimuangalia Innocent kwa macho ya mshangao.
“ Yah I’m Innocent” akasema Inno huku akimpa Brandon mkono.
“ Nimefurahi kukuona Innocent..Mimi na wewe tutakutana mara nyingi kuanzia sasa” akasema Brandon na Inno akashindwa kumuelewa akabaki anamuangalia.
“ Latoya waziri mkuu na ujumbe wake wanataka kuondoka.tunatakiwa tukawaage.” Akasema Innocent huku sauti yake ikitetemeka.
“ Brandon nadhani wewe tumekwisha malizana unaweza ukaondoka.Tutazidi kuonana” akasema Latoya akamshika mkono Innocent wakatoka mle chumbani huku Brandon akiwaangalia kwa macho makali akionekana kuwa na hasira.
“ Sharha..patakamos lahuut ba venda..Usskhoom sha lavia” akatamka maneno haya Brandon .Latoya hakumjali akamshika Inno mkono wakaondoka zao .Bado Inno alizidi kuchanganyikiwa aligeuka akamtazama tena Brandon aliyekuwa bado amesimama akiwaangalia .
" Huyu kijana ni nani na anataka nini kwa Latoya? Ni kwa nini Latoya mara tu alipomuona alistuka sana ? ..Innocent akawaza akiwa ameongozana na Latoya wakielekea sehemu ya wageni wa heshima kwenda kuagana na viongozi na wageni waliokuwa wamehudhuria mazishi yale ya mama yake.
" Brandon siko tayari kwa sasa…Utalazimika kunisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari.Nina jambo kubwa na la msingi sana ambalo lazima nilitimize kwani ni ahadi niliyojiwekea mimi mwenywe kuitimiza kabla sijafa.Kwa namna yoyote ile lazima niitimize ahadi hiyo..” kauli hii ya Latoya akimwambia Brandon ilizidi kujirudia kichwani kwa Innocent.
"Alikuwa na maana gani aliposema kwamba hayuko tayari kwa sasa? hayuko tayari kwa jambo gani? Ni jambo gani ambalo Latoya ameweka ahadi ya kulitimiza kabla hajafa?." Kichwa cha Innocent kikajaa mawazo mengi sana lakini hakuweza kupata majibu .
" Maisha ya Latoya ni fumbo kubwa .Kwa sasa nina hakika kabisa kwamba huyu ni mfuasi wa nguvu za giza kwa mambo niliyoyashuhudia kwa macho yangu mwenyewe leo." Akawaza Innocent wakiwa tayari wamefika eneo la jukwaa kuu alikokuwapo mheshimiwa waziri mkuu pamoja na baadhi ya viongozi wa ngazi mbali mbali toka serikalini.Latoya akamshukuru na kuagana na mheshimiwa waziri mkuu pamoja na ujumbe wake wote wakaondoka wakifuatiwa na baadhi ya watu waliohudhuria shughuli ile ya mazishi ya mama yake Latoya.Baada ya idadi kubwa ya wageni kuondoka Latoya akamuelekeza Irene amuandalie mzee Curtis chumba cha kulala katika moja ya vyumba vya watu maalum Latoya alipatwa na mshangao pale baba yake mzazi mzee Curtis alipokataa kata kata kulala katika jumba hili la Latoya na akataka apelekwe nyumbani kwake .
" Baba kwa nini hutaki kulala hapa kwangu? akauliza Latoya
" Utanisamehe Latoya lakini kwa sasa ninahitaji kulala nyumbani kwangu katika chumba nilichokuwa nikilala na mke wangu." akasema mzee Curtis.Latoya akaumia mno moyoni kwa kauli ile ya baba yake.
" Masikini baba yangu anateseka sana kwa kifo cha mama.Ingawa hawezi kunieleza wazi wazi lakini ni wazi ameumia mno na mambo yaliyotokea.Kifo cha mama hata mimi kimenihuzunisha mno kwani sikuwa nimetarajia kama kingetokea. Kifo hiki cha mama yangu kinazidi kuniongezea maumivu na mateso makali. " akawaza Latoya huku akimuangalia baba yake kwa macho ya huruma.
"Baba nafahamu ni kwa namna gani unavyoumia kwa kifo cha mama lakini kurudi tena pale nyumbani na kulala katika chumba kile kile ulichokuwa ukikitumia na mama kutakuongezea machungu zaidi na kukufanya uzidi kuumia.Baba sitakii uendelee kuumia zaidi.Kesho nitakuhamishia nje ya nchi kwa ajili ya mapumziko jambo ambalo linaweza kukusaidia kupunguza machungu ya kifo cha mama" akasema latoya
" latoya huna haja ya kuhangaika na mimi hata kidogo.Baada ya kifo cha mke wangu niliyempenda sioni thamani yangu tena hapa duniani. Mke wangu ndiye alikuwa kila kitu kwangu.Nimeshuhudia kwa macho yangu namna alivyofariki nimeumia mno.Sitaki kwenda sehemu yoyote ile ninataka kubaki hapa hapa nyumbani kwangu Tanzania niendelee kumlilia mke wangu.Sihitaji kwenda ulaya wala sehemu nyingine yoyote ile.Nataka nikaishi nyumbani kwangu katika chumba nilichokuwa nikilala na mke wangu " akasema mzee Curtis .Latoya alishindwa kujizuia akatoa machozi.
"Sawa baba nimekuelewa.Nitakurejesha kwako lakini utakuwa chini ya uangalizi maalum wa walinzi na wahudumu wangu." akasema Latoya
" sihitaji chochote toka kwako kwa sasa Latoya.Just forget me for a while.I need a world of my own." akasema Mzee Curtis.Latoya akazidi kuumia kwa maneno yake ya baba yake.
" Baba siwezi kukuacha hata sekunde moja.wewe ndiye baba yangu na familia yangu pekee." akasema latoya.Baba yake akamuangalia kwa macho makali na kusema
" Your father and your family is your money.Utajiri wako ndiyo kila kitu kwako kwa sasa.Money is everything to you.From now on forget that you have a father" akasema mzee Curtis kwa ukali.Latoya akashindwa kujizuia kuangusha machozi.
" Innocent take my father home.Take him away from here..." akasema Latoya huku akilia.
" Latoya......" Innocent akataka kusema kitu lakini Latoya akamzuia
" Fanya ninavyokwambia Innocent..Mpeleke baba nyumbani kwake" akaamuru Latoya.Bila ubishi Innocent akamshika mkono na kumsaidia mzee Curtis kutembea hadi katika gari .Wakati anamuingiza mzee Curtis katika gari mara akageuka na kukutana na sura yenye tabasamu ya Brandon akiwa ameegemea gari lililokuwa mita chache .Wakatazamana kwa sekunde kadhaa halafu Innocent akaingia garini na kuliwasha na taratibu akaanza kundoka . Mwili wake ulikuwa umesisimka sana baada ya kumuona Brandon akiwa pale tena akiwa na tabasamu
" Who is this guy?..Innocent akajiuliza
" Anataka nini kwa Latoya? Kwa nini hataki kuondoka pale nyumbani kwa Latoya? " Bado aliendelea kuumiza kichwa .Ujio wa Brandon hata yeye ulianza kumuogopesha .
" I must find out who is that guy...Lazima niufahamu ukweli Brandon ni nani" Innocent akajikuta akitamka maneno haya kwa sauti na kumfanya mzee Curtis kustuka.
" Innocent unaongea na mimi? akauliza mzee Curtis
" Hapana mzee.. Kichwa changu kina mambo mengi sana siku ya leo" akasema Innocent
" Innocent wewe ni kijana wangu.Ni zaidi ya mwanangu kwa hiyo ninaomba nikueleze ukweli." akasema mzee Curtis
" Nimeamua kukaa mbali na maisha ya Latoya.Ni binti yangu wa pekee na ninampenda sana lakini kwa maisha yake ya sasa imenilzimu kukaa mbali naye.Kifo cha mke wangu kimeniumiza mno na hasa nikikumbuka mazingira kilivyotokea.Moyo wangu unauma kiasi ambacho siwezi kuelezea.Siwezi tena kuendelea kuwa sehemu ya maisha ya Latoya kwa sasa.Fedha mali na utajiri ndivyo vitu vyake vya thamani kwa sasa.Ninahitaji kuwa mwenyewe niendelee kumlilia mke wangu" akanyamaza kidogo halafu akaendelea
"Innocent ninakuomba kitu kimoja kijana wangu"
" Omba chochote mzee usihofu" akajibu Innocent
" Ninakuomba usimuache Latoya hata kwa sekunde moja.Wewe ndiye mtu pekee ambaye anakuamini kwa sasa na ambaye unaweza ukamfanya akatabasamu na kuwa na furaha.Nina imani hata yeye mwenyewe anaumia sana kwa kifo cha mama yake na mtu pekee wa kumfariji ni wewe. Hana mfariji mwingine kwa sasa zaidi yako." akasema mzee Curtis.Innocent hakujibu kitu.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………